Story
“Nipeleke kitandani.” Mzee Masha alijaribu kumshika lakini alimtonesha. “Niache T. Unazidi kuniumiza.” “Wapi?” “Umenivunja mbavu mbili za upande wakushoto na kupasua mirija ya damu. Imebidi kufanyiwa upasuaji japo sio mkubwa lakini nina mshono upande huo huo.” “Basi ngoja nikushike upande wa kulia.” Bella alizidi kumchukia Mzee Masha. ‘Anashindwa hata kusema pole.’ Bella alianza kulia.
Baada ya muda akarudi. “Umemsumbua mdogo wako bure! Alikuwa amelala hana hata shida, imebidi aamshwe sababu hutaki kusikiliza kila ninacho kushauri.” “Naomba dawa ya maumivu.” Mzee Masha alimpa Bella dawa ya maumivu. Akapanda kitandani na yeye akalala pembeni ya Bella. “Unajua nilirudi hapa Tanzani kwa ajili yako Bella?” Bella akanyamaza. “Nimeahirisha mambo mengi sana, yanayohusu familia ili nije kuwa na wewe, halafu nafika hapa na wewe haupo ulikuwa unazurula, mpaka saa tano za usiku! Ndio maana nilikasirika sana.” Bella hakujibu kitu alibaki kimya.
Mke wa Mat aliogopa sana, huku analia, akampigia simu Mat. Eric aliingia mle ndani baada yakusikia dada yake analia huku anafanya fujo mle ndani. Alimkuta dada yake kama amechanganyikiwa. “Bella! Hey Enabella! That’s enough. Stop it!” Eric alimshtua dada yake. Bella akasimama huku anahema nakulia kwa uchungu sana. Watu walishajaa. Alitoka nje, akakusanya vyombo alivyokuwa akiosha mdogo wake, akatafuta jiwe akaanza kuvivunja, huku akitupa vijiko, visu na vyombo vyote vya plastiki.
“Mbona kama wewe una kazi nyingi kuliko wote?” Eric alimuuliza Elvin wakati wanazunguka. Elvin akacheka. “Nafanya kazi mbili kwa wakati mmoja. Namsaidia na baba yangu. Yeye ndio mwenye hii kampuni, na mimi nimeajiriwa kama Bella.” “Unaingia kazini saa ngapi?” “Mimi ndio mtu wa kwanza kufika hapa ofisini. Lazima saa kumi na mbili niwahi kufungua mlango.” “Ni sawa na mimi nikifika kesho muda huo, nione kazi unazofanya, tangia asubuhi?” “Hamna shida.” Walirudi ofisini kwa Elvin, Eric akiwa amejawa furaha sana.
“Twende tukale Eric.” Bella aliona aondoke tu, kwani ni kweli alikataa kwa nguvu sana na kumshtua kila mtu. “Twende wote Elvin.” Eric naye akamgeukia Elvin. “Sijawahi kumuona Bella anatoka kwenda kula mchana. Sijui hata kama anajua panapouzwa vyakula.” Bella alitabasamu. “Ningemkimbiza City Garden mara moja, napafahamu.” Elvin alibaki akimshangaa. “Kwa nini ukalipe mapesa yote hayo!? Twendeni niwapeleke mkale chips vumbi.” Wote walicheka na kuondoka.
“Mtaweza kula hapa au mnataka tukale ofisini?” Elvin akauliza. “Umesema leo tunakula chips vumbi, tule hapahapa kwenye vumbi.” Bella alijibu nakumfanya Elvin amwangalie huku akicheka. “Naona Bella huyu wa sasa ni bora zaidi.” “Jamani Elvin! Bella yupi sio mzuri?” “Yule anayevaa sura ya kazi kila wakati. Sijawahi kukuona ukicheka hivi Bella!” Bella alicheka tena na kuendelea kula. Waliendelea kula huku wakicheka, Eric ndiye alikuwa na furaha sana. Elvin alimuona vile Bella alivyokuwa akimtizama mdogo wake kwa makini huku akimuuliza maswali kila wakati. Kama anataka amuongeze hiki au kama amependa hicho chakula, au kama chakula kitamu. Alimuona vile akili zake zote zilivyokuwa kwa mdogo wake, akajua ndipo furaha yake ilipo.
Walipokuwa wakiingia tu ofisini huku wamejawa vicheko, walikutana na Irene pale mapokezi. Sura yake haikuwa na furaha hata kidogo. “Nimekupigia simu zaidi ya mara tano hujapokea.” “Niliacha simu ofisini, pole. Vipi lakini?” “Unaachaje simu ofisini sasa!?” Irene alionekana kukasirika. “Tuliongea muda sio mrefu Irene, na tukakubaliana nikitoka kazini nije nyumbani kwenu. Sikujua kama utapiga tena. Pole.” Bella alipoona hali sio shwari alimshika mkono Eric. “Twende ofisini kwangu.” Bella na Eric waliondoka na kuwaacha Elvin na Irene pale mapokezi wakiendelea kuongea.
“Ulikuwa wapi?” Bella alisikia Irene akimuhoji Elvin. “Nilienda nao kula. Yule ni mdogo wake Bella, amekuwa akinisaidia kazi siku nzima leo. Nikaona nimpeleke kula. Vipi Irene? Mbona kama umekasirika?” “Nashangaa nakupigia simu hupokei, kumbe umetoka kwenda kula na Bella. Kwanza tokea lini mmeanza kwenda kula pamoja?” “Naomba twende tukaongelee ofisini, Irene.” “Kwani unaficha nini?” “Tunasumbua watu maofisini kwao, Irene. Tuliposimama hapa, kila mtu anatusikiliza sisi. Naomba tuingie ofisini kwangu.” Irene alibaki amesimama. “Tafadhali Irene.” Waliingia ofisini kwa Elvin, pakawa kimya.
Wakati Bella anafunga ofisi yake, naye Elvin alitoka ofisini kwake akiwa na Irene. Eric aliwasogelea. “Samahani, mimi ndio nilimkaribisha Elvin kula naye chakula cha mchana. Naomba usimlaumu Bella.” Bella alishtuka sana. “Bella alitaka niende naye mimi tu, lakini kwa kuwa mimi nilikuwa na Elvin tokea asubuhi tukifanya wote kazi, nikaona nimkaribishe chakula. Sio Bella. Usimlaumu Bella. Bella hana kosa.” “Usiwe na wasiwasi Eric, kila kitu kipo sawa. Hukukosea. Na mimi nilifurahia tumepata muda wa pamoja. Usisahau kesho umeniahidi utakuja asubuhi ya saa 12 tuanze kazi pamoja.” Ilibidi Elvin amjibu kwa utani kidogo, kwani Irene alibaki kimya akimwangalia wakati Eric anamtetea dada yake. Eric alicheka kidogo. “Bella amesema atanileta.” “Sawa. Muwe na usiku mwema.” Elvin aliaga huku akimtizama Bella aliyekuwa amesimama kimya akimwangalia mdogo wake. “Asante.” Bella alijibu kwa hofu kidogo. “Twende Eric.” Bella alitangulia mlangoni, Eric akafuata.
“Sasa akisikia au kumuona mtu anamchukia au kumfanyia ubaya wowote, anaumia sana. Anazidi kuamini kuwa watu hawatupendi, wanatuchukia. Maana alishawasikia hata ndugu zake mama kipindi cha msiba wakitusema vibaya sana na zaidi walitukana mbele za watu. Hawakutaka kutuchukua wakatuacha pale pale kijijini tulipokwenda kumzika mama. Baada ya mateso ya pale tulipokuwa tumeachwa peke yetu kijijini kuwa makali sana, tukaamua kurudi huku mjini kwenye nyumba tuliyokuwa tukiishi na mama, kabla hajafariki. IIikuwa ni nyumba ya kupanga. Tulifika hapo usiku sana, tukiwa na njaa na hatujui pakulala. Tulikuta hiyo nyumba ilishapata mpangaji mwingine na vitu vyetu vyote vimeuzwa. Nilimuomba huyo mama tuliyemkuta, angalau atupe chakula cha Ric tu, lakini alikataa na kutufukuza pale, tukaenda kukaa nje ya geti, mbu walikuwa wakitung’ata, na Ric alikuwa akisikia wakati namuombea chakula. Anamaumivu mengi sana moyoni, amekuwa akishuhudia mambo ambayo yeye hawezi kumfanyia mtu, tukifanyiwa sisi. Na…” Bella alifuta machozi.
Akaamua kuwapigia simu wazazi wake kuwataarifu. “Hivi na sisi tupo njiani tunaelekea huko hospitalini. Mama yake ametupigia simu alikuwa analia sana. Nahisi hali yake ni mbaya sana.” Mama yake Elvin alimjibu, akisikika anawasiwasi sana. “Na mimi nitakuja huko muda si mrefu, ngoja nifunge ofisi.” Elvin alifunga ofisi, akaelekea hospitalini.
Mama yake akamsogelea. “Pole na kazi.” Elvin alishukuru Mungu, maana alikuwa ni kama ametegwa. “Asante mama. Vipi na wewe? Unajisikiaje?” “Leo nimeshinda nimelala tu. Najisikia vizuri.” Wakati wanaongea, kaka yake Elvin naye akaingia. “Vipi Dogo?” “Shikamoo.” “Marahaba. Poleni bwana. Mimi ndio nimepata taarifa sasa hivi, wife yupo njiani na yeye anakuja. Vipi anaendeleaje?” “Ndio madaktari wanahangaika humo ndani, naamini kila kitu kitaenda sawa.” Alimgeukia mama yake. “Shikamoo mama.” “Mbona midomo imekukauka hivyo!? Umekula kweli wewe?” Mama Mwasha alimuuliza mwanae mkubwa. “Mambo yalikuwa mengi, sijala. Nitakula baadaye nikifika nyumbani.” Mama Mwasha aliendelea kuongea na wanae mpaka daktari alipotoka kuongea nao.
“Kwani nyinyi, ni nani aliwaambia amekunywa sumu?” Mama Mwasha aliuliza. “Mimi nilikuta kikaratasi alichokuwa amekiandika, ni bora afe kuliko kumkosa Elvin, na yeye alikuwa amelala na kujifunika shuka mpaka kichwani.” Msichana wa kazi alijibu, kwa kuwa wazazi wa Irene na ndugu zake walikuwa wameingia ndani kumuona Irene. Wengine walianza kucheka kimya kimya.
Bella alikodisha vyumba
viwili vizuri sana kwenye hoteli hiyo ya Malaika Beach Resort, iliyojengwa
ndani kidogo ya Ziwa Victoria. Ilikuwa ni hoteli nzuri na ya kitalii. Hata
muonekano wake tu, ungejua binti huyo alimwaga mapesa yakutosha ili
kumfurahisha tu mdogo wake, ambaye tayari alishaonekana kupoteza ladha ya
kuwepo kwenye madhari ile.
Waliingia chumbani hapo akajitupa kwenye kochi bila hata kuzunguka na kuangalia madhari ya mle ndani chumbani kama kawaida yake ya kupenda kuchunguza kila sehemu mpya anayofika. Bella alimuomba yule muhudumu amsaidie kuingiza vitu vyote upande wa chumbani akarudi kukaa pembeni ya mdogo wake. “Tutakuwa na wakati mzuri Ric, naamini hivyo. Wakati wote tumekuwa na furaha tukiwa pamoja.” “Naamini hivyo Bella. Nataka nioge kwanza kabla yakulala.” “Nimebeba movie nzuri, tuangalie kabla ya kulala.” Ric akakubali. Wakaoga kisha wakapanda kitandani, na kuanza kuangalia movie yao.
Movie ikiwa katikati walisikia mtu akigonga. “Umeagiza kitu mapokezi?” Bella alimuuliza mdogo wake. “Hapana.” Mlango uliendelea kugongwa. Bella akajua atakuwa Mzee Masha tu. Akasimama haraka ili yeye ndio awe wakwanza kufungua na kumkabili kabla Eric hajamuona.
Alipofungua mlango
alibaki ametoa macho. Taratibu machozi yalianza kumtoka Bella huku ameziba
mdomo wake kwa mikono yote miwili. “Are you okay Bella? Ni nani?” Eric
alimuuliza dada yake baada ya kuona mlango umefunguliwa kisha pakawa
kimya. “Bella?” Eric alirudia tena, lakini Bella alikuwa
kwenye mshtuko ulimfanya ashindwe kuongea. Alijisogeza karibu kabisa na Elvin
akiwa bado nje ya mlango akamkumbatia huku akilia. Eric alipoona kimya, akaamua
kwenda kutizama, kwa kuwa Bella alichukua 'suit room'. chumba
kilichokuwa na sebule kabisa kwa hiyo ilikuwa ngumu ukiwa chumbani kuona
sebleni kwa urahisi.
Walirudi chumbani haraka, kila mmoja akabadili nguo, Bella alivaa gauni harakaharaka akatoka. “Hujachana nywele Bella!” Eric alimuwahi dada yake wakati anatafuta viatu vyake avae. “Who cares?” Bella alijibu huku anacheka. “Bella!!” Eric alimshangaa dada yake huku akicheka. “Yupo sawa tu, twendeni.” Bella alifurahi kuona Elvin hana shida kutoka naye vile alivyo. Hata hivyo hakuna jinsi Bella akaonekana asivutie kumwangalia. Alikuwa na kila kitu kizuri, kinachofanya urudie kumwangalia tena na tena. Lakini angekuwa na Masha, asingeruhusu atoke vile hata kidogo. Wakati wote Masha alimtaka awe msafi na kila kitu mwilini mwake kimuwakilishe vizuri. Wakati wote Bella alikuwa na kucha zilizotengenezwa vizuri, nywele safi tena zilizotengenezwa kwa ufasaha, na mavazi nadhifu, yaani kila kitu chake kilitakiwa kiwe kizuri. Na alienda kutengeneza kwenye saluni zamaana, sio uswahilini.
Waliingia chumbani kwao wote wakiwa wamejawa vicheko. Walicheka hata vitu visivyo na maana. Walikuwa wakicheka mpaka machozi ya furaha yalikuwa yakiwatoka. “Nilijua hautakuja Elvin, nikarudisha chumba chako.” Bella alimgeukia Elvin mara walipokaa kwenye makochi. “Hamna shida. Kwa usiku huu naweza kulala kwenye kochi, kesho tutaenda kuchukua chumba kingine. Nitataka kuoga tu, ili nibadilishe hizi nguo. Kwa hiyo naomba ruhusa kutumia chumba chenu na bafu.” “Nilikuwa nina wazo. Kwa kuwa nyinyi mpo wawili, mlale hapo chumbani, mimi nilale kwenye kochi.” Bella alitoa hilo wazo. Kuwa Elvin na Eric wao ndio walale chumbani. “Naomba nikaoge kwanza halafu tutakuja kupanga vizuri.”
Walikuwa
na wakati mzuri sana wapamoja. Wote walikiri hawakuwahi kuwa na mapumziko ya
namna hiyo. Kila siku walifanya kitu kipya na Elvin akiwa kiongozi wao.
Walishinda wakicheza ufukweni mwa Ziwa Victoria, walirudi kulala mchana, jioni
walizunguka kuangalia mji au waliota moto nje ufukweni mida hiyo ya jioni
wakati baridi imeingia, huku wakisimuliana hili au lile ambalo wote litafanya wacheke. Bella
na mdogo wake waliimba wakati wote kipindi hicho wakiwa wanaota
moto, au walikaa tu pembeni ya pool wakiongea huku wakila na kunywa
bila ya kujali muda wala watu waliokuwepo pembeni yao mida hiyo ya jioni.
Walikuwa kwenye ulimwengu wao peke yao, wao watatu tu. Walipiga picha nyingi
sana, ambazo Elvin alikuwa akiziangalia kila anapokuwa peke yake usiku
kitandani, kwani wakati wote yeye ndio alikuwa wamwisho kulala, na akajikuta
kila wakati macho yake yanagotea kwenye picha za Bella.
Eric aliingia bafuni na kutoka naye. Walipanda kwenye kitanda chake akamfunika dada yake, akabaki amelala pembeni yake. “Is gonna be fine Bella. Soon we are gonna be fine.” Bella alimsikiliza mdogo wake akijua hajui analoliongea, tayari alikuwa na ndoa ambayo alihakikishiwa haitakaa ikavunjika labda kifo. Alikumbuka anasubiriwa kwa hamu pindi atakaporudi nyumbani. Bella alijikunyata ndani ya lile shuka na kuficha uso wake huku akitetemeka kwa hofu na machungu. Alitamani mama yake arudi aje ampokee huo mzigo japo kwa siku chache apumzike kuwaza kesho itakuwaje kwake na hasa kwa mdogo wake.
“Nani anataka kuanza kusoma?” Bella aliuliza. “Mimi nitaanza.” Eric aliwahi akafungua cha kwake akaanza kusoma. “Hii inatoka kwa Elvin, ‘Natamani kupata mapumziko kama haya wakati mwingine’.” Wote walipiga makofi. “Kwa hiyo umefurahia, Elvin?” Bella akauliza huku akitabasamu na kumwangalia Elvin kwa upole. “Sana. Naamini wakati mwingine tutapata nafasi kama hii.” Walibaki wakiangaliana kwa muda, mwishowe Bella aliinama kama kukwepesha macho huku akitabasamu, akafungua kikaratasi cha Eric. “Mimi nitasoma wa pili, kinatoka kwa Ric. ‘Natamani kuwa na familia watakayo niweka mimi na Bella mbele.’” Walitulia kidogo kama wanaotafakari ule ujumbe. “Namimi nitasoma wish ya Bella.” Elvin alivunja ukimya. “Mko tayari kusikia wish ya Bella?” Elvin alitaka warudishe mawazo pale. “Soma Elvin, mimi nasikiliza.” “Sawa. Bella anasema, ‘Natamani kurudi kuwa mtoto tena. Hata kwa dakika moja tu, kupata mtu anayeweza kuwaza kwa niaba yangu. Kama wakati wa uhai wa mama. I want to be her little girl again. I want to get the place where I can hide my sorrow and fear again. I wish to be a little girl again.’” Machozi yalikuwa yakimtoka Bella. Na hiyo ndiyo ilikuwa shauku yake. Alikuwa akipigwa na kuonewa na Mzee Masha, lakini hakuwa na rafiki au mtu wakumwambia maisha anayoishi. Kila aliyemuona na Mzee Masha, alimuhukumu kama mwizi wa mume wa mtu, wasijue mateso anayopitia. Hakuruhusiwa kuwa na rafiki awe wakiume au wakike. Na simu yake ilikuwa ikifuatiliwa, kwa hiyo asingethubutu hata kumpigia mtu yeyote simu.
“Kwani mnataka kwenda lini?” “Hamna haja Elvin. Hamna sababu kabisa yakutusindikiza. Huwa tunaenda kila wakati Ric anapokuwa likizo, sio kitu kigeni, huhitaji kwenda. Najua una mambo mengi…” “Bella!” Elvin alimwita kama kutaka atulie. “Mnataka kwenda lini?” Bella alitulia kidogo. “Sijajua, naona siku za Ric kurudi shule zimekaribia, anatakiwa mpaka ifikapo Jumapili awe yupo shuleni. Kwa hiyo nilitaka kuomba kama naweza kupata siku zangu chache nyingine za likizo kabla hajarudi shule, ndio twende kwa mama.” “Na mimi si nimewaambia nipo likizo ya siku 10? Bado nimebakiza siku nyingi tu za kutosha. Mtakapokuwa tayari naweza kuwasindikiza.” “Huna sababu yakufanya hivyo Elvin, najua…” “Bella! Mimi ndio nataka kwenda. Labda kama una sababu nyingine.” “Hapana Elvin.” “Basi tupangeni safari.” “Nilifikiria labda turudi nyumbani, tupumzike hata siku moja, ndipo twende.” Bella alijibu.
“Nataka niwahi kulala leo.” Bella alivunja ukimya. Elvin akamwangalia, kisha akauliza. “Hatuangalii movie leo?” “Mimi nitatangulia niwahi kulala.” Bella alijibu kinyonge sana. “Sawa.” Bella alisimama akaingia bafuni kuoga ili alale. “Nimefurahi tunaenda wote kwa mama, Elvin.” “Hata mimi nimefurahi Ric. Unataka tuangalie wote movie kabla hujaenda kulala?” “Leo naomba tucheze game. Bella ameninunulia game mpya nataka nicheze sana kabla sijarudi shule.” Walikubaliana wakaanza kucheza. Elvin aliposikia Bella anapanda kitandani, akamwambia Eric amsubiri kidogo anakuja.
Elvin aliwasaidia kupandisha mizigo yao kwenye gari hilo la kifahari sana, akabaki akijiuliza bila majibu. Alipiga mahesabu ya kuacha hilo gari hapo uwanjani kwa siku zote nne, walizokuwa wamesafiri, alijua itamlazimu Bella kulipia pesa nyingi, lakini Bella hakuonekana na tatizo lolote juu ya pesa. Aliingia akakaa kwenye kiti chake cha dereva, Elvin akaenda kusimama dirishani kwake.
My Past - Sehemu ya 6
B
|
ella alijua wazi Mzee
Masha ndiye aliyetuma watu shuleni kwa kina Ric akachukuliwe
ili Bella arudi
nyumbani. Alikwenda kwenye hoteli ambayo huwa wanaishi na Eric kila anapokuwa
yupo likizo ili kuthibitisha hisia zake lakini hakumkuta. Alirudi nyumbani
akamkuta Mzee Masha. Bella alikuwa akitembea kwa hasira na maumivu. “Nitakuuwa
kama hutaniambia alipo Eric, T.” Mzee Masha alibaki akimwangalia
Bella. Bella aliingia jikoni akarudi na kisu mkononi. “Ric yuko wapi?”
“Utajiumiza bure Bella. Wewe huna roho ya kikatili. Rudisha kisu, halafu njoo
hapa.” Akiwa jikoni Bella alishindwa hata kusogea, akaanguka.
ili Bella arudi
nyumbani. Alikwenda kwenye hoteli ambayo huwa wanaishi na Eric kila anapokuwa
yupo likizo ili kuthibitisha hisia zake lakini hakumkuta. Alirudi nyumbani
akamkuta Mzee Masha. Bella alikuwa akitembea kwa hasira na maumivu. “Nitakuuwa
kama hutaniambia alipo Eric, T.” Mzee Masha alibaki akimwangalia
Bella. Bella aliingia jikoni akarudi na kisu mkononi. “Ric yuko wapi?”
“Utajiumiza bure Bella. Wewe huna roho ya kikatili. Rudisha kisu, halafu njoo
hapa.” Akiwa jikoni Bella alishindwa hata kusogea, akaanguka.
Mzee Masha alikwenda
kutaka kumbeba. “Usiniguse.” “Utafikaje kitandani?” Mzee Masha
alibaki akimwangalia. “Ric yuko wapi?” “Wewe ulikuwa wapi?” “Hospitali.
Nimetoroka baada yakusikia Ric haonekaniki. Umemuweka wapi mdogo wangu?” “Ukiacha
ukorofi nitakwambia alipo.” Mzee Masha alikuwa akicheka. “Twende
ukalale.” “Nitengenezee uji kwanza. Sijaweka kitu mdomoni tokea siku umenipiga,
nilikuwa naishi kwa dripu.” Mzee Masha alibaki akimwangalia. “Nipikie
uji T. haraka.” Bella alirudi kulala pale pale sakafuni.
Mzee Masha alipika uji
harakaharaka, akamwekea kwenye bakuli. “Nikulishe?” “Swali gani hilo?
Si unaona kabisa sina nguvu?” “Nimeona umerudi na mkakati mpya, hutaki
nikuguse.” Bella alijaribu kukaa mwenyewe kwa shida huku akigugumia
maumivu. “Ric yuko wapi?” “Nimekwambia yupo. Nilienda kumchukua, ili
wewe urudi nyumbani.” “Unataka nirudi hapa kufanya nini?” “Wewe ni wangu Bella.
Hakuna kitu wala mwanadamu atakaye kutoa mikononi mwangu. Nilikwambia kifo
pekee ndicho kitatutenganisha. Ukiwa hai, wewe ni wangu daima.” “Nisogezee huo
uji hapa. Halafu niwekee simu yangu kwenye umeme.” Bella alijaribu
kunywa uji, lakini akashindwa. “Acha ukorofi usio na maana Bella.
Unahitaji msaada ambao ni mimi peke yangu ndio naweza kukusaidia sasa hivi.
Ngoja nikunyweshe.” Mzee Masha alimnywesha Bella uji wote. Alimaliza
kisha akaomba kuongezwa. ‘Lazima nipone.’ Bella
aliendelea kuwaza huku Masha akiendelea kumlisha mpaka alipomaliza.
“Nipeleke kitandani.” Mzee Masha alijaribu kumshika lakini alimtonesha. “Niache T. Unazidi kuniumiza.” “Wapi?” “Umenivunja mbavu mbili za upande wakushoto na kupasua mirija ya damu. Imebidi kufanyiwa upasuaji japo sio mkubwa lakini nina mshono upande huo huo.” “Basi ngoja nikushike upande wa kulia.” Bella alizidi kumchukia Mzee Masha. ‘Anashindwa hata kusema pole.’ Bella alianza kulia.
Alimbeba mpaka
kitandani. “Niambie Ric alipo.” Mzee Masha alikuwa amemficha Ric mahali. “Waambie hao watu wako wamwachie mdogo wangu.
Tena wampeleke kwa kaka Mat.” “Sasa hivi?” Masha
akauliza. “Ndiyo, sasa hivi.
Mimi si niko hapa. Makubaliano yangu mimi nikiwa jela, mdogo wangu anakuwa
huru. Kwa hiyo nimerudi jela, mdogo wangu anakuwa huru. Piga simu sasa hivi.” Mzee Masha alianza kucheka. “Unakufuru
mbaya wewe! Unaiita hii jela? Nitakupeleka jela ukalale huko hata siku moja,
ili ukirudi kutoka huko uwe na shukurani.” “Ni heri wanaotesa mwili tu, kuliko wewe
unayenitesa mwili na nafsi yangu. Hakuna mateso ninayoweza kupata duniani,
yakafikia ukatili na unyama unao nifanyia wewe. Hakuna na kwa kuwa nilikubali mimi
mwenyewe, acha nilipe gharama yangu. Piga simu, T. Tafadhali nataka kulala.” Mzee Masha alikuwa anacheka sana. “Umeanza
kunifurahisha Bella. Nyumba ilikuwa inapowa kweli, nagomba peke yangu! Lakini
sasa hivi naona tutakuwa wawili.” “Piga simu T.” Mzee Masha alitoka kwenda kuongea na simu.
Baada ya muda akarudi. “Umemsumbua mdogo wako bure! Alikuwa amelala hana hata shida, imebidi aamshwe sababu hutaki kusikiliza kila ninacho kushauri.” “Naomba dawa ya maumivu.” Mzee Masha alimpa Bella dawa ya maumivu. Akapanda kitandani na yeye akalala pembeni ya Bella. “Unajua nilirudi hapa Tanzani kwa ajili yako Bella?” Bella akanyamaza. “Nimeahirisha mambo mengi sana, yanayohusu familia ili nije kuwa na wewe, halafu nafika hapa na wewe haupo ulikuwa unazurula, mpaka saa tano za usiku! Ndio maana nilikasirika sana.” Bella hakujibu kitu alibaki kimya.
“Nilipoondoka hapa siku
ile ya ugomvi, nikajilaumu sana kukupiga. Nikarudi kuja kukuangalia kesho yake
sikukukuta. Sikujua kama nilikuumiza kiasi cha kwenda hospitalini.” Bella alifungua macho kumwangalia kama
anamshangaa. “Kweli Bella. Sikujua kama nimekuumiza kwa kiasi hiki,
nikajua umeamua kunikimbia, ikabidi nikamuwahi mdogo wako ili urudi. Nilipotuma
watu shuleni kwao, wakaniambia amesafiri kwa michezo halafu wakirudi wanafunga
shule. Ndipo iliponibidi kumsubiria. Siwezi kuishi bila wewe Bella. Hata nifanyaje,
siwezi tena. Najua nimeshakutendea mambo mengi sana, nimejaribu kukuchukia
lakini najikuta wewe ndio mtu pekee ninayekuhitaji.” “Naomba
nifunike shuka vizuri, nilale.” Bella hakutaka kuendelea kusikiliza.
Yalikuwa ni maneno machungu sana kwake. Kwa namna nyingine, ni kama alikuwa
akitangaziwa kifungo cha maisha. Alipitiwa na usingizi akalala.
Mzee Masha alimuuguza
mpaka akapona kabisa wakati huo Eric yuko likizo nyumbani kwa Mat. Bella
alikuwa akimuhurumia sana Ric, alijua atakuwa na wasiwasi kuona yupo likizo
halafu Bella hayupo. Lakini Bella asingethubutu kwenda kwa Ric akiwa na hali
ile. Alijua atazidi kumuumiza mdogo wake, alitaka apone kabisa ndipo aende
kumchukua .
************************************************
Mat alioa na kuhamia
kwenye nyumba ndogo mitaa ya Mwenge, ambapo aliweza kufungua na duka la vitu
mbalimbali, kutokana na pesa alizokuwa akipewa na Bella. Maisha ya Mat
yalibadilika. Bella alishakwenda nyumbani kwa Mat, kwa hiyo alikuwa
akipafahamu. Hakuwa akifahamiana vizuri na mke wa Mat, kwani mara zote
aliwasiliana kwa simu na kaka yao, sio yeye. Hata Eric, ile ndio ilikuwa mara
yake ya kwanza kufika nyumbani hapo. Alipooa Bella aliamua kumuacha kwa muda
ili kumpa nafasi na mkewe. Waliwasiliana pale ilipokuwa ni muhimu sana, tena kama
alitaka kumtuma kwa mdogo wake huko Arusha au kwa babu yake kule kijijini.
Hakuacha kumtunza babu
yake. Alihakikisha anapata maendeleo yake mara kwa mara kupitia Mat. Sasa kwa
kuwa Mat alijua pesa anatoa wapi, au nani ameyabadili maisha yake, na mahusiano
yao tokea zamani, aliongeza heshima kubwa sana kwa Bella. Muda na wakati wowote
Bella aliomuhitaji, Mat hakusita kutoa ushirikiano, hata kama yupo katikati ya
shuguli nyingine, akipiga simu Bella, atapokea tu. Hiyo tabia ikaanza kumkera
mkewe ambaye hakuwa akijua na wala kumuelewa mumewe pale alipojaribu
kumuelewesha umuhimu wake yeye kwenye maisha ya yatima hao.
************************************************
Alipoona anatizamika,
ndipo alipoamua kwenda kumfuata Eric. Aliamka asubuhi hiyo, akakusanya baadhi
ya vitu vyake ambavyo alijua atavihitaji kwa muda huo atakaokuwa akiishi
hotelini na mdogo wake, akachukua na vitu vya Eric alivyokuwa akimnunulia
wakati alipokuwa shuleni. Nguo na viatu vya thamani, akaenda kwenye ile hoteli
akapanga kila kitu kumuonyesha mdogo wake kuwa pale ndipo anapoishi wakati
yeye anapokuwa shuleni. Alipojiridhisha kuwa pako sawa, ndipo akaenda
nyumbani kwa Mat. Alijipaka foundation zile za hali ya juu kama kawaida yake,
yakuficha makovu yake ili mtu yeyote asijue kama anamakovu. Kwa hiyo ilikuwa ni
ngumu kujua kama Bella anaalama yeyote usoni mwake.
Ilishakuwa mchana na jua
lilikuwa kali wakati anafika nyumbani kwa Mat. Alimkuta Eric anaosha vyombo nje
kwenye jua kali. Bella alitamani kuchanganyikiwa. Alikuwa amekaukwa mdomo
alionekana wazi hajala. Alifurahi sana kumuona Bella. Alimkimbilia dada yake na
kumkumbatia. “Bella!” Eric aliita taratibu huku amemkumbatia
dada yake. Hasira zilimpanda Bella. Alikumbuka mateso anayopata kwa ajili ya Eric.
Pesa nyingi anazokuwa anampa Mat, tena akimwambia kabisa atafute mahali ambapo
na wao itakuwa kimbilio. Hata kodi ya hiyo nyumba anayoishi sasa hivi na mkewe,
ni Bella alilipia, tena alilipa kodi ya mwaka mzima!
“Mbona unaosha vyombo
hapa nje? Tena kwenye jua kali hivi!? Umekula?” Bella akamuliza mdogo wake kwa upendo. “Mpaka
nimalize kazi.” Bella alianza kutetemeka kwa hasira. Alijua ndivyo
alivyokuwa amembiwa na mke wa Mat. “Kaka Mat, yuko wapi?” “Ameenda
kazini. Lakini mke wake yupo ndani.” Bella aliingia ndani na kumkuta
yule mwanamke anaangalia tv, amekaa kwenye kochi na kunyoosha miguu kwenye
meza.
“Kwa nini Ric, anaosha
vyombo kabla ya kula na yupo juani?” Bella aliuliza bila ya salamu. “Ulitaka aishi hapa
bila kufanya kazi?” “Mbona wewe unaishi hapa bila kufanya kazi?” “Wewe
umechanganyikiwa nini? Hapa ni kwangu.” Kama simba, Bella aliinyakuwa
ile tv na kuitupa chini, akaipasua vipande vipande. Akageukia kabati la vyombo
lililokuwepo karibu na sebleni, akaanza kuvipasua vyombo vyote huku akigonga
vioo vya ile kabati. “Hii
yote ni pesa yangu. Muulize mumeo.” Bella alikuwa akilia kwa uchungu sana. “Nahangaika, nateseka kwa ajili ya Ric, halafu
wewe unamtesa!? Muulize mumeo pesa anapata wapi.” Bella aliingia jikoni akachukua kisu. Akaanza kuchana makochi yote
kuanzia juu mpaka chini. Akageukia meza za kioo zilizokwepo pale sebleni na
kuanza kuvunja moja hadi nyingine huku akilia.
Mke wa Mat aliogopa sana, huku analia, akampigia simu Mat. Eric aliingia mle ndani baada yakusikia dada yake analia huku anafanya fujo mle ndani. Alimkuta dada yake kama amechanganyikiwa. “Bella! Hey Enabella! That’s enough. Stop it!” Eric alimshtua dada yake. Bella akasimama huku anahema nakulia kwa uchungu sana. Watu walishajaa. Alitoka nje, akakusanya vyombo alivyokuwa akiosha mdogo wake, akatafuta jiwe akaanza kuvivunja, huku akitupa vijiko, visu na vyombo vyote vya plastiki.
“Bella, please!” Eric alitoka tena huku akilia. Alipoona mdogo wake ameanza kulia,
akamsogelea, akamshika mkono. “Twende Ric.” Akamgeukia mke wa
Mat. “Na mwambie mumeo, kwa
kuwa amekuchagua wewe, na akaacha umtese mdogo wangu, leo undugu umekufa rasmi.
Asiwahi kusogelea shule ya Eric, wala asitutafute tena. Na siku nitakayo rudi
tena hapa, nakuja kuchoma moto duka analouza, maana pia ni pesa yangu yote
ile.” Majirani walianza
kucheka. “Kazidi huyu dada, na leo kapata kiboko yake.” “Jeuri kama
anamiliki ndege!” “Sura yenyewe mbaya, utafikiri kalamba ndimu.” “Na
angemkung’uta huyu, mpaka jeuri imwishe.” Kila mtu alisema lake huku
wakicheka. Bella alimfungulia mlango mdogo wake, wakaondoka. Alikuwa akilia
njia nzima. Mwishowe aliegesha gari pembeni ya barabara, akainamia usukani na
kuendelea kulia kwa uchungu sana, mkapa Eric alipomtuliza.
Bella alimlaani sana
Mzee Masha. Alijua isingekuwa yeye kumpiga, asingeshindwa kwenda kumchukua
mdogo wake kama kawaida, na kuishi naye. Bella aliendelea kulia. “Is
gonna be okay Bella. Don’t cry, please.” Eric alikuwa mwema sana na
hakupenda ugomvi na wala hakutaka kumuona mtu yeyote anashida, hasa Bella.
Walifika hotelini wakaingia kwenye chumba chao. Bella alipanda kitandani na
kuendelea kulia. Ric alipanda kwenye kitanda cha Bella, akatoa mto aliokuwa
amelalia dada yake, akaweka kichwa chake miguuni mwake na kuanza kumbembeleza
bila kujua dada yake analizwa na mengi.
Walikaa pale kwa muda
mpaka Bella alipotulia. “Samahani Ric, nilikuwa na hasira sana.
Nilichukia kukuacha peke yako unateseka.” “Usijali Bella. Nimefurahi umekuja
kunichukua.” “Alikuwa akikutesa sana.” “Kidogo, wakati kaka Mat hayupo.”
“Alikuwa anakufanyaje?” Eric alinyamaza kidogo. “Alikuwa
ananimbia nifue nguo zote. Nikamwambia sijui kufua, akasema lazima nijifunze na
nifue nguo mpaka zitakate, lasivyo hakuna kula. Sasa wakati mwingine mikoni
ilikuwa inavidonda. Nikimwambia mikono inavidonda siwezi kufua, anagomba sana.”
“Ulimwambia kaka Mat?” “Nilimuonyesha vidonda, nikamwambia anitafutie dawa,
akasema sawa. Lakini hakunipa dawa.” Bella alizidi kuumia,
alimuhurumia sana mdogo wake.
“Bella?” Eric aliita kwa upole, Bella akamgeukia
akiwa bado amemlalia. “Unafikiri tutakuja kuwa na sisi na nyumbani
kwetu kama zamani?” Bella alijaribu kuzuia machozi yake lakini
alishindwa. Alikaa vizuri akamkumbatia mdogo wake. “Usiwe na wasiwasi
Ric. Sasa hivi tukazane na shule kwanza. Ada ninayokulipia ni kubwa sana.
Sitaweza kujenga kwa sasa. Lakini nakusanya pesa, baadaye tutajenga, na sisi
tutakuwa na kwetu. Kwani hupapendi hapa?” “Napapenda sana, lakini sio kwetu
Bella. Natamani tuwe na nyumbani kwetu, ili nikiwa natoka shule, niwe najua
naenda nyumbani kwetu, hata kama wewe haupo.” “Wazo zuri Ric. Basi tuanze
kutafuta hata nyumba ya kupanga kwa muda. Ukimaliza shule, tutajenga nyumba
yetu.” Eric alifurahi sana. “Njaa inauma Bella.” “Na mimi njaa
inauma. Ngoja nipige simu watuletee chakula, sasa hivi. Halafu tukaogelee.”
Baada ya kula, Bella na
mdogo wake walitoka kwenda kuogelea hapo hapo hotelini. Wote wakiwa wametulia. Eric
alianza kumsimulia dada yake mafanikio makubwa anayoyapata huko shuleni. “Asante
Bella. Najua unalipia pesa nyingi, lakini nikija kushinda kwenye Olympic,
tutakuwa na mahela mengi sana.” Bella alianza kucheka. Angalau
aliliwazika. Akaona mateso yake sio bure. “Bado ndoto zako za kwenda
Olympic kwenye mashindano hazijafa tu?” “Nilimuahidi mama kuwa nitafika. Lazima
nifike Bella. Nitaenda kushindana kwenye kombe la Dunia, na ninajua nitashinda
tu.” Eric alikuwa mzuri sana kwenye michezo. Bella alifikiria. “Mwenzio
ndoto zangu zote zimekufa Ric.” “Najua Bella. Lakini tusikate tamaa, mimi
nitaenda kukuwakilisha. Wakati wananipa zawadi, nitakuita tupokee wote.” Bella
alianza kulia. “Unajua kwa nini ninakazana?” Bella alicheka
huku anafuta machozi. “Nakazana kwa kuwa najua nacheza kwa ajili yangu
mimi na wewe.” Bella alicheka. “Itabidi siku nyingine ukienda
kwenye mashindano na mimi nije kukutizama.” “Nitafurahi Bella. Mashindano mengine
tutaenda South Africa. Unajua kuna wanafunzi wengine wazazi wao huwa wanakuja?
Tunasafiri nao.” “Mbona hukuniambia sasa?” “Sikutaka kukusumbua, si uliniambia
ulianza kazi?” “Tena nina ofisi yangu.” Eric alianza kucheka. “Unakumbuka
yale mambo ya kompyuta tulikuwa tunafanya nyumbani wakati mama yupo?”
“Nakumbuka.” “Nilienda kuyasomea tena, ndio sasa hivi nafanyia kazi.”
“Wanakulipa vizuri?” “Sanaa.” Bella na Eric walikuwa wakiongea na
kucheka karibu usiku kucha. Bella alikuwa amepona kabisa. “Tulale Ric,
kesho mwenzio natakiwa kazini. Tutaenda wote ukanisaidie kazi?” “Nitafurahi
Bella.” Wakalala.
Kwa Mara ya Kwanza, Eric
kazini kwa Bella.
Bella na Eric waliamka
asubuhi kuelekea ofisini kwa Bella. Njia nzima walikuwa wakiimba kama kawaida
yao tokea utoto wao waliimba pamoja. Vilitawala vicheko kati yao, na Bella
alijawa na furaha sana. Elvin alibaki hamuelewi Bella. Bella aliyeachana naye
hospitalini au waliyezoea kumuona pale kazini sio huyu wasasa. Alijawa tabasamu
wakati wote. Eric alikuwa kila kitu kwa Bella. “Kumbe una dimpozi?” Elvin
alimtania Bella. Bella akacheka. Hakuacha kumwangalia mdogo wake kila wakati.
Ric naye alikuwa kama Bella. Anajiamini na alipenda kujua mambo. Kwa haraka
sana, akamzoea Elvin, na kuhamia ofisini kwake. Alishinda ofisini kwa Elvin
akiomba amsaidie kazi ndogo ndogo. Elvin alimzungusha ofisi nzima, akimuelezea
kazi anazofanya pale.
“Mbona kama wewe una kazi nyingi kuliko wote?” Eric alimuuliza Elvin wakati wanazunguka. Elvin akacheka. “Nafanya kazi mbili kwa wakati mmoja. Namsaidia na baba yangu. Yeye ndio mwenye hii kampuni, na mimi nimeajiriwa kama Bella.” “Unaingia kazini saa ngapi?” “Mimi ndio mtu wa kwanza kufika hapa ofisini. Lazima saa kumi na mbili niwahi kufungua mlango.” “Ni sawa na mimi nikifika kesho muda huo, nione kazi unazofanya, tangia asubuhi?” “Hamna shida.” Walirudi ofisini kwa Elvin, Eric akiwa amejawa furaha sana.
Bella alimfuata. “Mbona
umenikimbia?” “Namsaidia kazi Elvin. Tumekuwa marafiki.” Bella
alicheka. “Kweli. Muulize Elvin. Na kesho nitakuja saa 12 asubuhi,
nimsaidie kazi.” “Eric!?” Bella akamshangaa mdogo wake. “Kesho
unatakiwa kupumzika.” “Nimezoea kumka mapema nikiwa shuleni. Naomba unilete
Bella.” “Kama Elvin akisema ni sawa, nitakuleta.” “Au mimi mwenyewe naweza
kumfuata ili usisumbuke kuamka asubuhi asubuhi.” Elvin alitoa
wazo. “HAPANA!” Bella alisema kwa nguvu na kwa kushtuka sana.
Elvin na Eric walibaki wakimwangalia. “Namaanisha itakuwa usumbufu
kwako Elvin. Nitamleta tu mimi mwenyewe hapa kazini.” Wote walibaki
kimya, wakishangaa ule mshtuko wake. Haukuendana na ile kelele.
“Twende tukale Eric.” Bella aliona aondoke tu, kwani ni kweli alikataa kwa nguvu sana na kumshtua kila mtu. “Twende wote Elvin.” Eric naye akamgeukia Elvin. “Sijawahi kumuona Bella anatoka kwenda kula mchana. Sijui hata kama anajua panapouzwa vyakula.” Bella alitabasamu. “Ningemkimbiza City Garden mara moja, napafahamu.” Elvin alibaki akimshangaa. “Kwa nini ukalipe mapesa yote hayo!? Twendeni niwapeleke mkale chips vumbi.” Wote walicheka na kuondoka.
Ulitawala utani kati
yao, Eric akimtania Elvin. Alijiona ni kama amepata kaka. Walifika sehemu,
wakakuta watu wengi wamejaa wanasubiria chips, kila mtu alikuwa akimshangaa
Bella. Bella alikuwa na mvuto wa aina yake. Umbile lake, lilimfanya kila mtu
kumwangalia bila kujiiba. Alijaliwa uso mzuri sana na macho mazuri. Ilikuwa
ngumu kuelewa msichana kama yule, na mavazi ya thamani aliyovaa, na kiatu cha
juu vile, anafanya nini sehemu kama ile. Bella alifanana sana sura na rangi ya
mwili na mdogo wake. Na kwa kuwa Eric alikuwa mrefu, ungeweza sema ni mapacha.
Walikuwa wakicheka, bila kujali mtu.
“Mtaweza kula hapa au mnataka tukale ofisini?” Elvin akauliza. “Umesema leo tunakula chips vumbi, tule hapahapa kwenye vumbi.” Bella alijibu nakumfanya Elvin amwangalie huku akicheka. “Naona Bella huyu wa sasa ni bora zaidi.” “Jamani Elvin! Bella yupi sio mzuri?” “Yule anayevaa sura ya kazi kila wakati. Sijawahi kukuona ukicheka hivi Bella!” Bella alicheka tena na kuendelea kula. Waliendelea kula huku wakicheka, Eric ndiye alikuwa na furaha sana. Elvin alimuona vile Bella alivyokuwa akimtizama mdogo wake kwa makini huku akimuuliza maswali kila wakati. Kama anataka amuongeze hiki au kama amependa hicho chakula, au kama chakula kitamu. Alimuona vile akili zake zote zilivyokuwa kwa mdogo wake, akajua ndipo furaha yake ilipo.
“Mimi na Bella,
tutasafiri kwenda kutembea. Unataka twende wote?” Eric alimuuliza Elvin wakati wanaendelea
kula. Bella alitamani amfunge mdomo Eric. “Hapana Ric. Elvin
anatakiwa sana kazini. Hawezi kusafiri na sisi.” “Kwani mnataka kwenda lini?”
“Bella amesema ile week ya sabasaba, ndio itakuwa weekend ndefu. Ndio
tutasafiri kipindi hicho.” Bella alikuwa kimya kabisa, akiomba Mungu
Elvin amkatalie Eric. “Nafikiri tunaweza kwenda wote, hatutafungua
ofisi.” “Asante Elvin. Umeona Bella? Safari hii tutakuwa na wakati mzuri zaidi,
Elvin atakuwa na sisi. Wakati wote tumekuwa mimi na Bella tu.” Eric
alikuwa na furaha sana, lakini sio Bella. Angemwambia nini Mzee Masha akaelewa?
Lakini katika vitu ambavyo hawezi kufanya ni kumkatili Eric, mdogo wake
kipenzi. Walikuwa wakitembea kurudi ofisini, Eric na Elvin wakicheka sana,
lakini sio Bella.
Walipokuwa wakiingia tu ofisini huku wamejawa vicheko, walikutana na Irene pale mapokezi. Sura yake haikuwa na furaha hata kidogo. “Nimekupigia simu zaidi ya mara tano hujapokea.” “Niliacha simu ofisini, pole. Vipi lakini?” “Unaachaje simu ofisini sasa!?” Irene alionekana kukasirika. “Tuliongea muda sio mrefu Irene, na tukakubaliana nikitoka kazini nije nyumbani kwenu. Sikujua kama utapiga tena. Pole.” Bella alipoona hali sio shwari alimshika mkono Eric. “Twende ofisini kwangu.” Bella na Eric waliondoka na kuwaacha Elvin na Irene pale mapokezi wakiendelea kuongea.
“Ulikuwa wapi?” Bella alisikia Irene akimuhoji Elvin. “Nilienda nao kula. Yule ni mdogo wake Bella, amekuwa akinisaidia kazi siku nzima leo. Nikaona nimpeleke kula. Vipi Irene? Mbona kama umekasirika?” “Nashangaa nakupigia simu hupokei, kumbe umetoka kwenda kula na Bella. Kwanza tokea lini mmeanza kwenda kula pamoja?” “Naomba twende tukaongelee ofisini, Irene.” “Kwani unaficha nini?” “Tunasumbua watu maofisini kwao, Irene. Tuliposimama hapa, kila mtu anatusikiliza sisi. Naomba tuingie ofisini kwangu.” Irene alibaki amesimama. “Tafadhali Irene.” Waliingia ofisini kwa Elvin, pakawa kimya.
Eric alipooza
sana. “Usiwe na wasiwasi Ric, kila kitu kitakuwa sawa.” “Unafikiri
nilikosea, Bella?” “Nimekwambia usiwe na wasiwasi Ric, ulikuwa na nia nzuri.” “Unafikiri
nimekuharibia kazi?” Bella alicheka kumfariji mdogo wake. “Itabidi
uwe unakuja hapa kazini mara kwa mara, ili ujue mambo ya kazi. Huwezi kuharibu
kazi kwa kuwa mkarimu. Ulifanya vizuri, kumkaribisha Elvin kwenda kula na sisi.
Naamini kila kitu kitaenda sawa. Usiogope.” Eric hakuwa akipenda
kumuudhi mtu, alibaki kimya ofisini kwa Bella mpaka jioni wanakaribia
kuondoka.
“Ric! Wewe muoga bwana.
Nimekwambia usiogope.” “Ni sawa kwenda kuongea naye?” Bella alifikiria kidogo. “Kwa nini
usiongee naye kesho? Twende ukapumzike, halafu kesho ndio utaongea naye?”
“Sawa.” Bella aliweka vitu sawa, akabeba pochi yake akamwambia mdogo
wake muda wa kazi umeisha, waondoke.
Wakati Bella anafunga ofisi yake, naye Elvin alitoka ofisini kwake akiwa na Irene. Eric aliwasogelea. “Samahani, mimi ndio nilimkaribisha Elvin kula naye chakula cha mchana. Naomba usimlaumu Bella.” Bella alishtuka sana. “Bella alitaka niende naye mimi tu, lakini kwa kuwa mimi nilikuwa na Elvin tokea asubuhi tukifanya wote kazi, nikaona nimkaribishe chakula. Sio Bella. Usimlaumu Bella. Bella hana kosa.” “Usiwe na wasiwasi Eric, kila kitu kipo sawa. Hukukosea. Na mimi nilifurahia tumepata muda wa pamoja. Usisahau kesho umeniahidi utakuja asubuhi ya saa 12 tuanze kazi pamoja.” Ilibidi Elvin amjibu kwa utani kidogo, kwani Irene alibaki kimya akimwangalia wakati Eric anamtetea dada yake. Eric alicheka kidogo. “Bella amesema atanileta.” “Sawa. Muwe na usiku mwema.” Elvin aliaga huku akimtizama Bella aliyekuwa amesimama kimya akimwangalia mdogo wake. “Asante.” Bella alijibu kwa hofu kidogo. “Twende Eric.” Bella alitangulia mlangoni, Eric akafuata.
************************************************
Eric aliendelea kumganda
Elvin kila siku, kila alipokuja kazini na Bella, alishinda ofisini kwa Elvin.
Waliacha kwenda kula nje wakawa wakiletewa chakula pale pale ofisini na kula
jikoni wote watatu. Taratibu Elvin na Bella wakaanza kuzoeana. Minong’ona
ikaanza pale ofisini juu ya Bella na Elvin.
Muda wa safari yao
waliyopanga ukawadia. “Naomba siku ya Ijumaa niwahi kutoka Elvin,
tunasafiri na Eric.” Bella alimfuata Elvin ofisini kwake. “Mmeamua
kuniacha? Hutaki twende wote?” “Hapana Elvin, nilijua baada ya ile
siku, tusingeweza kwenda pamoja.” “Nilimuahidi Eric, tutakwenda wote. Siwezi
kubadilisha sasa hivi.” “Sitaki ije ilete matatizo Elvin. Naweza kuongea na
Ric, naamini ataelewa tu.” “Mbona kama hutaki niende? Eti Bella?”
“Hapana Elvin, ningependa twende wote. Najua Ric atafurahi zaidi, lakini
nisingependa tukusababishie matatizo.” “Usiwe na wasiwasi. Itakuwa sawa tu.” Kwa
upande mwingine Bella alifurahi lakini alimuhofia sana Mzee Masha.
************************************************
Eric alipolala, Bella
alitoka nje na kumpigia simu Masha. “Umenikumbuka leo?”
Bella akaanza
kulia. “Nini
Bella?” “Umesababisha
mdogo wangu ateseke sana. Nimemkuta ananjaa, tena yupo juani.” “Si
ulisema Mat atamtunza vizuri?” “Hakuna mtu anaweza kuishi vizuri na
Eric isipokuwa mimi mwenyewe. Mke wa Mat alikuwa anamtesa sana mdogo wangu. Na
yote hayo wewe ndio umesababisha, T. Ulinipiga bila kosa, ukasababisha niugue,
nikashindwa kukaa na mdogo wangu. Wewe unajua nafanya kila kitu kwa ajili ya
Eric. Naumia sana kuona wote tunaishia kuteseka. Inakuwa haina maana yeyote.
Kama nashindwa kumsaidia Eric basi hata wewe huna maana yeyote kwenye maisha
yangu.” Bella alikuwa amekasirika sana, alikuwa akiongea huku
analia. “Unanisikia?” “Nakusikiliza Bella.” “Mbona hujibu sasa?” “Unataka nijibu nini wakati umenipigia
simu usiku, tena nikiwa nimelala, halafu unagomba?” “Wewe ndio umesababisha yote haya T. Tunakuwa watu
wakutangatanga mchana kutwa. Hatuna nyumba, tunabaki kukaa hotelini tu.” “Kwa nini usimlete
hapa nyumbani?” “Tunataka
nyumba yetu. Sio yako ambayo ukiamua siku hiyo kunipiga unanipiga karibu ya
kuniua. Halafu nakujua T, unamtindo wakunipokonya vitu vyako ukikasirika. Siku
ukikasirika halafu ukatufukuza mimi na Eric? Heri niteseke nae hivi hivi huku mahotelini
kuliko siku moja aje kushuhudia unavyonipiga halafu ukatufukuza nyumbani kwako.
Itaniumiza zaidi ya unavyonipiga.” “Ninakuwa na hasira tu Bella, sina maana yakukuumiza au
kukunyanyasa. Nimekwambia sitakupiga tena.” “Sasa hivi ndio unaongea hivyo kwa kuwa unajua nipo na Ric
siwezi kuwa na mwanaume mwingine. Akiondoka tu utaanza kunipiga kama zamani.” “Nimeshawahi kukuahidi kitu na nikashindwa kutimiza?” Bella alinyamaza.
“Yote
haya nafanya kwa kuwa nakupenda Bella. Ninamatatizo yakifamilia yamenipanda
kichwani, lakini nimekubali kuwa hapa na wewe. Nakupenda na sitaki mwanaume
mwingine akuguse.” Bella alibaki kimya akilia. “Bella?” “Nataka tuwe na kwetu T. Tumechoka maisha ya
hotelini.”
“Basi chukueni hii nyumba.” “Hapana
T. Hapo utatusumbua tu. Wewe nipe pesa, nikatafute nyumba sehemu nyingine,
ambayo hutakuwa unapafahamu na wala hutakaa ukafika huko. Najua hiyo nyumba ni
yako na familia yako, haitakaa ikawa yangu hata siku moja.” “Kwa nini unasema hivyo?” “Nimeona hati ya nyumba T. Umeandika
jina la Junior, wala sio langu.” “Yaani unaingia mpaka kwenye Safe yangu
ile ndogo!?” “Ndiyo,
huwa naingia.” Mzee Masha akanyamaza.
“Tunasafiri
kwa siku nne, nataka Ric akapumzike. Lakini Ric amemuomba Elvin, yule mtoto wa
Mzee Mwasha, tuende naye safari.” Mzee Mwasha
alinyamaza. “Umenisikia?”
“Na mimi?” “Huwezi kuja T. Elvin akikuona?” “Basi na yeye asiende.” “Wewe
unajua siwezi kumkatalia Ric, kitu chochote.” “Katika hili itabidi uweze tu,
Bella.” “Labda hujanielewa. Nimekwambia SITAMWAMBIA Ric hapana.” Bella aligomba tena kidogo. “Huyu mtoto hana baba, wala mama, halafu
leo amepata rafiki anataka kwenda nae mapumzikoni, nimwambie hapana. Nitampa
sababu gani?” “Tafuta sababu yeyote Bella.” “Sitafanya hivyo T. Mimi nipo na
wewe wakati wote. Nina mwezi mmoja tu wakupumzika na mdogo wangu, nao huo pia
unataka kuumiliki!? Katika hilo hapana. Nisubiri mpaka nitakapo rudi.” “Hivi
unajua nimeacha familia yangu ili nije kuwa na wewe Bella?” “Basi rudi huko kwa
familia yako, likizo ya Ric ikiisha ndipo na wewe urudi kwangu. Nimekwambia
nimemkuta mtoto kwenye mateso, halafu unataka na mimi niendelee kumnyima raha?
Kama wewe unavyowawazia familia yako mambo mema, ndivyo hivyohivyo na mimi
ninavyomuwazia mdogo wangu mambo mema. Ulitaka nimpeleke kwenye shule ya bweni,
ili uweze kunimiliki utakavyo, nikakubali na nikafanikiwa kumshawishi na yeye
akakubali. Sasa hivi yupo likizo, pia hutaki niwe na mdogo wangu!? Nyumba
uninyime, unitenganishe na mdogo wangu karibu mwaka mzima, halafu hata
huu mwezi mmoja nao unataka pia uninyime raha na mdogo wangu! Haitakaa itokee
T. Kama unampango wa kuniua, naona huu ndio utakuwa wakati wako mwafaka.
Umesikia?” Mzee Masha
alicheka kidogo.
“Nani
amekwambia nimekunyima nyumba, Bella?” “Mbona umeandika jina la mtoto wako na
sio langu?” “Kwani tatizo liko wapi?” “Usinifanye mimi mtoto T. Naomba
nikalale. Ila ujue nitasafiri.” “Nimeelewa mama.” “Na ninakuomba T,
usianze fujo zako. Naomba uniache nitulie na mdogo wangu, akiondoka nitarudi
nyumbani. Tafadhali sana. Unanielewa?” “Si nimekwambia nimekuelewa Bella? Na
nimekuruhusu kwa kuwa nina mwamini sana Elvin, nikijana mwenye maadili,
vinginevyo nisingekuruhusu. Usije ukaja siku nyingine na mwanaume mwingine
ukafikiri nitakuruhusu Bella. Ni Elvin tu.” “Mimi nakwenda kulala.” “Mtakwenda wapi?”
“Sitakwambia T. Nakujua wewe huwezi kujizuia, lazima utanifuata. Sitakaa siku
nyingi, nitarudi. Naomba unisubiri. Na usianze kunitumia watu wanifuatilie.
Tafadhali T.” “Daah! Kweli umebadilika Bella.” “Naenda kulala T, usiku mwema.” Bella akakata simu.
***************************************************
Kesho yake wakati wa
chakula cha mchana, alimuacha Eric na Elvin akaenda kukata tiketi ya ndege.
Bella alikuwa na furaha sana, kuona ameweza kummudu Mzee Masha na amefanikiwa
kumpa mdogo wake kitu anachokitaka, Elvin. Alijitahidi kuwahi kurudi ofisini,
kabla muda wa kazi haujaisha. Alimkuta Eric na Elvin wapo pamoja. “Ric!
Naomba ukanisubiri ofisini kwangu mara moja, nataka kuongea na Elvin.” Eric
akatoka bila yakuuliza swali.
“Vipi?” Elvin aliuliza mara baada ya Ric
kutoka. “Nilitaka kuhakikisha kama bado unampango wa kusafiri na sisi,
au ulibadili mawazo.” Elvin aimwangalia Bella vizuri. “Naomba
uwe mkweli Bella, ni kweli unataka niende au hutaki?” “Nataka twende wote Elvin.”
“Sasa mbona una wasiwasi?” “Sina wasiwasi, nilitaka uhakika tu.” “Ni juzi tu
umeniuliza swali hilo hilo, na leo tena! Vipi?” Bella alinyamaza
kidogo akatoa zile tiketi. “Nimeshakata tiketi zetu wote, hizi hapa.
Nilitaka tu uhakika Elvin, sikutaka kumwambia Ric, akafurahia, kumbe ukawa
umebadili mawazo.” Elvin alibasamu kidogo. “Nitakwenda Bella,
na nilipanga mimi ndio nilipie tiketi.” “Basi wakati mwingine utafanya hivyo.
Asante Elvin.” Bella ni kama aliwaza kidogo. Kisha akakaa.
“Ni kweli nakushukuru,
Elvin. Unaweza usijue kitu unachofanya sasa hivi, lakini kina maana kubwa sana
kwangu na Ric. Baada ya mama kufariki, nimekuwa nikimlea Eric mimi mwenyewe,
nikisaidiana na kaka Mat tu. Kaka Mat, alikuwa dereva wetu wakutokea zamani.
Lakini kwa Ric ni zaidi ya dereva, amezaliwa akamkuta Mat. Amekuzwa na kaka
Mat. Ndiye aliyekuwa
anampeleka shule tokea mtoto. Hata alipokuwa akiumwa au akilazwa hospitalini,
kaka Mat ndiye aliyekuwepo kusaidia kumuuguza. Ndiye aliyemfundisha kucheza
mpira, kuendesha baiskeli na mambo mengine mengi hata kupiga kinanda na gitaa,
yeye ndiye alimfundisha. Alikuwa akienda naye kanisani kwao siku za
mafundisho ya kwaya. Alifanya mpaka mama akatununulia kinanda hapo nyumbani.
Yeye Kaka Mat, akawa anatufundisha. Ric hajui kama ni dereva, anajua ni kama
ndugu kwa vile alivyokuwa akiishi na mama. Na walikuwa marafiki sana na Ric.
Tulimuhesabu kama ndugu kabisa, lakini na yeye ameoa, nafikiri mkewe ameshindwa
kutupokea. Wakati ule naumwa, nilishindwa kwenda kumchukua Ric. Sikutaka anione
nikiwa nimeharibika mwili vile, nikamuomba Kaka Mat akae naye kwa muda mpaka
nipone kabisa. Lakini Kaka Mat, amebadilika sana, na mkewe amekuwa mkali sana
kwake. Sasa haya mabadiliko ya kaka Mat ya gafla yanazidi kumuogopesha. Ric ana
upendo sana, na hapendi kumuudhi mtu.” “Nimemuona. Ni mtoto wa tofauti.” Elvin
aliongeza. Bella alitabasamu.
“Sasa akisikia au kumuona mtu anamchukia au kumfanyia ubaya wowote, anaumia sana. Anazidi kuamini kuwa watu hawatupendi, wanatuchukia. Maana alishawasikia hata ndugu zake mama kipindi cha msiba wakitusema vibaya sana na zaidi walitukana mbele za watu. Hawakutaka kutuchukua wakatuacha pale pale kijijini tulipokwenda kumzika mama. Baada ya mateso ya pale tulipokuwa tumeachwa peke yetu kijijini kuwa makali sana, tukaamua kurudi huku mjini kwenye nyumba tuliyokuwa tukiishi na mama, kabla hajafariki. IIikuwa ni nyumba ya kupanga. Tulifika hapo usiku sana, tukiwa na njaa na hatujui pakulala. Tulikuta hiyo nyumba ilishapata mpangaji mwingine na vitu vyetu vyote vimeuzwa. Nilimuomba huyo mama tuliyemkuta, angalau atupe chakula cha Ric tu, lakini alikataa na kutufukuza pale, tukaenda kukaa nje ya geti, mbu walikuwa wakitung’ata, na Ric alikuwa akisikia wakati namuombea chakula. Anamaumivu mengi sana moyoni, amekuwa akishuhudia mambo ambayo yeye hawezi kumfanyia mtu, tukifanyiwa sisi. Na…” Bella alifuta machozi.
“Sasa kwa wewe kumkubali
hivi, ndio maana anakuganda kila mahali. Anaogopa anaona tutaishia kuwa peke
yetu tu, na anajua ni kama tumempoteza Kaka Mat, kwa hiyo anakutaka wewe.
Lakini nakuomba kitu kimoja Elvin.” Elvin aliwahurumia sana. “Naomba wakati mwingine Ric
atakapokuomba ufanye kitu, sio lazima ukakubali. Usijilazimishe kabisa kufanya
kitu usichotaka, lakini naomba kama haupo tayari, uwe unamwambia hivi, ‘nitafikiria,
halafu nitakupa jibu baadaye’, halafu mimi mwenyewe nitajua
jinsi yakumuelewesha, kuliko kumkatalia moja kwa moja au wewe
kujiona unawajibika kumkubalia kila kitu. Bado ana akili za kitoto. Haelewi
majukumu ya kazi, au hajui kama wewe una mchumba wako, na ni lazima wakati
mwingine mkubaliane na mwenzako kwanza. Mimi ninaelewa, kwa hiyo nitamsaidia
taratibu mpaka ataelewa maisha yakoje. Lakini naomba usimkubalie halafu
ukashindwa kumtimizia, anaumia sana na nisingependa aendelee kuumizwa.” Elvin
alikuwa kimya kabisa akitafakari. “Nimeelewa Bella. Lakini nina maswali
mengi sana, natamani unipe majibu yake.” Bella alitabasamu
kinyonge. “Nafahamu hilo, Elvin. Nakuahidi ipo siku nitayajibu yote,
lakini isiwe leo tafadhali. Leo naomba nikuachie tiketi yako tu.” Bella
aliiweka pale mezani na kutoka pale ofisini kwa Elvin akimuacha na maswali
yake.
************************************************
Ilikuwa siku ya alhamis
na walipanga kusafiri siku ya Ijumaa. Ndege yao ilikuwa ikiondoka saa tano na
nusu asubuhi. Kwa kuwa siku ya saba saba ilikuwa jumatatu, walipanga kukaa huko
kwa siku tatu ya nne ndipo warudi. Ric alikuwa anafuraha sana. Alikuwa
akimsimulia Elvin vitu wanavyofanya na Bella wakiwa mapumzikoni. “Huwa
tunaenda kucheza volleyball baharini na Bella. Usimuone Bella hivyo, anajua
sana kucheza mpira wa Volleyball, sijawahi kumfunga. Ila hajui basketball.” “We
Ric! Si kwa kuwa nakuhurumia, nakuacha ufunge tu? Angalau upate sifa kwenye
mchezo mmoja?” Elvin alikuwa akicheka. Eric aliinama
kumnong’oneza kitu Elvin. “Muongo,
hajui kucheza basketball. Tukifika huko wakati wa kucheza Volleyball unichague
mimi uwe upande wangu ili tumfunge.” “Haaa!” Bella
alishangaa. “Told you! You’re a bad whisperer. Muone hujui kunong’ona.”
“Kwani umesikia Bella?” “Kumbe!? Nimesikia njama zako zote. Na hiyo ni rushwa
Ric.” Wote walikuwa wakicheka sana. “Na ujue mimi nipo vizuri
sana, hata ukimkodisha ‘Ivan Zaytsev’ awe kwenye timu yako,
nitawafunga tu.” Bella aliongeza kwa kujigamba kidogo.
Bella alikuwa mchezaji
mzuri sana wa volleyball. Hata wakati yupo shuleni walimtegemea kwenye timu
yao. Na wakati wote alitamani kumfikia Ivan Zaytsev, kijana mashuhuri sana
kutoka Russia, aliyenunuliwa kwenye timu ya Itali kwa pesa nyingi sana. Bella
alikuwa akijifananisha naye, na alisema siku moja na yeye atakwenda kushindana
kwenye mashindano ya Dunia, na atakuwa na jina kubwa kama Ivan. Wote walikuwa
kwenye wakati mzuri sana.
************************************************
Walikuwa wakila jikoni,
pale pale ofisini siku hiyo ya alhamis. Vilitawala vicheko kati yao.
Wafanyakazi wengine waliingia kuchukua vitu vyao kwenye friji na kutoka, na
kuwaacha wao wakiongea. Kila mtu alishangaa kumuona Bella amekaa akiongea
na kucheka kwa sauti kiasi kile. Walishamzoea akifika kazini, akishaingia
ofisini kwake hatoki mpaka jioni anapoondoka, au labda awe ameitwa kwenye
kitengo fulani kufanya kazi. Alikuwa mtundu sana wa kompyuta, kwa hiyo kazi
zote za vitengo vyote alikuwa na uwezo wa kuziona kwenye kompyuta yake, ofisini
kwake.
Mlango wa jikoni
ulifunguliwa na Irene aliingia akiwa na tiketi ya ndege mkononi. “Nimekuta
hii tiketi mezani kwako, inaonyesha unasafiri kesho. Mbona mimi sina taarifa?”
“Ndio maana nilikutumia ujumbe jana nikakuomba tuonane, ukasema kunamahali
unaenda hatutaweza kuonana ile jana. Na leo nimekupigia simu, ukasema upo
mahali huwezi kuongea. Nikakwambia ni lazima leo tuonane. Nilitaka tuzungumzie
juu ya hii safari.” Elvin alijibu akionyesha ametulia kabisa
usoni. “Unaenda wapi?” Irene akauliza tena. “Tunaweza
kwenda kuongea ofisini kwangu?” “Kwani ni siri?” Irene
aliuliza kwa ujeuri kidogo. “Sio siri, lakini naomba tukazungumzie
ofisini kwangu.” Irene alibaki amesimama kwa muda, mwishowe akavuta
kiti akakaa. “Mimi sioni tofauti ya ofisini na hapa. Wewe nielezee tu.” Bella
aliamua kusimama. “Twende Ric.” Ric na Bella walitoka ili
kuwapa nafasi.
Bella na Eric waliingia
ofisini kwa Bella. “Usiogope Ric, kila kitu kitakuwa sawa. Umesikia?” Ric
aliinama kwenye kompyuta yake na yeye akiwa kimya kabisa. Baada ya muda
walisikia Irene akigomba huku anapiga meza. Gafla akatoka nakuingia ofisini kwa
Bella. “Nilishakwambia Elvin ni mchumba wangu. Unawezaje kwenda na
mchumba wa mtu mapumzikoni? Huoni aibu? Hujafundwa kwenu?” Wakati
Irene anagomba, Elvin akaingia. “Tafadhali Irene, naomba usifanye
hivyo. Please.” Irene alitoa simu. “Ngoja tuwaulize wazazi
wetu kama ni sawa. Huwezi kunichezea akili Elvin. Wewe ukisikia mimi nimesafiri
na mwanaume mwengine ungefurahi?” “Irene please. Naomba acha kufanya fujo
zisizo na maana. Mbona wewe ulikuwa ukisafiri na kina Junior mimi sikuwa
nikikasirika? Kwa kuwa nakuamini.” “Huwezi kumfananisha Junior na
huyu msichana. Junior ni mmoja wetu, huyu hatumfahamu kabisa. Hata wazazi wake
hutuwajui na wala hujui maadili yake. Kama ni msichana mwenye tabia ya kuiba
wanaume za watu, je?” Moyo wa Bella ulishtuka sana, alibaki
kimya.
“Ukute yeye ndio
anamtuma mdogo wake.” Irene alikuwa
akiongea kwa sauti, mpaka wafanyakazi wengine walianza kutoka maofisini kwao
nakuja kuangalia kulikoni. Irene alitoa simu palepale na kuanza kumpigia simu
mama yake Elvin, akamueleza kwa kifupi, kisha akampigia na baba yake. Baada ya
muda mfupi alishapigia simu watu zaidi ya wanne. Elvin alibaki akimtizama.
Bella na Eric walikuwa wameinamia kompyuta zao.
Bella alipoona mambo
yanakuwa mabaya, akaamua kumuandikia pale pale barua pepe, {email}, Elvin bosi
wake, kuomba siku ya kesho asije kazini kabisa. Walikuwa wamekubaliana siku ya
kesho, Ijumaa, wafike hapo kazini wakiwa na mabegi yao tayari kwa safari. Yaani
wafanye kazi mpaka muda wakwenda uwanja wa ndege, ndipo waondoke pamoja.
Alipomaliza kuiandika, na kuituma, Bella alifunga kompyuta yake, akaweka
vitu sawa pale mezani, akamgeukia Eric. “Twende
Ric.” Ric akasimama, akakusanya vitu vyake vyote, na laptop yake, wakatoka
na Bella na kuwaacha Elvin na Irene ofisini kwake, Bella. Kila mtu alikuwa
akiwashangaa.
************************************************
Bella alishindwa aongee
nini na Ric. Walirudi nyumbani/hotelini kwao wote wakiwa kimya kabisa. Bella
alishachukua vyumba viwili huko waendako, cha Elvin na chake yeye na Ric. “Unataka
twende tukaogelee?” Bella akamuuliza Ric, aliyekuwa kimya kabisa
akicheza game yake kwenye kompyuta yake. “Naona huu ndio muda mzuri
kama unataka kuogelea. Jua litaisha, halafu kutakuwa baridi, haitakuwa raha
tena kuogelea. Twende sasa hivi.” “Na leo tunashindana kama jana?” Bella
alicheka. “Hujachoka kushindwa?” “Bella wewe!” Eric alianza
kucheka. “Wakati mimi ndio nilishinda!” “Mimi naona unaanza kupoteza
kumbukumbu Ric. Jana nilikushinda. Twende leo nikakuonyeshe jinsi nilivyokuwa hodari.
Utaingia aibu.” “Twende Bella. Tukaone nani anaingia aibu.” Hawakutaka
kuzungumzia ule mkasa wa ofisini kabisa. Walikaa kwenye maji wakikumbushana
mambo yao yaliyowafanya wacheke sana. Walikula huko huko kwenye Pool mpaka
ilipofika usiku sana wakarudi kulala.
Wakati wanalala, Eric
alimwita dada yake. “Hey Bella?” “Yes.” “Are we gonna have fun there?”
“Like always. Usiwe na wasiwasi Ric. Tutakuwa na wakati mzuri sana. Cha muhimu
ni mimi na wewe tuwe pamoja. Maadamu wewe upo, nina uhakika mimi nitakuwa na
wakati mzuri sana. Sijui wewe?” “Nakupenda Bella.” “I know, Ric.” Walikaa kimya kwa muda. “Unafikiri Elvin
atakuja?” Eric akauliza tena. “Sijui Ric. Lakini ujue Elvin
ana majukumu mengi sana. Wakati mwingine inakuwa ngumu hata yeye mwenyewe
kupata muda wake binafsi. Lakini naamini ingewezekana, angeweza kuja.” Ric
akatulia kidogo.
“Unafikiri Elvin
anatupenda?” Bella alibaki
akifikiria, alijua Ric ameumia. Alihamia kitandani kwake na kujisogeza karibu
yake. “Sikiliza Ric, ninachojua Elvin ni mtu mzuri sana. Anapenda
kusaidia kila mtu, na asingependa kukuumiza. Lakini wakati mwingine katika
maisha, inakulazimu kuweka familia mbele. Kwa mfano mimi, inapokuja katika
swala la kuchagua, hata iweje, hata kama mtu mwingine ataumia, au hata kama
itanilazimu mimi kuumia, ni lazima nitakuchagua wewe kwanza. Kila kitu kinakuja
kwenye maisha yangu baada ya wewe, Ric. Ndivyo ilivyo hata kwake Elvin. Lazima
amchague mchumba wake kwanza, kwa kuwa ndiye mtu wa muhimu sana katika maisha
yake, lakini haimaanishi anachukia watu wengine. Ila ni kwa kuwa lazima kuweka
familia kwanza. Sijui umeelewa?” “Nimeelewa Bella. Na mimi
ninakuweka wewe kwanza. Wewe kwanza halafu wengine baadaye.” Bella
alianza kucheka. “Sasa hapo inamaanisha unachukia watu wengine?”
“Hapana Bella. Familia kwanza.” Waliendelea kucheka. “Sina
usingizi Bella. Unataka tucheze ‘game’ kwenye kompyuta yangu?” “Sawa.” Walichukua
kompyuta ya Ric wakaanza kushindana kucheza, karibu usiku kucha mpaka
panakaribia kupambazuka ndipo walipo lala.
“Mkasa
wa Irene.”
Huku nyuma Irene
alifanya fujo zakutosha, mpaka Mzee Mwasha akaja pale ofisini. Alimkuta Irene
akigomba sana, na Elvin yupo kimya akimsikiliza. “Naombeni tuzungumze
ofisini kwangu.” Mzee Mwasha aliingia nao ofisini. “Haiwezekani
Mzee Mwasha. Elvin anakitu na yule Bella. Nimeambiwa siku hizi wanakula wote
chakula hapa ofisini, na leo anataka kwenda nao mapumzikoni! Maana yake nini?
Elvin ni mchumba wangu mimi, au tuseme anakaribia kunichumbia. Inakuaje anatoka
na wasichana wengine?” Bado Irene alikuwa akigomba sana. Alikuwa
akiongea bila kunyamaza, Elvin na baba yake walikuwa kimya kabisa
wakimsikiliza. Alielezea mambo mengi sana juu ya uhusiano wao, jinsi Elvin
anavyoonekana kutokumthamini. Simu ambazo hakuwa hajibu kwa wakati, mpaka baba
yake alipokuja pale ofisini. Irene alianza kulia kwa baba yake, huku akiongea
kwa kulalamika sana. Elvin alikuwa kimya kabisa akisikiliza tuhuma zote.
************************************************
Irene alikuwa mtoto
wa Mzee Banda, mmoja wa wazee kwenye kundi lakina Mzee Mwasha. Ni
watoto waliokuwa wamekuzwa pamoja. Malezi yao yakifahari, huku wakiigiza uzungu
mwingi na kupewa kila wanachotaka. Tokea watoto Irene na Elvin walikuwa ni
marafiki wakawaida tu, mpaka baadaye walipokuwa wameshakuwa wakubwa tena Elvin
akiwa anakaribia kumaliza chuo, ndipo walipoanza mahusiano ya kimapenzi. Wazazi
walijua, na hakikuwa kitu cha ajabu kwani wazee hao walishazoea na kufurahia
jinsi watoto wao walivyokuwa wakioana. Tabia za Irene za kudeka na kutaka
kumiliki kila mtu, Elvin alizijua lakini alijiambia atakuja kubadilika. Irene
alipenda atambuliwe na kuheshimiwa kila alipo.
************************************************
“Hukufanya vizuri Elvin.
Unawezaje kusafiri bila kumtaarifu mwenzako?” Mzee Mwasha alimgeuki kijana wake. “Hapana Mzee
Mwasha, hapo unakosea. Ukisema bila kumtaarifu Irene tu, inamaanisha
unaidhinisha Elvin asafiri na msichana mwingine na sio Irene! Kama ni
mapumziko, kwa nini asisafiri na Irene?” Mzee Banda aliingilia. “Kweli daddy. Kama anataka kupumzika kwa nini
asiende kupumzika na mimi?” Aliendelea
kuongea Irene na baba yake akimuunga mkono, huku Elvin mtuhumiwa akiwa hajapewa
nafasi yakujitetea hata mara moja. Mzee Mwasha naye alikuwa kimya kabisa
akiwasikiliza mpaka walipomaliza na kuanza kumpa Elvin masharti huku wakimtaka
Bella afukuzwe pale kazini. Elvin alicheka kidogo.
“Umenielewa Elvin? Huyu
dada lazima afukuzwe kazi.” “Siwezi kumfukuza kazi Bella. Anahitajika sana hapa
kazini.” Elvin alijibu
taratibu tu. “Anahitajika au wewe ndio unamuhitaji?” Irene akauliza
kwa jazba. “Ni kweli Bella anahitajika sana hapa kazini. Hakuna jinsi
tukamfukuza labda aamue kuacha kazi yeye mwenyewe.” Mzee Mwasha
aliongeza. “Umeona daddy? Hata
baba yake anamtetea?” Irene alianza kulia.
“Unajua Irene
unanishangaza sana wewe! Unajua msimamo wangu jinsi ulivyo. Mimi siwezi kwenda
mapumzikoni na wewe, kwa kuwa najua mwisho wake utakuaje.” Elvin
alijibu. “Kama unahofia mapenzi, kwa nini sasa unakwenda na Bella?”
“Siendi na Bella, kama Bella. Nimekwambia mdogo wake ndiye aliyeomba niende
nao.” “Muongo Elvin. Kuna kitu anaficha.” Irene alijibu tena. “Kati
yangu mimi na wewe nani nimuongo, Irene? Unafikiri sijui uliyofanya na Phil
wakati mmesafiri na kina Junior Masha?” Irene alitulia. “Mimi
nilikuamini, ukasafiri nao, lakini ulifanya uchafu ambao hukutaka nije
niambiwe. Lakini nilikuja kuambiwa. Tena Phil alikuja kuomba msamaha yeye
mwenyewe, akijitetea ni kwa kuwa alikuwa amelewa sana siku ile, akawa
hajitambui. Nilikuacha makusudi bila kukuuliza. Nikijua labda siku moja ungeona
uliyofanya ni mabaya na kuja kukiri kwangu, lakini naona hujali, na unaendelea
kunidhalilisha mbele za watu na wafanyakazi wetu. Umenitia aibu mbele za watu,
wakati unanijua kabisa, au kila mtu anajua msimamo wangu. Nilikuapia Irene,
hata wewe sitakugusa mpaka ndoa. Inakuaje leo unafanya fujo kwa Bella, msichana
mgeni kabisa hapa, simfahamu, humfahamu! Umeishi na mimi muda wote huo,
umeshawahi kusikia nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mwingine
yeyote?” Elvin akamuuliza.
“Umeshafikiria maisha
yetu ya ndoa yatakuaje kama tukiishi kwa kutokuaminiana kwa kiasi hiki!? Mimi nilikuamini nikakuruhusu usafiri
na wavulana, nikijua utajiheshimu na kuishi ulichoniahidi. Lakini umefanya
tofauti, na bado hukuja kuniambia. Halafu bila hofu leo unaona nipo nakula na
watu, tena hadharani, unaleta fujo za namna hii! Umepiga simu kila mahali kwa
tuhuma zisizo za maana. Huogopi? Hivi unajua mimi ni kiongozi wao hapa ofisini?
Unanidhalilisha kwa tuhuma za uongo, mbele ya watu ninaowaongoza tena na
mfanyakazi wa humu humu ndani wanaemtegemea awasaidie kikazi! Unategemea kesho
akirudi hapa ofisini anafanyaje kazi na wenzake?” Elvin alifunga mdomo
kila mtu.
“Sasa na mimi nakupa
sharti moja. Usinitafute kwanza mpaka nitakapo kutafuta. Naomba upate muda wa
kufikiria, kabla hatujaingia kwenye hatua nyingine ya mahusiano yetu.
Inawezekana unampenda Phil kuliko mimi.” “Nakupenda Elvin.” “Naomba
usiniambie sasa hivi. Nenda, pata muda wakutosha, fikiria, nitakapokutafuta,
tutaongea.” “Nimeshafikiria. Nimekuchagua wewe.” “Sio kweli Irene. Ungekuwa
unanipenda kwa dhati, ungeniambia uchafu uliofanya na Phil, lakini umeficha,
ishara ya kwamba utakuja kurudia tena.” “Hapana Elvin.” “Basi kama wewe ulipata
muda wakufikiria, basi mimi nahitaji muda. Nipe muda, nitakutafuta. Nipo katika
wakati mgumu sana hapa kazini, nahitaji msaada ambao ni Bella peke yake
ameonekana anaweza kuutoa, tena kwa gharama ya chini. Tukiendelea hivi mimi na
wewe, tutazidi kuwachanganya wafanyakazi hapa kazini, mwishowe na hii biashara
itanishinda. Nahitaji muda Irene.” “Nitabadilika Elvin.” Irene
aliendelea kung’ang’ania.
“Mimi naona kitu
alichoongea Elvin ni cha msingi sana. Unahitaji muda wakufikiria Irene. Ndoa
sio kitu cha kuchezea. Mnaweza kuja kujuta sana baadaye.” Mzee Mwasha aliingilia. “Kama
hatanioa Elvin, ni afadhali kufa.” “Hayo ndio mambo nilikuwa nikizungumzia
Irene. Wakati wote unataka mambo yaende unavyotaka wewe, hutaki namimi nishauri
kitu katika mahusiano yetu. Sijakwambia tunaachana, nimekwambia tupate muda
wakufikiria.” Irene alinyanyuka. “Najua yote hayo amesababisha
Bella. Ulikuwa tayari kusamehe yote, mpaka alipokuja Bella.” Elvin
alitingisha kichwa kwa kusikitika. “Sidhani kama utabadilika Irene.
Wakati wote unatafuta mtu wa kulaumu na hutaki kuwajibika kwa makosa yako
mwenyewe.” Irene alitoka na baba yake akamfuata nyuma.
“Samahani sana baba.
Najua nimeharibu leo.” “Hapana, lakini nataka uniambie ukweli Elvin. Unampenda
Bella?” Elvin alikunja
uso. “Hapana baba, sio kimapenzi.” “Nimekuona jinsi ulivyohangaika
wakati alipolazwa.” “Bella ni mfanyakazi wetu baba, sikujua natakiwa nifanyaje
wakati alikuwa na matatizo. Hana ndugu, na alihitaji msaada. Umesahahu jinsi
alivyojitolea kwenye hii kampuni? Nafikiri haikuwa vibaya kumuonyesha na sisi
tunamjali. Na nimekubali kusafiri nao, kwa sababu ya mdogo wake. Alikuwa karibu
sana na mimi hizi siku mbili tatu alizokuwa hapa kazini. Aliponiomba nisafiri
nao, sikuona tatizo, kwa kuwa ni kweli nahitaji mapumziko baba. Nimekuwa na
kazi nyingi mfululizo na Irene yupo kila mahali. Sipumui baba. Sina raha, kila
kitu anataka iwe yeye. Na leo sio mara ya kwanza, hataki niongee na mtu wala
niwe na mtu yeyote ila yeye tu. Lakini yeye anataka awe huru na
kila mtu, na mimi nisiingilie. Na kila ninapomuhusisha kwenye mambo
yangu au kumkaribisha kwa marafiki zangu, nashindwa hata kuongea na wenzangu.
Anataka niwe naongea na yeye tu, au atataka watu wote wamsikilize yeye, wakati
wewe unajua aina ya marafiki zangu baba. Ni watu na heshima zao. Nahitaji
kupumzika. Na wala hutahitaji kuja kazini, nitaondoka hizi siku za sikukuu,
jumanne nitakuwepo kazini.” “Ni kweli tumekusahau Elvin, na wewe
unahitaji mapumziko. Akili zangu zote zimekuwa kwa mama yako, tukakusahau wewe.
Kwa kuwa sasa hivi anaendelea vizuri, unaweza kuchukua hata siku kumi, mimi
nitakuwepo hapa kazini.” “Asante.” Kila mtu aliondoka pale ofisini,
lakini Elvin alibaki ofisini kwake akifikiria.
************************************************
Maneno machafu aliyokuwa
akitupiwa Bella na Irene, yalianza kujirudia kichwani kwa Elvin. Alizidi
kuumia, alizunguka ofisi nzima akikumbuka hili na kutamani Irene asingesema
lile mbele ya Eric. Aliingia jikoni, akatoka. Akaingia ofisi za masoko asijue
ni nini kilimpeleka huko. Alizunguka huku sura ya Eric ikimjia jinsi alivyoonekana
kuumia mpaka usoni. Aliamua kurudi ofisini kwake angalau awapigie simu Bella na
mdogo wake angalau aombe radhi, lakini wakati yupo mlangoni alisikia simu yake
ikiita. Aliingia na kuichukua simu, kutoka mezani. Alikuwa dada yake Irene.
Elvin aliiangalia kwa muda kisha akapokea. “Irene amekimbizwa hospitali amekunywa sumu.” Elvin alibaki kimya. “We
Elvin, umesikia?” “Amepelekwa hospitali
gani?” Alipoambiwa, alijibu kwa kifupi. “Nakuja.” Kisha akakata simu.
Elvin alifikiria, akaamua kukaa. Alijua michezo ya Irene, alijua tu anataka
‘attention’.
Akaamua kuwapigia simu wazazi wake kuwataarifu. “Hivi na sisi tupo njiani tunaelekea huko hospitalini. Mama yake ametupigia simu alikuwa analia sana. Nahisi hali yake ni mbaya sana.” Mama yake Elvin alimjibu, akisikika anawasiwasi sana. “Na mimi nitakuja huko muda si mrefu, ngoja nifunge ofisi.” Elvin alifunga ofisi, akaelekea hospitalini.
Elvin alifika
hospitalini akakuta wazazi wa familia zote wapo hapo na baadhi ya watoto wa
familia zote wako hapo. Kila mtu alikuwa akimtizama Elvin wakati anaingia,
akajua tayari maneno yameshaanza kuenea. Alisogea mpaka alipokuwa amesimama
baba yake Irene, Mzee Banda. Alionekana na wasiwasi sana. “Vipi
anaendeleaje?” “Ndio yupo humo ndani na madaktari, wanajaribu kuokoa maisha
yake.” Mama yake Irene alikuwa akilia sana. “Poleni sana.
Naamini atapona.” Kila mtu alibaki akimwangalia yeye. Alikumbuka simu
alizokuwa akipiga Irene wakati amekasirika akiwa pale ofisini kwake, akajua
kila mtu anataarifa za yeye kutaka kwenda mapumzikoni na Enabella. Akaamua
anyamaze tu, kwani alijua hata angeeleza ukweli isinge saidia kitu.
Mama yake akamsogelea. “Pole na kazi.” Elvin alishukuru Mungu, maana alikuwa ni kama ametegwa. “Asante mama. Vipi na wewe? Unajisikiaje?” “Leo nimeshinda nimelala tu. Najisikia vizuri.” Wakati wanaongea, kaka yake Elvin naye akaingia. “Vipi Dogo?” “Shikamoo.” “Marahaba. Poleni bwana. Mimi ndio nimepata taarifa sasa hivi, wife yupo njiani na yeye anakuja. Vipi anaendeleaje?” “Ndio madaktari wanahangaika humo ndani, naamini kila kitu kitaenda sawa.” Alimgeukia mama yake. “Shikamoo mama.” “Mbona midomo imekukauka hivyo!? Umekula kweli wewe?” Mama Mwasha alimuuliza mwanae mkubwa. “Mambo yalikuwa mengi, sijala. Nitakula baadaye nikifika nyumbani.” Mama Mwasha aliendelea kuongea na wanae mpaka daktari alipotoka kuongea nao.
“Anaendeleaje?” Baba yake alisimama kwa haraka nakuuliza. “Anaonekana
hakuna sumu iliyokuwa imeingia tumboni. Mlimtapisha kabla yakuja hapa?” Daktari
akauliza. “Hapana.” “Basi nafikiri ni wasiwasi tu, vipimo vyote
vinaonyesha hakuna sumu yeyote mwilini mwake.” Watu walibaki
wakiangaliana, lakini Elvin alijua kabisa jinsi Irene anavyojipenda,
asingethubutu kujiua. Alichotaka nikushtua tu watu. Mama yake aliomba
wakamuone.
“Kwani nyinyi, ni nani aliwaambia amekunywa sumu?” Mama Mwasha aliuliza. “Mimi nilikuta kikaratasi alichokuwa amekiandika, ni bora afe kuliko kumkosa Elvin, na yeye alikuwa amelala na kujifunika shuka mpaka kichwani.” Msichana wa kazi alijibu, kwa kuwa wazazi wa Irene na ndugu zake walikuwa wameingia ndani kumuona Irene. Wengine walianza kucheka kimya kimya.
“Mama! Mimi naomba
utaniagia kwa Mzee Banda, nimechoka nataka nikalale.” Kaka yake Elvin akaondoka, na watu wengine nao
wakaanza kuondoka bila hata kuingia ndani na kumtizama huyo mgonjwa
aliyewashutua sana. Wote wakaondoka mpaka Elvin akajikuta amebaki peke yake
pale nje, akimfikiria Irene. Kwa vipimo vyote alivyokuwa amefanyiwa Irene,
mpaka kulipia matibabu, na daktari kupata muda wa kuongea kidogo na wazizi wa
Irene na Irene mwenyewe kwa ushauri, walijikuta wanaondoka hospitalini hapo
asubuhi. Na Elvin naye kama mchumba mtarajiwa ilibidi abaki nao pale mpaka
walipo ruhusiwa.
************************************************
Bella na mdogo wake
walifika uwanja wa ndege mapema kabisa. Walikaa pale wakisubiri muda wao
wakuondoka ufike, huku Eric akiamini Elvin atakuja tu. Bella alikuwa
akimwangalia vile anavyozunguka pale nje akifikiria labda angemuona Elvin,
akamuhurumia sana mdogo wake, asijue chakufanya. “Unafikiri Elvin
atakuja?” “Naomba uje ukae hapa, Ric.” Eric alikwenda kukaa pembeni ya
dada yake. “Unakumbuka nilikwambia Elvin anakuwa na mambo mengi?” Eric
alinyamaza. “Najua angeweza, angekuja.” “Lakini alituahidi kuwa
atakuja.” “Lakini si umeona jinsi familia yake wanavyomuhitaji? Kumbuka Ric,
familia kwanza.” “Kwa hiyo sisi hatuna familia? Mbona hakuna mtu
anayetuweka sisi kwanza?” “Mimi nakuweka wewe kwanza, Ric. Wewe ni
familia yangu.” “Hapana Bella. Unajua ni nini namaanisha. Unakumbuka ndugu zake
mama? Kumbuka kaka Mat. Hakuna mtu anayetuweka sisi kwanza.” Bella
aliishiwa maneno. Muda wa kupanda ndege ulifika, ndege ikaondoka, Ric asiamini
kama kweli wanaondoka jijini Dar bila Elvin.
Walifika mapokezi Bella
akijitambulisha ili kupata funguo za chumba kimoja na kurudisha cha pili
ambacho alikikodi maalumu kwa ajili ya Elvin huku mdogo wake akiwa amegeukia
mlangoni bado akiamini Elvin anaweza kuingia wakati wowote ule. Bella
alimalizana na muhudumu, akapewa funguo za chumbani kwao, huku akisaidiwa na
muhudumu mwingine kubeba mizigo yao kuingiza ndani. Eric bado hakuwa na taarifa
na kinachoendelea, kwani macho na akili zake zilikuwa zikisubiri mtu yeyote
anaeingia hapo huenda akawa ni Elvin.
Bella alisimama
akimtizam kwa muda, akamuhurumia sana. "Ric! We Ric!" "Namsubiri
Elvin." Bella alivuta pumzi kwa nguvu akazishusha. "Naomba
twende kwenye chumba chetu, kama Elvin atakuja, watu wa mapokezi watatupigia
simu. Twende angalau tukapumzike." "Mbona unamkatia tamaa mapema,
Bella? Tungemsubiri. Elvin atakuja." "Sijamkatia tamaa, ila sioni
sababu yakuendelea kukaa hapa mapokezi tukimsubiri. Naomba tuendelee na maisha
yetu Ric. Kama atakuja sawa, asipokuja pia ni sawa. Au hutaki kuwa na
mimi?" "Hapana Bella. Nafurahi kuwa na wewe." "Basi twende
chumbani kwetu." Eric aliondoka pale huku akigeuka nyuma kila
wakati.
Waliingia chumbani hapo akajitupa kwenye kochi bila hata kuzunguka na kuangalia madhari ya mle ndani chumbani kama kawaida yake ya kupenda kuchunguza kila sehemu mpya anayofika. Bella alimuomba yule muhudumu amsaidie kuingiza vitu vyote upande wa chumbani akarudi kukaa pembeni ya mdogo wake. “Tutakuwa na wakati mzuri Ric, naamini hivyo. Wakati wote tumekuwa na furaha tukiwa pamoja.” “Naamini hivyo Bella. Nataka nioge kwanza kabla yakulala.” “Nimebeba movie nzuri, tuangalie kabla ya kulala.” Ric akakubali. Wakaoga kisha wakapanda kitandani, na kuanza kuangalia movie yao.
Movie ikiwa katikati walisikia mtu akigonga. “Umeagiza kitu mapokezi?” Bella alimuuliza mdogo wake. “Hapana.” Mlango uliendelea kugongwa. Bella akajua atakuwa Mzee Masha tu. Akasimama haraka ili yeye ndio awe wakwanza kufungua na kumkabili kabla Eric hajamuona.
“Elvin!?” Eric alishtuka sana na yeye akasogea na
kumkumbatia Elvin. Wote waliendelea kulia huku wamemkumbatia Elvin.
Hawakutegemea kumuona Elvin pale, tena kwa wakati ule. Hata Eric mwenyewe
alishakata tamaa, akajua Elvin hawezi kuja tena. Elvin alizidi kuwahurumia, na
kuona alifanya vizuri kuja. Aliona ni kama watoto ambao wako wapweke.
Walisimama pale nje kwa muda huku Bella akirudia rudia “Asante, Asante Elvin!” wakiwa wote bado wamemkumbatia Elvin pale pale nje. Mwishowe Bella
alimpokea mizigo na kumkaribisha ndani. Walichukua muda kidogo, Bella na mdogo
wake kutulia. Wote waliingia ndani, wakakaa kwenye makochi wakaendelea kulia,
wasiamini kama kweli Elvin aliwafuata.
“Nilikusubiri sana
uwanja wa ndege, mpaka ndege ilitaka kuniacha.” Eric alikuwa akifuta machozi huku
akiongea. “Sikujua kama utakuja.
Bella aliniambia familia yako inakuhitaji, na wakati wote katika maisha unaweka
familia kwanza.” Eric aliendelea
kuongea akiwa bado analia. “Nilikuahidi nitakuja Ric, nisingeacha kuja.
Nilifika uwanja wa ndege nilikuwa nimechelewa sana, nikakuta ndege
imeshaondoka, ikabidi nichukue ndege ndogo tu niliyokuwa nimeikuta pale
uwanjani. Na kwa kuwa Bella alishaniambia hoteli tutakayofikia, haikuwa shida
kuwapata. Nilipotua tu uwanja wa ndege wa hapa, nikachukua taksii, ikanileta
mpaka hapa.” Bella bado alikuwa ameinama analia asiamini kitu Elvin
alichofanya. Eric alimsogelea karibu dada yake na kumkumbatia. “Asante
Elvin kwa kuja. Nimefurahi sana.” Eric aliendelea kushukuru.
“Mmekula? Mimi njaa
inauma, sijala tokea kile chakula cha jana mchana tulichokula pale ofisini.” Elvin aliwaangalia Eric na Bella. “Na
mimi njaa inauma.” “Ric! Wewe si nimekuuliza kama unataka kula, ukakataa!?” Bella
alimshangaa mdogo wake. “Nilikuwa sina njaa, sasa hivi nataka kula na
Elvin.” “Na mimi nataka kula.” Bella aliongeza. “Sasa mbona
mmeshavaa nguo za kulalia?” Elvin akauliza. “Tulikuwa
tunaangalia movie, kisha tulale.” Bella alijibu kinyonge kidogo. “Haiwezekani.
Mapema hivi! Kavaeni nguo tukazunguke kutafuta chakula.” “Bella anaweza
kuwapigia simu watuletee humuhumu chumbani.” Eric alijibu. “Hapana
bwana. Itakuwa hamna maana ya kuja huku kwenye jiji kubwa hivi halafu tukaishia
kujifungia humu ndani. Lazima tuzunguke na tupafahamu vizuri, ili tupate
chakusimulia.” “Yey…” Eric
alianza kushangilia.
Walirudi chumbani haraka, kila mmoja akabadili nguo, Bella alivaa gauni harakaharaka akatoka. “Hujachana nywele Bella!” Eric alimuwahi dada yake wakati anatafuta viatu vyake avae. “Who cares?” Bella alijibu huku anacheka. “Bella!!” Eric alimshangaa dada yake huku akicheka. “Yupo sawa tu, twendeni.” Bella alifurahi kuona Elvin hana shida kutoka naye vile alivyo. Hata hivyo hakuna jinsi Bella akaonekana asivutie kumwangalia. Alikuwa na kila kitu kizuri, kinachofanya urudie kumwangalia tena na tena. Lakini angekuwa na Masha, asingeruhusu atoke vile hata kidogo. Wakati wote Masha alimtaka awe msafi na kila kitu mwilini mwake kimuwakilishe vizuri. Wakati wote Bella alikuwa na kucha zilizotengenezwa vizuri, nywele safi tena zilizotengenezwa kwa ufasaha, na mavazi nadhifu, yaani kila kitu chake kilitakiwa kiwe kizuri. Na alienda kutengeneza kwenye saluni zamaana, sio uswahilini.
Walitoka pale ndani,
wote wakiwa na furaha sana. Walikodi gari ya hoteli ili iwapeleke mjini
wakazurule, kwa kuwa ile hoteli ilikuwa imejitenga, mbali kabisa na makazi ya
watu. Walishushwa katikati ya mji. Elvin aliwazungusha pale kwenye ule
mji. “Unajua unapokuwa mbali na nyumbani, unatakiwa kuweka kumbukumbu.
Na kufanya vitu vya ajabu, lakini vizuri kwa kuwa mpo ugenini hakuna
anayewafahamu.” Elvin aliwaambia. “Kama mimi nimetoka bila
kuchana nywele.” Wote walicheka. “Sasa leo tunaenda kula
gengeni.” “Kweli Elvin!?” “Ndiyo.” “Ric hataumwa tumbo?” Bella
alianza kuwa na wasiwasi na mdogo wake. “Hakuna kuumwa. Mbona watu
wanaenda kula kwa Mama Lishe na hawaumwi? Tena wanapika chakula kitamu sana.
Twendeni tukakae pale pale tule. Hakuna anayetufahamu huku.” Elvin
aliongeza. Wote wakakubaliana na wazo lake. Na kweli walizunguka wakitembea kwa
miguu huku wakicheka na kutaniana, huku wakitafuta Mama Lishe mwenye nafasi ya
kukaa wote watatu.
Wakakuta mmoja hajajaza watu
wengi. “Kunanukia?” Eric alinong’ona, wote wakacheka. “Sharti
la kwanza.” Elvin aliwaambia kabla hawajakaa. “Msiangalie wapi
wanapohifadhi sahani zao. La pili, usingalie jikoni. Mnasubiri kupewa chakula
chenu, unaangalia chakula chako tu, unaanza kula. Sawa?” Elvin
alinong’ona, wote wakacheka na kuitikia, “Sawa.” “Haya twendeni tukakae
tusubiri chakula.” Walikaa na kuanza kuongea bila hata kukumbuka wapi
walipo. Walikula wakamaliza na kubaki wamekaa pale pale wakiongea na kucheka
kwa muda mrefu sana, mpaka watu wote walipomaliza kula na wakataka kufunga
biashara yao. Bella alipiga picha nyingi sana pale walipokuwa wamekaa. Walikodi
tena taksii ikawarudisha tena hotelini.
Waliingia chumbani kwao wote wakiwa wamejawa vicheko. Walicheka hata vitu visivyo na maana. Walikuwa wakicheka mpaka machozi ya furaha yalikuwa yakiwatoka. “Nilijua hautakuja Elvin, nikarudisha chumba chako.” Bella alimgeukia Elvin mara walipokaa kwenye makochi. “Hamna shida. Kwa usiku huu naweza kulala kwenye kochi, kesho tutaenda kuchukua chumba kingine. Nitataka kuoga tu, ili nibadilishe hizi nguo. Kwa hiyo naomba ruhusa kutumia chumba chenu na bafu.” “Nilikuwa nina wazo. Kwa kuwa nyinyi mpo wawili, mlale hapo chumbani, mimi nilale kwenye kochi.” Bella alitoa hilo wazo. Kuwa Elvin na Eric wao ndio walale chumbani. “Naomba nikaoge kwanza halafu tutakuja kupanga vizuri.”
Elvin aliingiza mizigo
yake chumbani, akaingia kuoga na kurudi akiwa amevaa tayari nguo za
kulalia. “Ric zamu yako.” “Nilishaoga, Bella!” “Hapana, nenda ukaoge
tena. Ulioga kabla hatujatoka. Sasa hivi utakuwa umechafuka. Tumetembea na
kukimbia. Nenda kaoge.” “FINE.” Eric aliitikia kwa kutoridhika,
akasimama kuelekea bafuni kuoga kama dada yake alivyomwambia. “Elvin!” Elvin
alikuwa akiwaangalia wanavyoongea Bella na mdogo wake. Alitabasamu na kumgeukia
Bella vizuri. “Asante sana kwa kuja. Ric alikuwa...” Bella
alisita. “Nakushukuru sana, umeweza kufika.” Elvin alitabasamu
tena. “Wenzetu huwa wanasema ‘Thanks for having ME’. Na mimi nimefurahi kuja Enabella. Nilihitaji kutoa mawazo
yangu kutoka katika lile jiji la purukushani nyingi, angalau hapa tutapumzika
kidogo.” Bella alicheka kidogo.
Walikaa kwenye kochi
moja, kwa mara ya kwanza Bella alimuona Elvin akimwangalia kwa kutulia.
Alimtizama Bella huku akifikiria. “Umeacha kila kitu sawa nyumbani?” Bella
alijaribu kuvunja ukimya. “Sijui Bella. Ninachojua ni sasa hivi nipo hapa na
nyinyi, na ninataka kuutumia huu muda vizuri, sitaki hata kusoma ujumbe kutoka
sehemu yeyote ile.” “Na kazini!?” “Baba amenipa siku 10 zamapumziko. Yeye
ndio atakuwa pale ofisini. Tukitoka hapa, nitarudi nyumbani, nilale tu na
kumlea mama yangu kwa hizo siku zilizobaki ndipo nitarudi kazini. Sitaki
kusikia kitu kingine chochote. Nataka kupumzika kabisa.” “Ni jambo
zuri.” Eric alitoka.
“We Ric! Umepaka
sabuni kweli wewe!?” Bella alishangaa Eric ameshavaa nguo za kulalia
na hakumaliza hata dakika tano. “Hukuniambia nipake sabuni, umeniambia
nikaoge, Bella.” “Kila siku nakwambia kuoga ndio nakupaka sabuni, ukoje wewe!?”
“Hapana, kuoga nikutoa uchafu. Unaweza kutoa uchafu na maji bila
sabuni, kwanza ndio afya. Sabuni zina makemikali mengi.” Eric alirukia
kochi kwa nyuma na kukaa katikati ya Bella na Elvin akambusu dada yake. Bella
alimvuta sikio kwa nguvu. “Auuuu! What
did I do.” “Hiyo ni yakuoga bila kupaka sabuni.” Bella akaondoka. Wote
walikuwa wanacheka. Bella aliingia kuoga na yeye akarudi kukaa palepale kwenye
kochi lakini pembeni ya Elvin, wakajikuta wamemuweka yeye kati. Waliendelea
kuongea huku wakiangalia movie yao, wishowe Elvin akajikuta amebaki peke
yake, wote wawili walikuwa wamemuegemea wamelala.
Hapo ndipo Elvin
alipopata muda wakumwangalia Bella vizuri bila kupepesa macho. Walikuwa watoto
wadogo, na wote walikuwa wamemuegemea kama vitoto vilivyohitaji mapenzi.
Walifanana sana, karibu kila kitu, isingekuwa rahisi kujua kama ni watoto wa
baba tofauti. Elvin alimuweka Bella vizuri nakubaki akimwangalia. Alilala kama
mtoto mdogo, sura yake ni kweli alionekana ni mtoto. Lakini alikuwa na maisha
ya hali ya juu sana. Kila kitu alichoshika yeye na mdogo wake, kilikuwa cha
gharama sana. Hata hiyo hoteli ilionekana ni ya gharama sana. Maswali mengi
sana yalimsumbua Elvin.
Alikumbuka ni kama Bella
alizungumzia wapo peke yao katika maisha. Ndugu waliwakana na walikuwa
wakilelewa na mama yao, ambaye alishafariki. Na walipoteza kila kitu. Bella
alionekana ni msichana anayejitambua, na akili zake zinafanya kazi vizuri. Elvin
alipingana na wazo kuwa anaweza kuwa anachuna mabuzi. ‘Lakini ni
nani anampiga? Au anamwanaume ambaye alimfumania, akampiga sana? Lakini bado ni
mtoto mdogo, hawezi kuwa ameanza mambo ya wanaume. Au watakuwa wanautumia uzuri
wake kuwauzia madawa ya kulevya?’ Elvin alikuwa akiwaza, na
mwishowe akakubaliana na wazo hilo la mwisho. ‘Atakuwa anauza madawa
yakulevya. Maskini Bella, shida zimemsukumia kwenye biashara hatari.’ Elvin
alibaki akimwangalia huku akimuhurumia. Alimtengeneza nywele zake vizuri,
akamshika kwa upendo kama anayemuhurumia.
Alimnyanyua kwa nguvu
Eric, akamsimamisha na kumvuta kumrudisha kitandani. Alionekana kuchoka sana,
hata hakuwa na habari wakati Elvin amemshika mkono mpaka kitandani. Alimfunika
vizuri, akarudi kwa Bella. Akampandisha miguu yake vizuri kwenye kochi, akaweka
mto chini ya kichwa chake ili asiumie shingo, kisha akachukua moja ya shuka
kwenye kitanda cha pili kilichokuwa kimebaki, akamfunika mpaka shingoni akabaki
amekaa pembeni ya kochi akimwangalia kama mtu anayetaka kushibisha macho yake.
Muonekano wake alikuwa mtoto mdogo, lakini akifungua mdomo wake, alijawa hekima
tupu. ‘Unaweza kulipa gharama yeyote ile, ili kila siku uamke
pembeni ya hii sura.’ Elvin aliwaza kisha akatabasamu. Alikaa pale
kwa muda akimtizama mpaka alipolemewa na usingizi, akaamua kwenda kulala.
Alizima tv, nakuzima taa, akarudi chumbani.
Sura ya Bella ilibaki
machoni mwake, akabaki akikumbuka anavyocheka na kutabasamu huku dimpozi zake
kubwa zikipamba mashavu yake yakitoto. ‘Inaonekana Ric, ndiyo furaha
pekee ya Bella. Amekuwa watofauti sana, baada ya Ric kuja. Furaha yake itadumu
pindi Ric atakapo ondoka? Ataendelea kuwa karibu na mimi au mimi nimekuwa ni
njia yakumfurahisha mdogo wake tu?’ Elvin alianza kuona
anamuhitaji sana Bella. ‘Lakini hapana, Bella ni mfanyakazi wangu na
itabaki hivyo. Sitaki kujichanganya. Nina misingi yangu ya maisha nimejiwekea,
lazima niishi hivyo kwa kufuata kanuni hizo.’ Elvin aliendelea
kujikumbusha misimamo yake, huku mawazo mengine yakimfikiria Bella. Akapitiwa
na usingizi.
************************************************
Alihakikisha simu yake
inachaji kila wakati ili kuweza kuchukua picha zakutosha na ibaki ya
kuziangalia awapo peke yake kitandani. Bella naye alikuwa mwenye furaha kupita
kiasi. Alisahau kabisa maisha anayoishi jiji Dar akiwa na Mzee Masha. Kwa mara
ya kwanza baada ya muda mrefu, alisafiri bila Mzee Masha, na aliweza kuwa mtoto
tena, bila kuguswa au kulazimishiwa kufanya mapenzi. Alijiambia yupo kwenye
mapumziko ya akili na mwili. Eric ndiye aliyekuwa na wakati mzuri kuliko wote.
Alikuwa akiongea na kujisifia juu ya michezo anayocheza akiwa shuleni bila
kuchoka. Alijiona ni kama yuko katikati ya wazazi wake, gafla maisha yakaleta
maana. Wazo la Elvin kuchukua chumba kingine, walisha litupilia mbali,
wakaishia kutumia chumba hichohicho kimoja.
Kila siku walipokuwa
wakirudi hotelini Eric na Bella hawakuacha pia kuimba pamoja kabla ya kulala. Eric
alikuwa mtunzi mzuri sana wa nyimbo, lakini mama yake alimshauri atulie kwenye
michezo, kwani aliona atafanikiwa sana kwenye michezo kuliko uimbaji. Lakini
Mat hakuacha kumpeleka kanisani wakati wa mazoezi yake ya kwaya, kwa hiyo Eric
alijifunza kutumia vyombo vya mziki, kanisani. Bella naye alikuwa na uwezo
mzuri sana wakupiga kinanda. Tunu alipoona hivyo, akaamua kuwanunulia vyombo
hivyo na kuwawekea nyumbani kwao wawe wanatumia wawapo nyumbani. Alimwaga pesa
nyingi sana kwa watoto wake, na waliishi kama watoto wa milionea pale jijini.
Tokea wakiwa watoto Tunu aliwasogeza watoto wake kwenye vitu alivyoona
vitawasaidia baadaye. Eric alikuwa na uwezo wa kutunga nyimbo katika kila
tukio, mpaka alikuwa akimshangaza Bella na kila aliyekaribu naye. Hata kitu cha
utani tu, aliweza kutungia wimbo na kuimba vizuri sana.
“I miss my gutar,
Bella.” Ric alikumbuka
gitaa lake wakati akiimba. “I miss my piano.” Bella naye
alikumbuka kinanda chake. Elvin alikuwa akiwasikiliza wakati wanaongea. “Kwani
viko wapi?” Elvin aliuliza. “Tulipoteza kila kitu tulipoenda
kumzika mama. Tulirudi tukakuta wapangaji wapya, wakasema hawajui vitu vyetu
vilipo.” “Nakumbuka uliniambia, poleni sana.” “Asante.” Bella
alijibu. “Hey Bella! I made a knew song. You wanna hear it?” Eric
alitunga wimbo mpya, alitaka dada yake asikilize, usiku huo waliporudi hotelini
wakiwa kwenye nguo zao zakulali baada ya kutoka mjini kuzurula. “Mmmh!” Bella
aliitikia huku akijiweka sawa. “Wewe utakuwa kinanda na gitaa langu.
Sio mrefu sana, wala sio mgumu, nitaimba mara moja tu halafu tutaimba wote.”
“Sawa.” Elvin alikaa vizuri kuwasikiliza. Ulikuwa wimbo mzuri
sana, lakini uliwaliza Bella na mdogo wake, kiitikio kilikuwa hivi.
So soon you have gone,
So soon you left us,
See how soon the world have forgotten us,
Like a drop of tear in a sea, see how soon the world covered
us.
It was so soon, still so soon.
Bella alilia mpaka
akasimama na kwenda bafuni. Alishindwa kujizuia kabisa. Eric alitibua machungu
moyoni mwake, alikumbuka vile ilivyomlazimu kukua kwa haraka baada ya kifo cha
mama yake. Alikumbuka maumivu makali anayopata kila anapofanya mapenzi na Mzee
Masha, lakini ilimlazimu kucheka na kumuonyesha anafurahia kila kitu
anachomfanyia au anachofanyiwa kwenye mapenzi ili yeye na mdogo wake waendelee
kuishi. Bella alilia sana. Mwili mzima ulikuwa ukitetemeka kila akifikiria
jinsi Mzee Masha anavyompapasa na kumbusu mwili wake. Bella aliendelea kulia.
Vipigo anavyovipata tena bila kosa kutoka kwa Mzee huyo anayetumia mwili wake
bila shukurani, Bella alizidi kulia na kumkumbuka mama yake.
Eric aliingia bafuni na kutoka naye. Walipanda kwenye kitanda chake akamfunika dada yake, akabaki amelala pembeni yake. “Is gonna be fine Bella. Soon we are gonna be fine.” Bella alimsikiliza mdogo wake akijua hajui analoliongea, tayari alikuwa na ndoa ambayo alihakikishiwa haitakaa ikavunjika labda kifo. Alikumbuka anasubiriwa kwa hamu pindi atakaporudi nyumbani. Bella alijikunyata ndani ya lile shuka na kuficha uso wake huku akitetemeka kwa hofu na machungu. Alitamani mama yake arudi aje ampokee huo mzigo japo kwa siku chache apumzike kuwaza kesho itakuwaje kwake na hasa kwa mdogo wake.
Elvin alikaa pale sebleni
kwa muda asijue afanyaje. Alisogea karibu na chumbani akabaki amesimama
akiwatizama ndugu hao wawili ambao ni kama mapacha, wakibembelezana.
Alipoona wote wanaendelea kulia na hamna dalili ya kunyamaza, Elvin alimwambia Eric
ahamie kitandani kwake, alale. Na yeye akakaa pembi ya Bella aliyekuwa
amejifunika mpaka kichwani. Aliweza kuhisi jinsi Bella anavyotetemeka. Akaamua
kupanda na yeye kitandani, akamtoa ndani ya mashuka, akamvuta mpaka karibu
yake, alimuegemeza kichwa chake kifuni kwake, akamzungushia mikono yake, baada
ya muda Bella alitulia na kupitiwa na usingizi pale pale alipokuwa amekumbatiwa
na Elvin. Walikaa vile kwa muda, mwishowe Elvin akaamua asimtoe pale, amwache
alale tu mpaka atakapo amka, kwani Bella alikuwa amelala vizuri sana. Elvin
alivuta mto, akauweka nyuma ya mgongo wake, akajiegemeza vizuri, na yeye
akapitiwa na usingizi.
Bella alifungua macho
ilishakuwa asubuhi, tena yupo kifuani kwa Elvin, akiwa anamtizama. Alishtuka
sana, akajisogeza pembeni. “Ulilala salama?” Elvin aliuliza
kwa sauti ya chini ili wasimuamshe Eric. Bella alijisogeza pembeni zaidi, mbali
kidogo ya Elvin akatingisha kichwa kuashiria kukubali huku akikwepesha macho
yake. Elvin alibaki akimtizama. Bella alivuta shuka, Elvin akamsaidia
kumfunika. “Asante.” Bella aliongea kwa sauti ya chini sana
lakini Elvin alisikia. “Unataka kurudi kulala?” Elvin
aliuliza, Bella alitingisha kichwa kukubali. Elvin alinyoosha mkono kama
aliyetaka Bella amshike. Alikuwa amejisogeza mbali sana na yeye. Mwishoni
kabisa ya kitanda hicho kikubwa. Bella alibaki akiangalia mkono wa Elvin bila
kumtizama machoni, mwishowe alitoa mkono wake kwenye shuka taratibu akaushika
mkono wa Elvin, Elvin akamvuta karibu sana na yeye, akamgeuza kama ampe mgongo,
akamfunika tena vizuri. “Lala mimi nipo hapa na wewe.” Elvin
aliongea kichwani kwa Bella, akambusu kwenye kichwa chake, hapohapo akamsikia
Bella akihema akiashiria amepotelea usingizini. Hakutaka kumkumbatia tena, lakini
walikuwa wamelala karibu. Elvin alibaki akimwangalia huku akiwaza, mpaka na
yeye akapitiwa na usingizi mida hiyo ya asubuhi ya siku yao ya mwisho pale
hotelini. Walijikuta wote wanaamka saa sita mchana. Walikaa wakiongea palepale
kitandani, Bella na Ric wakitaniana, mpaka Bella alipoamua kuwaacha aende
kuoga.
************************************************
Walikuwa na mtindo kila
wanapokuwa wanakuwa mapumzikoni, usiku wa mwisho kabla ya kuondoka, wanaandika
vikaratasi na kila mtu anaandika kitu anachokitamani kitokee. Waliita ‘Wishing list game.’ Kila mmoja anaandika kwenye kikaratasi, kisha wanabadilishana na
kusoma kwa sauti ili wote wasikie. Eric alimuelezea Elvin huo utaratibu wao na
kutaka aungane nao. “Lakini sio lazima Elvin. Kama unaona haupo tayari,
unaweza kucheza wakati mwingine.” Bella aliingilia. “Hamna
shida, hata mimi ningependa kuandika kitu ninachotamani.” Bella
alitengeneza vikaratasi vitatu akawagawia kila mmoja. “Natakiwa
kuandika vitu vingapi?” Elvin akauliza. “Kimoja au viwili.
Visizidi viwili.” Kila mmoja alitulia akaandika, kisha Eric akampa Bella,
Bella akampa kikaratasi chake Elvin, Elvin akampa Eric.
“Nani anataka kuanza kusoma?” Bella aliuliza. “Mimi nitaanza.” Eric aliwahi akafungua cha kwake akaanza kusoma. “Hii inatoka kwa Elvin, ‘Natamani kupata mapumziko kama haya wakati mwingine’.” Wote walipiga makofi. “Kwa hiyo umefurahia, Elvin?” Bella akauliza huku akitabasamu na kumwangalia Elvin kwa upole. “Sana. Naamini wakati mwingine tutapata nafasi kama hii.” Walibaki wakiangaliana kwa muda, mwishowe Bella aliinama kama kukwepesha macho huku akitabasamu, akafungua kikaratasi cha Eric. “Mimi nitasoma wa pili, kinatoka kwa Ric. ‘Natamani kuwa na familia watakayo niweka mimi na Bella mbele.’” Walitulia kidogo kama wanaotafakari ule ujumbe. “Namimi nitasoma wish ya Bella.” Elvin alivunja ukimya. “Mko tayari kusikia wish ya Bella?” Elvin alitaka warudishe mawazo pale. “Soma Elvin, mimi nasikiliza.” “Sawa. Bella anasema, ‘Natamani kurudi kuwa mtoto tena. Hata kwa dakika moja tu, kupata mtu anayeweza kuwaza kwa niaba yangu. Kama wakati wa uhai wa mama. I want to be her little girl again. I want to get the place where I can hide my sorrow and fear again. I wish to be a little girl again.’” Machozi yalikuwa yakimtoka Bella. Na hiyo ndiyo ilikuwa shauku yake. Alikuwa akipigwa na kuonewa na Mzee Masha, lakini hakuwa na rafiki au mtu wakumwambia maisha anayoishi. Kila aliyemuona na Mzee Masha, alimuhukumu kama mwizi wa mume wa mtu, wasijue mateso anayopitia. Hakuruhusiwa kuwa na rafiki awe wakiume au wakike. Na simu yake ilikuwa ikifuatiliwa, kwa hiyo asingethubutu hata kumpigia mtu yeyote simu.
Baada ya kimya kirefu
kupita. Bella aliamua kumshukuru tena Elvin. “Tunashukuru kwa kuja na kuwa
pamoja na sisi. Asante sana.” “Na mimi nimefurahi kupata muda wakuwa pamoja na
nyinyi. Nimekuwa na wakati mzuri zaidi ya nilivyotarajia. Mimi ndio natakiwa
niwashukuru nyinyi. Asanteni.” Elvin alimwangalia Bella kidogo, kisha
akahamisha macho yake kwa Eric. “Asante Elvin. Utakwenda na sisi
kuangalia kaburi la mama kabla sijarudi shule?” “Eric!” Bella
alishtuka sana. “Hataweza. Elvin ana kazi nyingi sana. Hawezi
akaendelea kuwa anazunguka na sisi kila mahali. Hata hivi alivyofanya
tunatakiwa kushukuru.” Eric akanyamaza. Alishajua dada yake akimuita
jina lake lote kama lilivyo Eric, anakuwa hayupo kwenye
utani na amekasirika.
“Kwani mnataka kwenda lini?” “Hamna haja Elvin. Hamna sababu kabisa yakutusindikiza. Huwa tunaenda kila wakati Ric anapokuwa likizo, sio kitu kigeni, huhitaji kwenda. Najua una mambo mengi…” “Bella!” Elvin alimwita kama kutaka atulie. “Mnataka kwenda lini?” Bella alitulia kidogo. “Sijajua, naona siku za Ric kurudi shule zimekaribia, anatakiwa mpaka ifikapo Jumapili awe yupo shuleni. Kwa hiyo nilitaka kuomba kama naweza kupata siku zangu chache nyingine za likizo kabla hajarudi shule, ndio twende kwa mama.” “Na mimi si nimewaambia nipo likizo ya siku 10? Bado nimebakiza siku nyingi tu za kutosha. Mtakapokuwa tayari naweza kuwasindikiza.” “Huna sababu yakufanya hivyo Elvin, najua…” “Bella! Mimi ndio nataka kwenda. Labda kama una sababu nyingine.” “Hapana Elvin.” “Basi tupangeni safari.” “Nilifikiria labda turudi nyumbani, tupumzike hata siku moja, ndipo twende.” Bella alijibu.
“Mnaishi wapi?” Bella alishindwa kujibu kabisa. Alibaki
akibabaika. “Namaanisha nyumbani ni wapi mnapoishi kwa sasa?” Elvin
alirudia tena akidhani Bella hajaelewa. “Tunaishi Villa in Hotel. Ipo
Kawe.” Eric alijibu, na kumfanya Elvin ashtuke kidogo na kumgeukia
Bella. Bella aliinama. “Okay.” Elvin aliamua asiongeze kitu
katika hilo. “Kwa hiyo ni lini unafikiria tusafiri?” Elvin
aliendeleza maongezi akijitahidi kuficha hisia zake. Bella alibaki ameinama
akiwaza. “Bella?” Elvin aliita. “Nilikuwa nafikiria
labda twendeni Jumatano asubuhi na mapema, tugeuze jioni ili alhamis niwepo
kazini.” Bella alijibu kwa shida sana, akionyesha wazi ameishiwa
nguvu. “Ni sawa kabisa, wazo zuri.” Wote wakanyamza.
“Nataka niwahi kulala leo.” Bella alivunja ukimya. Elvin akamwangalia, kisha akauliza. “Hatuangalii movie leo?” “Mimi nitatangulia niwahi kulala.” Bella alijibu kinyonge sana. “Sawa.” Bella alisimama akaingia bafuni kuoga ili alale. “Nimefurahi tunaenda wote kwa mama, Elvin.” “Hata mimi nimefurahi Ric. Unataka tuangalie wote movie kabla hujaenda kulala?” “Leo naomba tucheze game. Bella ameninunulia game mpya nataka nicheze sana kabla sijarudi shule.” Walikubaliana wakaanza kucheza. Elvin aliposikia Bella anapanda kitandani, akamwambia Eric amsubiri kidogo anakuja.
Alimkuta Bella
ameshapanda kitandani kwake na amejifunika shuka. “Umeshalala?” Bella
alitoa kichwa nje. “Bado ndio nataka kulala.” Bella alikuwa
amepooza sana. “Upo sawa?” “Ndiyo.” “Mbona leo mapema wakati ulituahidi
leo hatuta lala?” “Naona nimechoka mapema.” “Njoo tuangalie hata movie moja
bwana. Usilale mapema. Tutumie huu muda vizuri.” Bella
alitabasamu. “Twende.” Bella alitoka ndani ya shuka na
kuongozana na Elvin kurudi alipokuwa Eric. Eric alikuwa na michezo yake
aliyokuwa ameunganisha kwenye tv hakutaka mtu aguse tv. “Huyo hapo hatatoka.
Hata ukimsemesha hatakujibu.” Bella alikuwa akimwambia Elvin. “Nimeona.
Maana aliniambia tucheze wote, naona mwenzangu amenogewa hanikumbuki
tena.” Wote wakacheka. “Ni sawa tukiangalia kwenye kompyuta
yangu?” Bella aliuliza kwa heshima kidogo akionyesha hofu kama ni sawa
au la. “Wazo zuri, ili tusimsumbue. Tumuache afaidi kwa mara ya mwisho
kabla hajarudi shuleni.” Walicheka wakarudi chumbani ili wakaangalie
huko.
Bella alianza kubabaika
ukaaji. “Tutaangalizia hapa kitandani au tukae chini tu?” Bella
akauliza. “Sakafuni tena? Baridi bwana. Tukae tu hapo kitandani.” Bella
alipanda kitandani akaingiza miguu ndani ya shuka, akapaka laptop yake. “Nilikuja
nazo nyingi, sijui hii itakuwa nzuri?” “Hata mimi sijawahi
kuiona. Tuangalie tu kupoteza muda. Unapenda sana movie?” Elvin
aliuliza. “Inanibidi kuangalia tu. Ric akiwa shuleni najikuta sina kitu
chakufanya.” “Mnaishi peke yenu?” Bella alinyamaza kwa muda mrefu
sana, mpaka Elvin alijua hatajibiwa.
“Eric akiwa likizo, huwa
napenda kuwa na yeye tu.” Hilo
jibu lilikuwa la jumla sana. Elvin alitamani kuuliza tena, lakini kutokana na
muda Bella aliochukua kujibu swali lililopita, alijua ni kiashirio kwamba
hayupo tayari kuzungumzia maisha yao. Movie ilianza, wakaanza kuangalia, wote
wakiwa kimya. “Unataka kujiegemeza hapa?” Bella hakujibu
akabaki amekaa wima kwa muda mwishowe akamuona anajivuta mpaka karibu yake na
kumuegemea. Elvin alihisi Bella anapitia wakati mgumu sana wamaisha. Ule
muonekano wa utajiri, alihisi unafunika machungu makubwa sana ndani yake.
Alitamani kujua zaidi, lakini aliona awe mvumilivu. Bella aliendelea kujivuta
mpaka alipojiegemeza vizuri kwa Elvin. Movie ilipoisha, Bella alikuwa
ameshalala kabisa. Elvin alimtizama kama mtoto anayetafuta sehemu ya kujificha,
na anapoipata ni kama akili zake zinatulia kabisa na kuweza kulala usingizi
mzito sana. Kila alipokuwa karibu na Elvin, Bella alilala muda huohuo, bila
kupoteza muda. Alimuweka vizuri kwenye mto, akamfunika na kurudi kumwangalia Eric,
ambaye ndio ilikuwa kama kuna kucha.
************************************************
Walitua jijini Dar, mida
ya jioni. “Niliacha gari hapahapa uwanjani. Unataka tukusindikize mpaka
nyumbani?” Bella aliuliza wakati wanashuka kwenye ndege. “Kama
hamjachoka sana. Vinginevyo naweza kuchukua taksii tu.” “Sawa.” Bella
alijibu. “Sawa nini sasa?” Elvin akauliza. “Sawa kama
ulivyosema, kuchukua taksii.” Elvin alimtizama Bella. “Nataka
uwe huru Elvin, sitaki tukupeleke halafu iibue matatizo mengine.” “Twendeni
mlipoegesha gari kwanza. Tutaongelea huko sio hapa.” Walifika kwenye
gari Eric akaingia na kulala kwenye kiti cha nyuma. Alikesha akicheza ‘games’
zake kwenye tv, mpaka palipo pambazuka. Bella aliamka na kumkuta bado anacheza,
ndipo alipompokonya ‘remote’ alizokuwa akichezea, na kumlazimisha alale japo
kwa lisaa kabla hawajaondoka, kwa hiyo bado alikuwa na usingizi.
Elvin aliwasaidia kupandisha mizigo yao kwenye gari hilo la kifahari sana, akabaki akijiuliza bila majibu. Alipiga mahesabu ya kuacha hilo gari hapo uwanjani kwa siku zote nne, walizokuwa wamesafiri, alijua itamlazimu Bella kulipia pesa nyingi, lakini Bella hakuonekana na tatizo lolote juu ya pesa. Aliingia akakaa kwenye kiti chake cha dereva, Elvin akaenda kusimama dirishani kwake.
“Naomba nichukue
taksii, ili wewe umuwahishe Ric akalale. Kuna foleni sana sasa hivi, mpaka
unifikishe mimi nyumbani halafu mje mrudi kwenu, itakuwa usiku sana.” “Sawa.” Bella
aliitikia. Elvin alimuangalia Bella kutaka kujua kama kweli ameridhika, lakini
Bella alikwepa sana kumuangalia machoni. “Nitakupigia simu basi baadaye
kujua kama mlifika salama.” “HAPANA.” Bella alishtuka, kama aliyetaka
kuruka kutoka kwenye kile kiti cha gari, nakutokea dirishani. Bado Elvin
alikuwa amesimama dirishani kwake akimtizama. “Namaanisha hamna sababu
ya kupiga, tutafika salama tu.” Elvin alibaki akimtizama wakati
anajitetea. “Sawa. Basi utanijulisha mkifika salama.” Bella
alinyamaza. “Bella?” Elvin alikuwa amekunja uso kama haelewi
tena.
“Kwa hiyo
hatutawasiliana tena? Yaani hapa ndio mwisho wa maongezi yetu!!?” “Ulisema
tutaenda wote kule kwa mama.” Bella alionyesha wasiwasi sana usoni. “Tunaendaje
bila mawasiliano, Bella? Sijui mnaishi wapi, wala hutujapanga mpango wowote
ule. Haya kwenu sipafahamu labla nije kuwachukua au niwafuate tuondoke pamoja,
sijui tunakutana wapi, sijui tunaondoka saa ngapi! Mpaka sasa sina uhakika kama
kweli unataka twende wote!” “Nataka twende wote Elvin, lakini..” Bella
alinyamaza nakuanza kufuta machozi. “Hata nikikwambia hutaelewa Elvin. Nitakutumia email.” “Unajuaje kama sitaelewa wakati hujajaribu
kuniambia kitu hata kimoja, nikashindwa kukuelewa?” Bella alibaki kimya. “Eti Bella?” “Naomba nikutumie email nikifika tu nyumbani.
Nitakuwa nimetulia na nitakuwa nimejua muda na mahali pa kukutania hiyo kesho
kutwa.” “Naweza nikaenda na
basi pia, ili kupunguza usumbufu. Halafu nitawatafuta tukifika huko. Muwe na
usiku mwema.” Elvin aliaga
akaanza kuondoka, Bella alijua kabisa Elvin amekasirika. Bella alishuka na
kumkimbilia.
“Elvin! Elvin! Naomba
usiondoke.” Elvin alisimama na
kumgeukia Bella akiwa kimya kama anayetaka kumsikiliza anachoongea. “Unakumbuka nilikwambia ipo siku tutaongea, na
nitajibu maswali yote?” Bella alikuwa akiongea huku akifuta machozi.
Alionekana anazidiwa na uchungu uliopo ndani, machozi yalikuwa yakichirizika
kama mvua. “Naomba univumilie,
ipo siku nitaweza kujibu maswali yako, lakini sio leo. Tafadhali Elvin. Naomba
usikasirike na naomba twende wote kwa mama. Nitakupitia mahali ambapo naomba
uniambie sehemu itakayokuwa rahisi kwako, na ninaomba iwe asubuhi sana.
Tukiondoka hapa Dar hata saa kumi na moja asubuhi itakuwa vizuri, ili tuweze
kugeuza siku hiyohiyo, ili kesho yake niwe kazini. Please!” Elvin alivuta pumzi akatulia kidogo. “Mtanikuta
nje ya kituo cha mabasi ya Ubungo, hiyo saa kumi na moja kamili ya asubuhi.” “Asante sana.” Bella akashukuru. “Muwe waangalifu
huko njiani. Tutaonana kesho kutwa.” “Usiku mwema Elvin.” Bella aliaga na kurudi
kwenye gari yake. Asingethubutu kumwambia ukweli Elvin hata iweje, si kwa ajili
ya aibu tu, hata usalama wa Elvin mwenyewe.
“Historia ya familia ya Mwasha.”
Elvin ni mtoto wa mwisho
katika familia ya Mzee Mwasha. Walizaliwa wanne, wote watoto wa kiume. Walilelewa
kwenye maadili yaki Mungu sana. Katika kundi la wazee la kina Mzee Masha, Mzee
Mwasha hakuwa miongoni mwa matajiri sana kama kina Mzee Masha. Mara nyingi
biashara yake ilikuwa inafilisika lakini kwa msaada wa kifedha wa Masha na
watoto wake Mwasha mwenyewe, alikuwa akifufua biashara hiyo na kuendelea.
Katika maisha yake, Mzee Mwasha alichoangalia ni kusomesha watoto wake na
kusaidia watu. Utajiri au kuwa na mapesa mengi haikuwa furaha yake au lengo la
kuhangaika kwake.
Furaha yake na mkewe
nikuona wana uwezo wa kusaidia watu. Kwa hiyo hata watoto wao waliwalea hivyo.
Katika watoto wa kundi lao, ni vijana wa Mzee Mwasha tu ndio walikuwa na
tofauti kubwa na hata wenzao waliwajua. Walikuwa na maadili mazuri sana,
isipokuwa anayemfuata Elvin. Wanasema katika kila familia hakosekani angalau
mwana mpotevu mmoja, basi ndivyo alivyokuwa Eli. Wengi walimjua kama ‘cha
pombe’. Alisomeshwa kama wenzake mpaka shahada ya kwanza, na kubaki kuwa
mlevi. Yeye na Elvin ndio walikuwa wakiishi nyumbani kwao. Japokuwa alikuwa ni
mlevi sana, lakini Eli alikuwa akimpendwa sana na mama yake. Alishasema
ni msalaba atakao beba mpaka kifo chake.
Na Eli alimpenda mama
yake sana, kila mtu alijua, hata kwenye baa alizokuwa akienda kunywa walijua
Eli anampenda mama yake. Alizunguka na picha ya mama yake kwenye walert yake.
Nakumuonyesha kila mtu. Chumbani kwake kulikuwa na picha moja tu ya mama yake.
Hapakuwa na siku Eli alirudi nyumbani bila kuwa amelewa na kila siku hata kama
alikuwa mbali vipi, alihakikisha lazima kila usiku akutane na mama yake kwanza
kabla mama yake hajalala, ndipo yeye arudi bar kwenda kunywa na hakuacha
kumletea zawadi, hata pipi alinunua na kumjia nayo mama yake, ndipo alipotoka
kwenda kunywa. Hata kama mama yake akisafiri, alihakikisha kila usiku anampigia
simu kabla hajalewa. Mzee Mwasha alishaongea naye sana, mpaka akashindwa.
Ilikuwa ngumu sana kumkuta Mzee Mwasha anaongea na Eli. Mbali na salamu,
hawakuwa na maongezi yeyote yale ya ziada.
Mtoto wa kwanza wa Mzee
Mwasha, alishaoa na alijaliwa kazi nzuri. Alimuoa mtoto wa kwanza wa Danny
Mwanja, mmoja wa Wazee wenzake Mzee Mwasha. Mtoto wa pili ndio alikuwa Daktari
nchini Dubai, ndiye aliyemtibu Bella, halafu Eli ambaye alikuwa akiishi kwa
pombe tu. Hakutaka kuoa wala hakuna aliyejua kama ana msichana. Alikuwa akinywa
karibia usiku kucha. Wakati mwingine alirudi nyumbani kubadili tu nguo na
kuwahi kazini. Alikuwa ni Muhandisi katika kampuni ya simu akisaidia mitambo ya
simu. Kila mtu alijua analipwa vizuri. Na hata kazini alikuwa akijituma sana.
Alishaombewa kwenye makanisa mbali mbali, akapelekwa kwa washauri, lakini
haikusaidia, alibaki kuwa mlevi wakupindukia. Hapakuwa na jinsi Eli
alikubali kuishi mbali na mama yake. Alipewa chumba cha nje kwenye nyumba
hiyohiyo ya Mzee Mwasha. Mbali na kitanda cha kifahari alichonunua ambacho
alilalia yeye, na gari zuri sana alilokuwa akiendesha, hakuwahi kununua hata
kiwanja. Alijua kuvaa, na alikuwa mcheshi sana. Hata wakikusanyika nyumbani
kwao, bila kuwepo Eli, wanakuwa wamepooza sana. Watoto wa kaka yake mkubwa,
yaani JJ, walimpenda sana Eli.
Elvin alisomea mambo ya
uongozi. Na ndugu zake walimuomba yeye ndiye abaki nyumbani kusaidia wazazi. Kuanzia
mambo ya biashara zao, na pale nyumbani, kwani Mama yao alikuwa akiugua mara
kwa mara na baba yao alikuja kuanza kusumbuliwa na pressure pia. Kwa hiyo mambo
ya kampuni yao yakabaki yakilegalega, kwa kuwa muda mwingi Mwasha aidha alikuwa
mgonjwa yeye mwenyewe au alibaki nyumbani akimuuguza mkewe. Kwa kuwa Elvin
alikuwa mtu sikivu sana, Mzee Mwasha alimpenda na kumtumia katika kila kitu.
Yeye ndiye alifuata njia zote za wazazi wake, ikiwemo kumcha Mungu. Alikwenda
kanisa moja na wazazi wake, na hakuwahi kusumbua kabisa tokea utoto wake.
Alipomaliza chuo, baba yake akamwajiri, na kuanza kumlipa mshahara mzuri tu. Na
kwa kuwa hakuwa na makuu, na msichana wake Irene alitoka kwenye familia
inayojiweza, hakuhitaji pesa yeyote kutoka kwa Elvin, kwa hiyo Elvin akajikuta
anauwezo wakutunza pesa yake. Alinunua kiwanja, akaanza kujenga taratibu
kutokana na mshahara anaolipwa na baba yake.
************************************************
Elvin alirudi nyumbani
kwao, moja kwa moja aliingia chumbani kwa mama yake. “Vipi, umekuwa na
wakati mzuri huko?” “Nimepata muda wakupumzika. Shikamoo mama.” “Marahaba.” Mama
yake alibaki akimwangalia kama anayemsoma. Elvin alijua, akataka kumtoa kwenye
mawazo. “Mbona upo peke yako?” “Eli ameondoka hapa muda sio mrefu, na
baba yako yupo njiani anarudi.” “Unajisikiaje?” “Kuchoka tu.” “Twende ukatembee
kidogo.” “Nimechoka Elvin.” “Sitakuzungusha sana. Tutoke ufanye mazoezi kidogo
tu. Ukirudi ndio utalala vizuri.” Mama Mwasha alitoka na Elvin
wakaanza kutembea mtaani kwao.
Alikuwa akimwangalia Elvin kwa makini
sana. “Vipi Elvin?” “Safi tu. Kwa nini?” “Nauliza tu.” Waliendelea
kutembea, lakini safari hii Elvin alionekana tofauti. Japokuwa hakuwa mcheshi
kama Eli, lakini angalau alikuwa akiongea na mama yake mambo mengi sana
yanayoendelea kwenye maisha yake. Hakuwa akimficha kitu. Lakini safari hii hata
yeye hakujua ni nini amwambie mama yake. Mengi yalikuwa yakiendelea kichwani
mwake.
“Mmewasiliana na Irene?” Mama yake alimtupia swali, Elvin akashtuka
kidogo, alishasahau kabisa habari za Irene. Akili yake ilijaa Bella tu.
“Nilimuomba anipe nafasi ya kufikiria. Nataka muda mama. Sitaki tuje tuoane na
Irene halafu wote tukaja kujuta.” “Ni kweli. Baba yako aliniambia juu yake na
Phil. Kwa nini hukuniambia?” “Nilikuwa nampa muda nione kama atajirudi. Phil
alisema sio kwamba walikuwa na mahusiano, ni kitu kilitokea akiwa amelewa na
alisema ni bahati mbaya.” “Na Irene?” Mama yake akauliza. “Sijui
mama. Wewe unamjua Irene. Hajaniambia chochote. Kitu kinachonichanganya zaidi
ninajua Irene hanywi pombe. Sasa najiuliza ni kwa nini alifanya hivyo? Je Phil
ndio mwanaume pekee anayefanya nae huo uchafu au wapo wengine nje ya kundi letu
ambao hatuwafahamu? Na mbaya zaidi Irene hawezi kukubali kosa lake hata iweje. Wakati
wote anatafuta kulaumu mtu ndio atoke kwenye kosa lake.” Mama Mwasha
alibaki kimya.
“Nitafanyaje mama?”
“Bado unampenda?” Mama
yake akamuuliza swali dogo tu, lakini Elvin alishachanganywa na Bella, mpaka
akawa hajui tena kumpenda mtu kimapenzi kukoje. Hakuweza kulinganisha hisia
anazojisikia akiwa na Irene na kile anachojisikia akiwa na Bella. Mtoto huyo
mcha Mungu tokea kuzaliwa, alianza kupatwa na hisia ambazo hakuwahi kusikia
hata alipokuwa chuoni alipokuwa akizungukwa na warembo wa kila namna. Bella
aliibua hisia mpya, ngeni tena za tofauti ndani yake na kuachwa hajielewi hata
kidogo.
************************************************
Mambo yanambadilikia Elvin.
Taratibu Bella anaanza kumchanganya. Wana miahadi ya kwenda kutembelea kaburi
la mama yao huko kijijini.
* Je, Masha atakubali
waongozane tena?
* Nini kitatokea kwa Elvin na
Bella anayechungwa kama roho ya Masha?
* Nini kitaendelea kati ya
Bella na Masha?
Usikose kuendelea kufuatilia
kwenye Sehemu ya 7.
0 comments: