Story
iku moja ya Jumapili wakiwa
wameamka, mhudumu alishawaletea kifungua kinywa, wakiwa wanakula huku
wanaangalia tv, walisikia mlango unagongwa. Bella alisimama kwenda kufungua
akijua muhudumu amerudi kuchukua vyombo, kumbe alikuwa Mzee Masha. “Shikamoo.” Bella akasalimia kwa heshima
sana. “Marahaba. Hamjambo?” “Hatujambo.
Karibu ndani.” Bella akampisha mlangoni. “Vipi hapa? Mnapaonaje?” “Tumepata wakati mtulivu, wametuhudumia
vizuri. Asante sana.” Bella akashukuru. “Vizuri.
Na mimi ndio nimerudi kutoka safari, niliwasindikiza familia yangu nchini
Uholanzi.” “Pole na safari.” Bella akaongeza. “Asante. Poleni na nyinyi kwa matatizo.” Mzee Masha alikaa kwenye
kochi.
My Past. Sehemu Ya 2.
“Kwa
Mara ya Kwanza Mzee Masha Kujitokeza.”
S
|
iku moja ya Jumapili wakiwa
wameamka, mhudumu alishawaletea kifungua kinywa, wakiwa wanakula huku
wanaangalia tv, walisikia mlango unagongwa. Bella alisimama kwenda kufungua
akijua muhudumu amerudi kuchukua vyombo, kumbe alikuwa Mzee Masha. “Shikamoo.” Bella akasalimia kwa heshima
sana. “Marahaba. Hamjambo?” “Hatujambo.
Karibu ndani.” Bella akampisha mlangoni. “Vipi hapa? Mnapaonaje?” “Tumepata wakati mtulivu, wametuhudumia
vizuri. Asante sana.” Bella akashukuru. “Vizuri.
Na mimi ndio nimerudi kutoka safari, niliwasindikiza familia yangu nchini
Uholanzi.” “Pole na safari.” Bella akaongeza. “Asante. Poleni na nyinyi kwa matatizo.” Mzee Masha alikaa kwenye
kochi.
Eric hakuwa hata na habari
ya mgeni, kwani alikumbana na show yake ya ‘Lab
Rat’ aliyokuwa akiifuatilia
tokea akiwa nyumbani kwa mama yake. Aliwapenda sana waigizaji hao. Walimfanya
acheke na kutamani kama siku moja angekutana nao. Akili zake hazikuwepo pale kabisa,
alikuwa akicheka na kuwasikiliza kwa makini sana, kwenye runinga iliyokuwa
mbele ya kitanda chake.
Bella alikaa kitandani
akimtizama Mzee Masha kwa hofu kidogo. “Sasa
nimeamua kuwasaidia.” Mzee Masha alimwangalia Bella. “Asante.” Bella alijibu kwa kifupi tu huku amejawa maswali mengi. “Chochote unachotaka unaweza kuniambia.”
Bella alibaki akiwaza huku ameinama. “Niambie
tu Bella. Nataka kujua sasa hivi unashida gani?” “Natamani turudi shule. Hata
kama hapatakuwa na pesa zakutosha kutupeleka shule sisi wote wawili, basi
angalau Ric yeye ndiye arudi shuleni.” “Hilo halina shida kabisa. Wote mtasoma,
lakini nashauri iwe kwa awamu. Aanze Ric, halafu ndio wewe.” Bella
hakuamini anachosikia.
Akasimama
na kumpa mkono Mzee Masha. “Asante sana.
Alikuwa akisoma hii shule ya hapo Masaki DIS. Najua ni garama sana, lakini
naweza kutoka kesho nikamtafutia shule nyingine.” Bella aliongea kwa
heshima sana. “Kuna shule nyingine ipo
Arusha, ndio nafikiria aende huko?” “Arusha!?” Bella akashtuka sana. “Ndiyo.”
Masha alijibu bila kusita, huku amemkazia macho Bella. “Kwa hiyo na mimi nahamia hukohuko? Siwezi
kuishi mbali na Ric.” Bella aliongea kwa hofu kidogo. “Ni shule ya bweni. Nilifikiria unahitaji muda wakujipanga tena, wakati
na yeye yupo kwenye mazingira mazuri huko shuleni! Unaweza kufanya huo ukawa
mpango wa muda mfupi. Utakapoweka mambo sawa, unaweza kumchukua mkaendelea
kuishi pamoja. Hata hivyo hiyo shule ni nzuri sana. Inakuza na vipaji. Walimu
wapo karibu sana na wanafunzi. Eric atapata malezi mazuri, kana kwamba yupo
bado na mama. Itakusaidia sana na wewe kujipanga ukiwa huna wasiwasi naye.”
Bella aliona ni wazo zuri. “Ni kweli.
Nafikiri hilo ni wazo zuri. Lini anatakiwa aanze?” “Nataka iwe haraka. Shule
zilishafunguliwa. Nitaongea nao, ili muondoke na ndege ya kesho asubuhi
kuelekea Arusha. Ukajaze fomu zote za huko shuleni, ili aanze shule mara moja.”
Bella alishindwa kujizuia, alisogea mpaka pale alipokaa Mzee Masha nakupiga
magoti. “Asante sana baba yangu. Asante.”
Akampa mkono. “Karibu sana Bella.
Kuanzia leo, nitakuwa na wewe bega kwa bega kukusaidia. Usiwe na wasiwasi.”
Bella alihisi yupo ndotoni.
*************************************
Tangia
mama yake alipoanza kuugua mpaka amefariki, hakuna mtu aliyewahi kuwasaidia kwa
kiasi hicho. Ndugu waliwakana, marafiki waliwakimbia, wakabaki na Mat tu ambaye
hawakuwahi kujua kama anaweza kuwa msaada wa namna ile. “Asante sana.” Bella akarudia. Kitendo cha mdogo wake kurudi shule,
kwake ulikuwa muujiza. Mzee Masha alitoka na kumuacha Bella akiwa amejawa
furaha sana.
Bella
alitafuta njia nzuri sana yakuongea na Ric, ili akubali aende kusoma mbali na
yeye. Kwa kuwa Eric na yeye alikuwa na hamu yakurudi shuleni, akakubali. “Lakini umeniambia ni kwa muda mfupi tu?”
“Ndiyo Ric. Nikishaweka mambo sawa, nitakuhamishia kwenye shule za hapa mjini
tuwe tunaishi wote.” “Asante Bella. Nitakuwa nakusubiri uje unifuate.”
“Nitakufuata Ric, usiwe na wasiwasi. Lakini nataka ujitahidi shule. Umesikia
Ric. Huyu baba anatusaidia tu, lazima tumuonyeshe na sisi tunathamini pesa
anayotumia kwa ajili yetu.” “Nitajitahidi Bella.” Waliongelea mambo ya
shule tu siku ile, Bella akijitahidi kumuhusia mdogo wake, na Eric naye
alionyesha kutambua umuhimu huo, lakini alirudia rudia, kumkumbusha Bella,
kuhakikisha anakwenda kumtoa huko Arusha ili arudi kuishi naye Dar. “Nitakufuata Ric. Usiwe na wasiwasi.”
*************************************
Asubuhi
Kasimu au K, kama walivyozoea kumwita, alirudi kuwachukua ili awapeleke
uwanja wa ndege, ili waelekee jijini Arusha. Bella alipewa pesa yakumtosha
kutumia akiwa huko, na ya kununulia vitu ambavyo angeona Eric angehitaji akiwa
shuleni. Alikwenda moja kwa moja kwenye hiyo shule mara tu walipotua kwenye
uwanja wa ndege.
Hiyo
shule ilikuwa nzuri sana. Wote wawili, Bella na Eric walifurahia mazingira
yake. Baada ya kukamilisha taratibu zote hapo shuleni, yeye Bella kama mzazi wa
Eric, alitoka na mdogo wake tena kurudi mjini kumnunulia vitu vyote
alivyohitaji. Alipojiridhisha amemuacha mdogo wake kwenye mikono salama na
mazingira mazuri , Bella aliamua kuwahi uwanja wa ndege ili arudi Dar. Njia
nzima alikuwa akimuwaza Eric. Ukweli hakutaka kumuacha popote ambako ni mbali
na yeye. Alitamani sana amlee mdogo wake yeye mwenyewe, lakini hakuwa na uwezo.
Kwa wakati ule alifanya kile alichoweza, na kama Masha ndiye anayeonekana
kuanza kutoa dira ya maisha yao kwa wakati huo, akaona afuate tu ushauri wake. ‘Lakini
ni kwa muda mfupi tu. Nitarudi kumchukua ili niishi naye.’ Bella
aliendelea kuwaza.
“Bella aanza maisha mapya, mikononi mwa Masha.”
Ndege
hiyo ilitua jijini Dar, giza lilishakuwa limeingia. Alimkuta dereva akimsubiri
nje ya uwanja huo wa Mwalimu Nyerere. Alimrudisha hotelini, Bella akaingia
bafuni moja kwa moja na kujiloweka kwenye sinki lakuogea, Jacuzzi.
Alikaa huko akiwaza, mpaka aliposikia hodi mlangoni. Kwa kuwa ilishafika jioni,
Bella alijua ni muhudumu ameleta chakula.
Akatoka
ndani ya maji, akajifunga taulo kubwa kifuani na kukimbilia mlangoni. Macho
yalimtoka, baada ya kukutana na Mzee Masha. Alirudia kufunga taulo lake tena na
tena huku mikono ikitetemeka.
“Unatokaje na taulo tu?” Masha aliuliza kwa ukali. “Nilikuwa
bafuni naoga, nikajua ni muhudumu analeta…” “Akiwa ni muhudumu ndio unatoka
uchi!?” Mzee Masha aliendelea kuuliza kwa ukali zaidi kitu kilichozidi
kumuogopesha Bella. “Sitarudia tena.”
Mzee Masha alisukuma mlango na kuingia ndani, akakaa.
“Umenichanganya hata sikumbuki nikitu gani
nilitaka kukwambia!” Mzee Masha aliendelea kulalamika. Bella
alifunga mlango na kubaki amesimama. “Ulijua
wazi kama ni muhudumu, tena wakiume, halafu ukatoka uchi! Unashida gani?”
Aliendelea kugomba. “Ni kweli
sikufikiria, nilikimbilia tu mlangoni bila kufikiria. Lakini sitarudia tena.”
Bella aliendelea kuomba msamaha kwa unyenyekevu sana. “Hebu vaa nguo.” Bella alichukua nguo zake na kurudi bafuni kuvaa.
Baada ya muda alitoka na kurudi kukaa kwenye kitanda.
“Samahani sana. Sitarudia tena.”
Bella aliamua kuvunja ukimya mara baada yakuona Mzee Masha amekaa kwenye kochi
akiwa bado na hasira. “Kuna safari ya
Dubai, kesho kutwa. Nataka twende wote.” Mzee Masha aliongea kwa kuamrisha
kidogo. “Dubai!?” Bella aliuliza kwa
mshangao kidogo, kwani alitegemea wazungumzie maswala ya shule yake, sio safari
nyingine. “Ndiyo, Dubai. Au ulitaka
safari yakurudishwa Kigogo?” Mzee Masha aliuliza kwa kejeli. “Sema kama ndiko unakotaka kwenda,
nikurudishe wewe na mdogo wako sasa hivi, mkaendelee kulala njaa.” Bella
alijisikia vibaya sana moyoni. Akainama chini. “Jiandae, kesho utakuja kuchukuliwa na Kasimu, upelekwe kutengeneza
hati yakusafiria. Umesikia Bella?” “Sawa.” Mzee Masha alisimama na
kuondoka. Bella alibaki amekaa pale kitandani akiwaza. Alijikunja taratibu na
kulala. Alishawapigia simu watu wamapokezi, wasilete chakula tena, kwani tumbo
lilijaa gafla mara baada ya maongezi yake na Mzee Masha.
*************************************
Aliamka asubuhi na
mapeka, akaoga na kubaki amekaa kwenye kochi akisubiria kuja kuchukuliwa.
Ilipofika saa nne, alikuja kuchukuliwa na Kasimu, akampeleka ofisi za uhamiaji.
Kwa kuwa yule dereva alikuwa akifahamiana na watu kadhaa pale ndani,
haikuchukua muda mrefu, Bella alipata hati yake yakusafiria. Akarudishwa
hotelini, akabaki amejilaza kitandani akiwaza. Bado hakuwa na hamu ya chakula.
Baada ya muda akiwa
amesinzia hapo kitandani, alisikia mlango unafunguliwa bila ya kubishwa hodi.
Bella aliogopa sana akajiweka sawa ili kumuona huyo anayeingia bila hodi, au
kufunguliwa, akadhani ni mwizi. Akashangaa kumuona Mzee Masha anaingia. “Shikamoo.” Bella akasimama. “Nimeamua kutafuta funguo yangu, ili niwe
huru kuingia hapa muda na wakati wowote ninaotaka.” Mzee Masha alikaa chini
baada yakuweka mifuko ya chakula mezani.
Chumba kizima kilikuwa
kikinukia kuku wakuchoma. “Nimekuletea
chakula, maana nimeambiwa tokea jana hujala kitu. Nilikuogopesha sana nini?”
Bella alibaki akimwangalia huku amesimama. “Kaa
chini ule. Lakini nataka ujue kuwa tokea mwanzo wa mahusiano haya, uwe
unajiheshimu. Sitaki uwe unajiacha uchi uchi au kuwa na mahusiano na wanaume
wengine.” Bella alishtuka sana. Maswali mengi yalipita kichwani mwake,
lakini aliogopa kuuliza kwani Mzee Masha hakuonyesha utayari wakumsikiliza hata
kidogo.
“Umenielewa Bella?” “Ndiyo.” “Nisiwahi kukusikia au hata kukukuta
na mwanaume yeyote yule. Nataka utulie kabisa. Umalaya, mwiko. Unaelewa?”
“Ndiyo.” Bella aliitikia. “Na ujue
sikutanii Bella. Ukianza ujinga tu, nitaenda kumtoa mdogo wako kule shuleni na
wewe nitakufukuza hapa, na nitahakikisha maisha yako yanakuwa magumu hapa mjini,
kuliko nilivyokukuta. Na hakuna utakachofanya nisijue. Popote utakapokuwa, au
chochote utakachofanya ujue nitajua
tu. Narudia tena, NATAKA UTULIE. Sasa kaa chini ule, nataka uwahi kulala, kesho
safari.” Taratibu sana, Bella akakaa.
Mzee Masha alisimama na
kuwasha tv kisha akapiga simu mapokezi aletewe sahani mbili, kisu na uma. Baada
ya muda mfupi sana muhudumu aliingia na sahani hizo, akaweka vyakula kwenye
sahani, Mzee Masha alichukua ya kwake, akaanza kula. Bella na yeye alivuta
chakula chake nakuanza kula kimya kimya. Mzee Masha alionekana kufurahia mpira
uliokuwa ukiendelea kwenye luninga. Alikula huku akiangalia mpira huo mpaka
ulipoisha. “Sasa ulale, kesho safari.”
Bella alinyanyuka kuondoa ile sahani aliyokuwa akitumia Mzee Masha, kwenye meza
ndogo pembeni ya kochi alilokuwa amekaa. “Mimi
naongea halafu haujibu kitu?” Mzee Masha alifoka. Bella alisimama
akimtizama bila kujibu kitu chochote. Mzee Masha akasimama, akaondoka bila hata
kumuaga. Mwili wa Bella ulianza kutetemeka asijue kama ni hasira au hofu. Baada
ya kusafisha pale, aliingia kuoga, na kurudi kulala.
*************************************
Hakuna usiku uliokuwa
mrefu maishani mwake kama ule. Hakuweza kufananisha na usiku wowote ambao alishawahi
kulala maishani mwake. Hata kwenye chumba cha Mat, kilichokuwa na mbu, joto na
harufu mbaya hakikumpa usiku mgumu kama ule aliokuwa amejilaza pale kwenye kile
kitanda cha kifahari na AC ikimpuliza. Alijigeuza kulia na kushoto mpaka palipo
pambazuka ndipo usingizi ulipompitia.
“Ndege inaondoka muda mfupi sana kuanzia sasa.” Bella alishtushwa na
Mzee Masha akiwa amemsimamia pembeni ya kitanda chake. Aliruka mpaka akaanguka
pembeni ya kitanda. “Nimekushtua sana?”
Bella hakujibu. “Pole. Lakini tunatakiwa
kuondoka muda huu.” “Nitajitahidi kujitayarisha kwa haraka. Shikamoo.” Mzee
Masha akatoa tabasamu bila ya kujibu ile salamu. Kidogo asubuhi hiyo alikuwa
amebeba uso wenye tabasamu.
Bella alisimama na
kuvuta taulo, akaelekea bafuni. Alioga harakaharaka na kutoka akiwa ameshavaa. “Sipendi hizo nguo zako. Haziniwakilishi
vizuri.” Bella alianza kujiangalia juu mpaka chini. “Hatuwezi kusafiri ukiwa hivyo. Itabidi tupitie sehemu, angalau upate
nguo moja ya kusafiria, na viatu ndipo tuondoke. Tukifika Dubai nitakuzungusha
kwenye maduka ya nguo nzuri, uchague.” Bella hakujibu kitu alikaa pembeni
ya kitanda akiwa kimya kabisa. “Upo
tayari?” “Ndiyo.” “Twende.”
Walikuta dereva akiwa
anawasubiri nje ya hoteli hiyo, sehemu ya kuegesha magari. Mzee Masha
alimfungulia mlango wa nyuma, Bella akaingia, akafunga mlango. Na yeye akaingia
upande mwingine. Wote walikaa nyuma. Bella aligeukia dirishani na kupotelea
mawazoni.
*************************************
“Ingia
humo ndani, ukachague nguo nzuri.” Alimshtua Bella ambaye hata hakujua kama walishaondoka pale
hotelini. Bella aliangaza vizuri macho. Akagundua wapo mbele ya Botique za
Kinondoni. “Na ninakuomba usichelewe. Tusije
tukakosa ndege.” “Sawa.” Bella aliitikia kwa upole. Akashuka na kuingia
ndani ya duka hilo la nguo. Wakati anachagua akashangaa kumuona Mzee Masha
amemsimamia nyuma yake. “Umepata
unachoona kinakufaa au hata hujui nini cha kununua?” Bella alinyamaza na
kendelea kutafuta. “Bella!” Aliita kwa nguvu kiasi ya kwamba kila mtu aliwageukia
wao. “Ndio natafuta.” Bella akajibu
taratibu na kubaki akimwangalia.
“Unajua
nini? Utanichelewesha wewe. Nimesahahu kuwa umetoka uswahilini, hujui hata nguo
za maana ni nini?” Bella alibaki
akimwangalia. “Samahani dada, naomba
msaidie huyu nguo moja nzuri, yamaana, ambayo atasafiria.” Mzee Masha
alimgeukia muuzaji. “Bila shaka.”
Alijibu na kusogea upande mwingine kulikokuwa kumetundikwa nguo. Baada ya muda
mfupi akatoa nguo tatu. “Karibu hapa
ndani ujaribishe.” Yule muhudumu alimgeukia Bella huku akimuashiria mlango
wa chumba hicho chakujaribishia nguo. Bella akamfuata nyuma bila yakusema
chochote.
Kila nguo ilimkaa
vizuri. “Umependeza na una umbile zuri
sana.” Yule muuzaji alimsifia Bella kila mara alipokuwa akitoka nje ya
chumba cha kujaribishia, kumuonyesha zile nguo alizokuwa amevaa nakumtaka
ushauri, ipi achukue. “Asante. Unafikiri
nichukue ipi?” “Hiyo jumpsuit yenye
nyeusi na nyekundu imekukaa vizuri zaidi. Chukua hiyo.” “Asante.” Bella
alitoka akiwa amependeza sana.
“Hiyo siitaki. Kila mtu atakuwa akikuangalia wewe! Imekubana sana
kwa chini.” Mzee Masha aliongea kwa sauti iliyojaa wivu na hasira kidogo, kila
mtu akamgeukia Bella. “Huyo mtoto, hata
umvalishe gunia, atakaa hivyohivyo. Chini mpana sana.” Mama mmoja mtu mzima
kidogo, ambaye Bella alihisi ndio mwenye duka aliingilia maongezi yao. “Mtachelewa bure huko muendako. Wewe nenda
tu baba yangu, hilo umbile halifichiki.” Kwa aibu Mzee Masha alilipia ile
nguo, akatoka na Bella akiwa amevaa ile nguo mpya na kiatu cha juu kidogo. “Asante kwa nguo.” Bella alishukuru mara
alipopanda kwenye gari. “Asante
kushukuru.” Mzee Masha aliitikia kwa ustaarabu sana kama sio yeye!
*************************************
Safari yakuelekea uwanja
wa ndege ikaanza. Kimya, hakuna aliyemuongelesha mwenzake. Walifika uwanja wa
ndege wakiwa hawajachelewa. Waliingia kwenye ndege, mara baada ya muhudumu
kusoma tiketi alizokuwa amepewa na Mzee Masha. Kisha wakaelekea upande wa ‘first class’. Bella alifurahia ule utulivu wa aina ya watu waliokuwepo huo upande
waliokuwepo. Wote walionekana ni watu wenye pesa zao, na hawakuwa watu wengi
sana. Palikuwa patulivu na Wahudumu waliwahudumia kwa heshima sana.
Alionyeshwa pakukaa,
akasogea moja kwa moja mpaka dirishani wakati Masha akitafuta sehemu ya kuweka
mzigo mdogo aliokuwa ameshika mkononi. Alivuta pumzi mara kadhaa huku
akizishusha taratibu, kisha akafunga macho. “Vipi?
Una usingizi?” Mzee Masha aliingia na yeye kwenye vile viti na kukaa
pembeni yake. Bella alitoa tabasamu lakinafiki na kunyamaza bila
kujibu lile swali. Alijirudisha nyuma kidogo, akajiegemeza vizuri, akageuzia
macho yake dirishani.
“Ulishawahi kupanda ndege zakutoka nje ya nchi?” Lile swali
lilimkera sana Bella, lakini ilimbidi ajibu tu. “Hapana.” Alijibu kwa sauti ya chini sana. “Kwa hiyo hii ndiyo mara yako ya kwanza kupanda ndege za kimataifa!?”
Alimuuliza tena kwa mshangao. “Ndiyo.”
Bella alijibu tena kwa upole kisha akageukia dirishani kuonyesha hayupo tayari
kwa swali jingine.
Nchini
Dubai!
Walifika Dubai, Bella akiwa amechoka sana,
haswa mawazo. Akili ilikuwa imemvurugika kupita kiasi. Alishadhalilishwa na
kunyanyaswa kihisia, kupita kiasi.
Waliingia kwenye taksii mpaka hotelini. Mzee Masha alisogea mapokezi, akaandika
vitu fulani mbele ya muhudumu akapewa funguo za chumba. Maswali mengi yalikuwa
yakiendelea kichwani mwa Bella, lakini aliogopa sana kuuliza.
“Twende juu. Chumba chetu kipo gorofa ya 10.” Bella alimgeukia kama
aliyeuliza swali. Akijua kabisa anachofanya, Mzee Masha alijitahidi kuonyesha uso
wa ukorofi ili kumuogopesha zaidi Bella, asiulize lile swali kwa sauti.
Walipofika gorofa ya kumi, Masha akaanza kutafuta chumba chao, kwani ilikuwa
hoteli kubwa sana, na kila gorofa ilikuwa na pande nyingi zilizokuwa na vyumba
vingi pia. Bella akaamua kukaa kwenye moja ya makochi waliyoyakuta katikati ya
vyumba hivyo hukohuko gorofa ya 10, wakati Masha akiendelea kutafuta chumba
hicho mpaka alipokipata ndipo alipomwita Bella. Walisogea mpaka mlangoni mwa
chumba hicho, akachomeka kadi mlangoni, na mlango ukafunguka. “Karibu ndani?” Bella aliingia na kukaa
kwenye kochi.
“Chumba changu ni kipi?” Bella alijikaza, akauliza. “Si hiki! Au ulikuwa ukitegemea nini?” “Sitegemei chochote, kwa sababu
pia sijui kwa nini tupo hapa?” Bella alijibu kwa ujasiri kidogo. “Huna shukurani kabisa wewe. Nakuleta Dubai
kupumzisha mawazo, badala yakushukuru, unasema nini!?” Mzee Masha alianza
kugomba, nakumuogopesha Bella. Alibadilika akawa mwekundu kwa hasira. Bella akabaki
akitetemeka pale kwenye kochi.
Alikuwa akisikia kutoka
kwa wanae vile yule Mzee alivyo mkorofi. Sasa leo ameangukia mikononi mwake,
hakuwa na ujanja. “Samahani, sikujua kama tupo hapa kwa ajili yangu. Naomba niingie
bafuni nioge, halafu nilale. Kichwa kinaniuma sana.” Bella alisimama na
kuingia bafuni.
Akiwa anaoga alishangaa
kumuona Mzee Masha na yeye anaingia mle bafuni akiwa uchi kabisa. Bella
alishtuka sana. “Nataka unisugue
mgongoni. Sijaoga vizuri muda mrefu sana. Mke wangu amekuwa na mambo mengi,
amekosa muda na mimi. Naamini mambo madogo madogo kama haya, hutashindwa
kumsaidia.” Bella alibaki ameshikilia matiti yake huku ameacha sehemu
nyingine zote wazi. “Au unaona shida
kunisaidia kusugua tu mgongo!? Maana kuna wanadamu wengine wameumbwa bila
shukurani. Unaweza kumsaidia jambo kubwa sana, yeye akashindwa kukufanyia kitu
kidogo tu!” Mzee Masha aliingia ndani ya maji, akajilowesha vizuri na kujipaka
sabuni. Bella alibaki anatetemeka pembeni ya bomba, akitamani afunge macho.
Bella alilingana umri kabisa
na mtoto wa pili au wamwisho wa Mzee Masha, Zera. Yaani alikuwa kama baba yake
wakumzaa. “Chukua hicho kitaulo hapo
pembeni ukipake sabuni unisugue mgongo.” Taratibu sana Bella alinyoosha
mkono huku akitetemeka sana. Akavuta moja ya taulo dogo kabisa yaliyokuwa
yamepambwa vizuri bafuni hapo. Maalumu kwa kujisugulia. Mzee Masha alikuwa
ametulia kimya na kumpa mgongo Bella. Alikilowesha, akanyunyuzia sabuni ile
yakuogea, na kuanza kumsugua taratibu mgongoni huku akitetemeka.
Alijifariji kumuona yule
Mzee amegeukia upande mwingine, kwa hiyo alijua hatageuka na kumwangalia.
Lakini baada yakumsugua kwa muda mrefu, Mzee Masha akamgeukia Bella. Bella
alirudi nyuma kwa haraka na kubaki wakiangaliana na Mzee Masha. “Unataka nikusugue na wewe?” “Hapana,
asante.” Mzee Masha akacheka. “Ona
anavyojidai kutetemeka. Unataka kuniaminisha kuwa eti unaogopa? Wenzako
wanalilia hata kunishika tu. Leo nimekupa bahati yakupanda ndege, nimekuvalisha
nguo za thamani, nakupa bahati ya kugusa mwili wangu, halafu unajidai unaogopa!
Acha unafiki wewe.” Bella alivuta taulo akajifunga nakutoka pale bafuni
bila yakuongeza neno. Alijikausha harakaharaka, akavaa nguo zake za kulalia
alizokuwa amenunua siku ya kwanza alipoenda kununua nguo na dereva wa Zera,
Kasimu. Akapanda kitandani huku akitetemeka.
Masha Amtoa Enabella Utotoni!
Baada ya muda, Mzee
Masha akaingia pale chumbani. Bella akafunga macho. “Unataka kula nini?” Mzee Masha akauliza lakini Bella akanyamaza,
akijidai amelala. Alipanda na yeye kitandani, akafunua shuka alilokuwa
amejifunika Bella, na yeye akaingia humo humo ndani. Wakawa wamejifunika shuka
moja. Akaanza kumpapasa taratibu, Bella akizidi kutetemeka mwili mzima kama
aliyekuwa akishikwa na mikono yenye baridi kali au kama aliyekuwa akitembewa na
barafu mwilini. Alionyesha wazi, lakini Mzee Masha hakujali. Aliendelea
kumpapasa mpaka alipofikia matiti yake. Akamgeuza taratibu nakuanza kumpandisha
gauni yake ya kulalia mpaka alipofika kifuani, mikono ikagoma kutoka hapo.
Ikaanza kuhama titi moja kwenda jingine, akiyapapasa matiti ya Bella taratibu
kwa hisia zote. Bella alibaki kimya kabisa. Alishindwa hata kujisogeza. Taratibu
machozi yakaanza kumtoka.
Kadiri alivyoendelea
kumpapasa ndivyo Bella alivyozidi kutoa machozi. Sauti ya shoga ya mama yake
ilianza kujirudia wakati akimsema mama yake kule kijijini walipoenda kumzika. Kama
aliyezidiwa na kitu wakati akichezea matiti hayo, akaamua kumtoa nguo yote
iliyokuwa juu kabisa ya matiti, karibu kabisa na shingoni. Wakati anamalizia
kumvua, Bella akakaa. “Naomba utumie
kondom.” Bella alijifuta machozi nakujifunika vizuri. Alibakiwa na chupi
tu, akavuta shuka na kujifunika. “Tafadhali tumia
kondom.” Bella aliongea huku akishindwa kujizuia nakujikuta akilia kwa
kwikwi.
Alikunja miguu yake na
kujiegemeza magotini mwake nakuendelea kulia. “Please!” Akarudia huku ameinama.
Alishindwa kumtizama Masha kwani alikuwa kama alivyozaliwa na yeye akionekana
yupo tayari kwa tendo. Bila kupoteza muda zaidi, Mzee Masha akatoka pale
kitandani, akavuta droo na kutoa kondomu. Alivaa harakaharaka na kurudi
kitandani. Alivuta shuka alililokuwa amejifunika Bella, akamvuta miguu kama
kumnyoosha, yeye akiwa amepiga magoti.
Alipofanikiwa kumlaza
chali ndipo akarudi kiunoni. Akampapasa kidogo tu nakuanza kumtoa chupi yake
taratibu. Aliishusha huku akimbusu kuanzia kiunoni, mapajani huku akishuka taratibu
akimbusu kadiri anavyovua ile chupi. Alipofanikiwa kuitoa yote, moja kwa moja
akarudi kifuani kwa Bella nakuanza kunyonya matiti yake. Napo alionekana ni
kama amelemewa hawezi kuendelea kwa muda mrefu, Bella akiwa amelala chali bila
hata kujitingisha au kujisogeza, ila kulia tu, Masha akajitahidi yeye mwenyewe
bila hata kuomba msaada, akamwingilia mtoto huyo ambaye bado alikuwa bikra
kabisa.
Bella alimsikia
akigugumia kwa hisia za ajabu, huku yeye akiendelea kulia. Akaendelea hivyo kwa
muda, akamuona anaongeza mwendo, huku akigugumia zaidi. Baada ya muda mfupi
sana, akamuona anaanza kupunguza mwendo, akatulia nakujilaza juu yake, kichwa
pembeni ya shingo yake kama anayetafuta pumzi. Akiwa ameweka uso wake shingoni
kwa Bella, pumzi zake zikitua kabisa kwenye shingo ya Bella, mkono wake wa
kushoto ulitulia juu ya hips la kulia la Bella. Alilipapasa taratibu huku
akihema kama kujiweka sawa baada ya shuguli nzito au kama aliyekuwa akikimbia.
Mikono yake iliendelea kutembea juu ya mwili huo kwa chini tu. Alifika kiunoni
na kurudi kwenye hips hilo, mpaka akatulia. Alijisogeza pembeni yake, akajilaza
na kupitiwa na usingizi mzito bila kuongea tena au kumgusa tena Bella,
aliyekuwa bado akilia kwa uchungu sana.
*************************************
Japokuwa Bella alikuwa mzuri
sana kwa kila kitu, lakini swala la wanaume au mahusiano ya kimapenzi
hayakuwahi kupita mawazoni mwake hata mara moja. Ukweli ule haukuwa wakati
alioona unafaa kufanya mapenzi. Tena kwa mtu ambaye siye mpenzi wake! Mbaya
zaidi ni kama alimbaka tu. Alifanya naye mapenzi bila hata kumuomba au
kumbembeleza. Zaidi ya yote alimuonyesha wazi anamdharau. Ilimuuma zaidi Bella.
Ni kweli alilelewa na
mama ambaye aliishi kwa kuhongwa sana na wanaume wa kila namna, lakini Tunu
alilinda sana watoto wake na kuwaambia kila wakati hasa Enabella kuwa yeye bado
ni mtoto mdogo sana, asifikirie swala la mapenzi hata kidogo. Kwa hiyo wakati
wote Bella alijiona bado ni mtoto, na mama yake ndiye aliyekuwa msiri wake mkubwa.
Aliongea na kuishi kile anachoambiwa na mama yake. Hakuwahi kuwaza juu ya maisha
au jambo lolote lile, mama yake ndiye aliyekuwa akiwaza na kufikiria kwa niaba
yake na kumpa yeye maelekezo ya kitu gani chakufanya. Kila mwanaume
aliyemtongoza, mtu wa kwanza kumwambia alikuwa ni mama yake.
Kwa hiyo Bella hakujua
mambo ya mapenzi, na kila mwanaume aliyekaa na Bella hata nusu saa tu, alikiri
Bella ana akili za kitoto. Kasoro darasani tu, ndipo Bella alipoweka heshima
shuleni hapo, nakumfanya hata Tunu ambaye hakuwa msomi, kuheshimiwa kwenye
shule hiyo iliyojaa watoto wa vigogo. Bella aliburuza madarasa yote, wakati
wote alikuwa akifaulu kwa alama za juu sana. Mwanzoni walihisi ni mtoto wa mtu
mmoja msomi sana, au wamezaliwa na mtu mmoja aliyevumbua kitu fulani, kwani
hata Eric alijulikana kwa utaalamu wa Kompyuta.
Tunu alihakikisha watoto
wake wanaishi maisha mazuri sana jijini. Sababu ya kuwalipia ada kubwa, na
kupanga nyumba maeneo ya gharama, na yeye hakuwa na kipato cha kueleweka
isipokuwa wanaume aliokuwa akitembea nao, Tunu hakuwa ameacha
urithi wowote kwa watoto wake zaidi ya hiyo elimu kichwani mwao. Hakuwa
amejiandaa kabisa na kifo chake. Kama mtu angemwambia Tunu angeugua na asipone,
asingeamini hata kidogo.
Alianza kuugua gafla, na
ni kweli aligua kwa muda mrefu sana kabla yakufariki kwake. Wakati mama yake ni
mgonjwa, hapo ndipo Bella alipoanza kuelewa maisha ni nini. Pesa alizokuwa
akizitapanya mama yake katika maisha yake na mdogo wake, zilianza kuisha,
wakabaki wakihangaika. Mama yake aliyekuwa akimpa maelekezo kipi cha kuuza ili
kuongeza kipato chao, alianza kupoteza kumbukumbu na kuwa kama amechanganyikiwa
kwa muda mrefu sana kabla ya kifo chake.
Alibakia Bella peke yake
akimuuguza mama yake, kwani hata msichana wa kazi aliyekuwa akiwasaidia kazi za
nyumbani aliondoka baada ya kukaa miezi miwili bila malipo na kugundua hakuna
dalili za kuja kulipwa tena. Pia aliingiwa na hofu baada ya kujua kwa hakika
gonjwa linalomsumbua tajiri wake au mama mwenye nyumba wake. Aliogopa asijefanya
makosa, akamuambukiza. Ndipo akaamua aondoke mapema akiwa mzima bila gonjwa,
kunusuru afya yake. Alimuacha Bella akimlilia abaki nao.
Ni Mat pekee, dereva wa gari hiyo ndogo aliyokuwa
amekabidhiwa na Tunu, ndiye aliyebaki kumsaidia Bella. Ndiye aliyekuwa akimpigia
simu hata usiku sana endapo akiona hali ya mama yake imebadilika. Naye Mat
hakuwahi kulalamika. Wakati wote alikuwa akifika hapo kwa haraka na kumsaidia Bella
kumpeleka mama yake hospitalini na kumrudisha baada ya kupewa huduma ndogo
ndogo. Kwani hata hospitalini kwenyewe walishindwa kumuweka kwa muda mrefu,
hapakuwa na matibabu yakumsaidia kabisa Tunu ila kumtuliza. Kwa hiyo muda
mwingi Tunu aliugulia nyumbani.
Akabakia Mat pekee kuwa
msaada wao. Ndiye aliyekuwa akiwaletea pesa kidogo, kila apatapo wateja, na
kumsaidia Bella kununua chakula na dawa za mama yake alizokuwa akitumia kwa
kila ugonjwa uliokuwa ukijitokeza zaidi kwa wakati huo. Viliibuka viugonjwa vya
hapa na pale mwilini mwa mama yake, na hivyo ndivyo Bella alivyokuwa akivitibu
mpaka kifo chake.
*************************************
Bella aliendelea kulia
kwa maumivu makali, huku damu nyingi zikimtoka. Alijinyanyua kwa shida sana
kutoka pale kitandani mpaka bafuni huku akiacha damu kitandani hapo na sakafuni
alikokuwa amepita. Hofu ilimuingia alipoona anazidi kuvuja damu asijue nini
chakufanya na nani wakumwambia. Hakujua kama damu ile inatokana na Masha kumchana
wakati wakufanya naye mapenzi au ndio kutolewa bikra yake! Mtoto huyo
aliyezoeshwa kubembelezwa na mama yake hata akijikata na wembe, usiku huo
ulikuwa usiku wa hofu kubwa zaidi. Damu zilikuwa zikitoka, maumivu yakimsumbua
akiwa peke yake bafuni. Aliendelea kulia kwa hofu, mwishowe alipoona anazidi
kumwagika damu na kuchafua kila taulo pale bafuni huku Masha akiwa amelala bila
hata habari, akaamua kuingia ndani ya sinki ya kuogea kusubiri hatima yake.
Kama ni kifo au kukatika kwa ile damu. Akabaki amekaa pale akilia peke yake.
Mawazo mengi ya hofu
yakaanza kupita kichwani mwake kwa mara moja huku akiona vile anavyokufa hapo
nchini Dubai na kumuacha Eric mdogo wake akiteseka peke yake. Akajua Masha
atamtoa kule shuleni na kuanza kuhangaika mtaani bila msaada wowote. Akamuona mdogo
wake akiwa mtaani akiomba omba huku usiku wahuni wakimwingilia kwa kumlawiti bila
huruma kama yeye alivyofanyiwa hapo na Masha. Tena aliwaona wanaume wengi
wakimng’ang’ania Eric sababu ya uzuri wa kike aliobeba mdogo wake. Alimuona
akilala usiku mtaani tu, tena kwa masaa machache sababu ya kuingiliwa na
wanaume wengi kila usiku bila yakumuhurumia. Hofu ilizidi kumjaa. Aliwaza hili
na like huku amejawa hofu mpaka akapata ‘Panic
attach’. Akapoteza fahamu pale pale kwenye sinki.
*************************************
Bella alishtuka
nakujikuta kitandani. “Pole Bella.”
Bella alijaribu kujigeuza kichwa chake taratibu kutafuta anaye msemesha,
akamuona Mzee Masha amekaa pembeni ya kitanda chake. Aliweza kujua kuwa hakuwa
amelala kwenye kitanda cha pale hotelini, kile chumba kilifanana na nyumbani
kwa mtu. Tena kidogo tu. Alitamani kuuliza, lakini alibaki akimwangalia Mzee
Masha aliyekuwa akimtazama kwa uso wa wasiwasi. “Unajisikiaje?” Mzee Masha akamuuliza tena. Wakati ananyanyua mkono
wake ili kujifuta machozi, akagundua amewekewa damu, akahisi yupo hospitalini.
Akarudisha mkono wake taratibu, nakufunga macho bila kutaka kujua nini
kilitokea, na alifikaje pale.
“Unataka nikulishe?” Akamsikia Mzee Masha akimuuliza
tena. Akiwa amefunga macho yake vile vile, Bella akatingisha kichwa kuashiria
kukataa huku machozi yakimtoka. “Hujakula
kitu chochote tokea jana Bella. Lazima ule chakula.” Bella alishangazwa na
ukarimu wa gafla wa Masha. Alikuwa akiongea kwa upole na upendo sana kama sio
yeye. Lakini Bella aliendelea kulia taratibu. Aligeukia ukutani akalala.
Alishtuliwa tena na
daktari aliyekuwa ameingia hapo akimwita kama kutaka atoke usingizini. “Enabella!” Akafungua macho kwani
haikuwa sauti ya Masha. “Unajisikiaje?”
Akamuuliza kwa Kiswahili kizuri na fasaha kitu kilichomshangaza Bella. Akajiuliza
daktari wa Kitanzania nchini Dubai! “Nipo
wapi?” Bella akauliza taratibu. “Nyumbani
kwangu.” Yule daktari akamjibu. Alizungusha macho kumtafuta Mzee Masha,
lakini yule daktari akamuwahi, “Ametoka,
amesema atarudi baadaye kidogo. Amekwenda kwenye kikao. Unajisikiaje?” “Nini kilitokea?” Bella akauliza. “Ulikutwa na Mzee Masha chumbani kwako,
asubuhi ya leo ukiwa umepoteza fahamu kwenye sinki. Amepoteza damu nyingi sana.
Lakini usiwe na wasiwasi, tumebahatika kupata damu, nimekuwekea, utakuwa sawa
tu. Nimekuwekea chupa moja, utaendelea kutumia vidonge baada ya hapo.”
Bella alifunga macho bila yakuongeza kitu. “Hapa
tunavyakula vya nyumbani pia. Kama utataka tukuletee chakula chochote kile
niambie, tutakutengenezea.” Bella alitingisha kichwa kukataa na kulala
tena.
Ilipofika usiku,
aliamshwa na kijana mwingine tena, aliyekuwa na bakuli la supu. “Nimekutengenezea hii supu. Naomba ukae
unywe.” Bella alibaki akijiuliza yule ni nani tena! Alibaki akimtizama kwa
muda bila kupata jibu, kisha akafunga macho. “Lazima ule Bella. Nikusaidie ukae ili ule?” Bella hakujibu.
Taratibu aliona machozi yanatoka pembeni ya macho ya Bella. Palizuka ukimya wa
muda, gafla mlango ukafunguliwa. “Vipi
bwana mdogo Elvin, Kaka yako yuko wapi?” Bella alisikia sauti ya Mzee
Masha, lakini hakutaka kufungua macho. “Shikamoo.
Umetoka kwenda kazini kwake, amepigiwa simu kuwa kuna dharula, ‘emergency’.
Lakini amesema atarudi pindi atakapomaliza. Nimeleta hii supu kwa mgonjwa.”
“Asante sana. Weka tu hapo mezani, atakunywa akiamka.” Bella alikuwa
akisikiliza kila kitu, lakini aliamua kujifanya amelala. Elvin alivuta meza pembeni
ya kitanda alicholalia Bella, nakuiweka ile supu.
“Vipi lakini shule?” Masha alimuuliza yule kijana, aliyemtaja kama
Elvin. “Ndio nipo likizo.” “Mwaka wa
ngapi sasa?” Mzee Masha aliendelea kuhoji. “Nipo wapili.” “Naona mama amekung’ang’ania kweli!” Elvin alicheka.
“Hata kuja huku kwenyewe kwa kaka,
ilikuwa shuguli kweli! Hataki nitoke pale nyumbani.” “Anakuwa mpweke. Anaona watoto wote wameshakuwa wakubwa wanamkimbia
pale nyumbani, inabidi akung’ang’anie wewe.” Elvin alicheka. “Utarudi lini sasa?” “Nimetoka kuongea naye
muda si mrefu, anataka nirudi nyumbani kwa kisingizio eti nikamsaidie Mzee kazi
ofini kwake, lakini najua yeye ndio anataka nirudi.” Mzee Masha akacheka
kidogo. “Lakini nitarudi tu, sitakaa sana
hapa.” “Safi sana. Naona na Mzee wako anakusifia sana.” “Hahahaha!” Elvin
alicheka tena.
“Wewe si unamjua baba? Anafurahia ninavyomsaidia kazi zake pale ofisini
kwake, halafu hanilipi mshahara, anaita posho, ili nisilalamike.” Wote wakacheka. “Kuna chakula kidogo. Utapenda kula kitu
chochote?” Elvin alimuuliza Mzee Masha. “Hapana,
asante sana. Nataka nikawahi kulala, naona huyu nitamuacha hapahapa, nitarudi
kumchukua kesho asubuhi nikishatoka kwenye kikao.” “Ndivyo mlivyokubaliana na
Eno?” “Aliniambia anatakiwa kupumzika angalau siku moja zaidi ili apate muda
wakumwangalia, kesho tunaweza kuondoka.” “Okay.” Elvin alitoka nakumuacha
Mzee Masha ndani ya kile chumba.
“We Bella! Bella! Amka ule.” Mzee Masha alimuamsha
Bella. “Nitakula baadaye.” “Itabidi
niondoke, nikuache hapa kwa ajili ya matibabu. Kesho nina kikao cha asubuhi
sana, lazima niwahi kulala, nikitoka huko nitarudi kukuchukua.” “Sawa.”
Bella alijibu nakufunga macho. Palizuka ukimya wa gafla, mwishowe Bella akasikia
mlango ukifunguliwa na kufungwa. Akajigeuza ukutani na kupotelea usingizini.
*************************************
“Ni leo tu, kesho
ataondoka.” Kwa
mbali akiwa anatoka usingizini, Bella alisikia watu wakiongea nje ya
chumba alichokuwa amelala. Lakini haikuwa sauti ya Mzee Masha. “Usiwe na
wasiwasi Eno. Mimi nipo sawa tu. Nikisikia usingizi nitalala hata hapo kwenye
makochi.” “Unauhakika?” “Mbona unawasiwasi?” “Namjua mama yako. Akipiga simu,
halafu akajua kama nimegawa chumba chako, huna pakulala, anaweza kuja kukufuata
mwenyewe.” Wote wakacheka.
“Ameshanipigia simu
anataka nirudi nyumbani.” “Hata mimi amenipigia, ananiomba nisikuweke sana
huku. Umeamuaje?” “Itabidi nirudi tu. Kuna kitu namalizia hizi siku mbili tatu,
nitarudi nyumbani. Sitaki kuendelea kumtesa. Najua huko halali vizuri.” Bella aliendelea
kuwasikiliza. “Amekula kitu chochote?” “Hapana. Naona amekataa kabisa. Hata
supu niliyompelekea amekataa kuinywa.” Elvin alimjibu kaka yake, Eno. “Ngoja nikamwangalie.” Bella
alisikia hatua za miguu zikisogelea mlango wake, kisha ukafunguliwa.
“Vipi Enabella?” Bella akafungua macho na kukutana na Eno,
ambaye alijua ndiye atakuwa daktari. “Nataka
kwenda chooni.” “Utaweza kwenda mwenyewe? Nasikia hujala kitu chochote. Lazima
ule, lasivyo kizunguzngu kitakusumbua sana.” “Nitaweza kwenda chooni mwenyewe.”
Eno alisogea, akafunga ile damu na kutenganisha ule mrija uliokuwa ukipitishia
damu ili aweze kwenda chooni bila chupa ya damu. Akampisha ilia toke pale
kitandani.
Bella alijikaza mpaka
chooni. Yalikuwa nimateso makubwa sana wakati akijisaidia haja ndogo. Alisimama
akiwa analia peke yake pale chooni. Wakati alipokuwa akifanya naye mapenzi, Mzee
Masha alimsababishia madonda. Hakumtayarisha kabisa. Alimparamia huku akijua
wazi Bella anahofu. Alifanya naye mapenzi kwa pupa, tena bila huruma.
Alimuumiza sana, hasa kwa kuwa ilikuwa mara yake ya kwanza. Alilia pale chooni,
akaamua arudi tu chumbani akalale.
Alirudi chumbani akiwa amejawa
machozi mengi sana usoni. “Pole sana
Bella.” Eno alijaribu kuongea kwa upendo, lakini Bella hakujibu kitu. Akapanda
kitandani na kufunga macho huku akifuta machozi yaliyokuwa yakiendelea kumtoka.
Eno alirudisha ule mrija wakupitisha damu mkononi kwa Bella, akafungulia damu
tena, nakuondoka pale chumbani.
Eno alitoka na kusimama
nje ya mlango, akabaki akifikiria. “Vipi?”
Alimsikia Elvin akimuuliza. “Sijui bwana!
Ngoja mimi nikalale. Nitarudi usiku kuangalia hiyo dripu kama itaisha ili
nimtoe.” “Usiwe na wasiwasi, mimi
bado nipo hapa naandika, nitakuwa nikimwangalia. Kama kuna tatizo nitakugongea,
au dripu ikiisha pia nitakuja kukuamsha. Wewe kapumzike tu.” “Hapo utakuwa umenisaidia.
Nimechoka sana na kesho nipo ‘on call’ sijui nitaitwa saa ngapi! Kuna upungufu
wa madajtari huko. Najua nitaitwa tu. Acha nikapumzike kidogo. Usiku mwema.”
“Na wewe.” Bella alisikia wakiagana.
“Elvin kwa
Bella.”
Baada ya muda kidogo kupita
Bella akasikia mlango unafunguliwa, lakini hakutaka kufungua macho. “Nitakuwa hapa kwenye meza nikifanya kazi
zangu kwenye kompyuta. Ukitaka kitu chochote unaweza kuniambia.” Elvin
alivuta kiti akakaa, lakini Bella hakujibu kitu. “Nikuzimie taa?” Bella hakujibu kitu. Elvin aliendelea na shuguli
zake kwenye kompyuta yake kimyakimya tu mpaka
baada ya lisaa, akamsogelea Bella. “Nikusindikize
kwenda kupiga mswaki kabla ya kula?” Bella akaanza kulia tena. “Upo mswaki mpya pale chooni, twende
nikuonyeshe ili usugue meno wakati nakupashia moto supu yako.” Sio kwamba
njaa haikuwa ikimuuma Bella, lakini alijawa na hasira na uchungu mwingi sana
moyoni, kiasi cha kushindwa kula.
“Twende!”
Elvin alirudia tena. Bella alikaa kidogo kama akifikiria, mwishowe akasimama.
Elvin alimbebea ile dripu ya damu, mpaka chooni akaitundika mlangoni. Alimuacha
akiwa anaosha uso na kupiga mswaki, yeye akaingia jikoni. Baada ya muda
alimfuata bafuni nakubaki akimsubiria, kwani Bella alikuwa akipiga mswaki huku
akilia sana. Elvin alibaki kimya, asijue aseme nini. Alimaliza, wakarudi
chumbani. “Usilale sasa. Kula kwanza.”
Bella alishusha miguu kutoka kitandani na kuanza kula taratibu.
Alikunywa ile supu mpaka
akamaliza yote. “Asante.” “Karibu.
Ungependa nikuongezee kitu chochote? Juisi, maji au maziwa?” “Maji, tafadhali.”
Bella alijibu, Elvin akatoka na kurudi na maji. Alipomaliza kunywa yale maji,
Bella alirudi kulala, mpaka aliposikia mtu akimvuta mkono. Alishtuka sana,
akakaa kwa haraka, akajivuta mbali kabisa, ukutani, huku akitetemeka. “Pole na samahani. Sikutaka kukuamsha. Nataka
nikutoe hiyo dripu. Imeisha.” Alikuwa Eno. Bella alimtizama kwa muda,
akafuta machozi, kisha akanyoosha ule mkono uliokuwa na sindano. “Samahani sana.” Eno alirudia baada
yakuona vile Bella alivyoshtuka. Bella aliendelea kujifuta machozi.
“Kesho utajisikia vizuri.” Eno aliongeza huku akitoa plasta zilizokuwa
zimezunguka ile sindano, mkononi mwake. “Itauma
kidogo, wakati nazitoa hizi plasta, lakini haitachukua muda mrefu.” Eno
aliongeza, huku akipiga miayo, akiashiria wazi ana usingizi. Alimtoa na
kurudishia plasta moja pale alipochomoa sindano kuzuia damu isitoke. “Pole sana Anabella. Unaweza kurudi kulala.”
Bella alibaki amejikunyata kwenye kona yakitanda, huku ameangalia chini. Eno
akasimama kwa muda akimtizama Bella, mwishowe akaamua kuondoka. “Usiku mwema Elvin.” “Asante na wewe.”
Elvin bado alikuwa mezani akiandika.
Baada yakumuona Bella
ameshindwa kurudi kulala, akaamua kuvunja ukimya. “Nikuwekee nini kwenye luninga?” Elvin alisimama na kuwasha tv. “Kuna sinema nyingi tu hapa, mpaka za wanyama.”
Alijua wazi asingejibiwa, lakini Elvin aliamua kuuliza tu. Alitafuta DVD
akaweka. “Jilaze vizuri, uangalie mpaka
utakapopitiwa tena na usingizi.” Bella alijinyoosha vizuri na kujifunika
shuka. “Nyanyua kichwa nikuwekee mto ili
uweze kuangalia luninga vizuri.” Bella alikaa vizuri, Elvin akamwekea mto
vizuri. “Unaweza kulala sasa.” Bila
kusema chochote, Bella alirudi kulala na kugeukia luninga. Aliangalia kwa muda,
mwishowe alisinzia. Elvin alisimama na kumfunika vizuri, akazima taa, akarudi
kukaa kwenye kiti chake, akitumia taa ya mezani bila ya kuwasha taa kubwa ili
asimsumbue mgeni huyo ambaye ni mgonjwa. Sababu ya kushiba vizuri, Bella
alipitiwa na usingizi mzito sana mpaka alipoamshwa na Mzee Masha tena.
“Twende. Utaenda kuoga hukohuko hotelini.” Bella alikaa kwa shida
sana. Hakutaka hata kumwangalia Mzee Masha usoni. “Asanteni sana kwa msaada wenu.” Mzee Masha alimshukuru Eno huku
akimkabidhi hundi. “Hapana Mzee Masha.
Hatuwezi kulipana bwana. Sisi ni ndugu.” “Acha uswahili Eno. Unafikiri kazi ya
pesa ni nini? Lazima izunguke ili inirudie. Sasa kama tusipojua kuenzi vya
kwetu, unafikiri wageni watatuthamini kweli? Wewe ndio umeanza maisha, upo
ugenini huku, unahitaji pesa. Chukua hii pesa.” Eno alicheka kidogo huku
akipokea. “Asante sana.” “Mimi ndio nawashukuru
nyinyi zaidi. Asante sana” Masha aliongea kwa tabasamu kubwa usoni. “Sasa Elvin?” Alimgeukia Elvin. “Ndio Mzee!” “Najua sisi tutaonana mjini.
Usije ukazamia huku.” Elvin akacheka. “Siwezi.
Nitarudi kusaidia wazee.” “Haya bwana.” Mzee Masha alimgeukia Bella. “Upo tayari?” “Ndiyo.” Bella alijibu kwa
sauti ya chini, wazi alionyesha anamuogopa Mzee Masha. “Simama sasa twende! Unasema upo tayari wakati umekaa?” Bella
alisimama na kutoka mle chumbani. Aliwaacha wote wakiwa chumbani,
wakimsindikiza kwa macho.
Masha na Bella.
Walipofika tu hotelini
chumbani kwao, Bella aliingia bafuni moja kwa moja. “Nikusaidie kuoga?” Mzee Masha aliingia bafuni. “Asante, lakini nitakuwa sawa tu.” Bella
alitamani yule Mzee aondoke pale bafuni na kumuacha peke yake, lakini alibaki
akimkodolea macho mpaka alipomaliza kuoga. Akatoka nakurudi kitandani. “Kabla hujalala, nataka nikupongeze kwa
kujitunza. Nimefurahi sana mimi kuwa mpenzi wako wa kwanza. Nimeamua
kukutafutia zawadi nzuri.” Alisimama na kusogelea meza. “Dhahabu za Dubai ni nzuri sana, na ni za
viwango vya hali ya juu.” Bella alibaki ameinama. “Na huna haja yakuogopa, yaliyokupata ni mambo yakawaida kabisa, kadiri
tutakavyoendelea ndivyo utakavyozoea, kwa hiyo usiogope. Na nina kuahidi,
wakati mwingine nitakuwa mwangalifu sana ili nisikuumize. Juzi ilitokea bahati
mbaya sababu yakuchoka na sikuwa najua kama hujawahi kulala na mwanaume
mwingine. Nitakutafutia mtu mzima kidogo, mwenye uelewa na mambo hayo
atakufundisha kila kitu, usiwe na wasiwasi.” Mzee Masha alirudi kitandani
akiwa na kimkoba kikubwa mkononi. “Umenisikia
lakini?” Aliuliza kwa ukali kidogo. “Ndiyo.”
Bella alijibu. “Hizi ni moja ya zawadi
nyingi na za thamani, zinazokujia.” Alimpa cheni ya shingoni, mkononi na
mguuni, kulikuwa na hereni pia. Na kweli vilionekana ni vitu vya thamani sana.
Kila kimoja wapo kilikuwa na uzito wa kutosha.
“Kwa uzuri ulio nao, na heshima uliyonipa, lazima nitakutunza
vizuri sana Bella. Nitakufanya uwe mrembo katika jiji zima lile la Dar.
Nitahakikisha unaishi kwenye nyumba nzuri sana na kutembelea gari la kifahari.
Nakuapia Bella utafaidi kuliko wanawake wote hapa duniani, ilimradi tu ufuate
masharti yangu. Ukikiuka au ukinizunguka, au hata nikihisi kuna mwanaume
mwingine katikati yetu, utajuta kuzaliwa Bella. Nitaanza na wewe, kisha
nitamaliza kwa mdogo wako. Dunia itasahau hata kama mlishawahi kuwepo hapa
duniani.” Bella alistuka sana. Akamtazama machoni.
“Mbona unashtuka? Ulipanga unikimbie nini?” Bella alikaa kimya. “Mimi ni wako Bella. Tena wakufa na
kuzikana, hakuna wakututenganisha tena.” Mzee Masha alijivuta karibu na
alipokuwa amejiegemeza Bella, akamkumbatia. “Nakupenda
sana Bella.” “Naomba nilale kidogo.” Bella alijitoa mikononi mwa Masha. “Kweli unatakiwa kupumzika. Usiwe na
wasiwasi Bella. Lala ukijua mimi nipo hapa pembeni yako. Ukiamka tunakwenda
kuzunguka madukani kutafuta vitu vyako.” Bella alijivuta pembeni, akajilaza
akiwa amekunja miguu yake. Mzee Masha alimsogelea, akalala pembeni yake huku
amemkumbatia. Bella alikuwa akitetemeka huku ameshikilia dhahabu alizo zawadiwa.
“Usiku wa jana umekuwa mrefu sana Bella.
Umelala mbali na mimi. Nimefurahi umerudi.” Mzee Masha alijaribu kumtupia
neno Bella, wakiwa wamelala. Lakini Bella alibaki kimya akiwa amefunga macho
yake, amegeukia upande mwingine akilia taratibu. Baada ya muda kidogo alimsikia
Mzee Masha, akihema kama aliyepitiwa na usingizi.
*************************************
Mambo ndio
kwanzaaa yanaanza. Masha ameahidi ni ‘mpaka kifo ndio kiwatenganishe’. Amemuonya asiwaze hata
kumtoroka.
Usikose Sehemu
ya 3.
0 comments: