Story
lijaribu kufikiria
anavyojisikia akiwa na Irene na Bella, akaona tofauti kubwa sana. Usiku Bella
aliolala kifuani mwake, alipata hisia ambazo hakuwahi kusikia kabla, tokea
azaliwe. Alikuwa ni kama amelala amekumbatia alumasi. Kila alipofikiria,
ilimjia sura ya Bella akimtizama na macho yake mazuri na matulivu. Elvin
aliendelea kumfikiria Bella, wakati mama yake akisubiria jibu. Alikumbuka jinsi
Bella alivyoonekana na furaha wakati wakicheza mpira ziwani, meno yake mazuri
na dimpozi zake zilizoongeza uzuri wa sura yake. Elvin aliendelea kufikiria.
Mpaka wanarudi nyumbani, Elvin hakuwa ametoa jibu.
My Past - Sehemu ya 7.
|
A
|
lijaribu kufikiria
anavyojisikia akiwa na Irene na Bella, akaona tofauti kubwa sana. Usiku Bella
aliolala kifuani mwake, alipata hisia ambazo hakuwahi kusikia kabla, tokea
azaliwe. Alikuwa ni kama amelala amekumbatia alumasi. Kila alipofikiria,
ilimjia sura ya Bella akimtizama na macho yake mazuri na matulivu. Elvin
aliendelea kumfikiria Bella, wakati mama yake akisubiria jibu. Alikumbuka jinsi
Bella alivyoonekana na furaha wakati wakicheza mpira ziwani, meno yake mazuri
na dimpozi zake zilizoongeza uzuri wa sura yake. Elvin aliendelea kufikiria.
Mpaka wanarudi nyumbani, Elvin hakuwa ametoa jibu.
Walimkuta Mzee Mwasha
amesharudi nyumbani. “Kumbe bwana mdogo
umerudi!?” “Shikamoo baba.” “Marahaba, likizo imeisha?” “Hapana, nitaondoka
tena kesho kutwa, alfajiri, lakini nitarudi usiku sana.” “Wapi tena?” Mzee
Mwasha akauliza. “Namsindikiza Bella na
Ric, kwenye kaburi la mama yao.” Mzee Mwasha na mkewe wakaangaliana, Elvin
aliwaona. “Mbona mnaangaliana?” “Hebu kaa
chini kwanza Elvin.” Elvin akakaa.
“Mazungumzo ya mwisho na Irene nilikusikia ukimwambia unahitaji
muda wa kufikiria. Umefikia wapi?” “Hata week haijaisha baba, unataka nitoe
jibu leo! Bado nafikiria.” “Kweli Elvin?” “Tangia lini umeanza kunitilia mashaka, baba!?” “Mimi sidhani kama hiyo
ni njia sahihi yakufikiria Elvin. Huwezi ukawa kwenye matatizo na msichana huyu,
ukasema unataka upate muda wakufikiria, halafu unakuwa na msichana mwingine,
ambaye ni msichana kama Enabella! Huwezi kufikiria vizuri.” “Bella ana nini?”
“Anakila kitu ambacho kinaweza kukufanya ushindwe kufikiria vizuri. Huwezi
kumfikiria Irene kama ukiendelea kujiingiza kwenye maisha ya Bella. Utafikia
mahali hutaweza kutoka tena.” Elvin alinyamaza.
“Unanielewa Elvin?” Elvin alikaa kimya. “Utajichanganya sana Elvin. Hujafikia mwafaka na Irene, unaanza tena na
Bella!” “Hamna kitu chochote kinachoendelea kati yangu mimi na Bella, baba.”
“Elvin!” Mama yake alimuita kwa kushangaa. “Kweli mama, nipo nao kwa kuwa mdogo wake aliniomba niwasindikize.
Hawana ndugu, wako tu wenyewe. Ni kama nawasaidia tu.” “Sikiliza Elvin, ukubali
au ukatae, kuna namna huyu msichana ameshaanza kukuingia kwenye akili yako.
Mimi nakufahamu mwanangu. Tokea
anaugua hospitalini, mpaka umeenda naye huko, umerudi umebadilika kabisa.” “Nimekuaje mama?” “Kuna kitu kimebadilika
Elvin. Nimekuuliza kama unampenda Irene wakati umenipeleka kutembea, unajua
hujajibu mpaka sasa?” “Ni kwa kuwa Irene amenisaliti mama. Unafikiri hisia
zinaweza kuwa vilevile?” “Ni lini umejua kama Irene amekusaliti?” Baba yake
akamuuliza swali lililomfanya Elvin kuishiwa nguvu kidogo.
“Ni muda kidogo, baba.” Elvin akajibu bila ujasiri. “Sasa kwa nini unafikiri sasa hivi ndio unahitaji muda?” “Kwa kuwa na
mimi nilijua Irene ni binadamu, anaweza kukosea baba. Nikaamua kumpa muda,
nimefungua moyo wangu wote kwake. Nimefanya kila kitu ili aamini nampenda na
kumuhitaji ili tu aniamini, angalau akiri kosa lake. Lakini ameshindwa. Wewe
ulikuwepo kwenye mazungumzo yetu, baba. Umemuona jinsi alivyojibu hata baada ya
kumwambia kama nimejua amenisaliti. Je unafikiri ni mtu kweli anayeweza kuja
kubadilika baadaye? Nyinyi wenyewe mmeona kitendo alichofanya cha kudanganya
kuwa amekunywa sumu wakati ni muongo, shida yake ni watu wamuonee huruma, na
kunilazimisha mimi niwe naye, bila kutaka kubadilika. Naombeni mnisaidie wazazi
wangu, kweli huyu ndio mwanamke mnataka niwe naye kwenye maisha yangu yote hapa
duniani? Leo amedanganya hili, na amefanikiwa kuniwekea picha mbaya kwa watu,
nikiwa sijamfanyia kosa lolote lile. Kila mtu sasa hivi ananisema vibaya. Haya,
nikija kumuoa je? Akinisingizia kitu kikubwa zaidi? Najua watu wanabadilika, na
ndio maana nataka nimpe muda Irene, nione kama atabadilika. Siwezi kukimbilia
kwa Bella. Hata hivyo Bella anafahamu kuwa Irene anakaribia kuwa mchumba
wangu, na ameonyesha kuheshimu hilo.” Mzee Mwasha na mkewe waliishiwa maneno kabisa. Elvin alikuwa
kijana mtulivu sana, hakuwa akipenda makuu, na hakuwahi kuwasumbu.
“Mimi nimeelewa Elvin. Nakuombea Mungu akupe busara katika maamuzi
yako.” “Asante baba.” “Mimi ninachotaka uwe na furaha tu. Lakini sitaki uje
kuwa njia panda. Maamuzi utakayofanya mapema yatasaidia sana. Kwanza wewe
mwenyewe, pili Irene na tatu jamii inayotuzunguka. Maneno yanaenea Elvin.
Sitaki ukageuka ukawa gumzo kwa marafiki zetu. Umekuwa kijana mzuri sana. Usikubali
ukaharibu sifa yako kwa kuchelewa kutoa maamuzi. Na pia nataka ufahamu hili,
hautalazimishwa na mtu yeyote kuoa. Sisi tupo nyuma yako tunakuombea Mungu
akupe mwanamke atakaye kufaa. Umesikia?” “Asante mama.” Elvin akasimama na kumbusu
mama yake. “Naomba nikaoge ili nilale.”
“Huli chakula?” Mama yake akauliza. “Nilikula
na kina Bella kabla hatujaanza safari. Kwa hiyo sina njaa. Nitawaona kesho.”
Elvin alienda chumbani kwake akaacha wazazi wake wakitizamana.
**********************************
Ni kweli alioga na
kupanda kitandani kwake, lakini usingizi ulikuwa hauji. Kila akifunga macho
alimuona Bella. Alitamani usiku ule uwe ni kama ule usiku aliokuwa amelala naye
akamuweka kifuani mwake. Alihangaika pale kitandani mpaka alipopitiwa na
usingizi. Alianza kuota amelala na Bella, huku amemkumbatia na kumfariji. Elvin
alishtuka akakaa kitandani. ‘Mungu
wangu! Inawezekana mama yupo sahihi. Bella ameshaniingia akilini mwangu!’
Elvin aliendelea kuwaza. ‘Lakini
hapana. Nikawaida tu, kwa kuwa nililala naye na kwa kuwa sikuwahi kulala na
mwanamke kwanza. Yeye ndio msichana wa kwanza kulala naye. Lakini Bella ni
mzuri sana.’ Elvin aliendelea kuwaza huku akicheka.
Alikumbuka utani
waliokuwa wakitaniana, jinsi Bella alivyokuwa akicheka mpaka machozi yalikuwa
yakimtoka kwa kucheka. Elvin alibaki akicheka peke yake pale kitandani. Alivuta
laptop yake kuangalia kama Bella alimwandikia kama alivyoahidi, moyo wake
ulijawa na furaha sana, kukuta email kutoka kwa Bella.
‘Elvin, hakuna neno linaloweza kuwakilisha shukurani zangu kwako.
Asante kwa kukubali kuwa na sisi, inamaana kubwa sana kwetu, hasa Eric.
Amefurahi sana. Najua unamaswali mengi ungependa kupata majibu kutoka kwangu,
lakini nakuomba Elvin, unipe muda. Ipo siku nitayajibu yote, bila kukuacha na
swali hata moja. Kama hakuna lolote litakalotokea hapa katikati, nategemea
kukuona kesho kutwa saa 11 asubuhi kama tulivyopanga. Asante kwa kila kitu
Elvin. Nakushukuru.’
Bella.
Ilimchukua muda mrefu
sana Elvin kumaliza kusoma huo ujumbe na kufunga hiyo laptop yake. Alikuwa
akirudia rudia na kujiuliza maswali. ‘Amesema Eric amefurahia sana, kwani yeye
hajafurahia? Lakini atakuwa amefurahia, mbona kila alipokua akiniegemea alikuwa
analala hapo hapo.’ Elvin
alitabasamu lakini taratibu tabasamu lilianza kupotea. ‘Kwa nini Bella hataki nimpigie
simu? Nani alimpiga Bella? Nini anaficha na ni kitu gani kinamnyima raha? Ni
kama anatamani kuniambia lakini anaonekana anaogopa sana. Nini anaficha? Na
lini ataniambia?’ Ulikuwa ni usiku mrefu sana kwa Elvin, alitamani
pakuche masaa yaende haraka, ili akiamka tena akaonane na Bella.
Huko kwa Bella baada ya kurudi
kutoka Safari.
Wakati anakaribia
kulala, aliona ujumbe unaingia kwenye simu yake, Bella akajua ni Mzee Masha.
Akavuta simu na kuanza kusoma.
‘Naona mmesharudi!’ Zikaanza kuingia picha
zake akiwa uwanja wa ndege na Elvin nje ya gari wakizungumza. ‘Nimechoka nataka kulala, T. Naomba tuongee kesho.’ Bella alijibu kwa
kifupi, akamtumia huo ujumbe. Baada ya muda mchache tu kupita simu ikaanza
kuita. “Ni nini tena T? Nimekwambia nimechoka nataka kulala.” “Kesho
nasafiri na nitakaa huko muda mrefu, nataka tuagane.” “Nitakuja kesho T,
nimechoka na nimeshalala.” “Amka uje chumba hicho kinachoangaliana na chako.
Sasa hivi, nakusubiri Bella.” Bella alibaki kimya akitaka kulia. “Unakuja au unataka mimi ndio nije huko?” Mzee Masha aliuliza kwa
jeuri.
Bella alibaki akimwangalia
mdogo wake huku akijutia kujibu ujumbe wa Masha. “Bella!” “Nakuja T.” Bella alitoka kwa kunyata mpaka chumba
alichokuwepo Mzee Masha. Alimkuta anamsubiria kwa hamu. “Njoo
kwanza hapa. Nilikuwa na hamu na wewe kupita kiasi.” Bella hakutaka kujibu. Akapanda kitandani.
“Mbona umenuna?” “Nimekwambia nimechoka
T.” “Kwani ulikuwa unalala na Elvin huko?” Bella alishtuka sana. “Unawezaje kufikiria uchafu kama huo?
Unafikiri watu wote wana mawazo kama yako? Maisha sio kufanya mapenzi tu, T.
Kuna mambo mengine yakufanya.” “Hata mimi sifanyi mapenzi tu, nafanya kazi na
mapenzi. Tena nafanya mapenzi na wewe
tu.” Bella aliguna.
“Wewe
si umesema unanichunguza? Sasa umeshaona kama nina mwanamke mwingine?” “Mkeo?” Bella akamuuliza. “Kama ningekuwa nalala na mke wangu,
ningekuwa hapa sasa hivi? Siku hizi muda mwingi sana natumia na wewe Bella,
kuliko hata mke wangu. Naweza nikaenda kule nisimguse hata mara moja mpaka
narudi kwako. Huoni nilikuwa nakusubiri tuagane ndio niondoke?” Bella
alikuwa amechoka sana. “Naomba tumalize nikalale T.” “Ukalale wapi wakati nakwambia
nipo hapa kwa ajili yako?” “Siwezi kulala hapa T, wakati Ric yupo chumba
kinachofuata.” “Leo utaweza. Anza kufikiria kitu cha kumwambia. Lakini leo
hutatoka humu ndani mpaka asubuhi. Unataka kuanza kunichezea akili.
Nimekuruhusu kwenda na Elvin, unarudi unaanza kuleta jeuri! Mara ngapi tumekuwa
tukisafiri na Ric, halafu mimi nalala na wewe, yeye analala peke yake?” “Kwa
kuwa tunakuwa safarini T. Hapa ni kama nyumbani kwetu. Nitamwambia nini
asubuhi?” Bella alitamani kulia.
“Hainihusu mimi, hiyo ni kazi yako. Hata hivyo unamasaa mengi sana
yakufikiria chakumwambia hiyo asubuhi, maana ndege yangu itaondoka kesho saa
sita ya usiku. Na hatutakuwa wote kwa muda mrefu sana. Nitakuwa na wewe mpaka
nitakapokuja kuchukuliwa kupelekwa uwanja wa ndege.” “Haiwezekani T. Unataka na
siku nzima ya kesho niwe na wewe humu ndani.” “Mbona unashindwa kuelewa Bella? Nakwambia naondoka na ndege ya KLM,
saa sita usiku. Wakati mimi naondoka, na wewe ndio utaendelea na mdogo wako.
Usitake kunifanya mimi mjinga. Nina mizigo yangu yote hapa. Nitaondokea hapa
hapa. Wewe mwenyewe hutaki mdogo wako anifahamu. Angekuwa ananifahamu angalau
mchana tungekula naye chakula pamoja.” “Mbona na mimi hutaki mkeo na watoto
wako wanifahamu? Tuondoke wote kesho ukanitambulishe kwa
wanao.” “Bella umekuwa mkorofi sana. Haukua hivi.” “Naomba kulala T. Wewe
mwenyewe ndio umenifundisha kuwa mkorofi. Unawezaje kunifungia humu ndani kama
mfungwa, halafu unajua mdogo wangu yupo chumba cha jirani!” “Kwa kuwa wewe mwenyewe
umechagua kuyaona haya maisha kama ni jela. Angalia wenzako wanavyohangaika
mtaani hawana pesa. Wewe unacheze pesa yangu utakavyo! Umesahau ulipotoka wewe
Bella? Huna shukurani kabisa. Nimewaokota wewe na mdogo wako mnatangatanga
mtaani, hamna hata chakula! Namsomesha mdogo wako kwenye
shule yakimataifa. Ada ninayomlipia hata watoto wangu sikuwahi kuwalipia hivyo.
Unaendesha gari ambayo hata mke wangu haendeshi gari kama hiyo na wala hakuna
mwanangu hata mmoja ameshawahi kuwa na gari kama yako! Unaishi kwenye nyumba ya
kifahari hapa mjini, umezungukwa na wafanyakazi, tena ninao walipa mimi. Mdogo
wako akiwa likizo mnaishi hapa, kila kitu mnafanyiwa. Unataka nikufanyaje
Bella? Ulitaka nikupe nini? Leo nakuomba tuwe wote kwa masaa machache tu,
unalalamika!”
“Hunithamini mimi kama Enabella. Unaniweka hivi kwa manufaa yako,
kwa kuwa hutaki watu wachafu, una kinyaa. Halafu subiri kwanza T. Unanipa vitu vya thamani au unaniazima?
Ukikasirishwa tu kidogo, mimi ndio sehemu yako yakutolea hasira zako. Utanipiga
karibu ya kuniua, halafu unaniacha hapo sakafuni navuja damu bila ya kujali.
Ukitoka hapo, wakati umeniacha nusu mfu hapo sakafuni unaanza kunipokonya kila
kitu chako, halafu ukirudi hutaomba msamaha, wala kunipa pole kwa mabaya
uliyonitendea, tena wala huniulizi kama nimepona au vipi, utatumia mwili wangu
hata kama ni siku mbili bila kujali maumivu unayonisababishia.” “Huna shukurani wewe Bella. Hakuna kitu
nitakufanyia ukaridhika.” Waliendelea kubishana kwa muda Bella
akijua baada ya hapo watalala. Lakini alimshangaa Mzee Masha, na ugomvi wote
ule waliokuwa wakibishana, alimgeuza kwa nguvu na kuendelea kufanya naye mapenzi
mpaka alipochoka ndipo alipomuachia, akalala hapo hapo. Bella aliingia bafuni
nakuanza kulia sana.
**********************************
Alitamani kama Elvin
angekuwepo chumba cha jirani akamkimbilia, amshike japo kidogo tu labda ule uchungu
alionao moyoni ungepotea, akalala tena. Alikumbuka kwa mara ya kwanza baada ya
muda mrefu wa machungu na kutokulala vizuri, jinsi alivyolala kifuani kwa
Elvin. Ilikuwa kama mtu aliondoa moyo wake wa uchungu na kuweka moyo mwingine
wakati amelala na Elvin. Hakuwahi kusikia hivyo kabla. Mzee Masha ndiye
mwanaume wa kwanza kumshika kimapenzi, lakini kila alipomshika alikuwa akisikia
kupiga kelele. Aliona ni mateso makubwa sana hata kulala naye wakiwa wamegusana.
Kwa kuwa alikuwa hapati
usingizi kwa haraka, alikuwa akisubiri kila Mzee Masha anapolala, na yeye
alijivuta mbali naye sana ndipo alipoweza kulala japo kidogo. Mara nyingi kila
alipokuwa akimalizana na Mzee Masha, alinyanyuka na kuhamia sebleni kufanya
mambo yake kwenye laptop yake ili kusafisha mawazo. Wakati mwingine alikuwa
akishindwa kulala kabisa kila baada ya kufanya mapenzi na Mzee Masha. Alijikuta
inamlazimu kuangalia movie nyingi sana ndipo aweze kulala.
**********************************
Alikaa ndani ya sinki la
kuogea, akiwa amejaza maji humo akiwaza hili na kupanga lile. Mwishowe alipoona
panakaribia kupambazuka alimwamsha Mzee Masha. “Nitarudi baadaye. Nawahi kabla Ric hajaamka.” “Uwahi kurudi Bella,
lasivyo nitakufuata huko huko.” Bella hakumjibu kitu. Alivaa harakahaka
nakurudi chumbani kwake. Alimkuta Ric bado amelala. Kama katoto kadogo, Bella
alipanda kwenye kitanda chake, akajikunja kama paka baada ya kulia kwa muda
mrefu akapitiwa na usingizi. Alishtuka ilishakuwa saa nne. Eric alikuwa bafuni
akioga. Alianza kuwaza jinsi ya kumuaga mdogo wake, maana alijua muda atakao
rudi mdogo wake atakuwa ameshalala.
Eric akatoka bafuni. “Uchovu umeisha?” “Najisikia vizuri.” Eric
akajibu. “Naomba leo uwahi kulala Ric,
ili kesho tupate muda mzuri kule kwa mama.” “Nitawahi kulala Bella. Kwani wewe hutakuwepo?”
“Kuna mtu anashida, anataka nikamsaidie. Anakaa mbali kidogo, itabidi niende
sasa hivi, nitarudi baadaye. Lakini hata nikichelewa nataka ulale. Umesikia
Ric?” “Naomba basi nicheze game wakati haupo.” “Usiache kula. Hakikisha
unaagiza chakula cha mchana na usiku, na ule.” Eric alifurahi sana kuachwa
peke yake ili acheze mpaka achoke. “Unanielewa
lakini?” “Nimeelewa.” “Nini?” “Nile
chakula cha mchana na usiku.” “Nikirudi hujala halafu bado unacheza game tu,
nakupokonya game zote hamna kucheza tena.” “Nitakula Bella.” Bella
alijitayarisha harakaharaka kwani simu yake ilishaanza kuita zaidi ya mara
tatu. “Nakuja.” Bella alijibu kwa kifupi
na kukata.
**********************************
Alitoka mle ndani,
akaenda alipokuwa ameegesha gari yake, akatafuta sehemu akalificha hilo gari,
ili ikitokea mdogo wake anatoka mle ndani, asilione gari la dada yake. Kisha
akarudi kwa Mzee Masha. Kweli, Bella alikaa huko ndani mpaka usiku wakati Mzee
Masha alipokuwa anataka kuondoka.
“Kesho tunaenda kwa mama.” Bella alikuwa akimtaarifu Mzee Masha wakati
anavaa ili aondoke. “Sawa. Au kuna kitu
unataka?” “Hapana. Lakini Ric alimuomba tena Elvin twende naye.” Mzee Masha
aliweka kila kitu chini na kumgeukia
Bella. “Eti nini!?” “Hujanisikia au ndio
unataka kuanza ukorofi, T?” “Usinichezee akili Bella. Ni wewe unamtaka Elvin au
ni Ric?” “Namtaka Elvin wa nini mimi
wakati nipo nae kazini kila siku?” Bella alijibu huku na yeye amekasirika. “Unawivu T, mpaka unashindwa kufikiria.
Elvin nipo nae kuanzia jumatatu mpaka Ijumaa. Tena wakati mwingine mpaka jumamosi
na jumapili kazi zikiwa nyingi nakuwa naye ofisini. Sasa ni kwa nini tena
nimtoe hapa nimpeleke huko kijijini? Hujawahi kuniamini na hutakaa ukaniamini,
hata nifanyaje. Ningekuwa Malaya, ungenikuta bado bikra? Zera mwenyewe hana tabia kama zangu. Ana wanaume
kila kona.” Mzee Masha alimpiga Bella kibao cha nguvu tena cha kushtukiza.
Bella alikuwa amesimama, kile kibao kilimfanya apepesuke mpaka akaanguka na
kujigonga kwenye kona ya kitanda. Alijigonga karibu sana na jicho, alianza
kulia kwa uchungu sana. “Usiwahi kumleta
mtoto wangu kati yetu.” Bella alibaki akilia pale chini kwa muda.
Kichwa kilianza kumuuma
sana. “Inauma ukifikira wapo wanaume wanaomfanyia
mwanao kama unavyonifanyia mimi?” “Nitakupiga
tena nikuumize Bella, naomba unyamaze.” Bella aliendelea kulia. “Uliniahidi hutanipiga tena. Mbona umenipiga?” Bella alikuwa akilia
sana. “Umenikorofisha wewe mwenyewe. Mimi
sikuwa hata na nia yakukupiga.” “Mkeo akikorofisha pia
huwa unampiga hivi, au ni mimi tu unanionea?”
“Naomba uondoke Bella. Unataka kuniudhi bure nikuumize.” Bella alikusanya vitu
vyake akataka kuondoka.
“Nikirudi nikuletee nini?” “Sitaki.” Mzee Masha alianza
kucheka. “Njoo Bella wangu.” “Naomba nikapumzike T. Umeniumiza sana, mpaka kichwa kinaniuma.
Halafu sasa hivi ni saa tano usiku, sijapata muda wakupumzika hata kidogo. Siku
nzima tuko wote hapo kitandani. Na kesho mimi ndio dereva, nataka tuondoke
asubuhi sana ili turudi usiku.” “Hamta lala?” “Hapana,
natakiwa kazini kesho kutwa.” “Usiendeshe. Mwambie Elvin aendeshe ili upumzike.” “Nani atamuonyesha njia?” “Kweli
nenda basi kalale. Lakini kabla hujaondoka njoo kwanza karibu yangu.” “Umetoka kunipiga T. Ona ulivyoniumiza, halafu sasa hivi unataka nini tena?” “Acha maneno mengi Bella. Njoo.” “Utachelewa ndege T na umeshavaa, kwa nini usiniache
nikapumzike?” “Nimekwambia njoo.” Mzee Masha aligomba kwa
nguvu sana mpaka Bella akatetemeka. Aliweka vitu vyake chini na kumsogelea.
“Kila ukinitizama na kuongea ndivyo unazidi kunifanya nikutamani
Bella. Nakupenda sana.” Kama sio yeye aliyempiga Bella na kumgombesha. Bila ya kumpa pole
au kuomba msamaha, Mzee Masha alimuweka Bella kitandani, hakumuachia mpaka
dereva alivyokuja kumgongea. “Ric
akiondoka tu, urudi nyumbani. Umenielewa Bella?” “Nimeelewa.” Bella alivaa
harakaharaka nakutoka pale.
“Mkasa
mwingine wa kutisha kwa Bella lakini Safari hii aiangukia mikononi kwa Elvin.”
Alifika chumbani kwao
akamkuta Eric ameshalala. Bella alipanda kitandani na kuanza kulia tena. Alilia
mpaka ilipofika saa kumi alfajiri. Kila alivyojitahidi kunyamaza alishindwa.
Kichwa kilikuwa kikimuuma sana, na pale alipojigonga palizidi kuuma. Hakuwa na
dawa yeyote yakupunguza maumivu. Aliendelea kuhangaika, mpaka alipoamua kwenda
kuoga. Alishtuka sana alipojiangalia kwenye kioo. ‘Nitamwambia nini Ric na
Elvin? Itabidi kuvaa miwani ya jua.’ Jicho lake lilikuwa jekundu sana,
na pembeni lilivilia damu pakawa peusi kabisa. Na kwa kuwa alikuwa na rangi
nyeupe, hata gizani alionyesha. Bella alianza kulia tena huku amejishika
kichwani. Kichwa kilikuwa kikimuuma sana.
Alioga na kurudi
chumbani. Alimwamsha mdogo wake, ili ajitayarishe, lakini alikataa kuoga,
akasema alioga kabla yakulala. Kwa kuwa Bella alikuwa akisikia maumivu makali,
hakutaka kubishana naye. Alitamani kama Elvin angekuwa haendi nao ili aahirishe
safari, aende siku nyingine, kwanza ili apumzishe mwili uliokuwa ukitumiwa
zaidi ya masaa 24, huku akiwa na michubuko mingi sana na pili labda jicho lake
lingekuwa limepungua. Alimfikiria babu yake jinsi atakavyoshtuka baada ya
kumuona. Alitamani asiende, lakini aliangalia saa, akajua Elvin atakuwa yupo
njiani kuelekea walipokubaliana wakutane. Alianza kuweka vitu kwenye gari na
michezo ya mdogo wake, aliyodhani angehitaji njiani. Akamuwekea mdogo wake mto
na shuka la kujifunika, kama akitaka kulala akiwa njiani. Alipohakikisha kila
kitu kipo tayari, ndipo alipomuamsha tena Eric. Alikuwa na usingizi sana,
alipanda kwenye gari, akajilaza viti vya nyuma, akapotelea usingizini.
Bella aliondoa gari kwa
kasi ili asimchelewe Elvin, kwani ilishakuwa saa kumi na moja kasoro.
Aliendesha kwa shida kutoka Kawe akapitia njia ya Coca cola, iliyomfikisha
Mwenge. Kwa kuwa ilikuwa bado mapema, na hapakuwa na foleni yeyote, haikuchukua
muda mrefu sana kutoka Mwenge mpaka Ubungo. Alipomuona tu Elvin, alichukua
miwani yake ya jua akavaa, kisha akajifunika mtandio aliouvuta mpaka usoni.
Alifanikiwa kuficha lile jeraha.
“Za asuhubi?” Bella alisalimia huku akiangalia mbele. “Nzuri. Mliamka salama?” Elvin alijibu na kuuliza swali kabla
hajafunga mkanda. “Naona Ric bado
amelala.” Akaongeza tena. “Atakuwa
amechelewa sana kulala.” Bella alijibu bila ya kumtizama. “Kwani mlilala saa ngapi?” Bella
alinyamaza, kama kawaida Elvin alikuwa akishamuona Bella amekaa kimya alijua
hataki kujibu hilo swali. “Bella! Hata
swali dogo kama hilo pia huwezi kujibu!? Au na lenyewe utakuja kunipa jibu siku
nyingine!?” Elvin alikuwa akishangaa, asijue lile swali, jibu lake limebeba
uchungu mzito sana kwa Bella.
“Hapana. Sijui yeye alilala saa ngapi?” “Haukuwa naye nyumbani?”
“Hapana.” Elvin alitulia kidogo.
“Mbona leo unaongea na mimi hutaki kuniangali? Kuna nini?” “Hamna kitu Elvin. Labda
usingizi.” “Unataka nikusaidie kuendesha?” “Nitashukuru, ili nilale kidogo.” Bella
alishuka wakabadilishana viti, Elvin akaanza kuendeshea baada ya kuelekezwa
kidogo. “Lakini kabla yakufika Chalinze
nitakuwa nimeamka.” “Hamna shida, nikiona napotea, nitakuamsha.” “Asante sana
Elvin.” “Karibu.” Bella alipandisha miguu kwenye kiti, akavua miwani,
akahakikisha amejifunika vizuri mpaka usoni akapotelea, usingizini.
Elvin aliendesha huku
abiria wote wakiwa wamelala. Bella alilala, lakini maumivu ya kichwa yalikuwa
yakimsumbua sana. Alikuwa akigugumia usingizini, sababu ya maumivu makali. Mwanzoni
Elvin alijua ni ndoto, lakini kadiri muda ulivyokuwa ukizidi kwenda, Bella
alizidi kulalamika usingizini. Elvin akaamua atafute sehemu asimamishe gari.
Alikuwa wameshafika maeneo ya Kibaha. Alitafuta sehemu wanayouza mafuta ya gari{gas
station}, akaingia hapo.
Akaegesha gari vizuri,
kisha akashuka na kuhamia upande alipokuwepo Bella. Alifungua mlango taratibu,
akamtoa ule mtandio usoni ili amwamshe kujua kulikoni. Baada ya kuutoa, Elvin
alishtuka sana mpaka akarudi nyuma. Upande mmoja wa uso wa Bella ulikuwa
unatisha sana. Ulikuwa umevimba na pakawa pamevilia damu. Ilikuwa ngumu
kumtizama mara mbili. Palikuwa peusi sana. Machozi yalijaa machoni kwa Elvin.
Alimgusa taratibu, bado
alikuwa akilalamika. “Bella! Bella!”
Bella alifungua macho, jicho lile moja lilikuwa jekundu sana. “Kichwa kinaniuma sana Elvin. Siwezi hata kunyanyua kichwa.” “Ngoja niulizie hospitali hapa karibu.” Elvin alimuulizia mtu
aliyekuwepo karibu yake, na yeye alikuwa akijaza mafuta kwenye gari yake,
akaelekezwa hospitali ilipo. Aliendesha kwa haraka mpaka pale hospitalini.
Alimwamsha Eric akamwambia afunge gari amfuate. Akaenda upande aliokuwepo Bella,
akafungua mlango, akambemba mpaka mapokezi.
“Safari ya kwenda kijijini kuona kaburi la mama yao, yaishia
hospitalini.”
Kila mtu alishtuka sana
walipomuona Bella. Alikuwa akilia huku anatetemeka. Walimpisha ili ahudumiwe
yeye kwanza. Elvin alimuweka kwenye kitanda kilichokuwepo kwenye chumba kidogo
pale pale mapokezi. “Kwa nini unapiga
wanawake, we kijana?” Daktari aliyekuwepo pale aliuliza. “Sijampiga.” “Ona alama ya vidole hii hapa
imevilia kabisa. Acha kusema uongo. Hasira hizo zitawasababisha kuua, mje kufia
jela bure!” Elvin alinyamaza asijue ni jinsi gani atajitetea tena na
kueleweka. Aliamua kurudi kumuangalia Eric wakati wakimshugulikia Bella.
Baada yafunga gari, Eric
aliingia ndani kwa haraka, akakutana na Elvin naye akimfuata. “Kwa nini tupo hapa hospitalini?” Eric
akamuuliza Elvin. “Bella anaumwa.”
“Bella!” Eric alishtuka sana. “Anaumwa
nini?” “Sijui.” “Is she going to be okay.” “Usiogope Ric. Atapona. Kwani jana
mlienda wapi?” Ilibidi Elvin aulize. “Mimi
sikwenda mahali, ila yeye aliniaga asubuhi kuwa anatoka kwenda kwa rafiki yake
anashida sana, anakwenda kumsaidia. Mpaka saa nne na nusu usiku mimi nina lala,
yeye alikuwa hajarudi. Hata sijui nimefikaje kwenye gari. Atakuwa aliniamsha
asubuhi akanisaidia kupanda kwenye gari. Sijamuona tokea jana asubuhi.”
Elvin alibaki kimya.
“Nataka nikamwone Bella.” Ric alianza kulia. “Ngoja kwanza wamtibu, halafu tutaenda kumuona. Njoo tukae hapa chini.”
Walipokaa tu, alitoka nesi, akamwita Elvin. Daktari anataka kuzungumza na wewe.
Elvin aliongozana na yule muuguzi mpaka ofisini kwa daktari. “Mgonjwa wako analalamika sana kichwa, nashauri
afanyiwe kipimo cha kichwa. Kina bei kidogo lakini naona ni muhimu. Je upo
tayari akapimwe?” “Kabisa. Itachukua muda gani mpaka kupata majibu?” “Leo leo.
Ngoja nesi aende akaangalie kama kuna watu wengi wanasubiri hicho kipimo. Kama
hamna, nitawaomba wampime sasa hivi, ili tupate majibu haraka.” “Nitashukuru
sana kama mtaharakisha. Naweza kuingia kwenda kumuona?” “Ingia tu. Na mimi
nitakuja baada ya muda mfupi kumchoma sindano” Yule nesi aliyemwita na kuwa
naye kwenye chumba cha daktari alijibu nakuondoka. Elvin alitoka pale kwenye
ofisi ya daktari kuelekea kwenye kile chumba alichokuwepo Bella.
“Elvin, Elvin! Nisaidie.” Akiwa nje ya mlango, Elvin alisikia Bella akiita
jina lake huku akilia kwa uchungu mkubwa sana. Aliharakisha kuingia ndani,
akamkuta Bella amefunga macho huku analia sana. Elvin alimsogelea mpaka pale
kitandani. “Bella! Bella! Niangalie.”
Bella alifungua macho. “Si ni kichwa
kinauma?” “Sana, nahisi
kuchanganyikiwa.” “Pole sana. Nimeongea
na dakatri wanakuja kukuchoma sindano ya kutuliza maumivu, lakini kwa sasa,
naomba usilie kabisa jaribu
kutulia, ili kichwa na chenyewe kitulie. Sawa?” Bella alitingisha kichwa. “Ric yuko wapi?” “Nimemwambia asuburi nje
kidogo. Ataogopa sana kukuona kwenye hiyo hali. Acha kwanza kichwa kitulie
kabisa, ndipo atakuja kukuona. Sawa?” “Asante.”
“Basi usilie kabisa, vumilia. Sasa hivi watakuja
kukuchoma sindano, halafu wakuchukue kwenda kwenye kipimo cha kichwa. Waangalie
kuna nini kinachoendelea huko kichwani.” Bella alitulia. Muuguzi aliingia, akamchoma
sindano, baada ya muda walimuona ametulia, wakajua maumivu yameisha. Elvin
alimshika kichwani pembeni ya ule uvimbe, kichwa kilikuwa cha moto sana. Alikaa
naye mpaka alipokuja kuchukuliwa kwenda kufanyiwa vipimo.
Elvin alirudi kukaa na
Eric. “Anaendeleaje?” “Wamemchukua kwenda
kumfanyia vipimo, akirudi utaenda kumuona.” Eric alikaa kimya kwa muda. “Elvin!” Eric akamwita, Elvin
akamgeukia. “Vipi?” “Asante kwa kutusaidia.”
Elvin alimuhurumia sana Eric. “Usiwe
na wasiwasi Ric, Bella atapona.” Eric alifuta machozi. “Asipopona Bella nitafanyaje? Mama alisema nisiwe na wasiwasi
nitakuwa na Bella.” “Usilie Ric. Bella
lazima apone.” “Bella aliniambia
hivyohivyo wakati mama mgonjwa. Lakini hakupona alizidi kuugua kila siku,
wakamrudisha nyumbani. Bella alihangaika naye sana, alikuwa peke yake akimuuguza. Unajua dada aliyekuwa akitusaidia kazi na yeye alitukimbia?” “Sikuwa najua hilo.” Elvin alijibu.
“Basi alitukimbia. Akatuacha peke yetu na mama
mgonjwa. Bella alikuwa akiniambia kila siku nisiwe na wasiwasi mama atapona,
lakini ujue nini?” “Eehee!” Ric alikuwa
akitia huruma sana.
“Mama alikufa akiwa amekonda sana, halafu akawa hatukumbuki
kabisa. Hata mimi hakuwa akinikumbuka tena. Wakati mimi ndio alikuwa akinipenda
sana. Nitaenda wapi Bella akifa?” “Bella hawezi kufa.
Usiogope Ric. Ni kichwa tu kinamuuma, amepewa dawa ametulia, na anafanyiwa
vipimo ili tukiondoka hapa tuwe na uhakika yupo salama. Usiogope.” “Naogopa sana Elvin.” Elvin aliweza kuhisi hali anayopitia Eric.
Alimuona mama yake akiugua mpaka kufa. Hapendi mtu aumwe kabisa, kila akiona mtu
anaumwa, anajua atakufa tu.
“Elvin!” Eric alikuwa akiwaza, kama aliyekumbuka
akamwita tena. “Vipi Eric?” “Tulikuwa na kaka yetu anaitwa Mat. Mama
alisema Kaka Mat pia atakuwa na sisi. Lakini nilimsikia mke wake akimwambia….” Eric
alitulia kidogo. “Alimwambia nini?”
Elvin alimuuliza aliposhindwa kusema. “Lakini
usimwambie Bella.” “Sitamwambia.”
“Naomba usimwambie. Bella ataumia sana.” “Niambie tu.” “Nilimsikia akimwambia Kaka
Mat, hapendi kumuona Bella pale nyumbani kwao, na hataki Bella awe anakwenda
hata kule dukani kwao. Na ili Kaka Mat asionane na Bella, alimwambia lazima
wanifukuze mimi pale nyumbani kwao. Sasa unajua kilichoniuma ni nini?” “Nini kilikuumiza Ric?” “Kaka Mat
hakututetea kabisa. Alinyamaza, wakati sisi ni wadogo zake. Mkewe alikuwa ananinyima
chakula, halafu ananiambia nifue. Unajua mimi sijui kufua?” “Sifahamu kama hujui kufua.” “Sijui kufua, halafu sipendi kabisa hiyo kazi. Nikiwa nyumbani
Bella ndio ananifulia nguo zangu zote mpaka soksii au anawalipa watu watufulie.
Sasa yule mke wa kaka Mat akawa ananipa nguo nyingi sana nifue, halafu ngumu
sana. Akawa hanipi chakula mpaka zitakate. Na mara nyingi nilikuwa nashindwa
kuzitakatisha, sababu ya vidonda. Nilikuwa natokwa na vidonda sana mikononi
sababu yakufua. Sasa nikawa namwambia Kaka Mat, amwambie mke wake asinipe nguo
za kufua, unajua kaka Mat aliniambiaje?” “Alikwambiaje?” Elvin alikuwa
akimsikiliza kwa makini Eric aliyejawa hofu. Alikuwa akiongea kwa kutetemeka.
Elvin aliona amsikilize tu, pengine angetulia. Na pia ilikuwa ni njia mojawapo
yakuwafahamu zaidi.
“Usimwambie Bella lakini, atalia sana.” “Sitamwambia.” “Alikuwa ananiambia nijikaze mimi mtoto wa kiume, hata vile vidonda
nisiviwekee dawa, vitageuka kuwa sugu nitazoea. Unafikiri vilipona?”
“Havikupona?” Elvin akamuuliza kama kumuonyesha bado yupo na yeye. “Havikupona kabisa. Tena ndio vilikuwa
vikizidi kuuma akiniambia nioshe vyombo. Si unajua ukiosha vyombo nilazima
utumie sabuni?” “Nafahamu Ric.” “Basi ile sabuni ikiingia kwenye vidonda
ilikuwa inauma sana. Usije kumwambia Bella kabisa. Atalia sana.” “Siwezi.” “Unajua siku alipokuja kunichukua kwa kaka
Mat akakuta naosha vyombo juani, Bella alilia sana mpaka akashindwa kuendesha
gari kwa kulia?” “Sikuwa nafahamu hilo.” “Alilia sana. Hata tulipofika hotelini
aliendelea kulia. Unajua Bella hapendi mtu anitese kabisa?” Eric akauliza
tena. “Nimemuona.” “Basi yupo hivyo tokea
tupo shuleni. Bella ananipenda sana mimi. Na ukitaka kumuona amekasirika,
unifanyie mimi kitu kibaya. Huwa hapendi kabisa, anakasirika sana. Unajua pia
huwa anafanyaje?” “Sifahamu Ric.”
“Huwa pia analia sana. Huwa anawaambiaga watu ni heri umfanyie yeye kitu chochote kibaya, lakini sio mimi
mdogo wake. Bella ananipenda sana kama mama alivyokuwa ananipenda. Usimuone
vile. Ananipenda sana, ni heri akose yeye ila mimi nipate.” Ric alitulia
kidogo kama anayefikiria kitu.
“Nataka kumuona Bella.” “Subiri, wakimrudisha tutaenda.” “Huko walipompeleka
si atakuwa peke yake? Labda mimi niende nikakae naye. Sipendi awe peke yake
sasa hivi akiwa mgonjwa.” Eric alitoa wazo. “Au mimi
ndio niende, wewe unisubiri?” Elvin alimuuliza swali lakumfanya yeye
mwenyewe amkubalie. “Sawa. Lakini
akiniulizia tu uje unite, ujue ananitaka mimi.” “Nitafanya hivyo, Eric.”
Elvin akasimama na kumuacha Eric amekaa kwenye benchi akiwaza.
Bella alifanyiwa vipimo,
lakini kila kitu kilikuwa sawa. Hakuonekana na tatizo lolote kubwa ndani ya
kichwa chake. Waliruhusiwa na kupewa dawa ya kutuliza maumivu. “Nina usingizi sana Elvin.” “Naona turudi tu
nyumbani ukapumzike. Unaonekana umechoka sana. Ric alikuwa anakuulizia,
anawasiwasi sana na wewe.” “Najua atakuwa na wasiwasi. Muoga sana. Yeye
akimuona mtu anaumwa ndio anachanganyikiwa kabisaa. Naomba mtandio wangu
nijifunike ili asilione hili jeraha. Atalia sana akiniona hivi, anaweza
asilale.” Elvin alimsogezea mtandio wake, kichwa kilikuwa kimeshatulia,
maumivu makali aliyokuwa nayo yalikuwa yameisha. Alijifunga vizuri, akavaa
miwani yake kubwa, mweusi kabisa iliyoweza kuficha macho yake, akajaribu kuvuta
pumzi mara mbili tatu, ili kujiweka sawa anapokukutana na mdogo wake. Elvin
alikuwa akimwangalia.
“Nikushike mkono.” “Asante,
lakini hapana Elvin. Nitamuogopesha sana Ric. Hata hivyo nipo sawa sasa hivi.
Ni kuchoka tu.” Bella alitoka akiwa anatembea. Eric alipomuona, alimkimbilia akamkumbatia.
“Nilikuwa naogopa Bella. Unaumwa nini?”
“Kichwa ndio kilikuwa kikiuma sana. Lakini wamenichoma sindano, kimepona
kabisa.” “Afadhali. Tutaenda kwa mama?” “Wamenishauri nikapumzike kabisa.
Inabidi turudi nyumbani nikapumzike. Najua unatakiwa shuleni siku tatu zijazo,
usiwe na wasiwasi, nitakuja kukufuata shule ili twende kwa mama. Sawa?” “Sawa. Upone Bella. Sipendi kukuona unaumwa.” Eric alianza kulia.
“Usiogope bwana. Mbona nimeshapona. Natakiwa kupumzika tu kwa kuwa wamenichoma
sindano ya usingizi ili nilale kabisa nipumzishe kichwa, lakini nimeshapona.” “Nakupenda Bella.” “Hata mimi nakupenda
Ric.” Eric alifuta machozi akambusu dada yake shavuni, lakini hakuona
jeraha. “Asante Ric. Twendeni sasa.” Walirudi
tena kwenye gari, ikabidi Elvin ndio awe dereva tena.
Alitamani kama waagane
njiani ili asifike pale hotelini wanapoishi, lakini Bella alikuwa amechoka sana,
asingeweza kuendesha tena. Alipomtajia wapi wanaenda, alijilaza kwenye kiti cha
gari na kupotelea usingizini.
Walifika hotelini, Eric
akamuelekeza sehemu ya kuegesha gari, ambapo anamuona dada yake kila wakati
akiliweka hapo. Alimwambia ni karibu na chumbani kwao. Bella alikuwa amelala
kabisa. “Unaweza kumbeba?” Eric
alimuuliza Elvin. “Naweza, unafikiri
nimbebe?” “Ingekuwa vizuri, ili tusimuamshe.” Eric alinong’ona, Elvin
akacheka. “Haya. Lakini itabidi wewe
ufunge gari.” “Nitabeba na pochi
yake.” Eric aliendelea kunong’ona. Elvin alienda upande alipokuwepo Bella,
akamfungua mkanda, akamtoa pale kwenye kiti taratibu akambeba. Eric alifunga gari
harakaharaka akakimbia mbele ya Elvin kuonyesha chumba chao na kufungua mlango.
Elvin alimuweka kitandani taratibu, akamfunika shuka vizuri, mpaka upande
wajeraha, akauficha ili Eric asimuone, kisha akakaa pembeni yake akimwangalia.
“Njaa inaniuma Elvin.” “Unataka nikakuletee chakula gani?”
“Hapana, nikupiga tu simu hapo mapokezi, halafu watatuletea. Wewe unataka kula
nini?” “Nitakula baadaye. Wewe agizia tu.” Elvin alikuwa haelewi maisha
anayoishi Bella na mdogo wake. Yalionekana ni ya gharama sana, mtu wakawaida
hawezi kuishi vile. Gari yenyewe ya Bella, ilimbabaisha sana. Ilikuwa gari ya
kisasa, ilibidi kutumia akili kuiendesha bila kuuliza uliza, kwani haikuwa na
sehemu ya kuingiza funguo kama gari nyingine, ilitumia rimoti tu na iliwashwa
kwa kubonyeza ile sehemu ya kuingizia funguo.
Eric alipiga simu
mapokezi. Akaagiza chakula chake. Baada ya muda Elvin akaona muhudumu anaingia
na chakula. Vile kilivyoletwa tu, jinsi kilivyobebwa na kigari maalumu, Elvin
alibaki na mshangao. Kilipambwa
maridadi. Juisi ilivutia kwenye glasi. Matunda yalipangiliwa vizuri. Visu na
uma. Vyote viliashiria pesa yakutosha, inamwagwa pale. Eric alikula, muhudumu
akarudi kutoa vyombo, akageukia tv na kuanza kucheza game.
**********************************
Ujumbe akaingia kwenye
simu ya Elvin. Elvin aliitoa simu yake mfukoni na kuanza kusoma. Ulikuwa ujumbe
kutoka kwa Irene. ‘Naomba leo usiku tuonane Elvin. Ninahamu
sana na wewe. Nahisi sijakwambia hivyo vyakutosha. Nakuahidi kubadilika Babe.
Umekuwa kimya kwa muda mrefu sana mpenzi wangu. Tafadhali mpenzi, naomba leo
tuonane. Hata kama ni kwa dakika chache tu, lakini nataka kukuona.’ Elvin alibaki akiangalia simu yake kwa muda,
kisha akarudisha mfukoni kwake, hakujua kama yupo tayari kuonana na Irene au
bado anahitaji muda. Alikaa pale zaidi ya msaa matatu akimsubiria Bella aamke.
Simu yake ilianza kuita
mfululizo ndani ya mfuko wake, alihangaika kuitoa, kwa haraka ili asimuamshe
Bella, lakini alishachelewa. Bella alijigeuza, giza lilishaanza kuingia. Elvin
aliikata ile simu. “Pole, nimekuamsha.”
“Hamna shida, hata hivyo nimelala vyakutosha.” “Vipi unajisikiaje sasa hivi?”
“Kichwa kimetulia kabisa na nimelala nimepunguza uchovu. Jana sikulala kabisa.”
“Pole.” Simu ya Elvin ilianza kuita tena, Bella alibaki akimwangalia,
mwishowe aliamua kupokea. “Vipi Irene?” “Ulipata ujumbe wangu?” “Ndiyo.”
“Mbona hujajibu sasa, na nimeona umekata simu yangu! Kwani uko wapi?” Elvin alitabasamu huku akitingisha kichwa kama
kusikitika. “Elvin?” Irene aliita kwa ukali. “Umepiga kutaka kujua nilipo au umepiga kwa kuwa umesema unahamu na
mimi unataka kuniona?” Irene akanyamaza. “Naomba nikupigie baadaye.” Elvin akamuaga. “Irene? Unanisikia? Naomba tuongee baadaye. Nitakupigia.” “Sawa.” Elvin alikata simu na
kuirudisha mfukoni.
“Elvin!” Bella akaita
kwa utulivu sana. “Unaweza kwenda tu hata
sasa hivi, mimi najisikia vizuri. Tutakuwa sawa tu, nakushukuru.” Elvin
hakujibu kitu alikaa kimya kwa muda kama anayefikiria kitu. “Unataka kula nini?” Akamuuliza Bella. “Nasikia njaa, lakini sina hamu yakula
kabisa.” “Ngoja nikatafuate chakula, tuje kula wote.” “Asante Elvin. Nakushukuru.”
Elvin alimtizama Bella akatabasamu. “Karibu.
Nitarudi baada ya muda mfupi.” “Kwa nini tusiagize chakula hapahapa? Wana vyakula
vizuri sana.” Elvin alisita kidogo. “Sitakawia,
nitarudi baada ya muda mfupi sana. Kwani kuna chakula maalumu unachokitaka?”
“Hapana. Sijisikii kula kabisa. Natamani kulala tu. Mwili umechoka. Hata
nikilala bila kula ni sawa tu.” “Lazima ule kidogo, ndio ulale. Sitachelewa,
nitarudi baada ya muda mfupi.” Elvin alitoka, Eric alikuwa kwenye michezo
yake, hakuwa hata na habari na mtu. Kila anapokuwepo kwenye games zake, aliweka
akili zake zote huko. Na aliweza kukaa siku nzima bila kula wala kunywa, akiwa
anacheza tu. Mara nyingi Bella alikuwa akimpokonya remote, na kutoa headphones
masikioni mwake ili angalau waongee, au ale na kuoga, lasivyo hakuwa akikumbuka
kabisa.
**********************************
Bella hakutaka
kumsumbua. Alijivuta ndani ya shuka akabaki anawaza. Alikumbuka vitendo vyote
vibaya, Mzee Masha anavyomtendea, jinsi anavyompiga na bado akimlazimisha
mapenzi hapo hapo, Bella alianza kulia. Hofu ya kifo cha gafla ilimjia. ‘Ningeanguka vibaya
jana, ningeweza kufa. Au jinsi anavyojua kunipiga mateke anaweza kupasua kitu
cha hatari ndani yangu, akaniua. Ric atabaki na nani? Nitaendelea kuishi hivi
mpaka lini?’ Bella aliendelea kuwaza huku akilia mpaka Elvin aliporudi. “Kaa tule Bella. Nimeleta chakula, naamini
utakipenda.” Kimya. “Bella?”
Elvin alimsogelea. “Mbona unalia?”
Bella alijitahidi kunyamaza lakini alishindwa, kilio cha kwikwi kilimkamata,
alishindwa kuongea kabisa.
Alisimama kwenda chooni
na simu yake. Akaanza kujipiga picha uso mzima, akajaribu kuosha uso wake ili
kutulia, kisha akatoka akiwa ametulia kidogo. “Tunaweza kwenda kula hapo nje?” Bella akauliza. “Sawa.” Elvin alibeba chakula wakatoka
kwenda kukaa sehemu inayoangalia bahari.
“Hofu ya
kifo, yamfanya Bella kumkabidhi Eric kwa Elvin.”
Kitendo cha Elvin
kuendelea kuwepo pale pamoja nao, bila kuonyesha kuchoka, kilimgusa sana
Enabella. Akaona ndiye mtu pekee anayeweza kumkabidhisha Eric, mdogo wake. “Elvin!” Bella aliita baada ya kukaa
kimya muda mrefu kidogo. “Maisha yangu
hayatabiriki, sijui hata kesho kama nitakuwa hai. Nakuomba nikukabidhi hii kadi
ya benki, inapesa nyingi kidogo, ndipo hata mshahara wangu unapoingia. Sijawahi
kutoa humo hata shilingi. Nahifadhi kwa ajili ya Ric tu. Zinaweza kumtosha Ric
kumaliza shule yake, mpaka atakapofika chuo. Mungu akiendelea kunipa uzima,
nitakuwa naweka mara kwa mara. Nakuomba sana Elvin, ukisikia nimekufa, au
usiponiona kwa siku hata tano mfululiza, na usione hata email yeyote kutoka
kwangu, ujue kuna kitu kibaya kimenitokea. Cha kwanza naomba ukamchukue Ric
shuleni, ukae naye mpaka utakapojua nilipo au kama nimekufa iwe mpaka umeona
nimezikwa kabisa. Hakikisha mtu yeyote hamfikii mpaka utakapoona nimezikwa
ndipo unaweza kumuacha awe huru. Unafikiri utaweza kunisaidia?” Elvin
alikuwa kwenye mshtuko mkubwa sana.
“Sitaweza Bella, mpaka uwe umeniambia nini kinaendelea.”
“Nitakwambia Elvin, lakini sio leo. Kama Mungu akinipa uhai, nitakwambia kila
kitu. Lakini naomba isiwe leo?” “Kwa nini
Bella? Au huniamini.” “Nakuamini sana Elvin, lakini wewe ukijua tu
kinachoendelea, nitakuweka matatizoni. Halafu tutamuacha Ric peke yake, tena
kwenye matatizo makubwa sana. Sina mtu mwingine ninayeweza kumwamini na Ric,
ila wewe. Kaka Mat angekuwa yupo na sisi, ningekuwa nina tumaini jingine.
Lakini sasa hivi naogopa Elvin, naona nimebakiwa na wewe tu. Jana nilianguka
vibaya sana, nafikiria kama sikuwa nimeangukia uso, nikaangukia upande mwingine
wa kichwa labda sasa hivi ningekuwa nimekufa halafu Ric angeteseka sana. Ndio
maana nakushirikisha ili ujue. Tena hizo siku tano nilizokwambia nikama yuko
shuleni. Lakini kama yuko nyumbani,
unajua yuko likizo na mimi, halafu ikafika hata jioni hujanisikia, naomba
mtafute Ric tafadhali. Nitajitahidi niwe nawasiliana na wewe angalau mara moja
ndani ya masaa 24. Japo salamu tu ili kukujulisha kama nipo. Tafadhali Elvin.”
“Nitafanya hivyo Bella.” Elvin alifikiria kidogo.
“Nikuulize kitu Bella?” Bella alifikiria. “Kama nitaweza kujibu nitajibu Elvin, uliza tu.” “Mtakuwa mnaishi hapa
maisha yenu yote?” “Nitatafuta nyumba haraka sana. Yaani nikipona tu,
nitatafuta nyumba ninunue. Sidhani hata kama nitajenga, na nikiipata tu wewe
ndio utakuwa mtu wa kwanza kukuonyesha ili upafahamu. Na nitaomba ukae na hiyo
hati ya nyumba kwa ajili ya Ric, ili asiishi maisha ya kutangatanga. Sifurahii hivi tunavyoishi Elvin, lakini kwa
sasa sina jinsi nyingine.” Elvin alibaki kimya akifikiria.
“Labda naweza kukusaidia Bella. Kwa nini usinishirikishe.” Bella alianza kulia. “Siwezi Elvin. Naomba tuyaache kabisa, ila ujue nakushukuru, na
ninaomba unisamehe. Najua nakupa majukumu mazito, tena ukiwa hutufahamu hata
kidogo, lakini sina jinsi. Sina mtu mwingine. Nahisi Mungu amekuleta kwenye maisha
yetu kwa wakati sahihi, sitaki kuchelewa kukuomba msaada, nikisubiri tuzoeane
sana, kwa kuwa sijui hata kesho itakuaje.” “Hamna shida Bella, naomba uache kulia kichwa kitauma. Kula kidogo,
kisha twende ukalale.” Bella alijitahidi kutulia.
Akala, wakarudi chumbani
wakamkuta bado Eric amevaa ‘Headphones’
zake huku anacheza. “Hivi huyu alikula kweli?” Bella akauliza. Eric hakuwa hata na
habari na kinachoendelea. Akili zake zote zilikuwa kwenye mchezo anaocheza. “Aliagiza chakula, akala.” “Hapo ni mpaka nimpokonye hiyo michezo yake
ndio akili yake inamrudia. Hapo alipo hajui hata kama kuna watu ndani ya hiki
chumba.” Elvin alicheka huku akimtizama Eric.
“Nataka nioge kwanza ndipo nilale. Sitaki kukuchelewesha. Unaweza
kwenda tu.” “Nitakwenda Bella, usiwe na wasiwasi.” “Usije ukafikiri nakufukuza,
sitaki uwe matatizoni.” “Nenda ukaoge.” Bella alitabasamu na yeye, akaingia kuoga,
akatoka akiwa ameshavaa nguo zakulalia. “Njoo
hapa ulale vizuri.” Bella alicheka kidogo. Akapanda kitandani, akajivuta
karibu na Elvin. “Nisikilize Bella.
Naomba niangalie.” Bella alikaa vizuri akamgeukia Elvin. “Ninatisha sana?” Bella aliuliza. “Usijali, utapona. Nimeshakuona ukiwa kwenye
hali mbaya kuliko hiyo, na ukapona, najua utapona tu.” Elvin alitoa ule
mtandio na kuacha sura ya Bella wazi. Alimshika taratibu na kwa upendo pale
penye jeraha. “Pole sana.” Machozi
yalianza kumtoka Bella. “Asante.”
Elvin alimfuta machozi
nakumshika mikono yake yote miwili. “Nisikilize
Bella. Naweza nisiwe msaada mkubwa
sana kwako, lakini amini Mungu yupo na anauwezo wa kukusaidia. Wazazi wangu
walinifundisha kitu kimoja kikubwa sana, ambacho huwa nakitumia tokea mtoto na
kinanisaidia.” “Kitu gani?” Bella akauliza. “Waliniambia hivi, kila ninapokuwa kwenye matatizo, nakuona nimekwama
kabisa, sina msaada wa aina yeyote ule, na hakuna mwanadamu anayeweza kunisaidia,
waliniambia huo ndio wakati pekee wa kumuachia Mungu. Mama yangu huwa anamwita
Mungu wa ‘imposibilities’, yaani Mungu wa yasiyowezekana. Anasema yale ambayo ndio
magumu sana kwetu au kwenye akili za binadamu, yeye Mungu ndio anapenda
kuyafanya ili apate sifa au atukuzwe. Sasa cha msingi ni kufanya hivi,
unamuomba yeye Mungu, halafu unamuachia yeye afanye.” Bella aliguna.
“Mbona unaguna?” “Unajua kuna wakati Kaka Mat alikuwa akitupeleka
kanisani. Nilisikia Mungu hapendi watu wenye dhambi, Elvin. Na mimi naishi
kwenye dhambi, na sijui lini ninatoka kwenye hayo maisha. Sasa namuombaje huyo
Mungu?” “Japokuwa sijui unaishije
kwenye dhambi, au sijui unatenda dhambi gani ambayo huwezi kuacha, lakini
lazima ujue Mungu hachukii wenye dhambi, ila anachukia dhambi. Kama hivi
unavyoongea na mimi, ndivyo hivyohivyo mwambie yeye atajua jinsi gani anaweza
kukusaidia. Umesikia Bella? Usiache kabisa kuongea na Mungu. Hata iweje, pata
muda wa kuongea na Mungu, mwambie kila kitu unachotamani, utashangaa mambo
yanavyokubadilikia.” “Kweli Elvin?” Bella alianza kulia. “Kabisa Bella. Jaribu uone.” Bella
alifikiria.
“Nipo katika wakati mgumu sana Elvin, ni kweli nahitaji msaada.”
“Basi usilie, tuombe wote.” “Sijui kuomba.” “Hakuna maneno sahihi yakuomba. Ila
ujue wewe unaongea na baba yako. Ongea nae chochote unachotaka. Hata ukiongea
naye mawazoni, ukaomba bila yakutoa sauti, yeye anasikia. Tuombe wote, ili
usikie mimi ninavyoongea naye, halafu na wewe unaweza kuomba kimya kimya.”
“Sawa.” Elvin alishika tena mikono ya Bella akaanza kumuomba Mungu taratibu.
Akamuombea Bella na Eric, akawaombea ulinzi, amani na furaha, kisha akamaliza.
Machozi yalikuwa
yakimtoka Bella. “Nimefurahi sana
Elvin, asante.” Elvin akacheka. “Umeona
ilivyorahisi?” “Sana. Umeanza kwa kumuomba Mungu msamaha kwa yote uliyotenda,
kwa kuwaza, kutenda au hata kutotimiza wajibu, kisha, ukaanza kumshukuru, ndio
ukaanza kuomba.” Elvin akacheka. “Kumbe
ulikuwa ukisikiliza?” “Sana tu.” Wote walicheka. Elvin aliongea naye maneno
yakumfariji Bella, mpaka akaona sura ya huzuni ya Bella imebadilika, ikawa ya furaha.
“Nitakuwa nikikuombea Bella. Kila siku.”
“Kwa kuwa sasa hivi na mimi najua kuomba, nitakuwa nikikuombea wewe na Ric kila
siku.” “Asante. Basi naomba ulale, naamini mpaka kesho uvimbe utakuwa
umepungua.” “Nikipitiwa na usingizi, kabla hujaondoka, naomba umwambie Ric azime
tv, aache kucheza alale.” “Hatanikasirikia?” “Hapana. Ric ni mtoto rahisi sana
kuishi naye. Nimsikivu sana. Hata hivyo amechoka, akizima tu hapo atalala.”
“Basi usiwe na wasiwasi, nitaongea naye.” Bella alijisogeza kwenye
mto vizuri ili alale. Elvin naye akajivuta karibu kabisa na Bella, akaegemea
kwenye kitanda, akamfunika vizuri, kabla hata Elvin hajakaa sawa, tayari
alimsikia Bella akihema vizuri, akiashiria ameshalala. Alicheka kidogo na
kubaki akimtizama kwa muda. Alihakikisha Ric ameoga, akawazimia taa,
nakuwaacha wamelala.
**********************************
Wakati anatoka tu, Irene
akapiga tena simu. “Nimeona nikupigie, naona
masaa yanazidi kwenda, halafu hupigi simu kama ulivyoniahidi.” Elvin alinyamaza. “Sasa unakuja?” “Ulitaka tuonane wapi?” Elvin akamuuliza. “Popote tu.” “Kwa kuwa nimechoka, naomba uje nyumbani kama baada ya
saa moja kuanzia sasa, nitakuwa nimeshafika nyumbani na nitakuwa nimetulia.”
“Kwani ulikuwa wapi? Maana nilikufuata leo mpaka ofisini kwako, baada ya
kutokujibu ujumbe wangu, baba yako ameniambia upo likizo. Nyumbani haukuwepo na
ofisini hukuwepo pia, na mama yako alishaniambia ulirudi tayari kutoka safari
yako na Bella. Sasa leo ulikuwa wapi? Maana hata Bella mwenye hakuwepo ofisini
mpaka jioni hii wanafunga ofisi, au ulikuwa naye?” Irene aliendelea kumkaba
Elvin. “Nitakuona baadaye Irene, kwaheri.” Elvin alikata simu.
Alipofika tu nyumbani
kwao, alimkuta Irene alishafika. Alisimama mlangoni akabaki akimwangalia. “Unaweza kuingia tu ukaoge, mimi nitakusubiria.”
Elvin aliinamisha kichwa, akabaki akifikiria pale pale mlangoni.
*Tumaini jipya kwenye maisha ya Bella. Je itasaidia?
*Maji yameanza kuzidi unga kwenye maisha ya Elvin. Wanawake wawili,
wote wakionyesha kumuhitaji sana. Irene
king’ang’anizi wa Penzi la Elvin, na
Bella kiumbe anayeanza kumfanya achukie kuwa naye mbali japo anazidi
kumchanganya
Nini kitatokea? Usikose
Sehemu ya 8.
0 comments: