Story
ella hakuwa na usingizi hata kidogo. Alipojiridhisha kuwa
amelala kabisa, akajisogeza pembeni zaidi ili asigusane na Mzee Masha,
akaendelea kulia taratibu. Ilikuwa ngumu kwa Bella kujua kama ametatua matatizo
yake yeye na mdogo wake au ndio ameongeza matatizo zaidi. Alikaa akiwaza, mpaka
ilipofika mchana Mzee Masha alipoamka. “Tuwahi
kuzunguka madukani, Bella. Nataka ukanunue nguo za kutosha.” Katika
maongezi yao, Mzee Masha ndiye aliyekuwa akitoa maagizo tu na Bella alikuwa lazima
kuitikia jibu moja tu, la ‘ndiyo au Sawa’.
Eric alifurahi sana kumuona dada yake. Alimkumbatia kwa muda mrefu sana. Ilikuwa kama mtu anaosha moyo wa Bella, moyo wake ulifunguka, furaha ya ajabu sana ikaingia nafsini mwake. Kwa muda mrefu wa matatizo, Bella alijikuta akicheka baada yakumuona Eric.
Waliondoka pale kwenye viwanja vya ndege vya Mwalimu Nyerere, giza ndio lilikuwa likiingia, na kwa sababu ya foleni njiani, alifika nyumbani kwake usiku. Alimkuta Mzee Masha akimsubiri sebleni. Alishtuka kidogo. “Pole na safari.” Bella alisalimia kwa hofu asijue nini kitafuata. “Asante na wewe pole na safari. Eric anaendeleaje?” “Asante. Anaendelea vizuri tu." Bella alitulia kidogo kama anayesubiria aone kinachofuata. Masha alikuwa ametulia kwenye kochi, akazima tv, na kufunga gazeti alilokuwa anasoma, akaweka pembeni. "Asante kwa maandalizi ya safari. Sijasumbuka hata kidogo!” Bella aliongeza. "Afadhali na karibu." Masha alijibu na kubaki akimtizama Bella. “Umeshaoga?” Bella alimchokoza kama kumpooza. Alishajua udhaifu wake, akaamua kuutumia ipasavyo. Mzee Masha alicheka kidogo. “Nakusubiri wewe.” “Twende basi.” Bella aliongea kwa upole, na kumfanya Mzee Masha aliwazike. Aliweka pochi yake juu ya meza, akaanza kufungua zipi yake pembeni ya ubavu wa gauni hilo alilokuwa amevaa huku akimtizama Masha, akaelekea chumbani. Masha naye akasimama kumfuata na tabasamu usoni. Alishangazwa na ushirikiano wa mara ya kwanza alioupata kutoka kwa Bella.
“Sasa hapa si itakuwa imekugharimu sana?” Bella alijaribu kuhoji siku hiyo ya tatu, ilikuwa jioni walipokuwa ufukweni wakitembea kwa mara ya kwanza tokea wafike visiwani hapo. Kwani kwa siku mbili walibaki chumbani tu. Bella akisema anahitaji sana ule muda wa mapumziko kwani alimlalamikia Masha kuwa alikuwa na shuguli nyingi sana huko nyumbani hakuwa akipata muda naye. Na ni kweli hata Masha alionekana akihitaji hayo mapumziko. Alikuwa akila na kupata muda wakutosha wakulala vizuri, kwa kuwa hakuwa akiwaza kazi, na Bella mrembo wake akiwa pembeni yake. Siku hizo mbili ilikuwa mapenzi, kula na kulala tu. Aliamshwa na mabusu, alilala kwa mabusu ya Bella. Mungu ampe nini Masha!
Ilikuwa rahisi kwao kutembea pamoja, au hata Bella kumbusu Masha na kuonyesha mapenzi yao waziwazi, hadharani bila shida katika maeneo hayo, kwani hakuna aliyemjali mwenzake. Kila waliyekutana naye huko, alikuwa akiangalia mambo yake. Kwa hiyo hata Mzee Masha hakusita kutembea akiwa amemshika Bella kiuno, akijivunia mapenzi ya mtoto huyo.
Walikuwa wakikutana kijijini kwao vipindi vya sikukuu za krismasi, lakini pasaka, walikuwa wakiwa pamoja mjini. Walitafuta nyumba moja, walipika pamoja na kula pamoja. Mpaka walipokuza familia zao, utaratibu uliendelea. Watoto wao walisoma shule nzuri sana kwa kupitia michango yao wao wenyewe. Waliofanikiwa kwenda vyuo vikuu, hawakusubiri mikopo ya serikali ili kupeleka watoto wao shule, wao wenyewe walichanga na kusomesha watoto wao.
Haikutokea tokea tu mama huyo kuteuliwa kuwa balozi. Alianza kujijengea jina tokea zamani, na alikuwa ni mama aliyejulikana sana nchini Tanzania. Kuteuliwa huko, kwake ilikuwa ni moja ya ndoto zake alizotamani kuja kutimia, kwani alikuwa na ndoto za kwenda juu zaidi ya hapo.
Junior alijitahidi kuacha pombe kwa muda, akimuahidi Bella atatulia lakini Bella alimkatalia kabisa. Zera alisha mbembelezea kaka yake, na kumwambia Bella, endapo angemkubali Junior kaka yake, itamsaidia kutulia na labda angependa shule kama wenzake. Lakini Bella alikataa kata kata, hata kunakipindi urafiki wao uliisha sababu ya Bella kumkataa kaka yake. Mwishowe walikubali kuwa Bella haingiliki.
Watoto hao wakiongozwa na watoto wa Masha, upande wa mabinti kiongozi wao alikuwa Zera Masha na upande wa vijana wakiume wale wenye tabia za ajabu, waliongozwa na Junior Masha, walikuwa wakitapanya pesa za wazazi wao, bila kujali kesho. Zera ndiye alikuwa kipenzi cha baba yake, kwa kiyo hata kama Mzee Masha alikuwa na kazi nyingi kiasi gani, anapohitajika kuhudhuria kitu chochote alichoandaa binti yake, alikwenda. Na ndipo huko alipokuwa akionana na Bella akiwa uchi au wamevaa yale mavazi yao wanayodai ya watoto wakizungu na kuacha sehemu kubwa za miili yao nje. Na ndio tokea wakati huo, kwa mara ya kwanza maishani, mbali na mkewe, jicho la Mzee Masha ndipo lilipoanza kupata matatizo juu ya mtoto huyo Bella.
Ndicho kipindi hicho Bella ilimbidi ajifunze maisha au kazi za nyumbani. Alijifunza biashara, kwani ilimbidi kuanza kuuza baadhi ya vitu vya thamani walivyokuwa navyo ili kuweza kumudu matibabu ya mama yake, na ada ya mdogo wake ambaye bado alikuwa shuleni. Bella alikuwa msaada mkubwa sana kwa mama yake. Zile akili za kitoto na kupenda starehe, akizunguka kwenye magari ya kina Zera Masha, na kulala kwenye mahoteli ya gharama na familia hiyo ya Masha, zilibadilika, akarudi kwenye uhalisia wa mambo, akaanza kushika majukumu ya mama yake.
Ukweli Masha alishakuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa mkewe. Hakuwahi kuwa na mwanamke wa nje, Bella pekee ndiye wakwanza. Alipogundua uovu wa mkewe, alichanganyikiwa sana, na kujiambia labda atakuja kutubu leo, au kesho. Siku zilizidi kwenda bila mkewe kutubu ila kulalamikia tabia za mumewe. Kila baya alilokuwa akifanyiwa na Masha kwa makusudi, mama huyo alimkumbusha kuwa yeye ni mkewe, na aliapa katika shida na raha. Kwa hiyo kifo pekee ndicho kitawatenganisha. Hana mpango wakumuacha hata akizidi kumtenda ubaya. Mzee Masha alikuwa akikasirika sana kila akisikia kauli hiyo, kwani alimjua vile mkewe alivyo. Ni mwanamke aliyekuwa akijua ni kitu gani anataka maishani, na hata kama ni kigumu namna gani, akisema atapata, lazima atakipata tu, kama mumewe alivyo. Hata hivyo alikuwa na sababu kubwa sana iliyomfanya abaki na Masha.
Nyumbani kwa Mama Mwasha ndio kilikuwa kituo chao kikubwa, kwani mama huyo alikuwa mama mwenye hekima sana, na alijawa na upendo. Kwa hiyo ni kama alikuwa ndiye kiongozi wao, hao kina mama. Walifanyia vikao vyao vyote nyumbani kwa Mwasha. Waliambizana kuwa Mama Masha yupo nchini na angeomba wote wakutane, ana jambo la kuwashirikisha.
Alikaribia kurukwa na akili. Mwili ulikuwa kwa familia yake, akili kwa Bella, aliyekuwa akienda na kurudi shuleni peke yake, tena akijua wazi Masha yupo mjini kwa mkewe, lakini hafiki nyumbani kumuona. Hiyo ndiyo ilizidi kumchanganya Masha. Alikosa ujasiri hata wakupiga simu kwa Bella aliyekuwa akimkataza kuwa na wanaume wengine, wakati yeye yupo na mkewe nyumbani kwake, na kushindwa hata kumuona.
My Past - Sehemu ya 3.
|
B
|
ella hakuwa na usingizi hata kidogo. Alipojiridhisha kuwa
amelala kabisa, akajisogeza pembeni zaidi ili asigusane na Mzee Masha,
akaendelea kulia taratibu. Ilikuwa ngumu kwa Bella kujua kama ametatua matatizo
yake yeye na mdogo wake au ndio ameongeza matatizo zaidi. Alikaa akiwaza, mpaka
ilipofika mchana Mzee Masha alipoamka. “Tuwahi
kuzunguka madukani, Bella. Nataka ukanunue nguo za kutosha.” Katika
maongezi yao, Mzee Masha ndiye aliyekuwa akitoa maagizo tu na Bella alikuwa lazima
kuitikia jibu moja tu, la ‘ndiyo au Sawa’.
Walitoka hapo hotelini akachukua taksii, wakapanda. Alimzungusha
kwenye maduka ya thamani matupu. Alimnunulia nguo, viatu, pochi na pafyumu za
gharama sana. Bella alibaki kimya kabisa akiangalia jinsi Mzee Masha
anavyomwaga mapesa mengi sana juu yake. Walirudi hotelini Mzee Masha akionekana
anafuraha sana, lakini sio Bella.
“Mbona upo kimya?
Unafikiria nini?” Masha aliuliza lakini
Bella hakujibu. “Ninapouliza swali, au
ninapoongea na wewe nataka uwe unanijibu, Bella. Umenisikia?” “Ndiyo.” “Sasa
nakuuliza, kwa nini upo kimya?” “Nasikia maumivu makali sana, na…” Bella akashindwa kuendelea, akaanza kulia kwa kwikwi. “Ngoja nikupe dawa za kutuliza maumivu,
nitaagizia chakula tule humuhumu ndani. Pole sana.” Kidogo Mzee Masha
alionyesha ubinadamu. Alimpa dawa, na kurudi kukaa naye pale pale kitandani
mpaka alipolala. Walikaa pale hotelini kwa siku kama nne zaidi akimuuguza.
Asubuhi Mzee Masha alikuwa akitoka na kumuacha Bella hotelini mpaka mida ya
mchana ndipo anaporudi na kuwa naye siku nzima, huku akimuhudumia kwa karibu,
bila kumtaka tena kimapenzi. Alipunguza ukali kidogo, akawa na ubinadamu kiasi.
**************************************************
Bella hakujua ni nini Mzee Masha anafanya, na wala watoto wake
hawakuwahi kuzungumzia biashara ya baba yao, lakini alijulikana kuwa ni
milionea. Hata uzee ambao watu walikuwa wakimwita ni sababu ya pesa nyingi,
lakini hakuwa mzee kihivyo. Wakiwa wanarudi Tanzania, wakiwa wapo kwenye ndege,
alianza kumuuliza Bella. “Ungependa
kuishi maeneo yapi?” “Popote tu.” “Nataka ufikirie, kisha uniambie ili nijue
nakununulia nyumba maeneo yapi. Hatuwezi kuendelea kuishi hotelini tena.”
Bella alitamani kuruka nje ya ile ndege. Kila alipofikiria kuwa ndio
ameshaolewa, na nilazima aishi na yule baba, alihisi kuchanganyikiwa. ‘Lakini
kwa sababu ya Eric, acha nikubali kujitoa kafara.’ Bella aliwaza.
“Hili ndilo gari
nimekununulia jana wakati umelala. Unalionaje?” Mzee Masha alitoa ‘Ipad’ yake na kuanza kumuonyesha Bella
picha ya gari la thamani sana alilomnunulia. “Wamelisafirisha leo, kuelekea Dar.” “Asante sana.” “Umelipenda
lakini?” “Ndiyo, nimelipenda.” Masha alifurahi sana. “Sasa bado sehemu ya kuishi. Nataka tukaishi kwenye nyumba yetu, Bella.
Mimi na wewe. Umesikia?” “Ndiyo.” Mzee Masha alikuwa na sura iliyojaa
furaha sana. Tabasamu halikumwisha usoni.
“Maisha ya Bella na Masha yaanza
rasmi.”
Bella alinunuliwa jumba la kifahari, Mbezi Beach.
Ninaposema beach, namaanisha ufukweni. Hakujua yule mzee alifanyaje, kama
alihamisha mtu au la, lakini Bella alitolewa hotelini na kuhamishiwa kwenye
nyumba hiyo. Mzee Masha alikuwa ni kama amechanganyikiwa na Bella. Alijawa na
furaha aliyoshindwa kuificha. Japokuwa alijulikana kama katili sana, lakini kwa
kitendo cha kufanikiwa kummiliki Bella, furaha ilijidhihirisha usoni mwake.
Huku hofu ya kuporwa Bella mjini hapo ikimsumbua, kwa tofauti ya umri wao. Ili
kumdhibiti na kumtawala yeye peke yake, akaamua kuendeleza kutumia mabavu yote
kumuogopesha Bella, ilimradi tu yeye ndiye awe mwanaume pekee kwake.
Baada ya kuona bado kuna utoto mwingi na hofu kwa Bella,
yule dereva wa Masha kwa kujipendekeza kwa Masha, alimpa wazo la kumtafutia
Bella, mama mtumzima anayeweza kumfundisha Bella maisha ya kuishi na mume na ya
unyumba kwa ujumla. Masha alilipokea hilo wazo kwa furaha sana, yule dereva
akamleta huyo mama aliyekuwa akilipwa mapesa mengi sana, ili awe anakuja
kumfundisha Bella. Alikuwa akifika nyumbani hapo kila siku, kwa masaa matatu,
mara Masha anapoondoka kwenda kazini, kasoro siku za Jumamosi na Jumapili
ambazo Masha anapokuwepo nyumbani.
Mzee Masha hakutaka mtu yeyote pale nyumbani kwao siku hizo
au muda huo yeye awapo nyumbani. Alitaka abaki yeye na Bella tu. Nyumba ilijaa
wafanyakazi wa kila namna, na wote walikuwa wakimtumikia Bella. Walikuja
asubuhi na kuondoka wote jioni kabla Mzee Masha hajarudi nyumbani hapo. Wapo
waliokuwa wakisafisha ndani, wengine nje. Wapo wafanyakazi waliokuwa wakifua,
na wanaohusika na mambo ya jikoni. Kazi yake Bella ilikuwa ni kumfurahisha Mzee
Masha na usafi wa chumbani kwake tu.
**************************************************
Kwa kuwa Masha alikuwa msafi wa kupitiliza, ile nyumba
ilikuwa ikiwaka wakati wote. Hata Bella mwenyewe ilimlazimu kuwa nadhifu wakati
wote. Masha alikuwa na kinyaa ambacho Bella alihisi ni ugonjwa. Hakuwa akitaka
harufu mbaya au tofauti na harufu anazozichagua yeye. Nyumba yao ilinukia
manukato aliyoyachagua yeye mwenyewe Mzee Masha, na Bella alitumia losheni,
sabuni zakuogea na pafyumu alizochagua Masha, sio vinginevyo. Nguo za ndani za
mzee huyo, zote zilikuwa nyeupe sana. Alijaliwa weupe na kwa kuwa alijua usafi,
kwa kumwangalia tu, utajua ni msafi. Ngozi yake yenyewe iliwaka kama taa.
Alitumia vitu maalumu kwenye mwili wake. Hakuwa akiogea kila sabuni au kupaka
kila mafuta. Alikula na kujali mwili wake, kitu kilichokuwa kikimshangaza sana
Bella, aliyezoea kuyaona hayo mambo kwa baadhi ya wanawake. Kila kitu cha Masha
kilikuwa na usafi wa aina yake. Ilimlazimu Bella kujipenda zaidi yake ili
kumridhisha na kuweka amani pindi arudipo nyumbani. Chumbani kwake hakutaka mtu
yeyote aingie wala aguse hata kitanda anacholalia isipokuwa Bella tu. Na
wafanyakazi wake wote walikuwa wasafi, na walivaa sare maalumu kila wajapo
kazini.
**************************************************
Yule mama aliyekabidhiwa kumfundisha Bella aliporidhika na
kuona amefanikiwa kumtoa Bella kwenye kundi la watoto na kumfikisha kwa watu
wazima, ndipo alipomkabidhisha rasmi kwa Mzee Masha. Mzee Masha alimlipa pesa
nyingine nyingi kama shukurani yake kwake. Bella alibadilika sana, na kwa kuwa
mafunzo yote alikuwa akipewa kutokana na matakwa ya Mzee Masha, alijitahidi
kumridhisha huyo Mzee kwa kadiri ya uwezo wake. Alikuwa kama mtumwa kwa Masha.
Kwa kuwa pia alikuwa mtoto sana, na alifanya kwa kuamrishwa, na yeye alikubali
kwa kumlinda mdogo wake. Kwani Mzee Masha alirudia rudia sana, kumtishia Bella
uhai wake na mdogo wake, pindi Bella atakavyo fanya vinginevyo.
Kwa hiyo Bella hakuwahi kufaidi mapenzi hayo hata kidogo.
Alihesabu ni moja ya wajibu wake anaotakiwa kutimiza kila Mzee Masha atakapo
muhitaji. Wakati mwingine Mzee Masha alitoka asubuhi akisema anaenda kazini,
lakini baada ya muda mfupi alirudi nyumbani akisema anamuhitaji Bella.
Alimtumia huyo mtoto kwa muda na wakati anaotaka yeye. Asubuhi, mchana au
usiku, kwa kadiri alivyojisikia yeye siyo Bella. Sehemu pekee aliyopata
ya kutoa dukuduku lake ni kipindi akiwa chooni au Mzee Masha anapokuwa amelala
au yupo kazini. Bella alikuwa akilia sana. Jumba lile la kifahari na mavazi ya
thamani aliyonayo, hayakumpa furaha hata kidogo. Alijiona mtumwa wa kila kitu. ‘Lakini kwa sababu ya Eric,
nitavumilia. Atakuja kumuua Ric bure. Huyu baba ni mkatili sana.’ Bella aliendelea
kujifariji.
Muda mwingine Bella aliokuwa akiupata wakupumzisha mwili na
akili zake, na hata kupata nafasi ya kwenda kumtembelea mdogo wake shuleni,
huko Arusha ni pale tu Mzee Masha anapokuwa amekwenda nchini Uholanzi kuona
familia yake. Hapo ndipo Bella aliweza hata kufikiria kitu kingine sio Mzee
Masha pekee. Alinunuliwa simu, lakini hiyo simu ilikuwa imewekwa ‘GPS’, ambayo
ilikuwa ikimuonyesha Mzee Masha kila mahali Bella alipo, kana kwamba isitoshe,
aliitegesha jinsi ya kujirikodi. Kwa hiyo endapo simu yeyote ingeingia au
kutoka kwenye simu hiyo, ingejirikodi namba na mazungumzo yote. Alimchunga
Bella kupita kiasi. Alikuwa kama aliyekuwa amechanganyikiwa na mtoto huyo.
**************************************************
Siku moja Mzee Masha akiwa safarini, Bella akaamua
kumtafuta dereva wao, Mat. Kwani ilishapita muda mrefu sana tokea siku ile
alipowapeleka kwa Mzee Masha kwenda kuomba msaada, hawakuonana tena wala
kuwasiliana. Aliwashusha nje ya geti na kuwaahidi angewafuata jioni yake.
Alijua wazi Mat angekuwa na wasiwasi, kwani hakujua alijibiwa nini siku
aliporudi kuwafuata. Hakuweza kumtafuta kwa kipindi chote hicho kwani alikuwa
akifungiwa ndani, hakuruhusiwa kutoka mle ndani isipokuwa yupo na Mzee Masha
tu, hata simu yenyewe alinunuliwa si kwa ajili yake, ni kwa ajili ya Mzee Masha
mwenyewe pindi awapo mbali naye. Uzuri wa Bella, tofauti ya umri na mambo
aliyokuwa akimfanyia Mzee Masha, ilimbidi Mzee Masha azidi kuwa makini sana
kuhakikisha vijana wa mjini hawamzidi mahesabu.
Kwa mara ya kwanza Bella alitumia simu hiyo kumpigia mtu
mwingine mbali na Mzee Masha. Na wala hakujua kama simu hiyo inauwezo wa
kurikodi na kuonyesha alipo. “Nimewatafuta mpaka nimekata tamaa. Uko wapi?” “Nipo
kaka. Nilitaka kukusalimia na kukujulisha tupo salama.” “Asante sana Bella.
Nataka nije niwaone.” Bella asingeruhusu hata iweje Mat kufika hapo nyumbani
kwake yeye na Mzee Masha, kwani kulikuwa na camera kila kona, na zote alikuwa
akimuona Mzee Masha akizipitia kuziangalia kila arudipo nyumbani. “Tunaweza kukutana
mahali.” Bella alimuwahi. Mat alikaa kimya kwa muda. “Hata hivyo
Eric hayupo. Nipo mimi peke yangu. Kwa hiyo ni bora nije tu mimi.” “Kwani
unaishi wapi?” “Naomba tuongee kila kitu tutakapo kutana.” “Lini?” Mat alihoji. “Hata leo. Au una kazi nyingi?” Bella aliuliza. “Kukuona wewe ni muhimu Bella. Sijui uko wapi,
sijui mnaishije huko, lazima tuonane. Wakati wowote ule utakapokuwa tayari
ukiniita, nitakuja.” “Basi naomba tukutane mida ya mchana. Tunaweza tukapata
chakula cha mchana pamoja.” Bella
alimpa maelekezo yote, muda na hoteli watakayo kutania na Mat. Mat akakubali,
wakaagana.
Alivaa kawaida sana, ili asimstue Mat, lakini kutokana na
uzuri wake, alipendeza kama kawaida yake. Tena hakutaka hata kuvaa vito vya
thamani. Alivua dhahabu alizokuwa amenunuliwa na Mzee Masha, na kurudisha cheni
aliyokuwa amepewa zawadi na mama yake, tena ilikuwa na kidani chake,
ambacho kilibeba kumbukumbu zilizokuwa zikimpa nguvu za kuendelea kupambana na
maisha anayoishi sasa. Swala la usafiri ndio lilianza kumsumbua, kwani gari
alilokuwa amenunuliwa lilikuwa la kifahari sana, alijua lingeibua maswali mengi
sana kwa Mat ambaye hakuwa tayari kumwambia maisha anayoishi kwa wakati ule,
kwa kulinda usalama wake. Lakini sehemu waliyokuwa wakiishi hapakuwa na taksii,
wala daladala, na simu aliyokuwa nayo kichwani ilikuwa ni ya Mat tu mbali na ya
Mzee Masha. Kwa hiyo ilimlazimu aondoke na gari yake.
Alimkuta Mat akimsubiri sehemu ya kuegesha magari. Alibaki
akimwangalia Bella alipokuwa akishuka kwenye gari hiyo. “Shikamoo kaka Mat.” “Ulisema
unaishi wapi!?” Hilo ndilo
swali la kwanza Mat, alilomuuliza Bella mara baada ya kushuka kwenye lile gari,
tena yeye akiwa dereva. “Bella?” Bella alishindwa kujibu kabisa. “Mtoto yuko wapi?” “Nimempeleka
shule ya bweni, Arusha.” Bella
alijibu kwa hofu kidogo. “Ndivyo
alivyokuwa amekwambia mama yako hivyo?” Bella
alinyamaza kimya. “Hiyo gari
ni ya nani?” Bella alinyamaza. “Unaishi wapi na unaishi na nani?” Kimya. “Bella?” Kimya. Mat alibaki akimtizama Bella. “Ulisema kwa nini umenipigia simu?” Mat aliuliza kwa ukali kidogo. “Nilitaka kukusalimia tu, Kaka
Mat.” “Naona kweli kilichokuleta hapa ni salamu. Si tumeshamaliza kusalimiana?
Basi kwaheri.” Mat alitaka
kupanda kwenye gari yake ili aondoke. Bella
akamuwahi. “Naomba usiondoke kaka
Mat.” Bella alianza kulia. Mat alikuwa ni kijana mwenye maadili
na alijiheshimu sana.
“Naomba usiondoke kaka Mat. Nipo kwenye mazingira magumu
sana, ambayo siwezi kukwambia. Lakini huku kukuona tu, kunanifariji kaka yangu.
Naomba usiondoke. Angalau tukae kidogo. Wewe unanijua tokea mtoto, sijabadilika
kaka.” “Hukua hivyo Bella!” “Naelewa kaka. Nakuahidi nitakujibu maswali yako yote
siku nyingine, lakini sio leo. Naomba leo angalau nipate muda na wewe tu. Hata
kama hatutaongea kitu, lakini hujui ni kiasi gani nafarijika hivi ninavyokuona
tu. Tafadhali kaka Mat.” Mat akarudi.
“Umekula?” Mat akamuliza. “Sijala kaka.” Waliingia ndani, wakaagiza
chakula, wakaanza kula, kila mtu akiwa kimya. “Naomba nikwambie kitu kaka,
lakini usiniulize swali lolote, nitakujibu maswali yako yote wakati mwingine,
lakini sio leo.” Bella
alirudia tena, Mat alimtizama Bella kwa makini. Hali aliyokuwa nayo Bella na
gari aliyokuwa akiendesha, viliibua maswali mengi kwa Mat, lakini kwa kuwa
alimfahamu sana Bella tokea mtoto, kwa kumwangalia tu aliweza kujua kuna jambo
kubwa sana linaendelea ndani ya ule unadhifu na utajiri aliobeba kwa nje.
“Kwanza nataka kujua kama huwa unakwenda kumuona mtoto?”
“Ndiyo, huwa naenda. Na kesho pia nitakwenda kumtembelea. Lakini nataka ujue nafanya haya yote kwa ajili yake.” Bella alianza
kulia. “Nataka asome sana, na awe na maisha mazuri.” “Na wewe? Unajifikiria na wewe mwenyewe lakini? Usiwe kama
mama yako Bella. Mama yako amekufa akiwa anawahangaikia nyinyi. Umeshafikiria
maisha ya Eric bila wewe wala mama yenu?” “Niko
makini kaka.” “Sawa Bella. Naamini umejifunza
kutokana na mama yako. Na aliongea na wewe bila kukuficha. Naomba usije
ukasahu, ukarudia makosa. Shida tulizokuwa nazo wakati mnaishi na mimi pale
Kigogo niza muda tu. Rudini nyumbani, tutahangaika, maisha yataendelea kwa
kadiri Mungu atakavyojalia, lakini sitaki ujitoe kafara.” “Ulipata ile tenda uliyokuwa ukifuatilia siku ile
ulipotuacha kwa kina Zera?” “Sikupata. Waliniambia gari ni ya zamani sana. Kama
ingekuwa angalau ya 2014, ndio wangenikodisha. Kwa hiyo bado nahangaika. Lakini
hatutashindwa kuishi Bella, rudi nyumbani.” “Sitaki Eric aendelee kucheza mpira
tu mtaani, kaka. Lazima asome.” “Kwa nini tusimpeleke shule za kawaida? Rudi
nyumbani Bella. Unaonekana wazi huna furaha.” “Unakumbuka shule tulizokuwa
tukisoma wakati wa uhai wa mama? Elimu yake ni ya tofauti kabisa na elimu ya
hapa Tanzania, kaka. Itamuia ngumu kuelewa darasani. Mpaka aje awe sawa na
wenzake atakuwa ameshakuwa mtu mzima. Sipendi vile alivyokuwa anashinda pale
mtaani, atajiingiza kwenye makundi mabaya, itakuwa ngumu kumrudisha tena kwenye
mstari. Eric ana moyo mzuri sana, na sasa hivi ni msikivu. Akipoteza hiyo, ataharibikiwa
kabisa.” Mat akanyamaza.
“Natamani mambo yangekuwa kama zamani, Kaka Mat.” Bella akaanza kulia tena. Mat alimuonea sana huruma.
Alimfananisha Bella na mama yake. Tunu alikuwa hawezi kumuona mtu yeyote
akiteseka akaacha kusaidia. Alikubali yeye akose, ili mwingine apate, hata kama
itamgarimu vipi. Ikitokea upo kwenye shida, alisaidia bila kujali uadui wenu na
ndio maana alidumu sana na Mat. Alimpenda Mat, kama mdogo wake wakuzaliwa tumbo
moja. Hakumchukulia kama mfanyakazi wake.
“Ulitaka kuniambia nini?” Mat alimuuliza baada yakutulia. “Sasa
hivi nina pesa nyingi sana. Sina jinsi ya kumfikishia babu kule kijijini.
Naomba umpelekee kiasi, na wewe uchukue. Nimekuja na pesa nyingi sana, zipo
kwenye gari. Naomba uende kijijini ukamuone babu, mnunulie vyakula vingi.
Msaidie kuvipanga vizuri, visiharibike ili awe anapata chakula chakutosha kila
wakati na wewe naomba ubadili maisha yako.” “Mimi sihitaji msaada wako Bella.”
“Naelewa kaka. Lakini naomba ufanye hivyo kwa ajili yetu. Ili siku moja na sisi
tupate pakukimbilia.” Mat alibaki kimya.
Bella alingalia saa, kisha akasimama haraka kama mshale. “Lazima niondoke sasa hivi. Naomba
twende kwenye gari.” Mat
alisimama akiwa anafikiria sana huku akimfuata Bella kwa nyuma. Walipofika
kwenye gari, Bella alitoa mfuko uliokuwa umejaa pesa. Mat alishtuka sana. “Beba mkoba mzima, utaenda kuhesabu
hukohuko.” “Pesa zote hizi? Umezitoa wapi Bella?” “Nilikuomba leo usiniulize maswali
kaka yangu. Wewe chukua na uondoke. Halafu Kaka Mat, hii karatasi nimeandika
shule na jina kamili la Eric. Uwe unaenda kumtembelea. Nakuomba usiwahi
kunipigia simu, hata iweje, mimi ndio nitakuwa nakupigia.” Mat alibaki akimtizama Bella huku
haamini. Kwa kipindi hicho ambacho kila Mtanzania analia hali ngumu ya uchumi,
lakini Bella alikuwa na pesa ambazo alimpa bila kujali atazitumia vipi. Bella
aliingia ndani ya gari na kuondoka kwa haraka.
**************************************************
Alikuwa akiwahi nyumbani kwake, kwenda kuongea na Mzee
Masha, kwa kutumia kompyuta ya mezani kwake. Mzee Masha alikuwa akitumia njia
hiyo makusudi, ili kuhakikisha Bella yupo nyumbani. Na alipiga kila siku muda
ambao Bella alijua anakwenda kulala huko nchini Uholanzi alipo kwa familia
yake. Pesa alizompa Mat, alijua Mzee Masha hawezi kugundua, au kujali kwani
alikuwa akimuona akiingiza mle ndani mamilioni ya pesa mara kwa mara. Wakati
mwingine alikuwa akiingia nazo usiku kwenye mabegi, na wakati mwingine alitoka
na baadhi ya hizo pesa bila kumuona akihesabu. Ni yeye na Bella tu ndio walijua
zilipo hizo pesa alizokuwa akizifungia kwenye SAFE kubwa ya chumbani kwake,
nyuma ya chumba cha nguo. Ilikuwa ngumu kwa mtu yeyote kuiona hiyo SAFE kwa
haraka kama ukiingia chumbani humo, kwani ilifichwa nyuma ya suti zilizokuwa
zimening’inizwa za Masha. Ni yeye na Bella tu ndio walijua kama kuna Safe humo
ndani na jinsi ya kuifungua. Alimruhusu Bella kutumia atakavyo.
**************************************************
Wakati anaingia ndani, alisikia simu ya Mzee Masha ilikuwa
ikiita kwenye kompyuta. Bella alitamani kulia kwani alikuwa amechelewa kama kwa
dakika mbili tu. Alikimbia, lakini alipoikaribia kompyuta ili apokee ile
simu kwa njia ya skype ilikata. Bella alikaa chini nakuanza kulia. Alijua wazi
adhabu inayofuata kwa kutopokea simu yake. Baada ya muda mfupi kupita, zilianza
kuingia kwenye simu yake picha zake akiwa na Mat na zote zilitoka kwa Mzee
Masha. Bella aliitupa ile simu kwa hofu kubwa sana na kuanza kufikiria.
Japokuwa alishapigwa marufuku kumpigia simu Mzee Masha
akiwa na mkewe, Bella aliisogelea ile kompyuta na kumpigia simu Mzee Masha.
Iliita bila kupokelewa. Alipiga tena na tena mpaka alipopokea. “Muonyeshe Zera
hizo picha, anamfahamu huyo kaka, anaitwa Mat alikuwa dereva wetu. Ndiye
aliyekuwa akitutunza mimi na Eric, wakati tukiishi Kigogo. Unanisikia Masha?
Usije kumdhuru hata kidogo. Amekuwa kama ndugu sasa hivi, na ndiye mtu pekee
tuliyebaki naye maishani. Umenisikia?” Kwa mara ya
kwanza Bella aliweza kuongea na Mzee Masha kwa hasira na kumfanya ashtuke
kidogo na kubaki bubu kwa muda. “Ukimdhuru tu au ukimfanyia kitu chochote, utakuta
maiti humu ndani. Nakuapia kwa Mungu, Masha. Hutanikuta, nitajiua.” Bella alishajua udhaifu wa Mzee Masha, kuwa ni yeye. Alijua
wazi hawezi kuishi tena bila yeye. Kuna vitu alivyokuwa akimfanyia, ambavyo
Mzee Masha alikiri ni Bella pekee ndiye anayeweza kumfurahisha kwa kiasi hicho.
Upendo wake kwa Bella ulizidi, japo wivu ndio ulizidi kipimo, nakumfanya awe
mbabe kwake.
Bella alikuwa anatetemeka sana. “Umenisikia?
Usikate simu bila kunijibu na nataka uniahidi hutamfutailia Kaka Mat. Na
nimempa pesa za kumpelekea babu kijijini, kwa kuwa nilijua hutaniruhusu niende
mimi mwenyewe.” Bella aliendelea kuongea
bila kujibiwa. “Sema kitu chochote T. Please. Usipojibu kitu,
ninakata hii simu, na hutakaa ukasikia sauti yangu tena.” Mzee Masha alishamkataza Bella kumwita Mzee Masha,
alitamani sana awe anamwita jina lake Tito. Sasa kusikia anaitwa T, ilimtuliza
zaidi. “Narudi kesho, tutaongea vizuri.” “Hapana, huwezi
kurudi kesho. Kesho naenda Arusha kwa Eric.” “Nisubiri twende wote.” “Haitakaa
ikatokea Eric akatuona mimi na wewe tuko pamoja, hata iweje. Umenielewa?” Mzee Masha alizidi kushangaa ujasiri wa Bella, wa siku
hiyo. “Kwa nini?” Mzee Masha aliuliza. “Kwa nini unataka kumuona Ric?” Bella aliuliza kwa ukali kidogo, nakumfanya Masha anyamaze.
“Wewe shida yako ni mimi. Nimekubali kukufanyia
kila kitu unachotaka, kaa mbali kabisa na Eric. Tena wala nisikusikie hata
umemtembelea shuleni wala kumsogelea. Wewe sio baba yake na wala huna maadili
mazuri yakumfundisha Eric kitu chochote kile. Eric ni jukumu langu mimi. Kesho
nakwenda kumuona, na kesho kutwa nitakuwa hapa nyumbani. Mtume dereva aje
anichukue anipeleke uwanja wa ndege, nataka tiketi ya asubuhi.” Bella alikata simu
nakuanza kuhema kwa nguvu. Hata yeye hakuamini kama ameweza kuongea na Mzee
Masha nakuweza kumudu kumbadili mawazo.
Haraka sana aliokota simu yake iliyokuwa vipande vipande
pale sakafuni, akaiunganisha na kumpigia simu Mat. “Kaka Mat? Kaka Mat?” Bella aliita kwa wasiwasi kwani simu ilipokelewa lakini
hakuna aliyeongea. Mwishowe alisikia sauti ya mtu mwingine lakini sio Mat. “Mpe simu Mat
haraka sana.” Bella aliongea kwa ukali. “Kuna nini Bella? Nini kinaendelea na hawa vijana
ni kina nani?” “Wamekuumiza?” “Hapana. Lakini wamenitoa kwenye
gari na kunipokonya kila kitu. Ngoja kwanza.” Mat alinyamaza kwa muda. “Kaka Mat!” Bella aliendelea kuita kwa wasiwasi. “Nipo nipo.
Subiri kidogo Bella.” Baada ya
muda, Mat akaita. “Bella?” “Nipo kaka.” “Wamenirudishia kila kitu
changu na kuniomba msamaha. Ni kina nani hawa?” “Samahani kaka, na pole. Hawatakusumbua
tena. Rudi tu nyumbani. Usisahu maongezi yetu.” Bella alikata simu nakuanza kulia sana. Alilia siku nzima
akiwaza juu ya maisha yake yalivyogeuka kuwa yakitumwa. Alijuta na kulaani siku
aliyopata wazo la kwenda kuomba msaada nyumbani kwa kina Zera. Hakujua kama
analindwa kwa kufuatiliwa kwa kiasi kile. Alijua ndio amepoteza uhuru wake
kabisa. Hana tena maisha yake binafsi, na kila atakayemsogelea yeye atakuwa
hatarini. Alilia asijue chakufanya.
**************************************************
Asubuhi alikuja kuchukuliwa kupelekwa uwanja wa ndege wa
Mwalimu Nyerere tayari kwa safari yake ya Arusha. Alitua uwanja wa ndege wa
KIA, bado ilikuwa mapema tu. Akatoka nje ya uwanja huo akiwa na lengo la
kutafuta usafiri wa kumpeleka jijini Arusha, lakini akakuta mtu amebeba bango
lenye jina lake hapo nje akimsubiria. Alimsogelea. “Mimi ndio Enabella.” Bella alijitambulisha,
wakasalimiana kwa kifupi sana, yule mtu akionyesha heshima kubwa sana kwa
Bella. “Nimeagizwa nikufuate.
Una mizigo yeyote?” “Hapana.” Hakutaka
kuuliza maswali mengi, alijua tu ni mmoja wa watu wa Mzee Masha. Akapanda
kwenye gari mpaka jijini Arusha, shuleni kwa Eric.
Eric alifurahi sana kumuona dada yake. Alimkumbatia kwa muda mrefu sana. Ilikuwa kama mtu anaosha moyo wa Bella, moyo wake ulifunguka, furaha ya ajabu sana ikaingia nafsini mwake. Kwa muda mrefu wa matatizo, Bella alijikuta akicheka baada yakumuona Eric.
“Unazidi kuwa mrefu na kunenepa. Unasoma kweli?” Bella alianza kumuuliza mdogo wake. “Shule ni nzuri sana Bella. Nimeipenda.
Kwani utanihamisha tena?” Bella
alifurahi sana kuona mdogo wake anafurahia hiyo shule, kwani yeye alijawa na
hukumu moyoni. Aliona ni kama amemtelekeza mdogo wake, kitu alichokuwa ameonywa
na mama yake. Lakini alishindwa kumuhamishia Dar, hakutaka mdogo wake ajue
maisha anayoishi na Mzee Masha. “Unauhakika
unataka kubaki hapa?” “Lakini kama ni gharama sana, nitaenda popote kule.”
“Usiwe na wasiwasi na pesa, Ric. Ninachotaka ni wewe uwe na furaha.” Eric alianza kucheka.
“Ninafuraha sana Bella. Ujue nini?” Bella alicheka na yeye, alimuona vile Eric alivyojawa na
furaha, akajua mateso yake sio bure. “Nini?”
“Nimechaguliwa kwenye timu ya mpira wa kikapu, {basketball} wamesema mimi ni
mrefu sana na ninaujulia huo mchezo. Halafu kocha wa mpira wa miguu pia amesema
niingie kwenye timu yake.” “Sasa unaenda kwenye timu ipi?” “Ndio nataka
nikwambie wewe kwanza, unisaidie kuchagua. Maana vyote natakiwa kulipia. Lakini
kama huna hela naweza kusubiri tu, hamna haraka.” “Kwa nini usicheze michezo
yote, halafu baadaye ndipo ukafanya maamuzi?” “Kweli Bella? Utanilipia!?”
“Lakini uniahidi utasoma Ric. Kumbuka mama alivyosema tusome sana.” “Na wewe
umeanza shule?” Bella
alipooza kidogo. “Nitaanza tu Ric.” Bella akapotelea kwenye mawazo. Akakumbuka
kwa wakati ule anaishi kama mke wa Masha, sio kama mtoto anayefikiriwa swala la
shule. Akazidi kujihurumia.
“Umependeza sana Bella.” Eric alijaribu kumtoa dada yake kwenye mawazo. Bella akacheka
kinyonge. “Asante Ric. Lakini
nimefurahi sana kukuona.” Walikaa
siku nzima wakicheka, angalau Bella alisahau maisha yanayomsubiri jijini Dar.
**************************************************
Usiku ulipoingia, aliamua kurudi hotelini kupumzika. Usiku
kucha wakati yupo hotelini hapo, Bella alikuwa akijiambia jinsi ya kuyabadili
maisha yake na kujaribu kumpokea Mzee Masha moyoni mwake, ili aendelee
kumnufaisha mdogo wake. Bella alikuwa mtoto mdogo sana, ndio alikuwa ameingiza
miaka 18 tu. Alibaki akilia na kutamani kama mama yake angekuwa hai abaki kuwa
mtoto sio kama sasa hivi anaishi kama mke wa Mzee Masha. Alijihesabia miaka
yake, nakujilinganisha na Zera, ambaye ni mtoto wa Mzee Masha, ambaye kwa
wakati huo alikuwa shuleni. Eric alimuuliza swali lililomfanya ajiulize na yeye
zaidi. ‘Mzee Masha
ataniruhusu kutoka pale ndani kila siku na kwenda shule? Nina zungukwa na
walinzi wake kila mahali! Ukute hata hapa hotelini yuko mtu ananilinda. Sina raha hata kidogo! Alinisamehe
kukutana na Kaka Mat, nafikiri sababu ya kumwita T. Labda nibadilike, nimuonyeshe
nampenda, labda ataacha ukatili. Lakini
anafanya kazi gani? Mbona anapesa nyingi sana?’ Bella aliendelea kupanga mikakati ya
maisha yake, mpaka alipopitiwa na usingizi.
Asubuhi alipoamka na kujitayarisha, akatoka mle chumbani na
kushuka chini mpaka mapokezi. Akakuta yule dereva akimsubiria. Alimuomba amrudishe
tena shuleni kwa kina Eric, kama alivyomuahidi. Alilipia kila kitu kilichokuwa
kikitakiwa, muda wa ndege yake kuondoka Arusha ulipofika, ilimbidi Bella amuage
mdogo wake ili asichelewe ndege. Alitamani kulia, lakini aliapa kutomuonyesha
mdogo wake hisia zake za ndani. Aliamua kufa ndani kwa ndani.
**************************************************
Akiwa kwenye ndege Bella aliendelea kuwaza huku machozi
yakimtoka. ‘Narudi tena jela.’ Mama aliyekuwa amekaa pembeni yake, alijaribu kumuuliza
kama yupo sawa, lakini kama kawaida ya Bella ya kuongea pale anapoamua yeye,
alinyamaza bila yakumjibu yule mama. Ni Mzee Masha tu ndiye ilimlazimu kumjibu.
Bella aligeukia dirishani na kuendelea kuwaza. ‘Lazima nibadili maisha yangu.
Lazima niyakubali hivi yalivyo sasa, ili niweze kuishi na Mzee Masha vizuri.
Hakuna dalili ya kutoka kwenye maisha ya yule mzee, sio leo wala kesho.
Ameniapia kifo pekee ndicho kitatutenganisha. Lazima nifanye maisha yangu yawe
rahisi mle ndani.’ Bella
aliendelea kupanga mipango yake huku akitokwa na machozi. Yule mama alishindwa
kukwepesha macho yake, kwani uzuri wa Bella aliokuwa nao, na vitu vya thamani
alivyokuwa amevaa, na harufu nzuri aliyokuwa akinukia, ilikuwa ngumu kujua kama
ni mtoto wa milionea, au ana mwanaume mwenye pesa nyingi. Na kwa kuwa alikuwa
akitokea Arusha, alijua lazima ni mmiliki wa mgodi ndiye anayemmiliki binti
huyo. ‘Kitakuwa kinatembea na waume za watu hiki kitoto!’ Yule mama alijisemea moyoni.
**************************************************
Alifika uwanja wa ndege wa Dar, akakuta dereva akimsubiri.
Aliendelea kushangaa jinsi Masha ambavyo anamuhangaikia bila hata kumuomba.
Alimwandalia kila kitu. Kuanzia usafiri wa kumtoa sehemu moja kwenda kwingine
mpaka hoteli aliyofikia jijini Arusha. Dereva huyo alimpeleka hotelini bila
hata Bella kujua kama alishaandaliwa sehemu ya kulala jijini hapo.
Waliondoka pale kwenye viwanja vya ndege vya Mwalimu Nyerere, giza ndio lilikuwa likiingia, na kwa sababu ya foleni njiani, alifika nyumbani kwake usiku. Alimkuta Mzee Masha akimsubiri sebleni. Alishtuka kidogo. “Pole na safari.” Bella alisalimia kwa hofu asijue nini kitafuata. “Asante na wewe pole na safari. Eric anaendeleaje?” “Asante. Anaendelea vizuri tu." Bella alitulia kidogo kama anayesubiria aone kinachofuata. Masha alikuwa ametulia kwenye kochi, akazima tv, na kufunga gazeti alilokuwa anasoma, akaweka pembeni. "Asante kwa maandalizi ya safari. Sijasumbuka hata kidogo!” Bella aliongeza. "Afadhali na karibu." Masha alijibu na kubaki akimtizama Bella. “Umeshaoga?” Bella alimchokoza kama kumpooza. Alishajua udhaifu wake, akaamua kuutumia ipasavyo. Mzee Masha alicheka kidogo. “Nakusubiri wewe.” “Twende basi.” Bella aliongea kwa upole, na kumfanya Mzee Masha aliwazike. Aliweka pochi yake juu ya meza, akaanza kufungua zipi yake pembeni ya ubavu wa gauni hilo alilokuwa amevaa huku akimtizama Masha, akaelekea chumbani. Masha naye akasimama kumfuata na tabasamu usoni. Alishangazwa na ushirikiano wa mara ya kwanza alioupata kutoka kwa Bella.
“Umekuwa na wakati mzuri huko?” Bella
alihoji taratibu. “Akili yote
ilikuwa huku.” Bella alicheka
kidogo. “Nimekuudhi?” Bella aliuliza huku amemuegemea
kwa karibu sana. “Sio
sana. Lakini ningependa uwe unanitaarifu mambo mapema, Bella. Unanichanganya
kweli! Nimeshindwa hata kuendelea kukaa huko.” “Pole. Nilijua nikikwambia mapema
ungeweza kunikatalia. Wakati yule kaka alitusaidia sana. Usiwe na wasiwasi T,
bwana. Siwezi kukuzunguka.” “Kweli Bella? Au unanidanganya tu?” “Nakwenda wapi?
Wakati kila kitu unanipa?” Kichwa
kilikuwa kinakaribia kupasuka, kwa sifa. Furaha iliyomuingia iliondoa hasira
zote. “Haya bwana.” “Kwanza
nimefurahi umerudi mapema, nilikuwa nimepooza!” Bella aliamua kuendelea kumdanganya.
“Sijakuletea zawadi lakini. Nimeondoka nikiwa na haraka
haraka sana.” Bella akacheka kidogo. “Unanicheka?”
“Wivu utakuuwa Tito. Sasa ulifikiria nini?” “Hawakawii watoto wa mjini
kunipora. Na uzuri wote huo!” Bella
alimbusu mgongoni alipokuwa akimsugua wakiwa wamekaa kwenye jakuzi lenye maji
vuguvugu. “Hamna wakukupora
bwana. Twende ukanipe zawadi yangu.” “Nimekwambia sijakuletea kitu chochote,
Bella.” “Wewe ndio zawadi yangu bwana.” Mzee
Masha alihisi yupo ndotoni, kwani wakati wote ilimbidi kutumia nguvu kulala na
Bella, lakini usiku huo, Bella ndiye aliyekuwa akimtaka kimapenzi! Hakuamini.
Alimgeukia Bella, akambusu na kutoka naye bafuni, kurudi naye chumbani.
**************************************************
Ukweli Bella aliamua kubadilika, na akaziteka fikra za Mzee
Masha kupita kiasi. Alimfanya ajione kama kijana kabisa. Alimwita majina ya
mapenzi tena kwa utaratibu. Bella alikataa kabisa kutoka mle ndani bila Mzee
Masha. Alimfanyia utundu mwingi sana wakitoto, uliozidi kumchanganya. Taratibu
alianza kujisahau kama ameoa na alikuwa ni mtu wakuheshimiwa sana kwenye jamii.
Alirudia tabia za ujanani, angalau kujifananisha na Bella. Bila hofu au haya
alianza kutoka na Bella sehemu mbalimbali za starehe. “Huwezi kuendelea kujifungia humu
ndani Bella. Unakuwa kama mama mzee!” Bella
alicheka, lakini moyoni alijua wazi kabisa, salama yake ni kuwa mle ndani,
kwani akijichanganya tu, akatoka, ataibua matatizo kati yao, kwani alimjua
jinsi Mzee Masha alivyo na wivu na katili. “Wewe
hufurahii hivi unavyonikuta nakusubiri nyumbani?” “Nafurahi, lakini sitaki ukaja kuyachoka
haya maisha.” “Siwezi T. Labda unikimbie.” “Naenda wapi Bella?” “Ukipata
dogodogo mwingine?” “Wewe umeshakutana na mwingine kama wewe?” Bella alicheka sana. “Haya bwana. Lakini kama nikutoka
lazima tutoke wote, sitaki kutoka peke yangu.” Mzee Masha aliona kama amekabidhiwa
dunia. Akaanza kuwahi sana kurudi nyumbani kukaa na Bella.
Safari za Uholanzi kwa familia yake zikaanza kupungua, huku
akimkataza mkewe asirudi Tanzania kwa kisingizio kuwa yeye anakuwa safarini.
Aliona shida sana kumtaja mkewe kwa Bella, na Bella naye kama alivyofundishwa
na yule mama, mwalimu wake, hakutaka kwenda kinyume naye. Alimwambia iwe mwiko,
kumtajia mkewe, na wala asionyeshe wivu. Tena anapomtajia mkewe, aonyeshe
kumuheshimu sana, akamwambia ndio njia pekee ya Mzee Masha kuwa upande wake
yeye. Alimfundisha mapishi mengi mazuri ya kiswahili, na huo ujuzi wa mke,
uliokuwa ukimchanganya Mzee Masha.
Waliongozana kama kumbikumbi, vicheko na amani vilitawala
kati yao. Mzee Masha akageuka kuwa mwema kupita kiasi. Akaanza kumshirikisha
Bella baadhi ya mambo yake. Alipotoka kwenda kazini, Bella hakuacha kumwandikia
kiujumbe kidogo, na kukiweka kwenye shati lake, huku akimwambie akasome
akishafika kazini kwake. Alimwambia ni jinsi gani alivyo wa thamani na hakuacha
kumshukuru kwa kumtunza yeye na mdogo wake. Alimwandikia jinsi anavyomsubiri
arudi nyumbani, ili wafanye hili au lile, ilimradi tu, kumchanganya Mzee Masha.
Akaanza kwenda naye Arusha kumtembelea mdogo wake, lakini yeye alimuacha
hotelini. Kwa kuwa alisafiri naye, safari za Arusha zilianza kuwa kila mwisho
wa juma. Walisafiri wawili hao, walilala siku ya kwanza hotelini bila kutoka,
kisha siku inayofuata Bella alikuwa akienda shuleni kwa mdogo wake, nakurudi
jioni hotelini alipokuwa akimuacha Masha. Mzee Masha alikuwa akiona
anathaminiwa sana na Bella. Penzi lake kwa Bella lilizidi kukua.
**************************************************
Siku zilizidi kwenda, Masha akiendelea na kazi zake nyingi,
huku Bella akibakia nyumbani akimsubiria. Alitamani sana kurudi shule japo
aliogopa kumwambia Mzee Masha. Kwani alishamuonyesha Bella hakuna sababu
yakurudi tena shule, yeye ameshampa kila kitu na alishamfungulia hata dola
akaunti. Ni kweli Bella alikuwa na pesa nyingi sana, lakini bado alitamani sana
kurudi shuleni. Kila alipotaja swala la yeye kusoma, alimuona jinsi Mzee Masha
anavyobadilika gafla. “Walimu
watakuchezea tu Bella. Kwanza unataka kusoma ili iweje? Una kila kitu. Unayo
pesa yakukutosha benki, nyumba nzuri unayo, gari ya kifahari unayo, sema hutaki
tu kuiendesha mwenyewe.” “Nataka tuwe tunakuwa wote T. Haya mambo ya kuendesha
kila mtu gari yake, ndio chanzo cha kuanza kupishana mlangoni.” “Kweli Bella
umetulia. Nakushukuru mpenzi wangu.” Bella alitoa tabasamu.
Aliendelea kuwaza jinsi ya kumfanya Masha amkubalie arudi
shule, bila mafanikio. Mwishowe akapata wazo. Lakini alimuona vile alivyo na
kazi nyingi, akirudi amechoka, akaamua amtoe pale jijini ili akajaribu kutupia
ndoano nyingine, sehemu tulivu. Alimsubiri siku hiyo baada ya kutoka kazini,
akiwa amepumzika, akajisogeza mpaka alipokuwa amening’iniza miguu yake kwenye
stuli, akainyanyua, akakaa na kuipakata miguu ya Masha, na kuanza kuiminyaminya
taratibu. Alipitisha vidole vyake
taratibu kwenye miguu na nyayo zake. Akamuona kabisa amelemewa, hata gazeti
alilokuwa akisoma alishindwa kulisoma zaidi. Akabaki akisikilizia mikono laini
ya Bella ikipita miguuni mwake.
“T!” Bella
alimwita taratibu. “Naona
tumekaa sana nyumbani. Halafu umekuwa nashuguli nyingi kweli! Ukirudi unakuwa
umechoka tunakosa muda wa pamoja mpenzi wangu. Nakuwa nahamu na wewe, lakini
nakuhurumia. Naomba twende tukajifungie mahali. Mimi na wewe tu. Tena unazima
na simu yako kabisaa.” Mzee
Masha alifurahi sana. “Chagua
basi wapi unataka twende Bella.” “Tutafute
sehemu ambayo na wewe hujawahi kufika. Tukajifungie huko, hamna hata kutoka nje
mpaka niridhike.” “Utaniua
Bella wewe! Ujue mwenzako Mzee?” Wote
wakacheka. “Usijizeeshe bwana.
Bado unadai kabisa.” Kwa
kuchanganyikiwa na mapenzi, Mzee Masha alikuwa akiamini kila anachodanganywa na
Bella, na kusahau kabisa kuwa Bella ana umri sawa kabisa na binti yake wa
mwisho.
Akapiga magoti katikati ya miguu yake pale alipokuwa amekaa
kwenye kochi. Bella akapitisha mikono yake yote miwili kuzunguka kiunoni kwa
Masha. Akampandisha t-sheti yake, midomo
ikatua kwenye kitomvu cha Masha. Akambusu na kuendelea kuchezea vinyweleo vilivyozunguka
kitomvi cha Masha, kwa ulimi wake. Masha alianza kuhangaika pale kochini huku
mikono ya Bella ikiendelea kutembea mgongoni na kifuani kwa Masha. Akaendelea kumpapasa
taratibu huku ulimi wake ukiendelea kumchezea. Hakuacha kumbusu na kuendelea kutumia
ulimi wake kupita kule alipoweza kufika. Akaendelea kumchezea mpaka alipoona
hali yake inazidi kuwa mbaya, akamtoa suruali. Aliishusha tu mpaka chini ya
magoti, na yeye akatoa tu chupi yake na kumkalia pale pale kwenye kochi bila
kuvua gauni alilokuwa amevaa. Kwa kuwa alishamchezea kwa muda mrefu, Bella
hakusumbuka sana. Masha alikuwa ameshikilia makalio yake kwa nguvu na kwa uchu
wote, akigugumia. Alishakuwa amefika juu sana. Bella alipanda juu na kushuka
taratibu, baada ya muda mfupi sana akaona Masha amemaliza. Akataka kunyanyuka
pale. “Naomba usishuke Bella. Baki hivyo
hivyo, ila unikumbatie.” “Okay.” Bella akaweka kichwa chake vizuri kifuani
kwake, wakatulia pale kwenye kochi huku amemkumbatia vizuri na kwa upendo.
Masha akaendelea kutafuta pumzi kifuani kwa Bella.
Japokuwa ni kweli aliwahi kuzaa, lakini bado Mzee Masha
kama wengi walivyozoea kumwita sababu ya pesa zake, alikuwa mkubwa kwa Bella.
Masha alikuwa na miaka 48 na Bella 18. Mtoto wa kwanza wa Masha alikuwa na
miaka 20, wakati Zera alikuwa na umri unaolingana na Bella, miaka 18. “Asante.” Alimsikia Masha akimshukuru. “Umeridhika?” Bella alirusha swali na
busu la kichwani akiwa amepakatwa vile vile. Masha akamtizama. “Nimefurahia. Nashukuru.” “Naona umechoka T,
twende ukalale.” Bella alimpa mabusu kadhaa, akamkumbatia tena na tena huku
akimpapasa kichwani, kisha akashuka. “Natamani
tulale hapa hapa.” Bella akacheka. “Ndio
maana nakwambia tunahitaji muda wetu. Mbali na kazi na kelele za huu mji.”
Masha akavuta pumzi kwa nguvu. “Unanifanya
nitamani tuondoke hata kesho.” Bella akacheka. Wakahamia chumbani.
“Bella akanyaga visiwa vya Caribbean, kwa
mapumziko.”
Kwa kuwa ulikuwa msimu wa joto nchini Marekani, Mzee Masha
alitafuta sehemu nzuri sana ya kwenda kupumzika, kama Bella alivyoomba.
Walikwenda kwenye visiwa vya Caribbean. Wakati wengine wakilia njaa, Bella
aliponda raha kana kwamba anaishi nchi nyingine siyo Tanzania. Walitua visiwani
humo ikiwa ndio mara yao ya kwanza kufika visiwani hapo. Japokuwa Bella hakuwa
akifurahia chochote kinachoendelea kati yao, hususani mapenzi, lakini
alifurahia sana utulivu wa visiwani hapo. Walikuwa na wakati mzuri sana.
Masha alianza mapenzi ya kumbembeleza Bella na ustarabu
ukaongezeka. Ukali akaacha kabisa, akawa mtulivu. Na kweli walijifungia bila
kutoka kwa siku mbili mfulilizo. Bella akimtumikia Masha ipasavyo bila kuchoka,
huku Bella akionyesha yeye ndio anafaidi zaidi yake. Alikuwa akitoa milio ya
kimahaba kila wafanyapo mapenzi. Alikuwa akimng’ang’ania akimuomba penzi tena
na tena. Mida mingine anapokuwa amelala aliamshwa na mabusu ya Bella mwilini
mwake. Mara amkute chini au juu akicheza na mwili wake kitu kilichokuwa
kikimfurahisha sana Masha. Alifanikiwa kumwaminisha Masha kuwa wakati wote
alipokuwa akimgusa, aliridhika, kumbe ulikuwa ni uongo kabisa. Bella alijivunia
nakumshukuru sana kwa kila anachomfanyia hapo kitandani. Alimpamba kwa sifa, uthamani
wake ukaongezeka. Akajiona mwanaume kwelikweli.
“Sasa hapa si itakuwa imekugharimu sana?” Bella alijaribu kuhoji siku hiyo ya tatu, ilikuwa jioni walipokuwa ufukweni wakitembea kwa mara ya kwanza tokea wafike visiwani hapo. Kwani kwa siku mbili walibaki chumbani tu. Bella akisema anahitaji sana ule muda wa mapumziko kwani alimlalamikia Masha kuwa alikuwa na shuguli nyingi sana huko nyumbani hakuwa akipata muda naye. Na ni kweli hata Masha alionekana akihitaji hayo mapumziko. Alikuwa akila na kupata muda wakutosha wakulala vizuri, kwa kuwa hakuwa akiwaza kazi, na Bella mrembo wake akiwa pembeni yake. Siku hizo mbili ilikuwa mapenzi, kula na kulala tu. Aliamshwa na mabusu, alilala kwa mabusu ya Bella. Mungu ampe nini Masha!
Ilikuwa rahisi kwao kutembea pamoja, au hata Bella kumbusu Masha na kuonyesha mapenzi yao waziwazi, hadharani bila shida katika maeneo hayo, kwani hakuna aliyemjali mwenzake. Kila waliyekutana naye huko, alikuwa akiangalia mambo yake. Kwa hiyo hata Mzee Masha hakusita kutembea akiwa amemshika Bella kiuno, akijivunia mapenzi ya mtoto huyo.
“Unastahili Bella. Hakuna gharama inayoweza kufikia mapenzi
unayonipa. Unanipenda, unanitii, na kuniridhisha kwa kila hali. Unastahili
Bella wangu.” Bella aliona
jinsi Mzee Masha alivyokolea, akaamua kutoa ombi lake, kabla hajabadilika. “Asante T. Lakini unajua nini?”
“Nini?” Mzee Masha alimgeukia
Bella kutaka kujua anachotaka. Bella alisita kidogo. “Niambie tu Bella. Usiogope.” Bella alitabasamu na kumbusu kwa muda
kisha akajisogeza karibu na mabega yake. “Natamani
nikianza shule, wewe ndio uwe unanipeleka na kuja kunichukua.” Kidogo Mzee Masha alitulia, Bella
akaogopa kwani alijua wazi ni kiasi gani asivyopenda aende shule kwa kuhofia
atamsaliti pindi atakapokutana na vijana wengine.
“Au hutaki watu watuone tupo pamoja?” Bella aliendelea ili kuzidi kumpoteza. “Hapana Bella. Mimi nilidhani
unahofia kuonekana na mimi?” “Jamani T! Kwa nini?” “Huwezi jua bwana! Unaweza
ukakutana na vijana wenzako ukaniona sifai tena.” “Umeanza wivu T. Nitakuwa
natafuta nini tena?” “Sijui.” “Siwezi T. Nimeshakwambia zaidi ya mara kumi,
nimeridhika na wewe. Usiwe na wasiwasi. Umesikia?” “Nakusikiliza.” “Wewe mwenyewe
uliniambia kifo ndicho kitatutenganisha, au umesahau?” “Natamani na wewe ungesema hivyohivyo
Bella. Angalau nikusikie hata mara moja tu ukiniambia unanipenda.” “Mimi ni
mzuri wa vitendo T. Unanijua sio muongeaji sana. Sasa heri ni lipi?
Niongee sana halafu nihangaike na wanaume wengine huko nje au nikuonyeshe
vitendo vyangu kuwa nimetulia na kuridhika na wewe?” “Heri kutulia. Siwezi
kuvumilia na sitakaa nikusamehe hata siku moja nikisikia umenisaliti Bella.
Nitamuua huyo mwanaume.” Bella
alishtuka sana. “T!?”
“Nakuapia kwa Mungu. Hiyo ndiyo itakuwa adhabu pekee itakayomstahili mwanaume
atakaye kutoa kwangu. Sitasamehe Bella. Wewe ni wangu.” Bella alitamani kukaa chini.
Alipooza gafla, uongo wote ukamwisha.
Ukweli hakuwa na hisia zozote zile za kimapenzi kwa Mzee
Masha. Moyo wake ulijaa machungu yakupitiliza. Kila alipokuwa akimshika, alijikaza
sana ili kuweza kuishi na kuendelea kumsomesha mdogo wake aliyekuwa akilipiwa
mamilioni ya pesa. Hata milango ya kutoka kwa Mzee Masha ilishafungwa, alimuwahidi
kifo pekee ndicho kitakachomtoa kwake. Hakuwa na jinsi isipokuwa kukubaliana na
hali halisi.
“Unataka kuanza shule lini?” Mzee
Masha alimua kuvunja ukimya wakati wanalala, kwani ni kweli Bella alipooza
sana. Tokea wapo baharini, alipomwambia vile, Bella hakuongea tena, wakarudi
chumbani wote wakiwa kimya, na Mzee Masha alionyesha hakuwa akitania,
alimaanisha kila kitu alichomwapia Bella. “Wakati
wowote utakao ona unafaa.” “Mbona tena umebadilika?” “Unanitishia sana, T.
Nimejaribu kukuonyesha kuwa nimetulia, lakini bado huniamini.” “Sikuogopeshi
Bella. Nakwambia ukweli ili ujue na ujihadhari. Sitakubali kukuona na mwanaume
mwingine hata iweje. Umenisikia Bella?” “Ndiyo.” “Kwa hiyo hata kama ulikuwa na
wazo hilo, tafadhali Bella, nakuomba ulifute kabisa. Sitataka kukudhuru, kwa
kuwa itabidi na mimi nijidhuru. Nitapoteza kila kitu hapa duniani, lakini sio
wewe. Unaelewa?” Mzee
Masha hakuwa akitania kabisa. Kila alipokuwa akizungumzia hilo, alihakikisha
Bella anaelewa.
“Unamaanisha utaniua?” Bella aliuliza kwa taratibu huku akimuangalia Mzee Masha
usoni kwa mshangao kidogo. “Tutakufa
wote, Bella. Sitakaa nikakushiriki wewe na mwanaume mwingine yeyote, labda
nisiwepo hapa duniani. Ni heri kufa kuliko kukupoteza au kukuchangia na kiumbe
mwingine yeyote yule. Wewe ni wangu mimi.” Mzee
Masha hakukwepesha macho hata kidogo. Alimaanisha alichokuwa akisema. Bella
aligeuka upande mwingine, akalala.
Bella aanza Chuo.
Kwa kuwa alifaulu vizuri kidato cha nne, Bella alianza chuo
katika ngazi ya ‘diploma’ ya mambo ya ‘Information technology’{IT},
chini ya ulinzi mkali sana. Kwa kuwa alijua anachunguzwa sana, alijitahidi
kukwepa si marafiki wa kiume tu, bali hata wakike huko darasani kwao. Hakuwa na
rafiki yeyote yule pale chuoni. Watu walikuwa wakimuonea wivu sana, kwa vitu
vya thamani alivyokuwa akimiliki. Uzuri wake ulivutia kila mtu, na kutaka kuwa
karibu naye, lakini alijitahidi kuwakwepa kwa kadiri ya uwezo wake. Hata salamu
hakuwa akitoa kwa mtu yeyote yule ili kusijengeke mazoea. Alijitahidi kuwahi
kuingia darasani na mara kipindi kilipoisha, alitoka bila kukaa humo darasani
hata zaidi ya dakika moja. Kila alipofika darasani alikaa kwenye kiti chake na
kufungua laptop yake na kuendelea na shuguli zake kimya kimya. Hata mtu
alipomsalimia, hakujibu.
Hata hivyo alishaona marafiki hawana maana yeyote ile.
Alikumbuka maneno machafu kutoka kwa rafiki ya mama yake, alivyokuwa akimsema
marehemu mama yake, wakati hata hajazikwa! Yaani maiti ikiwa bado ndani. Bella
alichukia sana wanawake. Hakutaka ukaribu nao kabisa. Kwa upande wa wanaume
asinge thubutu hata kuwatazama machoni, kwa kuhofia asije kumsababishia yeyote matatizo.
Alijua endapo Mzee Masha, hata akihisi kuwa ana mwanamme tu, atamuua. Kwa hiyo
hakutaka kuingiza mtu yeyote matatizoni. Alijitenga na kila mtu. Alisikia
wanafunzi wenzake wakimsema kuwa anaringa sana, lakini Bella hakutaka
kujihusisha nao hata kidogo. Alibaki kujichunga na mara nyingi sana Mzee Masha
ndiye aliyekuwa dereva wake, ili tu kuepusha shari.
Waliendelea kuongozana kama kumbikumbi. Bella hakuonekana
maktaba wala kwenye makundi yakujisomea. Alimpa Masha ratiba yake yote ya
vipindi vya darasani. Kwa hiyo kila kipindi kilipoisha, alimkuta Masha
anamsubiria nje. Kwa kuwa alikuwa na msingi mzuri sana wa elimu, na yeye na
mdogo wake wote walikuwa watundu sana wa kompyuta, kwani mama yao aliwanunulia
kila mtu kompyuta yake tokea zamani, walishinda nyumbani kwao wakishindana
kutumia kompyuta, yeye na mdogo wake. Kwa hiyo hata alipokuwa shuleni alikuwa
na uwezo mkubwa sana wakuelewa mambo. Alikuwa akijisomea yeye mwenyewe na
alifaulu vizuri sana. Amani ilikuwepo na Mzee Masha hakuwahi kulalamika hata
mara moja. Bella alifuata masharti yote bila shida.
**************************************************
Maneno yakaanza kuenea mtaani. Minong’ono ikawa mikubwa
mpaka ikafika kwa wazee wenzake Mzee Masha. Kwani Mzee Masha alibadilika sana.
Hakuwa akionekana mahali popote hata kwenye vikao. Ilikuwa ni yeye, kazini
kwake na Bella tu. Akili na mawazo ya Masha yalikuwa kwa Bella pekee, wakati
wote. Kwani naye Bella alizidi kupamba akili za Masha. Maneno matamu na ujumbe
wa hapa na pale havikuisha kwa Masha.
Kulikuwa na kundi moja la kabila la kina Mzee Masha,
walikutana hapo jijini Dar, tokea miaka ya 70, wakitafuta maisha. Wanaume hao
wakaamua kuunda kundi lao na kusaidiana katika hali na mali. Wote walianza
wakiwa chini sana kimaisha, na wakamua kwa pamoja, kunyanyuana na kuapishana
kuwa kamwe watoto wao hawatakuja kuwa masikini. Walikuwa na kanuni zao ambazo
walizifuatilia sana. Walikuwa na umoja na mshikamano wa hali ya juu. Hata wake
zao walio waoa pia iliwalazimu kushikamana sana na kujikuta kama ndugu.
Mwishowe watoto wao wakajikuta wakioana wenyewe kwa wenyewe, kwani ndio walikuwa
wakikutana mara kwa mara.
Walikuwa wakikutana kijijini kwao vipindi vya sikukuu za krismasi, lakini pasaka, walikuwa wakiwa pamoja mjini. Walitafuta nyumba moja, walipika pamoja na kula pamoja. Mpaka walipokuza familia zao, utaratibu uliendelea. Watoto wao walisoma shule nzuri sana kwa kupitia michango yao wao wenyewe. Waliofanikiwa kwenda vyuo vikuu, hawakusubiri mikopo ya serikali ili kupeleka watoto wao shule, wao wenyewe walichanga na kusomesha watoto wao.
Ilikuwa ni rahisi pia kwa watoto wao kuwa pamoja au kuona,
kwani ni kama walilelewa na mama mmoja. Kina mama hao walikuwa wacha Mungu.
Walikuwa wakikutana pamoja na kuombea familia zao kila siku za jumamosi asubuhi
kwa wale walioweza. Waliwekeana njia mbalimbali za kuwakuza watoto wao kwenye
maadili ya kiMungu na hata walipopata mtoto mwenye tabia mbaya, walisaidiana
kuomba. Hapakuwa na mtoto wa familia fulani, wote walikuwa watoto wa wote.
Huo umoja ulidumu kwa muda mrefu sana. Hapakuwa na mwenye
shida kati yao, iwe pesa au ndoa zao. Hata kama kulikuwa na mambo mabaya
yanayoendelea katikati yao, ilikuwa ni kwa siri, na yalimalizwa kimya kimya.
Sasa Mzee Masha ndiye alianza kuleta sifa mbaya kati yao.
Walianza kumlaumu mkewe kuondoka na kumuacha mumewe nyuma, lakini hayo yalikuwa
ni makubaliano ya familia nzima. Mzee Masha alimpa mkewe baraka zote, na
kumwahidi kuwa akienda kumtembelea mara kwa mara. Mzee Masha alikuwa akiingiza
pesa nyingi sana katika biashara aliyokuwa akifanya. Hata mkewe alikubaliana
naye, isingekuwa jambo la busara kuacha biashara zao huku Tanzania na kwenda
kuishi kwa mshahara wa mkewe aliokuwa akilipwa na serikali huko nchini
Uholanzi.
Kwa mara ya kwanza Masha alimshirikisha Bella baadhi ya
biashara anazofanya, kuwa alikuwa ameingia mkataba na serikali kuwauzia kampuni
ya umeme, nguzo za umeme na kwenye makampuni ya simu, aliwauzia minara ya simu
pia. Alimwambia pia kampuni anayomiliki huwa inachukua tenda za serikalini na
makampuni mbalimbali, endapo itashinda kwa tenda anazochagua yeye Masha, na
anazoona zitamlipa pesa nyingi, tena kwa haraka bila kuwekeza pesa nyingi
kwenye tenda hizo. Alimwambia ndio maana haachi kusoma magazeti ili kujua tenda
zinazotangazwa na yeye kujaribu kuzifuatilia mpaka anaposhinda tenda hizo.
Alimwambia kinachohitajika ni umakini katika kuchagua aina
ya tenda, kushindana na makampuni mengine kuweka bei nzuri ili kupata tenda
hizo, na akishapata kuhakikisha anapeleka vitu vizuri ili kujenga jina zuri,
ili kudumu kwenye soko. Kwa hiyo ni kweli yeye ndiye alikuwa akiingiza pesa
nyingi sana kuliko mkewe. Na ndio maana walikubaliana yeye abaki na mkewe aende
kushika nafasi hiyo aliyoipata kwa bahati sana, na mkewe alimwambia ni kitu
alichokuwa akikitamani tokea zamani.
Haikutokea tokea tu mama huyo kuteuliwa kuwa balozi. Alianza kujijengea jina tokea zamani, na alikuwa ni mama aliyejulikana sana nchini Tanzania. Kuteuliwa huko, kwake ilikuwa ni moja ya ndoto zake alizotamani kuja kutimia, kwani alikuwa na ndoto za kwenda juu zaidi ya hapo.
**************************************************
Kwa kuwa Masha alikuwa na pesa nyingi sana kuliko wazee
wote kwenye kundi lao, yeye ndiye alikuwa akitegemewa sana kwenye michango ya
kundi lao. Hakusoma sana kama wenzake walikuwa wamefika mjini kwa lengo la
kujiendeleza kielimu. Yeye alipotua tu jijini miaka hiyo ya 70, alijitupia
kwenye biashara moja kwa moja. Kwa hiyo enzi hizo wakati wapo vijana, Mzee
Masha aliyekuwa ameshajua njia nyingi za kupata pesa, aliwainua sana wenzake
walipokuwa wakitoka chuoni. Aliwasaidia kuwaombea kazi kwenye kampuni
mbalimbali na watoto wao pia aliwasaidia. Alikuwa mtoaji sana na hakuwa Mzee wa
kukata tamaa.
Alipokusudia jambo kubwa litokee katikati yao, hata kama
wote watakata tamaa, lakini Mzee Masha huwa hakati tamaa, atasimamia hilo jambo
mpaka litokee. Iwe upande wa watoto wa rafiki zake, au marafiki zake wenyewe.
Alihakikisha wote wanahali nzuri za kimaisha kwa kuhimizana na kuwafundisha
njia zakuwaingizia pesa zaidi. Kwa hiyo yeye ndiye alikuwa msemaji mkuu kati
yao, na walimuheshimu sana katika hilo kundi. Hakuna jambo au kikao
kilichopitisha jambo bila Mzee Masha kuidhinisha, japokuwa yeye ndiye aliyekuwa
mdogo kidogo kuliko wote. Na hakuwahi hata mara moja kuwa na sifa mbaya katika
jamii, ila Bella ndiye aliyemchanganya na kumwingizia dosari kwenye ndoa yake.
Alijisahau kabisa kama anatizamwa kwenye jamii. Hakujali mtu yeyote isipokuwa
Bella tu, ambaye kwake alikuwa kila kitu.
“Historia ya Bella na familia hiyo
ya Masha.”
Haikuwa kwa bahati mbaya kutokea kumpenda Bella. Ni mtoto
aliyekuwa akilala mara nyingi tu nyumbani kwake. Alishamuona akiwa uchi, yaani
na vinguo vya kuogelea, alishamuona akiwa amevaa taulo tu wakiwa wanaenda
kuoga, hapo nyumbani kwake na hata kwenye mahoteli waliyokuwa wakienda kama
familia. Zera rafiki yake kipenzi, alikuwa akimwalika Bella kusafiri nao kila
wanapokuwa wanasafiri kwenda mapumzikoni. Bella alikuwa na maumbile ya
kutamanisha sana. Japokuwa alikuwa mtoto, lakini hakuna aliyeacha kutupia macho
kwenye mwili wa binti huyo aliyekuwa na akili za kitoto. Kama mama yake
alivyokuwa anamshauri kusubiri na kumwambia hana haja ya kuwa na mpenzi kwa
wakati ule, kweli Bella naye alijiona mtoto, hakuwahi kufikiria swala la
mapenzi hata kidogo.
Hata kaka yake Zera, Junior Masha, alimsumbua sana Bella,
akimtaka awe mpenzi wake, lakini Bella alishamkatalia katakata, akimwambia yeye
ni mtoto na hataki mambo ya wakubwa. Zera alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na
wanaume tofauti tofauti, hata Junior alikuwa akimwambia Bella, kuwa haina shida
kwani hata Zera rafiki yake anao wanaume na haimletei matatizo, lakini Bella
alimkatalia, tena kwa kitoto sana.
Junior mtoto mkubwa wa Masha,
alijua kutapanya pesa ya baba yake. Alivuma jijini, kila mtu alimjua Junior
Masha. Alijua kuweka heshima kila alipokanyaga na wenzake kwa starehe.
Alikunywa pombe kwenye baa za kisasa na wanawake walikuwa wakimkimbilia kwa
kuwahonga pesa za maana. Marafiki zake ni watoto wavigogo watupu. Kila
wanapofika baa, Junior na rafiki zake walianza kulipa kwanza, ndipo wakae na
kunywa. Waliacha mapesa kaunta, ndipo wanatafuta meza yao maalumu nakuanza
kunywa vinywaji vikali. Walitembea na warembo na wasichana maarufu sana hapo
nchini. Katika kundi lao, mtu aliyewazungusha akili, na kubaki kitendawili
kigumu kati yao alikuwa Bella pekee. Walimtamani binti huyo na kumtafutia njia
nyingi za kumpata lakini walishindwa.
Junior alijitahidi kuacha pombe kwa muda, akimuahidi Bella atatulia lakini Bella alimkatalia kabisa. Zera alisha mbembelezea kaka yake, na kumwambia Bella, endapo angemkubali Junior kaka yake, itamsaidia kutulia na labda angependa shule kama wenzake. Lakini Bella alikataa kata kata, hata kunakipindi urafiki wao uliisha sababu ya Bella kumkataa kaka yake. Mwishowe walikubali kuwa Bella haingiliki.
Bella hakuwa akitoka kwenye familia yenye pesa sana kama
wao na wala mama yake hakuwa msomi kama mama yao, lakini mama yake Bella
alijinyima sana kuhakikisha watoto wake wanasoma katika shule za matajiri na ni
kweli walifiti kwenye
jamii hiyo ya watoto wenye pesa. Kwa hiyo Enabella na Eric, walijikuta
wakifikiri, walitazama mambo yao, na kuongea kama watoto wa matajiri. Na
ndio maana Bella aliweza kupenya kirahisi sana na kuishi katikati ya
kundi hilo la kina Zera, la watoto wa matajiri wa jijini bila shida. Mara
nyingi walikuwa wakila na kutembea kama kikundi wawapo shuleni, na baada ya
kutoka shuleni pia hawakuacha kuwa pamoja. Sherehe zao zakuzaliwa walizifanya
pamoja, tena kwenye mahoteli makubwa na ya kisasa pale jijini, huku wazazi wao
wakiwa ndio wafadhili wao.
Watoto hao wakiongozwa na watoto wa Masha, upande wa mabinti kiongozi wao alikuwa Zera Masha na upande wa vijana wakiume wale wenye tabia za ajabu, waliongozwa na Junior Masha, walikuwa wakitapanya pesa za wazazi wao, bila kujali kesho. Zera ndiye alikuwa kipenzi cha baba yake, kwa kiyo hata kama Mzee Masha alikuwa na kazi nyingi kiasi gani, anapohitajika kuhudhuria kitu chochote alichoandaa binti yake, alikwenda. Na ndipo huko alipokuwa akionana na Bella akiwa uchi au wamevaa yale mavazi yao wanayodai ya watoto wakizungu na kuacha sehemu kubwa za miili yao nje. Na ndio tokea wakati huo, kwa mara ya kwanza maishani, mbali na mkewe, jicho la Mzee Masha ndipo lilipoanza kupata matatizo juu ya mtoto huyo Bella.
Siku moja kwenye birthday ya Zera akiwa anatimiza miaka 15,
walienda kufanyia sherehe hiyo kwenye hoteli moja ya kitalii iliyokuwa
pembezoni mwa bahari. Zera alikodi vyumba kadhaa ambavyo angelala na marafiki
zake mara baada ya kusherehekea na wazazi wao. Alialika marafiki zake, watoto
wa matajiri wa hapo jijini, wazazi wao pia walihudhurua na Bella naye
alikuwepo. Kasoro mama yake Bella hakuwepo siku hiyo kwani alishaanza kuumwa,
kwa hiyo kama kawaida, Mat, dereva wao ndiye aliyempeleka Bella kwenye tafrija
hiyo.
Walipofika tu hotelini hapo, wakati wazazi wao wakila na kunywa, watoto hao
waliingia chumba cha kubadili nguo, na wote wakatoka na nguo za kuogelea.
Wazazi wengine, waliwatazama binti wale kama watoto, lakini Mzee Masha tamaa
ilianza kumsumbua sana juu ya Bella. Kila alipokuwa akimtizama Bella, alitamani
awe mtu mzima kidogo, ili angalau arushe ndoano yake. Kadiri muda ulivyozidi
kwenda, wakati watoto wao wakiogelea na kucheza bila hofu mbele ya wazazi wao,
wakiwa na nguo za kuogelea, ndivyo Mzee Masha alivyokuwa akitokwa na mate kwa
Bella. Alitaka kuongea naye usiku huo wakati mabinti hao wanapoingia kwenye
vyumba vyao, hotelini hapo kulala, lakini Bella alikataa katakata kulala,
akasema anataka kurudi nyumbani kumuuguza mama yake na kweli aliondoka mapema
sana, kitu kilichomuumiza sana Mzee Masha, na kuapa kumsaka Bella kwa wakati
wake.
Mzee Masha alishatafuta njia nyingi za kumvutia Bella,
akijidai kutoa misaada ya hapa na pale, ilimradi tu kumvutia Bella, lakini
Bella alijawa na utoto mwingi sana akilini mwake, hakuwa hata akimuelewa,
alimuhesabu kama baba tu. Alishasaidia kulipa baadhi ya garama pale shuleni,
akijidai kumpongeza Bella kama rafiki wa karibu wa binti yake Zera, ambaye
alimuhimiza masomo. Bella ndiye alikuwa akimsaidia sana Zera shuleni. Ndio
maana hata mama yake Zera alimkubali Bella aendelee kuwa karibu na mwanae, na
kusafiri naye sehemu mbalimbali za starehe ili kumsaidia Zera mambo ya shuleni.
Kila walipotoka kama familia na kwenda mapumzikoni sehemu
mbalimbali hapo nchini, Masha alimruhusu Zera kualika rafiki mmoja tu, akijua
wazi Bella ndiye angealikwa ili ikiwezekana apate naye muda, lakini aliambulia
patupu kwani Bella hakuwa akielewa kitu juu ya mapenzi. Kila jambo alilokuwa
akiambiwa sirini na baba yake Zera, Mzee Masha, alilisimulia wakiwa wamekaa
familia nzima mezani huku akicheka, bila hofu mbele ya mkewe na watoto wake
Masha. Ndipo Masha alipoona ni heri amwache kwanza, kwani ni kweli alikubali
Bella ana akili za kitoto. Baada ya kumaliza shule, kidato cha 4, Bella akiwa
na umri wa miaka 16, mama yake alizidiwa sana, akapotea kabisa katikati ya
kundi hilo la marafiki. Hata walipokuwa wakimpigia simu aungane nao kwenye
starehe zao, Bella alikataa. Alibaki akimuuguza mama yake tu.
“Bella kabla ya kifo cha mama yake.”
Ilifika kipindi Tunu, alikuwa hawezi kuamka kabisa
kitandani, kwa hiyo yeye kama nguzo ya familia, mtu mmoja tu aliyekuwa
akiingizia familia hiyo kipato aliposhindwa kuleta pesa nyumbani, mambo
yalianza kuyumba. Msichana wa kazi za ndani na kijana wa maua walipo wakimbia,
akabaki Bella akimuuguza mama yake kwa karibu sana akisaidiana na Mat. Na hapo
ndipo Bella alipojifunza maisha. Tunu aliugua kwa muda mrefu sana, lakini
ilikuwa ni kipindi ambacho ni kama Mungu alikuwa akimuandaa Bella, mtoto aliyekuwa
haelewi kama kuna watu wanaweza kukosa pesa, au hata kulala njaa hapa
duniani.
Ndicho kipindi hicho Bella ilimbidi ajifunze maisha au kazi za nyumbani. Alijifunza biashara, kwani ilimbidi kuanza kuuza baadhi ya vitu vya thamani walivyokuwa navyo ili kuweza kumudu matibabu ya mama yake, na ada ya mdogo wake ambaye bado alikuwa shuleni. Bella alikuwa msaada mkubwa sana kwa mama yake. Zile akili za kitoto na kupenda starehe, akizunguka kwenye magari ya kina Zera Masha, na kulala kwenye mahoteli ya gharama na familia hiyo ya Masha, zilibadilika, akarudi kwenye uhalisia wa mambo, akaanza kushika majukumu ya mama yake.
Tunu alikufa akiwa na furaha sana, akijua angalau amemuacha
Eric kiziwanda wake, kwenye mikono ya dada yake aliyekwisha jua maisha ni nini,
na alijua alikuwa amewaachia angalau mali ambazo zingewasogeza kimaisha.
Tunu alijua kujipamba kwa dhahabu, tena za hali ya juu.
Viatu, nguo zake, vitu vya thamani alivyokuwa amejaza kwenye nyumba yake,
alijua kila kimoja ambacho Bella angeuza, angepata pesa nzuri sana. Alimwambia
Bella, auze kila kitu, akipata pesa, wahamie kwenye nyumba ya kawaida sana,
aanzishe biashara itakayowasaidia kuishi. Na alishamwandaa kukatisha masomo.
Alimshauri asiende kidato cha tano na sita, ili kupunguza gharama, bali akosome
chuo cha miaka miwili tu cha mambo ya IT, kisha atafute kazi ili amsaidie mdogo
wake.
Mipango hiyo alikuwa akipanga na mwanae, Tunu alijua kabisa
asingepona. Alikuwa ameathirika na ugonjwa wa UKIMWI, na alichelewa kuanza
matibabu. Kwa hatua aliyokuwa amefikia, alijua wazi ana siku chache sana
zakuishi, angekufa tu. Alimwandaa Bella kiakili. Alimfundisha mambo yakufanya,
changamoto atakazokutana nazo, na jinsi gani yakupambana nazo, kukabiliana na
maisha. Kwa hiyo Bella alishakubali kuwa mama yao atawaacha, na alijua ataweza
tu maisha bila mama yake.
Mat dereva wake, alikuwa mcha Mungu sana. Alikuwa msaada
sana kwao. Aliomba na Tunu, bosi wake kila siku huku akisoma naye neno la Mungu
kumjenga Kiroho na kumwandaa na kifo chake. Alimtoa wasiwasi juu ya watoto
wake, akamwambia Mungu atawalinda na yeye atakuwa nao bega kwa bega. Kwa hiyo
Tunu alikufa akiwa na amani kubwa sana moyoni akijua anawaacha watoto wake kwa
Mat ambaye alimpenda sana Tunu. Ile gari ilikuwa kama ya Mat. Alimpa Tunu pesa
atakavyo yeye. Tunu hakuwa akimdai ila Mat mwenyewe ndiye alikuwa akikusanya
pesa na kumuwekea benki.
Kwa hatua aliyokuwa amefikia Tunu, walijua hatakaa muda
mrefu, atakufa, kwa hiyo hata yeye mwenyewe hakutaka kulipa tena kodi ya nyumba
waliyokuwa wakiishi. Tofauti na matarajio yake, Tunu hakufa kwa haraka. Baada
ya hospitalini kumrudisha nyumbani wakisema hakuna chakufanya, Bella na Mat,
wakisubiri siku yeyote afe, Tunu aliugua kwa muda mrefu sana. Wakati mwingine
Bella alipata matumaini kuwa mama yake angepona lakini hali yake ilikuwa
ikibadilika badilika sana, mpaka alipochanganyikiwa kabisa, kufikia hatua
yakutotambua kabisa mtu yeyote yule hata Eric kipenzi chao na mwishowe kukata
kauli mpaka kifo.
Walimzika Tunu, wakiwa wameshafilisika vyakutosha. Bella
alikuwa ameshamaliza pesa zote benki kwa kulipa ada kubwa ya mdogo wake, na
alishauza vitu vingi vya thamani wakati akimuuguza mama yake. Hata vitu
walivyokuwa wameviacha wakati walipoenda kijijini kuzika pia vilipotea. Ndipo
Bella akajikuta amebakia yeye na Eric tu, nyumbani kwa Mat ambaye naye alikuwa
akihangaika na maisha yake yeye mwenyewe. Kwa hiyo mipango aliyokuwa ameachiwa
na mama yake yote haikufanya kazi hata mmoja. Akajikuta amebaki hana urithi
wowote ule.
Siku aliyokwenda kuomba msaada nyumbani kwa Mzee Masha, na
mkewe kumfukuza kikatili Bella aliyeonekana ni kama amegonga mwamba, ndipo Mzee
Masha alipopata mwanya wa kumnasa binti huyo. Wakati Mama Zera anamfukuza
Bella, huku wakisaidiana na Zera mwanae kumkejeli, Mzee Masha alimtumia ujumbe
dereva wake aliyekuwa upande wa pili, mezani akisoma gazeti, amkimbilie Bella
na mdogo wake, awachukue na kuwapeleka kwenye moja ya hoteli zake. Na kweli,
bila maswali mengi, Bella akiwa kwenye shida, akaingia kwenye lile gari
alilokuwa amezoea kulipanda, kumbe safari hii alikuwa akijiingiza kwenye mtego
aliokuwa ametegeshewa kwa muda mrefu sana.
“Ndoa
ya Masha, matatani.”
Ndoa ya Mzee Masha ilianza kuleta matatizo. Habari za
kuwepo binti mdogo kwenye maisha ya Masha, zilimfikia mpaka mkewe hukohuko nchini
Uholanzi. Na kutokana na mabadiliko aliyoonyesha mumewe, Mama Masha aliamua
kurudi nchini kufuatilia ukweli. Alichanganyikiwa sana aliposikia mumewe
anaishi na mtoto mdogo. Kwani sifa za Bella, zilienea kila mahali. Uzuru wake
ulikuwa haufananishwi na mtu yeyote. Ila Mama Masha aliambiwa ni mtoto mdogo,
mzuri sana. Kazi ilianza kumshinda Mama Masha. Safari za Tanzania zikaanza ili
kunusuru ndoa yake, bila mafanikio yeyote. Kwani Mzee Masha alishajiingiza kwenye penzi la Bella, hakujua jinsi
ya kurudi kwa mkewe au jinsi ya kuwa nao wote wawili.
Mapenzi yalilemea kwa Bella, msichana asiye na jukumu
lolote isipokuwa kumfurahisha yeye tu. Bella hakuwa akiwaza pesa wala kitu
chochote kile. Kila kitu alichotaka alitamka tu, Mzee Masha alileta. Hata hivyo
alifundwa. Bella hakuwa mtoto tena kama alivyoonekana. Alipata mwalimu
aliyehakikisha anamfundisha na kuelewa. Tena alifundishwa vizuri sana jinsi
yakuishi na mume, hasa Masha. Shule yake ilikuwa ya uhakika kwani alifundishwa
akiwa tayari akiishi na Masha. Kwa hiyo yule mwalimu wake alihakikisha Bella
anamwambia tabia zote za Masha, ugumu anao pambana nao kwenye maisha yake na
Masha, na yeye akamuelekeza jinsi ya kuishi kutokana na vile Masha alivyo.
Bella alimjulia Masha, kuanzia akili yake mpaka mwili wake. Tofauti na Mama
Masha aliyekuwa na majukumu mengi tena yote yakimsubiri yeye. Watoto wawili
wote waliolewa utajiri wa baba yao, waliokuwa wakimsumbua mama huyo mchana na
usiku, huku akiwa na kazi ya kuwakilisha taifa la Tanzania nchini Uholanzi,
hapakuwa na jinsi ya kumlinganisha na Bella hata kidogo.
Alikubali kuonekana na mkewe, sababu ya kuridhisha jamii tu
kutokana na nyadhifa walizokuwa nazo wote wawili, lakini si mapenzi tena.
Alijitahidi kuonyesha kwa nje kila kitu kipo sawa lakini ndani akiwa na mkewe
alikuwa akimjibu vibaya sana. Kila Mama Masha alipotaka wazungumzie swala la
mwanamke mwingine aliyenaye, Masha alikuwa mkali sana. Na alipiga marufuku
asiwahi kumfuatilia maisha yake tena. Ilikuwa ngumu sana Mzee Masha kuwa naye
nyumbani pindi anapokuwa amerudi kumtembelea hapa nchini. Kwani Masha
alishahama nyumbani hapo muda mrefu sana, akawa akiishi na Bella. Kitendo cha
mkewe kurudi, na kumlazimu arudi nyumbani aishi naye kama mume, kilikuwa
kikimkasirisha na kumuharibia utaratibu wake mzima. Ilibidi Masha awe anaibua
safari za dharula pindi mkewe awapo nyumbani, akimdanganya anasafiri nje ya
nchi, ili tu awe nyumbani kwa Bella.
Inapomlazimu kulala nyumbani kwake mkewe akiwepo, usiku
kucha anakuwa na wasiwasi labda Bella ataondoka nyumbani na kwenda kwa wanaume
wengine. Alikuwa akiamka katikati ya usiku, au alfajiri sana kumpigia simu ya
skype na ilikuwa lazima Bella apokelee simu hiyo kwa kompyuta ya mezani sio
simu yake ya mkononi, ili kuhakikisha amelala nyumbani. Alikuwa kama
amechanganyikiwa kati ya mahusiano hayo. Na ukali ulikuwa ukiongezeka mara
mbili pindi wanawake hao wote wawili wawapo kwenye mji mmoja. Hofu yake kubwa
ni kumuacha Bella peke yake. Kila alipokuwa mbali na Bella, alihisi anaibiwa
tu. Hakuamini hata njia alizokuwa ameweka za kumlinda huyo Bella. Alihisi
Bella anaweza kumzidi ujanja sehemu, akamtoroka wakati yeye akiwa na mkewe.
**************************************************
Masha aliendelea kumuadhibu mkewe kimya kimya kwa kosa
kubwa sana alilomtendea, ambalo Masha hakuwa amemwambia mkewe kuwa anajua uovu
wake. Mkewe naye alizicheza karata zake kwa makini sana. Alibadilika akawa mke
mwema, huku bado akiwa anaficha kwa makini sana siri aliyokuwa ameibeba
moyoni mwake, kwa miaka mingi, asijue kuwa mumewe alishajua uovu wake. Hasira
zilikuwa zikimsumbua Masha kadiri alipokuwa akimtizama mkewe jinsi
anavyojionyesha mke mwema, huku akijua wazi amemkosea na anashindwa hata
kutubu.
Ukweli Masha alishakuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa mkewe. Hakuwahi kuwa na mwanamke wa nje, Bella pekee ndiye wakwanza. Alipogundua uovu wa mkewe, alichanganyikiwa sana, na kujiambia labda atakuja kutubu leo, au kesho. Siku zilizidi kwenda bila mkewe kutubu ila kulalamikia tabia za mumewe. Kila baya alilokuwa akifanyiwa na Masha kwa makusudi, mama huyo alimkumbusha kuwa yeye ni mkewe, na aliapa katika shida na raha. Kwa hiyo kifo pekee ndicho kitawatenganisha. Hana mpango wakumuacha hata akizidi kumtenda ubaya. Mzee Masha alikuwa akikasirika sana kila akisikia kauli hiyo, kwani alimjua vile mkewe alivyo. Ni mwanamke aliyekuwa akijua ni kitu gani anataka maishani, na hata kama ni kigumu namna gani, akisema atapata, lazima atakipata tu, kama mumewe alivyo. Hata hivyo alikuwa na sababu kubwa sana iliyomfanya abaki na Masha.
Mama Masha aliishi na mumewe kwa malengo makubwa sana,
ambayo hakuna mtu aliyeyajua isipokuwa yeye mwenyewe. Wala si penzi la Masha
alilokuwa akilihangaikia, bali ni mali na heshima ile ya ndoa ndivyo vilikuwa
ngazi yakumfikisha aendapo au kutimiza malengo yake makubwa sana aliyokuwa
ameyabeba tokea anaolewa na Masha. Asingekubali msichana aliyejitokeza
karibuni, avunje ndoto zake. Aliamua kupambana kufa na kupona ili Masha
asimuache, mpaka atimize lengo lake. Alifanya kila njia ili kumdhibiti mumewe,
hasa kwenye upande wa talaka. Alikubali yote, lakini hakuweka mwanya wa
kuachana na Masha.
Masha alipoona mkewe ameng’ang’ana akaanza kuanzisha ugomvi
usio na maana, ilimradi apate sababu yakutoka hapo nyumbani na kwenda kwa
Bella. Wakati mwingine aliondoka usiku usiku katikati ya ugomvi wao, kurudi kwa
Bella, aliyekuwa akimkuta mara zote amelala nyumbani kwao bila wasiwasi. Ulinzi
kwa Bella uliongezeka, lakini hakuwahi kumkamata na mwanaume hata mmoja. ‘Lazima tu atatafuta mwanaume
huko chuoni. Kwani
naingia naye darasani?’ Mzee
Masha akaanza kujutia uamuzi wake wa kumruhusu Bella kwenda shule. Alitamani
amkatize masomo, lakini hakuona kosa lolote lile kwa Bella. Alikuwa ametulia
kama maji kwenye mtungi. Heshima yake kwa Mzee Masha ilikuwa palepale, na
hakuacha kumliwaza kila aliporudi nyumbani kwake akiwa na hasira, bila kutaka
kujua kulikoni.
“Penzi la Bella lavunja umoja wa kinamama hao.”
Mama Masha alivumilia kuficha tena aibu ya familia yake,
lakini akashindwa. Mwishowe aliamua kuwashirikisha wanawake wenzake akitaka
ushauri na waombe kama kawaida yao. Mara nyingi watoto wake ndio waliokuwa
wakiombewa mara kwa mara na kina mama hao. Kwani wote wawili, Zera na Junior,
ndio walionekana ni washawishi wabaya kati ya kundi la watoto hao. Kwa hiyo
kila walipokuwa wakikutana waliwaombea watoto wa Masha. Siku hiyo ya jumamosi
alipokuwa nchini akaamua kujikaza akaenda nyumbani kwa Mama Mwasha kukutana na kina mama hao.
Nyumbani kwa Mama Mwasha ndio kilikuwa kituo chao kikubwa, kwani mama huyo alikuwa mama mwenye hekima sana, na alijawa na upendo. Kwa hiyo ni kama alikuwa ndiye kiongozi wao, hao kina mama. Walifanyia vikao vyao vyote nyumbani kwa Mwasha. Waliambizana kuwa Mama Masha yupo nchini na angeomba wote wakutane, ana jambo la kuwashirikisha.
Siku hiyo asubuhi Mama Masha akiwa amechelewa kidogo,
wakati anaingia aliwasikia wenzake wakimsema vibaya sana. “Kwani ni
jambo gani Mama Masha anataka kutushirikisha tena?” Alimsikia mmoja wao akiuliza. “Itakuwa
janga la mumewe tu.” Mwingine alijibu na kufanya wote wacheke
kidogo. “Alipokuwa anaondoka alifikiri nini?" "Eti sasa
hivi ndio anakumbuka shuka wakati kumekucha!” Aliwasikia wakimcheka
tena. “Nilimshauri kweli Mama Masha aachane na mambo ya Ubalozi.
Walikuwa wamefika mbali na muwewe, yeye akaondoka. Alikuwa anatafuta nini na
utuuzima huu?” “Sasa ndio ajue, alichokitafuta kakipata. Kavunja nyumba yake
kwa mikono yake yeye mwenyewe! Sasa hivi mtoto mdogooo ndio anaijenga.” “Kitoto
chenyewe mmekiona lakini?” “Namsikia tu!” “Si mchezo. Huwezi kumfananisha na
Mama Masha hata kidogo.” “Lakini mwenzetu msomi jamani! Acheni
akaishi majuu.” Aliongeza mama mwingine kwa kejeli. “Basi
ndio atulie sasa huko huko majuu na elimu yake. Aache watoto wamtunzie mume.” Wote
waliendelea kucheka taratibu huku wakigonga. Mwishowe Mama Masha akaamua
kuingia pale sebleni, wote wakanyamaza, wakidhani hakusikia, kumbe alisikia kila
kitu wakati yupo nje. Mama mwenye nyumba hiyo, Mama Mwasha, alikuwa
jikoni akiwaandalia kitu chakula wakati marafiki hao wakiendelea kusengenya.
Ulizuka ugomvi mkubwa sana ndani ya hiyo nyumba ya Mwasha, wakisutana kwa hili na kutukanana
mpaka Mama Mwasha alipoingilia kati na kuwatuliza. Hapakuwa na maombi siku hiyo
zaidi ya ugomvi. Walivurugana kupita kiasi, kila mmoja aliondoka kwa njia yake.
Kwani walisemeana siri zao zote. Kila mmoja alisema vile huyu alivyomsema huyu,
na huyu alivyosema vile. Na huo ndio ukawa mwanzo wa kuvunjika umoja huo wa
wakina mama hao. Hakuna aliyemtafuta mwenzake, kila mmoja alikuwa na hasira na
mwenzie, huku wakisemeana kwa waume zao, wakati huo Bella ametulia tuli na Mzee
Masha nyumbani kwao. Bella hakuruhusu ugomvi wowote ule katikati yao. Alimuunga
mkono Mzee Masha kwa kila uamuzi anaotaka kufanya na alipoona ni mambo ya
familia yake, alinyamza kimya, hakutaka kuingilia hata kidogo. Alitimiza wajibu
wake, pesa yake ikawa inaendelea kuingia benki na ada ya mdogo wake ikawa
inaendelea kulipwa.
**************************************************
Njia hiyo ya kina mama iliposhindikana, Mama Masha akapata
wazo la kutumia watoto wao, kuwa awe anarudi nao Tanzania kumsalimia baba yao sio
kumsubiria tena kule Uholanzi kwani Masha alishaanza kutoa udhuru wa kutokwenda
kwa familia yake. Kuna kipindi alishindwa kurudi kwa Bella kwa siku mbili
mfululizo, mchana na usiku, kwa kuwa mkewe alirudi nyumbani na watoto
wote, Masha akashindwa kuleta fujo au kuacha familia nzima nyumbani, kwani
hakuwa amewaona wanae kwa muda mrefu, na wote walimganda baba yao wakionyesha
kuwa na hamu naye sana.
Alikaribia kurukwa na akili. Mwili ulikuwa kwa familia yake, akili kwa Bella, aliyekuwa akienda na kurudi shuleni peke yake, tena akijua wazi Masha yupo mjini kwa mkewe, lakini hafiki nyumbani kumuona. Hiyo ndiyo ilizidi kumchanganya Masha. Alikosa ujasiri hata wakupiga simu kwa Bella aliyekuwa akimkataza kuwa na wanaume wengine, wakati yeye yupo na mkewe nyumbani kwake, na kushindwa hata kumuona.
Baada ya siku ya tatu, Masha alikuwa na hali mbaya.
Alishindwa kujizuia kila mahali walijua kuna tatizo. Si nyumbani kwake wala
kazini, alikuwa akigomba sana. Walinzi aliokuwa amewaweka wamfuatilie Bella
kila aendapo, walitoa ripoti nzuri tu juu ya Bella, lakini bado dhamira ya
Masha ilikuwa ikimsumbua sana. Aliamua kwenda nyumbani kwa Bella bila kujali
litakalo tokea tena kwa familia yake. Siku hiyo hata ufunguliwaji wa geti na
walinzi waliokuwepo zamu nyumbani kwa Bella, ulikuwa sio sahihi. Alidai
wanahatarisha maisha ya Bella. Alianza kugomba kuanzia getini. Alikuwa akiwaka
kama moto. Alianza kufukuza kazi wafanyakazi wote pale kwa Bella. Kuanzia
kampuni ya ulinzi getini kwa Bella, mpaka wafanyakazi wa nyumbani hapo.
Aliitisha wafanyakazi wote kikao cha dharula nje kwenye ua, mara tu dereva
alipoegesha gari.
Bella akiwa chumbani kwake akijisomea, alimsikia akigomba
sana huko nje. Akaamua asimame, amchungulie ajue kulikoni. Akamuana jinsi
anavyofoka, na kupiga teke vyungu vya maua. Alibadilika kuwa mwekundu kama
nyanya kwa hasira. Hata huo muda haukuwa ni muda wake ambao Bella alimtarajia
pale nyumba. Bella alijua kile kinachoendelea kichwani mwa Masha. Alijua wazi
wivu na hofu juu yake, ndivyo vinavyomsumbua Mzee huyo. Alijaribu kwa kadiri ya
uwezo wake kumuhakikishia kuwa hatathubutu kumsaliti, lakini kila Masha
alipokuwa akikumbuka uzuri wa Bella na umri wake, alijua hawezi kuepuka kulizwa
mjini.
Bella alikimbilia simu yake kwa haraka kabla hajaendelea
kuharibu vitu pale nje na kujiumiza yeye mwenyewe, akampigia simu huku
anamchungulia dirishani. Akamuona jinsi alivyopokea simu yake kwa haraka. “Vipi T?” “Safi tu.” “Nilikuwa nasoma
hapa, lakini naona hata sielewi.” “Nini tena?” Masha aliuliza kwa wasiwasi kidogo. “Sijui. Labda nikikuona
akili yangu itafanya kazi vizuri. Hamna ninachoelewa hapa hata kidogo.” Bella alimuona jinsi Masha alivyoanza kujikusanya na
tabasamu usoni. “Na
nimekuandalia masaji nzuri kweli T, sio ile ya kila siku. Unajua nitafanyaje?” Bella alikuwa akimuuliza kwa taratibu sana. “Utafanyaje?” Masha alianza kutabasamu huku akiondoka katikati ya
wafanyakazi wake na kujisogeza pembeni. “Sitakwambia
mpaka uje uone kwa vitendo. Siunanijua nilivyo mzuri kwa vitendo?” Masha alicheka, akisikika ametulia kabisa. “Unajua nipo hapa nje?” Masha akauliza. “Mbona
sasa huingii ndani? Huna hamu na mimi?” Bella aliuliza kwa
deko kidogo. “Hapana,
nimekuja kwa ajili yako Bella. Ila kuna mambo nilikuwa naweka sawa hapa nje.” Bella alimuona anawageukia wafanyakazi wote na kuwaambia
waendelee na kazi na wale wa ndani waondoke mpaka kesho, Bella ataongea nao,
yeye amepata dharula kidogo.
“Bella!
Bella!” Masha alimuita, kutaka kujua kama alishakata simu. “Nipo T, nakusubiri.” Bella alijibu, haraka sana akakusanya madaftari yake na
kompyuta, akaweka pembeni ili kumpokea Masha, aliyekuwa akiingia ndani kwa
haraka sana. Alikaa hapo chumbani na Bella, akifurahia mapenzi mpaka usiku sana
alipoona Bella amepitiwa na usingizi mzito, ndipo aliporudi kwa familia yake,
akiwa ametulia kabisa. Kama kawaida yake, Bella hakutaka kumuuliza alikuwa wapi
na kwa nini alipotea kwa siku hizo mbili, bila kuonekana wala kupiga simu.
Alimfurahisha tu huyo mzee, na kuacha mambo mengine kama yalivyo, kitu
alichokifurahia sana Masha, kwani hakujua ni jinsi gani atajitetea kwake.
**************************************************
Mama Masha alipoona ndoa yake inakwenda kuvunjika kabisa,
na Masha hakusikia la mtu, na waziwazi alionyesha yupo tayari kwa lolote,
lakini si kumpoteza Bella, akaamua kwenda kulalamika kwa wazee wenzake Masha.
Aliwasihi sana wazungumze na mumewe. Alionyesha uthamani wa ndoa yake, jinsi
anavyo ihitaji hiyo ndoa na wakati huo yupo tayari kufanya lolote ili kunusuru
ndoa hiyo. Hata kama itamlazimu kuachia ngazi kwenye hiyo nafasi ya ubalozi,
mama huyo aliwaambia wazee hao, yupo tayari kulipa garama hiyo, ilimradi tu,
kunusuru ndoa yake. Japokuwa hakuwa akimaanisha lolote alilokuwa akisema kwa
machozi kwa wazee hao, lakini Mama Masha alihakikisha anavuta jamii nzima iwe
upande wake, wamuhurumie na kumsaidia ili ndoa hiyo isivunjike. Wale wazee
walimuhurumia sana mama huyo, wakaamua kumwitisha Masha ili wazungumze naye.
*Je Ni
siri ipi hiyo Masha ameigundua ya mkewe?
*Japokuwa
si mapenzi yanayomuhangaisha Mama Masha kulilia ndoa yake, nini anachotaka
kutoka kwa mumewe?
*Je
Wazee wenzake Masha wataweza kunusuru ndoa ya Masha, aliyekuwa amechanganywa na
Bella kiasi cha kushindwa hata kujitambua tena?
“Kweli wanawake ni viumbe vinavyoonekana dhaifu sana,
lakini Mungu amewapendelea nguvu ya ajabu sana.” Dereva wa Masha, aliyekuwa akimfahamu Masha kwa miaka mingi
sana, alirudia rudia sana usemi huo kila wakati alipokuwa na marafiki zake.
Kila alipokuwa akimfikiria bosi wake jinsi alivyobadilishwa na penzi la Bella
na kuwa kama mjinga! Hakuwa akiamini. Masha aliyekuwa akiogopewa na kila kiumbe
aliyemfahamu, alibadilika akawa kama mjinga kwa Bella. Mbele ya Bella, Masha
alikuwa kama ombaomba mbele ya tajiri mkubwa sana duniani, au mtumwa mbele ya
mtwana. Kama si kufungiwa ndani masaa 24 au ulinzi mkubwa aliojua unamzunguka
Bella, yule dereva angejua Bella anamloga sana Masha. Alisharudi mara kadhaa
kwa yule mama aliyemtafutia Masha ili amfundishe Bella, akimuuliza alimfundisha
nini binti huyo, au kama kuna dawa alimpa Bella ili amuwekee Masha, basi
angalau amdokeze yeye, lakini yule mama alikuwa akicheka sana, huku akimpa
maneno ya kuwakejeli wanaume huku akimsisitizia yule dereva kwamba, ‘hakuna kiumbe kirahisi kuishi
nacho hapa duniani kama mwanaume’.
Usikose sehemu ya 4.
0 comments: