Story
Ile hali ya kumfumania Zac
ilimuathiri sana kiasi ya kwamba hakujua kama hata akirudia ile mitihani
anaweza kufaulu. James alijua kuna tatizo tu. Nanaa alikuwa ni kama amepigwa na
kibumbuwazi wakati wote. Wakiwa wamekaa sehemu, macho yake yakiangalia kitu,
hayatatoka hapo hata kwa nusu saa. Ndipo James ikabidi kumuuliza taratibu huku
akimsihi asimfiche. Akawa mtu wa kwanza kumsimulia kilichompata. Hakuwa na
ujasiri wa kumwambia mtu yeyote. Hata Zena na Tia hakuwa amewaambia. Ila walijua
kuna tatizo. Kwani hapakuwa tena na simu za usiku wala za asubuhi kutoka kwa
Zac. Simu ya Nanaa ilikuwa imefungwa kipindi chote cha maandalizi na wakati wa
mitihani. Hawakumuona hata akisoma ujumbe.
Urafiki ukarudi kati yake
na marafiki zake, Zena na Tia, kwani Nanaa aliwaambia juu ya Jamal baada
yakumuona anapilika pilika zisizoisha. Kama hakuwepo kwenye simu, basi anakuja
kuchukuliwa na kuondoka. Ndipo Tia akamuuliza kulikoni. Ikabidi kuwaambia
habari za kuvutia za mpenzi mpya mwenye gari na nyumba, si kama Zac.
Alinyanyuka kwenda kuoga
baada ya maumivu kuendelea. Akaona akajisafishe labda maumivu yatatulia.
Akanywa na dawa na kurudi kulala huku mikakati mikali ikiendelea kichwani
mwake. Alishahangaika akidhani atapata mwanaume atakayempenda na kumthamini,
akaishia kujidhalilisha. Alishagawa penzi kwa wanaume hao, lakini hakuna
aliyeona uthamani wake. “Mhhh! Inatosha sasa.” Nanaa
alijisemea moyoni. “Labda kweli shule ndio itakuwa mkombozi wangu pekee. Mapenzi
yamenikataa. Nitulie, nishike moja. Shule tu.” Nanaa aliazimia moyoni.
is mine - ni Wangu! Part 1, Sehemu ya 5.
...ni Wangu!
Sehemu ya 5.
Ile hali ya kumfumania Zac
ilimuathiri sana kiasi ya kwamba hakujua kama hata akirudia ile mitihani
anaweza kufaulu. James alijua kuna tatizo tu. Nanaa alikuwa ni kama amepigwa na
kibumbuwazi wakati wote. Wakiwa wamekaa sehemu, macho yake yakiangalia kitu,
hayatatoka hapo hata kwa nusu saa. Ndipo James ikabidi kumuuliza taratibu huku
akimsihi asimfiche. Akawa mtu wa kwanza kumsimulia kilichompata. Hakuwa na
ujasiri wa kumwambia mtu yeyote. Hata Zena na Tia hakuwa amewaambia. Ila walijua
kuna tatizo. Kwani hapakuwa tena na simu za usiku wala za asubuhi kutoka kwa
Zac. Simu ya Nanaa ilikuwa imefungwa kipindi chote cha maandalizi na wakati wa
mitihani. Hawakumuona hata akisoma ujumbe.
James alimuona vile
alivyoumia. Alimuelezea kwa kuumia sana tofauti na vile alivyokuwa amemueleza
juu ya kusalitiwa na Alex. “Kwa
hakika huyu nilijua ni wangu!” Nanaa
alimalizia kwa kaka yake huku amenyong’onyea pale kwenye kochi. Ilibidi James
achukue nafasi ya umama na kuanza kumtia moyo ili asiharibikiwe zaidi. James
akiwa ameumia sana, alizungumza naye kwa upendo kama mama au dada yake
anayempenda sana. Akamkumbusha wajibu alionao kwa wakati ule wa kwanza ni
shule, ndipo ije ndoa kama Mungu atamjalia mwanaume atakayemthamini. Alimwambia
kwa wakati huo ni lazima kutuliza mawazo na kufanya ile mitihani.
Mungu akamsaidia tena
kipindi hicho kigumu cha machungu na kusalitiwa kikapita. Angalau akaanza
kulala mpaka asubuhi bila kugeuka geuka kitandani. Nanaa alipata nafuu,
akarudisha akili shuleni, akaanza kujiandaa kurudia mitihani hiyo wakati
wenzake wakiwa likizo.
*******************************************
Tia na Zena wao walifaulu
vizuri tu. Tena kwa alama za juu sana. Walihakikisha habari zinamfikia Nanaa.
Ili ajue wao wamempita kielimu. Kwa hiyo hawakuwepo kwenye kundi la wanao takiwa
kurudia mitihani. Baada yakumaliza mitihani, Tia alibaki jijini kwa muda.
Akarudi kuishi nyumbani kwa kina Zena.
Walihakikisha wanajua kinachoendelea. Tena kutoka kwa rafiki wa Karibu wa Zac.
Vicheko viliwajaa kujua
kilichompata Nanaa. “Yako
wapi!? Yako wapi shoga yangu?” Zena
alicheka mara baada ya kukata simu waliyokuwa wameweka kwenye ‘loud speaker’ wakimsikiliza rafiki wa
Zac, akieleza mkasa mzima. “Kitanda
hakiangalii kiuno chembamba, wala rangi ya mwili. Ukilalia tu, mchezo
unachezwa.” Tia
alizidi kupasua mbavu huku machozi yakimtoka kwa furaha ya kumcheka Nanaa. “Alivyoshushuka! Ndio
maana kujidai kote kulimwisha.” “Alikuwa hawezi hata kututizama.” “Kwa mabusu
yale na zawadi! Hata mimi ningenyong’onyea.”
Wakaendelea
kupokezana. “Kawa
mdogoooo! Eti Zac atanioa. Yako wapi? Ndoa Bongo?” Zena akaongeza huku akicheka na
kuongeza. “Halafu
Zac alivyomshenzi, umeona mwanamke aliyelala naye? Ndio ujue havichagui sura
wala umbile.” Walizidi
kucheka na kugonga mikono wakifurahia anguko la penzi la waliyemwita shoga yao.
“Lakini hizo sio habari njema sana
kwangu, Tia.” Akili
ilimrudia Zena wakiwa wanamcheka mwenzao. “Zena bwana! Eti havichagui kiuno.” Tia aliongeza na kuzidi kucheka
akiunga mkono hoja ya shoga yake Zena. “Subiri kwanza Tia. Terry akijua kama
sasa hivi Nanaa hana mtu si ndio atahamisha majeshi kwake?”
Zena aliingiwa na hofu ya gafla. “Ataambiwa na nani huyo Terry? Hakuna
kumtafuta tena Nanaa. Akakae huko huko kwao. Anaweza kurudi na hasira,
akatembea na wanaume zetu wote. Akuu! Atuondolee balaa lake na mkosi. Hata simu
zake hakuna kupokea tena.” Tia aliongea kwa hakika akijihami.
Mikakati ya kumkwepa Nanaa ikakamilika.
Kipindi hicho kabla Tia hajarudi kwao, akiwa jijini kwa kina Zena,
walihakikisha wanamkwepa kabisa Nanaa. Hawakumpigia tena simu. Kwa hiyo kila
walipokuwa wakitoka, hawakutaka kumwambia Nanaa. Evan alikuwa akienda
kuwachukua wao wawili tu. Na kila Terry alipouliza alipo Nanaa, walimwambia
yupo na Zac. Utulivu ukawepo. Zena akaendelea kujisogeza kwa Terry bila uwepo
wa Nanaa.
Nanaa & Jamal.
Maisha ya kuamka asubuhi
nakujisomea yakaanza tena. Wakati mwingine anarudi chuoni kusoma na kukutana na
wenzie wanaorudia mitihani hiyo. Wanasoma pamoja. Akichoka anapanda daladala
mpaka maktaba ya jiji, anaanza kujisomea tena. Ile ilikuwa kama njia yakutoa
uchovu na kubadili mazingira kuanza upya. Kisha jioni anarudi nyumbani.
Akaendelea kufanya hivyo akiongeza bidii ili kutimiza lengo. Ilikuwa ni lazima
amalize chuo.
Akiwa kwenye maandalizi
hayo, akajikuta anakutana na kijana mmoja hapo hapo kwenye hiyo maktaba. Eneo
analopenda kujificha yeye kusoma, ndilo huyo kijana naye alikuwa akipendelea
kwenda hapo. Nanaa alimuona akitua vitabu vyake na kuanza kujisomea. Hakuwahi
kumuona na mtu yeyote, ila yeye tu akijisomea. Wakajikuta kila siku kwenye kona
hiyo wao wawili tu. Kila mmoja kimya, akisoma kivyake.
*******************************************
Wakaanza kusalimiana kila
mmoja wao anapomkuta mwenzake na kuagana kila mmoja wao anapoondoka na kumuacha
mwenzake. Ikabidi kufahamiana majina. Nanaa akajitambulisha kwa Jamal. Siku
hiyo nayo ikapita kwa kujuana majina tu.
“Naona haya ndio maeneo yako ya
kujidai! Hukosi!” Nanaa
akatabasamu. Akanyanyua uso akiwa amezama kitabuni. Alijua ni Jamal tu ndiye
aliyezoea kuwepo hapo, japo siku hiyo alichelewa kidogo. “Inanilazimu. Nimeshikwa. Lazima
kurudia mitihani.” Nanaa
akawa muwazi. “Pole. Inatokea kabisa. Lakini kwa
juhudi hizo, lazima utapita tu.” Jamal akamtia moyo. “Nashukuru. Na hayo
ndio maombi yangu.” Ikawa siku ya kwanza angalau
kumuongelesha kidogo. Akavuta kiti sehemu yake, Jamal akapotelea kwenye vitabu vyake.
Siku nyingine, Jamal
aliingia na kumkuta tena Nanaa alishaingia hapo maktaba. Akamsalimu na kuvuta
kiti pembeni yake. “Vipi?”
“Safi tu. Habari za kutwa?” Nanaa naye akatoa salamu. “Nzuri, namshukuru
muumba.” Jamal
akajibu, Nanaa akatabasamu. “Mbona
na wewe huishi kuja hapa?” Na yeye siku hiyo Nanaa akauliza. “Elimu ya utuuzimani.
Tulikimbia shule wakati vijana, sasa hivi maisha yanaturudisha huku.” Jamal akajibu kwa kifupi. Nanaa
akacheka lile jibu. Kwani Jamal hakuwa hata na dalili ya uzee. “Haya bwana. Hongera.” Nanaa hakuhoji zaidi. Akaishia hapo.
*******************************************
Taratibu wakaanza kutoka
muda mmoja. Jamal anapanda gari yake na kuondoka, Nanaa anaelekea kituo cha
daladala kusubiri usafiri wa kumshusha kituo kilichopo karibu na nyumbani kwa
kaka yake. Baada ya siku mbili, Jamal
akajitolea kumsindikiza kituo cha daladala na kumsubiri mpaka apande kwenye
daladala ndipo na yeye aondoke. Alimwambia hajisikii vizuri kumuacha tu bila
kuwa na uhakika amepata usafiri na kuondoka pale salama. Nanaa akamwangalia kwa
tabasamu, akakubali kusindikizwa. Napo hapakuchukua siku zaidi ya mbili. Baada
ya kusubiri kituoni kwa muda mrefu siku ya tatu, Jamal akaona amsogeze tu, japo
hakuwa akielekea pande hizo.
Nanaa hakuona sababu. “Daladala huwa
zinachelewa tu. Lakini nitapata usafiri. Wewe usijali. Nenda tu, mimi
nitaendelea kusubiria.” Nanaa
alijaribu kukataa lifti hiyo. Lakini Jamal akasisitiza. “Siwezi kukuacha
mrembo kama wewe barabarani hapa na kiza hichi. Ukipatwa na janga? Vijana
wamjini hawawezi kujizuia kwa mrembo kama wewe. Acha nikusogeze japo mpaka Karibu
na nyumbani.” Nanaa akacheka. Wakaongozana mpaka
kwenye gari ndogo ya kawaida tu ya Jamal.
*******************************************
Lifti zikaendelea.
Ikajengeka tabia ya kurudishwa mpaka kituo cha daladala karibu kabisa na
nyumbani kwa kaka yake. Hapakuwa na mazungumzo mengi humo garini. Kila mmoja
akiongea kwa kujiwinda. Lakini Jamal uzalendo ukamshinda. Akaamua kuvunja
ukimya. Alimwambia alivutiwa naye, na angependa wazidi kufahamiana zaidi.
Ukweli Nanaa alikuwa ni
dada mwenye vitu vya kuvutia macho ya mtu yeyote kwa haraka. Hakuwa gumzo la
jiji, lakini ukifanikiwa kuwa naye karibu, lazima utavutiwa tu. Nanaa akacheka
kwa aibu kidogo wakati anakaribia kushushwa kituoni. “Ni sawa baada ya
kusoma siku ya jumamosi, tukaelekea nyumbani kwangu?” Tayari uchu
ulishamlemea Jamal. Kumbeba Nanaa kwenye gari lake na kukaa pembeni yake na
kuyaona mapaja yaliyotulia kitini kila akibadili gia, halikuwa jambo rahisi.
Rangi nyeupe usoni aliyokuwa akiiona ikiwaka, akajua ndivyo atakavyokuta ndani
pindi atakapomfunua. Anavumiliaje tena?
“Sitakuchelewesha. Nitakurudisha hapa
muda kama huu.” Jamal
akasisitiza. “Hee!
Kwa hiyo unataka nishinde kwako siku nzima? Maana unajua siku za jumamosi huwa
namaliza kusoma mapema.” Nanaa alihoji na tabasamu la soni, usoni.
“Nakuahidi
kutokuchoka.” Nanaa
akainama kwa muda kama anayefikiria.
“Ana nyumba na gari!
Ngoja nikajionee. Huwezi jua.” Nanaa akawaza.
Akanyanyua sura na kumtizama Jamal aliyekuwa akisubiria jibu lake. “Lakini sitakaa sana.”
“Ukitaka nikurudishe wakati wowote ule, utaniambia. Lakini ukitaka kulala pia,
sitakuwa na neno.” “We Jamal!” Nanaa
akashangaa kwa pozi. “Hakuna
neema kubwa kama kumiliki Kito cha thamani kwenye maisha ya mwanadamu yeyote
yule hapa duniani. Nitakuwa nimenyimwa shukurani na Mungu hatanikumbuka tena,
kama nikikataa baraka ya uwepo wako nyumbani mwangu. Sasa Mungu anipe nini
tena?” Nanaa
akamtizama kama kuhakiki yale maneno, akabaki natabasamu asijue ajibu neno gani
kwa maneno mazito kama yale. Jamal alijua wazi amekubaliwa.
*******************************************
Siku hiyo ya jumamosi
Nanaa akawahi kufika hapo maktaba akiwa na shauku ya kumkuta Jamal. Mpaka inafika
saa sita kasoro, Jamal hakuwepo. Wasiwasi ukampata Nanaa. Akajuta kujirahisisha
kwa kiasi kile. “Kwa nini nilimkubalia?” Akajilaumu huku ameinamia vitabu
vyake. Mara akasikia mtu anamgusa begani. Akageuka. “Jamal!” “Ahadi ni
deni Nanaa. Saa sita ndio hii. Nimekuja kukuchukua.” Nanaa akacheka kwa furaha. “Mbona hukuja tokea
asubuhi?” “Si kwa ugeni nilio nao mimi.” Jamal alijibu na
kumfanya Nanaa acheke. “Kwa
hiyo ulikuwa ukijiandaa na ugeni?”
Nanaa
akauliza. “Kumbe!?
Sio mgeni wangu anafika nyumbani, hamna chakula wala maji! Sikulelewa hivyo.”
Jamal alikuwa na lafudhi iliyomvutia Nanaa. Lafudhi ya watu wa pwani. Nanaa
akatabasamu na kurudi kukusanya vitu vyake vyote vilivyokuwepo hapo mezani.
Jamal akamsaidia kubeba, na kutoka pale maktaba.
Nanaa
nyumbani kwa Jamal.
Jamal akaendesha mpaka
nyumbani kwake Temeke. “Huku
ndiko nilikopata sehemu ya kuishi.”
Jamal
aliongea wakati anamfungulia Nanaa mlango. Nanaa ambaye hachagui sura ila mtu
tu wakuwa naye, hakuona shida. Ilikuwa nyumba ndogo tu. Kwa haraka Nanaa akajua
anaishi peke yake. Palikuwa pasafi sana. Nanaa akaona asiwe mchoyo wa sifa. “Jamal wewe unaonekana
ni msafi sana.” “Subiri mpaka uangalie kila mahali ndipo usifie. Unaweza
ukajuta baadaye.” Nanaa akacheka.
Akaingia na kutaka kukaa.
“Twende
nikutembeze kila mahali. Sitaki tena siku nyingine ukawa mgeni humu.” “Kwani
unampango wa kunikaribisha tena?” Nanaa akauliza kwa
tabasamu. “Hata!
Nataka siku nyingine na mimi uje unikaribishe.” “Humu humu ndani?”
Nanaa akauliza huku akicheka. “Kumbe?
Na mimi nataka siku nyingine nikirudi, nisikute makochi yakinitazama. Bali nikukute
na wewe kitini unanisubiri.” Nanaa
akacheka sana.
“Au hutaki?” “Sijui.” Nanaa akajibu kwa aibu. “Yaani unataka leo
ndio iwe mwisho!? Haiwezekani Nanaa. Nimekukaribisha hapa kwa kuwa
nimekuheshimu na ninakuona ni mtu utakayenifaa. Si ningekukaribisha tu hata
baa? Kukuleta hapa kwangu, ujue nimekuheshimu sana.” “Nakushukuru.”
Nanaa akasuuzika roho. Mungu ampe nini tena? Nyumba, gari na Jamal
anayemtangazia wenyeji mchana kweupee!
“Twende sasa
nikuonyeshe kila mahali. Au njaa inakuuma?” “Hapana. Nipo sawa tu.” “Kwa hiyo
unaniruhusu nikutengee chakula baadaye?” “Hamna shida.”
Nanaa alijibu kwa kuridhika kabisa kitu kilichomfurahisha Jamal aliyekuwa
akimezea mate mapaja aliyokuwa akiyaona ndani ya gauni. Sasa hivi yapo ndani ya
nyumba yake. Nanaa si mtoto!
Akarudi kumshika mkono
kumuongoza atakapo yeye Jamal. Bila hiana, Nanaa akafuata kwa tabasamu.
Walifanikwa kuona chumba cha kwanza, choo cha wageni wakaishia chumbani kwa
Jamal. Humo ndipo alipojua ni kweli Jamal alikuwana uchu naye. Chumba kile
kisafi, Jamal alikitumia ipasavyo kukata kiu. Na Nanaa naye hakumzuia.
Akajituma ipasavyo. Hapakuwepo tena na Zac wakumfanya ashindwe kumvulia nguo
Jamal. Akamkumbuka Terry, akajiambia kama angekuwepo wakati ule, yeye ndio
angefaidi. Lakini akakumbuka uchu wa Zena kwa Terry. Akaona ajiachie tu. Akahangaika
siku nzima kumfurahisha Jamal kwenye kitanda hicho bila hata kujali hisia zake.
*******************************************
Nanaa akaanza kujifikiria ndio anakuwa mama wa
ile nyumba, na kwa usafiri ule aliokuwa nao Jamal, sio pabaya sana kuanzia
maisha. Hakuona chakupoteza kama akitoa penzi lake kwa Jamal, pengine atamvutia
zaidi. Na kweli, hapakuwa na jinsi ungesema Jamal hakumfurahia Nanaa siku hiyo
pale kitandani. Nanaa alitoa ujuzi wake wote siku ile kumfurahisha Jamal bila
hata kujijali yeye. Alijituma kwa kadiri ya uwezo wake. Yale aliyokuwa akimfanyia
Zac, ndio alipewa Jamal siku ile tena kwa juhudi huku akiongeza mautundu, asije
kukimbiwa tena. Kwa Nanaa alikuwa ni kama yupo kazini. Lengo moja tu, ndoa. Awe
na kwake, aepukane na kuishi au kuwa mzigo kwa mtu. Yeyote mwenye mafanikio
kidogo ya maisha, huyo alimfaa. Hapakuwa na vigezo eti mwanaume mrefu. Sijui
kifua kipana. Rangi sijui iweje! Hapana. Bora mwanaume, basi.
*******************************************
Mapenzi yakachanganya,
ratiba za maktaba zikaanza kuongezeka. Siku ambazo Jamal haendi kazini, siku
hizo za jumamosi, Nanaa alifika nyumbani kwake asubuhi. Walipata kifungua
kinywa pamoja, mapenzi kidogo, kisha kujisomea. Ikifika jioni, mapenzi tena
yakuagana, ndipo anamrudisha Nanaa nyumbani kwao.
Mambo yakaenda vizuri,
wakiwa wanatumia muda mwingi kusoma na mapenzi. Hapakuwa na maongezi mengi sana
kati yao, kwani Jamal alionekana kumtaka zaidi Nanaa kitandani kuliko kitu
kingine. Kile kitendo chakuonyeshwa anahitajika na mtu, kilimfariji sana Nanaa.
Simu na ujumbe wakutakiwa usiku mwema, huku akiambiwa ni jinsi gani anasubiriwa
kesho yake wakafanye hiki au kile havikuisha. Pengo la Zac likazibika kwa
haraka sana. Yale aliyokuwa akifanyiwa na Zac, akakutana nayo kwa Jamal. Tena
akimsifia vilivyo huku akimlaumu kumuacha akiwa bado anamuhitaji kwa mapenzi
zaidi.
*******************************************
Muda wa Nanaa wa kurudia
mitihani yake ikafika. Akafanya akiwa ametulizwa kwenye penzi la Jamal
aliyekuwa akimpa vihela vya hapa na pale vyakujikimu. Matokeo yakatoka, yale
masomo akawa ameyafaulu, akaendelea mwaka wa pili na penzi la Jamal.
*******************************************
Zena akapata habari ya kuzidi kumchafua Nanaa
kwa Terry, ili kumvuta kwake. Nanaa hakuwa akitoka nao tena, kwani alikuwa akija
kuchukuliwa mara baada ya kipindi chao cha mwisho siku ya ijumaa. Kila
alipokuwa akitoka kwenye lecture siku hiyo ya ijumaa, alimkuta Jamal akimsubiri
nje. Alikuwa akimchukua siku za ijumaa anakuwa naye nyumbani kwake mpaka
jumatatu asubuhi wakati Jamal akienda kazini ndipo anamshusha chuoni.
Nyumbani kwa kaka yake
alikuwa akienda siku ya jumapili. Atakaa naye kidogo, na kumuaga. Kulala nyumbani
kwa kaka yake akapunguza. Kama siku hiyo ya jumapili akienda kumtembelea kaka
yake akapakuta pachafu, basi atamsaidia kusafisha na kufua. Akishaacha kila
kitu sehemu yake na chakula, ndipo anaondoka kurudi kwa Jamal mpaka siku
inayofuata, jumatatu.
Ilimbidi kuongeza juhudi
ya kusoma hizo siku za kati kati ya juma. Maana siku hizo anazokuwepo kwa
Jamal, kuanzia hiyo ijumaa jioni mpaka jumatatu asubuhi wanapotoka hapo kwa
Jamal, Nanaa alikuwa mke kweli kweli. Kujituma kumpikia na penzi kitandani.
Kufua na kufanya usafi kwenye kijinyumba hicho kidogo, ambacho Nanaa alishajiona
ni mama mwenye nyumba. Yaani yupo kwake.
Asubuhi ya jumatatu pia Jamal
alimuaga kwa kujiridhisha kweli kweli akimwambia kwa kujifidia kwa siku hizo
ambazo Nanaa hatakuwepo hapo. Walifanya penzi la kufidia jumanne, jumatano na alhamisi.
Ijumaa usiku alirudishwa kitandani hapo. Na jumatatu asubuhi alitoa sex ya
nguvu ndipo wanapooga, nakuanza siku. Jamal kazini, Nanaa chuoni. Maisha
yakaendelea.
*******************************************
Penzi alilokuwa akipewa
Jamal halikuwa kama la Zac. Kwani Zac alipewa kwenye hosteli na nyumbani kwa
rafiki yake. Hapakuwa na uhuru. Alipewa penzi la kimya kimya sababu walijua
wapo wanachuo wengine wanapita nje ya chumba chao, au walijua wapo wanachuo
wengine chumba cha jirani. Wakiwa nyumbani kwa rafiki yake Zac, pia iliwalazimu
kuwa wastaarabu japo walijua anajua kinachoendelea huko chumbani. Lakini hapo kwa
Jamal, Nanaa alikuwa huru.
Kwanza ni nyumba
anayoishi peke yake. Majirani wapo mbali. Jamal hakuwa na maneno mengi.
Alimuonyesha wazi anamtaka kitandani tu. Kila asubuhi anapokuwepo hapo nyumbani
kwake, nilazima amwamshe kwa kumtaka kimapenzi. Tena penzi la haja. Jamal
hakuwa mvivu hata kidogo katika hilo eneo. Kitu kilichomlazimu Nanaa mwenyewe
kujituma kweli kweli hata kama ni asubuhi. Ndipo aamke akaandae kifungua
kinywa. Na baada ya hapo tena warudi tena kitandani.
*******************************************
Alimshangaa vile Jamal
alivyokuwa mkimya. Hakuwa akizungumza sana. Kama sio wanafanya mapenzi, basi
wanaangalia mpira. Mechi za timu za nchi za bara la Ulaya au tamthilia za hapo
hapo nyumbani. Alikuwa na mikanda mingi sana ya filamu ambayo walikuwa
wakiangalia kila wanapokuwa pamoja. Na alimuonyesha wazi, pindi anapoangalia
vitu vyake kwenye luninga, angependa kusikia na maneno. Kwa hiyo kunakuwa na
utulivu wa aina yake.
*******************************************
Siku moja ya jumapili
wakati Jamal anaogo na Nanaa yupo kitandani, baada ya shuguli nzito hapo
kitandani. Tena Nanaa akiwa anaugulia maumivu kwa mapenzi ya muda mrefu. Simu
ya Jamal ikaanza kuita akiwa yupo bafuni. Nanaa akiwa hoi hapo kitandani,
akigugumia maumivu ya michubuko mingi aliyoipata katikati ya tendo, nakushindwa
hata kusema, au kumwambia Jamal ili tu kumfurahisha. Alibaki hapo kitandani
akigugumia maumivu sehemu za siri huku akiitazama simu ya Jamal iliyokuwa
ikiita na kukata.
*******************************************
Tokea siku ya ijumaa wanafika
hapo nyumbani mpaka siku hiyo ya jumapili, Jamal alionekana anataka kufanya
mapenzi tu. Tangia anamchukua Nanaa chuoni, Nanaa alishamuona hayupo sawa. Alipoingia
kwenye gari akajua kuna tatizo. Nanaa alimsalimia kama kawaida. Akarudisha salamu
kwa kifupi tu. Baada ya kuona amekuwa kimya sana au mzito wa maongezi, akaamua
na yeye anyamaze. Walipofika tu nyumbani siku hiyo ya ijumaa, akamshusha
nakutoka kufuata chakula. Hakutaka Nanaa apike. Alimwambia aoge, nakumsubiria.
Ndipo mapenzi yakaanza
bila maongezi mengi. Kila alipomuuliza kulikoni, alimbusu, na kuanza tena mapenzi. Jumamosi nayo ikawa hivyo hivyo.
Anatoka kwenda kununua chakula. Baada ya muda anarudi, kazi inaendelea. Kwa
ukavu ule aliokuwa akikutana nao kwa Nanaa nakuendelea kufanya naye mapenzi
bila kujali, wala kutaka kumlainisha kwanza, japo Nanaa alishamjua si mtu wa
kujali anachojisikia yeye wanapokuwa kwenye mapenzi, lakini siku ile
alizidisha. Hapakuwa na mapumziko marefu wala maongezi. Wakati wote alitaka
Nanaa amchezee na kuanza mapenzi tena na tena. Nanaa alijua lipo jambo.
Alimchubua vilivyo. Mpaka inafika siku hiyo ya jumapili, Nanaa hakuwa na hamu
tena yakuwepo pale.
Mara hiyo ya mwisho kabla
yakuingia bafuni kuoga na kumuacha hapo kitandani, Nanaa alihangaika naye sana
ili kumfikisha. Alishasahau hata walianza saa ngapi. Alifanya naye huku
akigugumia na kujikaza sana. Alishamuomba Mungu wake amkumbuke kipindi kile,
Jamal amalize, apumzike. Mpaka anafanikiwa, Nanaa hakuwa na hamu. Alilala pale
kitandani akiwa hoi na maumivu makali. Akiwaza kama amuage Jamal na kumwambia
amepata zarula anatakiwa kuondoka, au amwambie ukweli kama anavidonda vinavyompa
maumivu makali sana. Hataweza kufanya tena mapenzi siku ile. “Ataniona
sifai. Heri niendelee kujikaza, lakini nimkwepe mapenzi leo. Angalau nijiuguze
mpaka tena ijumaa ijayo atakapokuja kunichukua. Nitakuwa nimepona.” Simu
ya Jamal ikaita tena na kumtoa kwenye mawazo.
Nanaa alizwa
tena.
Akamwita Jamal mara
kadhaa kumuuliza kama ampelekee simu hiyo huko bafuni au ajibu yeye, lakini
Jamal hakusikia. Ikaita mara tatu, kisha ujumbe ukaingia. ‘Mtoto bado
ni mgonjwa, mume wangu. Pesa uliyonitumia haijatosha matibabu na chakula.
Uliniahidi kuja leo. Mpaka sasa hujafika na simu hupokei. Nimeamua kwenda kwenu
ili wanisaidie. Mama yako ameamua kumrudisha Fatma hospitalini Barabara ya
kwanza, ili afanyiwe vipimo upya. Homa ipo juu sana. Hapa tulipo tupo
hospitalini. Naomba upokee simu mume wangu. Unatutia wasiwasi, hasa baba.’ Nanaa alikaa kwa mshtuko.
Wakati anafikiria na
kurudia ule ujumbe, Jamal aliingia pale chumbani. “Mbona umeshika simu
yangu bila ruhusa? Unatafuta nini?” Jamal aliiuliza kwa
hasira. “Kwa
nini hukuniambia kama umeoa na unafamilia!?” Nanaa aliuliza. “Uliuliza?” Jamal alijibu kwa kuuliza swali
nakumfanya Nana ashindwe chakujibu. Alitamani kulaumu, lakini akakumbuka
hamfahamu Jamal hata kidogo. Ni kweli hakudanganywa. Alitamani kulia. Lakini
akajisuta moyoni. Anamlilia nani pale? Jamal hakuonyesha kufumaniwa hata
kidogo.
Alichukua simu yake
kutoka kwa Nanaa bila shida. Akavaa pensi yake, akatoka pale chumbani bila hata
maelezo ya ziada kwa Nanaa. Bila kupoteza muda wala kuoga, Nanaa akavaa
harakaharaka, akakusanya vitu vyake nakutoka. Alikutana na Jamal nje
akizungumza na simu, akampita na kuondoka bila ya kumuaga.
*****************************************
Kwa kutumia pesa
alizokuwa amepewa na Jamal siku chache zilizopita, akachukua taksii kurudi
chuoni. Hakutaka hata kupeleka sura yake kwa kaka yake. “Vipi Jamal? Mbona
umerudi leo badala ya kesho?” Zena alimrushia swali mara alipofika
chumbani kwao. Aliwakuta wakiangalia
tamthilia, kila mmoja akiwa kitandani kwake. “Wewe Nanaa? Si huwa unarudi jumatatu
asubuhi?” Nanaa alijitupa kitandani kwake, akalala bila kujibu
kitu.
Kwanza alikuwa na madonda
ya penzi alilokuwa akilitoa tokea siku ya ijumaa alipochukuliwa hapo chuoni.
Kwa hiyo alikuwa na maumivu makali sana. Alijichukia na kujidharau sana vile
alivyokuwa akivumulia, ili kumridhisha Jamal. Alijinyima raha yeye, ili kumpa
raha mume wa mtu! Kwa kipi? Kwa nini?
Pili alijichubua yeye
mwenyewe donda la moyoni. Kwa haraka gani jamani? Hata muda mrefu haukuwa
umepita tokea atendwe na Zac, akajitupa kwa Jamal. Bila kumfahamu Jamal, siku
ya kwanza tu kukaribishwa nyumbani kwake, tayari kitandani, tena kwa sarakasi
kibao. Nikulogwa au ujinga ulioje! Haraka hiyo ya kujigawa hivyo kama karanga
za kwenye kapu zinazoonjeshwa kwa kila mtu, ili zinunuliwe hata kwa wasiokuwa
na lengo nazo, ni za nini?
Hayo yote yakazua ububu.
Hakujua awaeleze nini wenzake. Walishamshuhudia akiwa kwenye mahusiano ya
mapenzi na wanaume wawili. Kwa muda mfupi mfupi, ndani ya mwaka mmoja, tena
walijua ni mahusiano mazito. Kwani Nanaa
alikuwa akihama kabisa na kwenda kuwaridhisha hao wanaume zake. Halafu mahusiano
yote hayakudumu! Anawaambia nini wao waliokuwa wakimsifia uzuri wa kila kitu?
Alijua hata marafiki zake watamshangaa.
*****************************************
Tia bado alikuwa kwenye
mahusiano na Evan. Na hakuwahi kumsikia akimlalamikia huyo Evan hata mara moja.
Habari za Evan zilizokuwa zikiletwa humo chumbani, ni sifa zake tupu. Vile
anavyojua kumjali, basi. Tena Tia msichana wa kawaida kabisa. Hakuna cha rangi
nyeupe wala umbo namba 6 au 8. Hakuna alikopita wanaume wakageuka au hata
kuhisi kama amepita msichana wa ajabu. Lakini alitangaza kuenziwa na mwanaume aliyeanza
naye tokea yupo kidato cha 5. Sasa yupo chuoni mwaka wa pili. Tena sio na
mwanaume wa kijijini. Evan. Mtoto wa jijini. Ametoka kwenye familia ya wasomi,
wenye exposure. Anajua warembo na sifa zake. Lakini Tia alijisifu vile
alivyotulia kwake.
*****************************************
Alinyamaza pale
kitandani, akijuta kwa nini aliwasaidia kutafuta chumba. Tena kuwafanya waishi
nao chumba kimoja. Kama asingekuwa kuwasaidia kuwatafutia chumba, wala
wasingeishi chumba kimoja. Usiku huo angekuwa na watu wengine. Wasiojua historia
yake ya mapenzi. Wala si Zena na Tia. Na wala wasingejua kinachoendelea. Nanaa
akajuta sana.
*****************************************
Kipindi Nanaa yupo hapo chuoni akijiandaa na
kurudia mitihani yake, Zena alimtafuta na kumuomba awasaidie kutafuta chumba
kwa kuwa yeye alikuwa maeneo ya hapo chuoni, na walijua kuna matron alikuwa
akimpenda sana Nanaa, wakajua wakimpanga vizuri Nanaa, watapa chumba hapo hapo main campus, wanapopapenda, tena
kwenye sehemu nzuri.
*****************************************
***********************************************
Alipopona tu madonda
aliyoachiwa na Jamal. Tena alijiuguza kwa kujipaka mafuta kila wakati bila
kumwambia mtu. Huku asijue kama inasaidia au la! Kama anajiongezea sumu mwilini
au la! Kila alipooga na kujisafisha, alipaka mafuta mpaka akapona. Maswali ya
hofu yalipita kichwani mwake akijiuliza mbali na madonda yale, ni nini kingine
Jamal alichomuachia!? Yalimtesa sana. Mwishowe akaona asijichoshe na maswali
ambayo anaweza kupata majibu yake.
Nanaa ambaye hakujua kama
ni mchaga au vipi, akapiga moyo konde mpaka hospitali ya kulipia. Mbele ya
daktari aliyemkuta siku hiyo akamwambia shida yake ni moja tu, kujua kama
ameathirika au la! Alipomuuliza kwa nini hakwenda kwenye vituo vya ushari
nasaha, akasema moyo wake ulimtuma hapo. Hataki kuulizwa maswali wala hataki
kushauriwa. Yeye anataka kupimwa UKIMWI, apewe majibu yake, basi. Mengine
atajua mbele ya safari.
Kwa kuwa ilikuwa ni
hospitali ya kulipia, pesa yake tu. Nanaa akapimwa. Alikaa pale akisubiri
matokeo yake huku mawazo yakizunguka huku na kule. Yalipotoka na kuambiwa
hajaathirika, akatoka pale bila kuaga. Akajiwekea mikakati yake. Akajiambia
lazima kuitimiza hata iweje.
*******************************************
Na kweli Nanaa aliamua
kutulia na shule tu. Aliachana na kila aina ya marafiki na vishawishi
vitakavyoingilia shule yake, akatuliza mawazo shuleni tu. Muda wa kuwepo hapo
hosteli ukapungua. Akaanza kuishi nyumbani kwa kaka yake zaidi labda kuweo na
test au kipindi cha mitihani. Alifanya hivyo ili kupunguza kero za wanaume
walioanza kumfuata mpaka pale chumbani anakoishi na kina Tia.Walipojua tu Nanaa
ameachwa tena na Jamal, Tia na Zena wakaanza kumkwepa huku wakimcheka waziwazi.
Nanaa akajua. Akaamua kujitenga nao kabisa.
Wakiwa wanamsengenya
Nanaa kwa mafumbo bila kujua Evan dereva wao aliyekuwa akiwaendesha
anawasikiliza. Zena na Tia wakiwa wamekaa kiti cha nyuma wakicheka bila habari.
Wakajikuta wanaropoka jina la Nanaa na kusema kuwa ameachwa tena. Evan
hakuchelewesha zile habari. Wakiwa wamesimama kwenye mataa, Evan akamtumia
ujumbe Terry kwa haraka sana. ‘Naona Mungu amesikia sala zako. Nanaa hana mtu tena. Nasikia ameachana
na huyo mwanaume mwingine. Changamka. Huu ndio wakati wako kabla hajakupiku
mwingine.’ Evan alituma ule ujumbe pale pale wakati Zena na Tia
wanaendelea kumcheka Nanaa.
*****************************************
Terry akamtafuta Evan,
wakapanga weekend inayofuata, lazima Evan arudi jijini ili kumsindikiza
hosteli, kwenye chumba cha Tia na Zena wakijua ndipo watakapompata Nanaa, kwa
kuwa walijua wakipanga kuwaita Zena na Tia mahali, Nanaa hatakwenda.
Na kweli ijumaa usiku
Evan alitoka chuoni SUA akaenda moja kwa moja nyumbani kwa kina Terry.
Wakazungumza na kupanga asubuhi na mapema waamkie chuo kikuu cha Mlimani. Ili
tu Terry ambaye alikuwa akisubiri muujiza wake, akamuone Nanaa. Na kweli Evan
rafiki watokea utotoni mwa Terry akawasili nyumbani kwao. Akamchukua, safari ya
Mlimani ikaanza. Njiani alikuwa kimya. Evan alijua wazi anapanga hoja zake
pindi atakapofanikiwa kumkuta Nanaa ambaye hawakuwa wamemuona kwa kipindi
kirefu. Kila alipokuwa akimuulizia, Zena alimtinga na majibu aliyodhani
yatavunja moyo wa Terry, lakini asijue ndio alikuwa akiongeza shauku ya Terry kuja
kummiliki Nanaa.
Mungu alikuwa upande wao,
walifika kwenye chumba cha kina Tia, saa nne asubuhi. Wakamkuta kweli Nanaa
yupo. Lakini alikuwa kwenye simu. Mtu wa upande wa pili akiongea, ambaye
alikuwa James. Nanaa alishawasalimia kwa kuwapungia mkono mara walipoingia
chumbani hapo, akiwa na simu sikioni imeshikiliwa na mkono wa shoto. Wakulia
ndio ulifanikiwa kuwapungia wakati wanaingia, akaendelea kukusanya baadhi ya
vitu huku akizungumza kwenye simu.
Terry alijawa na furaha
baada ya kumkuta Nanaa hapo ndani na kupata tabasamu lililosindikizwa na
dimpozi nzuri za Nanaa. Akafarijika moyoni. Wakaendelea kusalimiana na Zena na
Tia wakati Nanaa bado yupo kwenye simu. Ndipo wakasikia Nanaa akijibu, “Pole sana kaka
yangu. Basi nakuja kukusaidia. Labda uji utakaa tumboni.” Hapo hapo
Nanaa akachukua kijibegi chake kama pochi. Akawapungia tena mkono. Safari hii
alikuwa akiwaaga, akatoka akiwa bado anazungumza kwenye simu.
*****************************************
Haikuwa weekend nzuri
hata kidogo kwa Terry. Pale pale alibadilika. “Twendeni basi.” Zena aliongea kwa sauti ya
kuchangamka. Kwani waliingia na ofa ya kuwachukua na kuwapeleka kwenye kifungua
kinywa. Terry alishabadilika mpaka alionekana usoni. “Hata mimi nipo
tayari.” Tia
naye aliongea huku akimsogelea Evan mpenzi wake. “Naombeni niwe muwazi. Mimi
sitaongozana na nyinyi. Nilimfuata Nanaa, naona na yeye ameondoka. Sina kawaida
ya kwenda kupata kifungua kinywa asubuhi asubuhi kwenye mabaa. Kwanza mimi sio
mlevi, na pili kwetu wanakuwa na kifungua kinywa kizuri sana zaidi ya mahoteli
mengi sana hapa mjini.” Akiwa
na hasira, Terry akatoka.
Zena aliumia sana. Hapo
hapo na yeye akakubaliana na matokeo. Kuwa hata iweje, Terry hawezi kumpenda. Wala
hatawahi kuwa wake. “Nilidhani Terry atakuwa wangu!” Zena aliwaza moyoni, akiwa
amejawa simanzi usoni. Japokuwa alishamuonyesha wazi kuwa anamtaka awe mpenzi
wake, lakini Terry hakuonyesha kumtaka hata kidogo.
Akakubali pia kosa
halikuwa la Nanaa. Nanaa alishajitoa kwao muda mrefu sana. Na alikuwa na
uhakika Nanaa na Terry hawakuwa wakiwasiliana hata kidogo. Kumuwekea kinyongo
Nanaa alijua ni kumuonea tu. Nanaa mwenyewe alishamruhusu amchafue vile
atakavyo kwa Terry ili tu kumvutia kwake.
Alielewa maumivu aliyonayo Terry kwa wakati ule, ‘kupenda asipopendwa!’ Inauma. Akamuhurumia kwanii na yeye
ndipo alipokuwepo kwa wakati huo. Alitamani ingekuwa vinginevyo ili mambo yawe
tofauti. Lakini mapenzi ni kitu cha ajabu. Akaamua awaache tu Tia na Evan
watoke wao peke yao. Yeye akabaki.
Nanaa ahama hostel na kurudi kwa kaka yake.
Akiwa njiani yale
yaliyokuwa yakiendelea pale chumbani akiwa anazungumza na kaka yake kwenye simu
yakamjia. Akakumbuka jinsi Zena alivyobabaika mara Evan na Terry walipoingia. “Zena
bado anaonekana hajafanikiwa kwa Terry.” Nanaa akawaza. “Inabidi
nijiweke nao mbali kabisa. Hata pale chumbani nihame. Nisije nikarudi, akapata
sababu yakunichukia zaidi.” Nanaa alishajua wanamchukia. Hakutaka wamrushie
yeye lawama. Akakusudia kutulia nyumbani kwa kaka yake moja kwa moja. “Hakuna
kulala kwengine tena isipokuwa kwa kaka tu.” Nanaa akakusudia kuhama
kwenye hicho chumba ambacho ni kama yeye ndio aliwakaribisha wenzake. Akaanza
kuhamisha kitu kimoja baada ya kingine bila kuaga.
Sio wanafunzi wa mwaka wa tatu wala wa kwanza
waliokuwa wakimtafuta Nanaa tu. Hata wenzake wa darasa moja walimtafuta. Alikuwepo
kama hayupo. Akiwa mahali alinyamaza kimya kama hayupo. Kwanza angezungumza
nini wakati habari zake zilishasambazwa kila mahali na kina Zena na Tia. Wakidhani
wanamuharibia zaidi, kumbe ndio wanaamsha wale waliokata tamaa kwenda kujaribu
bahati zao na wao kwa Nanaa.
Lakini Nanaa alikusudia. Alikataa
katakata swala la shule na mapenzi. Hata uwe na pesa na kumuahidi kumpa yeye
gari, Nanaa asingekubali tena. Waliposhindwa kwa Nanaa mwenyewe, waliwafuata
marafiki zake ili wawasaidie kuwatongozea Nanaa. Alipoona fujo za Zena na Tia
zanazidi. Wanachukua pesa zawatu kwa lengo la kugawa namba yake kwa watu
asiowafahamu, akabadili namba na kuhamisha vitu vyake vyote pale chumbani. Maana
wakati mwingine wa mchana, alikuwa akirudi kujipumzisha pale chumbani kwao, na
ndipo hapo kina Zena hutoa habari kwa wanaume kuwa yupo chumbani. Akaamua
kukusanya kila kitu chake mpaka kalamu. Na kweli akaacha kabisa kulala nje na nyumbani
kwa kaka yake. Ikawa ni nyumbani kwa kaka yake James ambaye alikuwa kama ndiye
ndugu wa pekee na mzazi wake Nanaa. Basi. Iwe karibu ya mitihani au la, Nanaa
alihakikisha usiku analala nyumbani kwa kaka yake. Ikitokea anachelewa kumaliza
kujisomea na wenzake, alimsihi James awe anamfuata chuoni ili arudi naye
nyumbani.
*******************************************
Hakika Nanaa hakuwa
ametania. Alikusudia. Mpaka kina Tia wakaanza kuwa na hamu naye na kuanza
kujirudi. Lakini aliyeng’atwa na nyoka, kang’atwa tu. Nanaa akawa makini kwa
kila mtu anayemsogelea. Hakuonyesha hasira, lakini aliishi na kila mtu kwa
tahadhari. Maisha yake ikawa shule, na nyumbani. Zena na Tia ndio waliobaki
kusumbuliwa na wanaume. Na ndio waliokuwa wakipokea hongo ili kusaidia
kumtongoza Nanaa, lakini Nanaa alibaki akiwacheka. “Mtakuja kubembwa juu juu nyinyi! Endeleeni kupokea pesa za watu.”
“Sasa kama huyu kaka mwingine kwa nini unamkataa?” Tia alimuuliza. “Hana lolote. Anataka anivue nguo tu, ili aniangalie hili tako likiwa
halina nguo. Anichezee aje kuniumiza moyo wangu. Sitaki.” “Bwana huyu kaka
anachanganywa na miguu yako.” “Sio miguu tu. anasema anapenda kiuno cha Nanaa.”
Zena alidakia. “Basi mpeni pole.
Mwambieni atakiona kwenye gauni, lakini hatawahi kuniweka kitandani.” “Basi
nenda hata kazungumze naye, Nanaa shoga yetu. Tumekula pesa yake.” Nanaa
alicheka sana. “Mtajijua wenyewe. Aliyewaambia
mpokee nani? Nishamaliza kazi ya kuvulia wanaume nguo. Kama hawakubahatika
kipindi kile cha mgao, wapeni pole. Waambieni Nanaa ameshamaliza mgao.” Akawacheka
na kuondoka mapema kabla giza halijaingia kuwahi kwa kaka yake.
*******************************************
Kweli mapenzi
ni kitendawili! Je ni mara zote, au mara nyingi, “Utapenda usipopendwa, na kupendwa, usipopenda”?
Usikose Sehemu ya 6.

0 comments: