Nilipotea! - PART 3 - Sehemu ya A
Gabriel alimuona vile Net
alivyobadilika. “What Net? Nini?”
Gabriel aliuliza kwa kujihami baada ya kumuona jinsi Net anavyomuangalia. “No man! Hamna neno.” Net alijibu na uso
ulionekana kusikitishwa sana na rafiki yake. “No. Say it. Just say it Net. Kumbuka mimi
nakufahamu wewe vizuri sana Net. Wewe ongea tu kile kilichopo mooni mwako.
Maana ni wewe mwenyewe ndiye uliyeniambia niachane na huyu msichana. Tena kwa
mikwara mingi sana! Nilikwambia jinsi ninavyompenda Nancy.” “Hujawahi kumpenda. Ulikuwa ukitumia tu mwili wake, lakini si
kumpenda.” Net akamkatalia Gabriel
na kumshangaza.
“Unajuaje!?
Nilimpenda na….” “Please don’t. Just Don’t. Nyamaza tu.” “What’s wrong with you Net? Unatatizo
gani Net!? Mbona mimi sikuelewi?” Net aligeuka akataka kuondoka,
kisha akamgeukia rafiki yake tena. “Na
kwa taarifa yako tu Gabriel, jina lake ni Tunda, sio Nancy.” Gabriel
alibaki ametoa macho asielewe, huku manyunyu ya mvua yakiongeza kasi kuashiria
mvua kubwa inakaribia kumwagika.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Tunda alienda kuchukua mizigo
yake aliyokuwa ameiacha pale mapokezi asijue anarudije Dar, na hata usiku huo
anakwenda wapi. Alitoka pale hotelini taratibu huku akilia kwa uchungu sana.
Mvua kubwa na radi iliyoanza gafla ilimfanya akimbilie kwenye moja ya jengo la
hoteli hiyo. Alikimbia mwisho kabisa kwenye kona akajibanza huku akilia kwa
hofu.
Kwa asili Tunda alikuwa muoga
sana wa radi. Alianza kutetemeka baridi, kwani pale alipojificha pia mvua
ilikuwa ikimfikia na hali ya hewa jijini Arusha ilikuwa baridi haswa. Tunda
hakuwa hata amevaa sweta. Baridi na hofu vilimjaa, na kila aliposikia ngurumo
za radi alizidi kutetemeka na kuzidi kulia. Pesa ya kuchukua taksii hakuwa
nayo. Halafu akajiuliza, hata akichukua taksii, inampeleka wapi usiku ule!
Akaendelea kulia. Mambo yamembadilikia gafla.
Aliona gari ikizunguka pale,
ikienda na kurudi mara kadhaa. Tunda aliendelea kulia. Baada ya muda akamuona
mtu akikimbia, kwenda na kurudi. Mvua kubwa bado ilikuwa ikinyesha. Kwa mbalii
akasikia mtu akiita jina lake. “Tundaa!
Tundaaaaaa!” Alihisi ni mawazo. Lakini kila alipojaribu kupuuzia ile sauti
ndivyo alivyoisikia kwa karibu zaidi.
Akasimama kutaka kuthibitisha
kama ni mawazo yake au la. Akajitokeza pale alipokuwa amejificha na kuchungulia
nje huku radi ikipiga sana. “Tundaaa!” Ana kwa ana na Net, aliyekuwa
amelowa chapachapa. Net alikuwa akimwita kama mwehu. Alipomtambua kuwa ni Net,
Tunda alifunika uso wake nakuzidi kulia kwa aibu na uchungu.
Net alimsogelea karibu kabisa,
akasimama mbele yake asijue aseme nini tena. Alibaki akihema kama mbwa
aliyekimbia mwendo mrefu sana. Akabaki akimtizama Tunda. Tunda akajua ni yeye
ndiye aliyemuona akikimbia. Wakabaki wamesimama pale. Tunda akilia huku
amejificha uso, akiwa amebeba mizigo yake, Net akihema.
“Twende
kwenye gari.” Net alimpokea mabegi yake, akayabeba kwa mkono
mmoja, kisha akamshika mkono Tunda kwa mkono wake mwingine, akamuongoza
lilipokuwepo gari yake. Wote wawili walikuwa wamelowa haswa. Akamfungulia
mlango wa gari, kiti cha mbele, Tunda akapanda na kujikunja kwenye kile kiti
huku akitetemeka baridi. Net aliwasha heater ili kuleta joto mle ndani ya gari.
Tunda aliendelea kulia mpaka alipopitiwa na usingizi. Hakujali anapopelekwa na
Net, akalala.
Net aliendesha mpaka hoteli
nyingine mbali kidogo na ile hoteli aliyokuwepo Gabriel na mkewe pamoja na mama
yake Net, akaingia yeye mwenyewe kwanza akachukua chumba ndipo alipoenda
kumuamsha Tunda. “Twende ukalale ndani.”
Net alimbebea vitu vyake akaongoza mpaka chumbani. Kilikuwa ni chumba chenye
kitanda kimoja tu, kochi na choo humo humo ndani.
Akamuwekea mizigo yake mle ndani
nayo ilikuwa inachuruzika maji. “Pumzika
nitakuona kesho.” Tunda alishindwa hata kumtizama Net usoni. Alibaki akilia
sana, huku amefunika uso wake. Net alibaki kimya huku bado amesimama pale
asijue aseme nini.
“Nenda
kabadili nguo utaanza kukohoa. Nitawaambia hapo mapokezi wakuletee chakula.
Utataka kula nini?” Tunda akatingisha kichwa kukataa bila hata
kumtizama. “Basi nitakuoana kesho. Usiku
mwema.” Net alisimama tena mlangoni kwa muda bila kusema kitu. Lakini ni
kama maneno mengine yaligoma kutoka, gafla akajikuta hajui aseme nini tena.
Akaona ni heri aondoke tu. Alipomuona Tunda anaelekea bafuni, akatoka na
kufunga mlango.
Kesho yake asubuhi aliletewa
kifungua kinywa na muhudumu wa ile hoteli, bila hata yakupiga simu kuagiza.
Mchana akaletewa tena chakula cha mchana. Lakini ilipofika jioni aliamua kupiga
simu mapokezi kuwaomba wasilete tena chakula kingine usiku.
Ilipofika saa mbili, akasikia
mlango ukigongwa. Alisimama kwenda kufungua. Alikuwa Net. Mwili mzima wa Tunda
ulikuwa ukitetemeka baada yakumuona Net. Alimpisha mlangoni, Net akaingia.
“Mbona
wameniambia umekataa chakula cha usiku?” “Bado nimebakiza kile cha mchana.
Sikula, nilikuwa bado nimeshiba” “Sasa sikitakuwa kimeharibika?” “Hapana. Bado
kizuri tu.” Net alikaa kwenye kochi nakujiegemeza. Tunda
akabaki amesimama pale pale mlangoni, Net akamgeukia. “Vipi! Mbona hukai?” Tunda alikwenda kukaa pembeni ya kitanda
akainama.
“Tumefungua
ofisi nyingine huku Arusha, nimekuwa huku kwa muda mrefu kidogo. Nipo kwenye
kutafuta watu wakunisaidia kazi. Kama unataka kazi, unaweza kupata.” Tunda
akatulia tu kama hakuwa akiongeleshwa yeye. Akabaki ameinama. “Tunda?” “Sijasoma Net. Sina kitu kichwani. Elimu niliyonayo ni kama ya darasa
la pili tu.” Net alitulia akimwangalia mrembo mwenye elimu ya darasa la
pili. Bado Tunda alikuwa ameinama nakushindwa kumwangalia kabisa Net.
“Kila
kitu ni kujifunza Tunda. Ukiwa na nia hakuna kinachoshindikana. Hata hivyo sio
kazi zote zinahitaji elimu.” “Nitaishi wapi huku Arusha?” “Sio lazima
ukaendelea kuishi huku. Nahitaji msaada kwa sasa mpaka nitakapopata watu wa
kudumu. Ukipenda kubaki sawa, ukitaka kuondoka baadaye pia siyo mbaya.”
“Asante.” “Huwa unafanya kazi siku za jumamosi?” “Sina kitu chakufanya kwa
sasa, naweza kufanya tu kazi.” “Basi nitakuja kukuchukua kesho twende wote
kazini.” “Asante Net. Asante sana.” “Karibu. Nitakuona kesho.” Net
akaondoka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
“Ninae
dada mmoja tu anayenisaidia. Naona kama analemewa kuwa peke yake. Jumatatu
utakutana naye, atakuelekeza baadhi ya mambo ya kufanya.” “Sidhani kama
nitaweza. Naona kama…..”
Tunda akasita. “Sijui Net! Sina uwezo
huo.” Net alibaki akimwangalia anavyojitetea kwa kubabaika. “Siwezi kukaa kwenye ofisi kama hii!
Nitakuwa nikifanya nini?” “Mbona unashindwa kitu ambacho hata hujajaribu Tunda?
Umeshajua kazi yenyewe? Au hutaki kuwa hapa? Kama hutaki upo huru kuondoka
Tunda. Sitaki niwe nakulazimisha.” Tunda alianza kulia.
“Sina pakwenda Net. Ila nahofia kuharibu.” “Usigope. Utafundishwa taratibu mpaka utaweza.
Kwani ulikuwa ukiishi wapi?” “Nilikodi nyumba. Lakini nimeshindwa kulipa kodi. Mwenye
kampuni ya Ulinzi amenitumia ujumbe jana usiku kuwa, mlinzi aliyekuwepo pale
nyumbani akinilindia vitu vyangu, amempigia simu usiku huo kumwambia mwenye
nyumba ameenda pale na kuanza kunitolea vitu vyangu nje.” “Pole sana. Unataka kwenda kuvichukua?” “Nitaviweka
wapi? Nipo kama nilivyo hivi.” “Hatuwezi
kukosa pakuviweka. Tunaweza kuondoka kesho siku ya jumapili na ndege ya asubuhi
nakurudi jioni.” Kwa kulia, Tunda hata hakusikia kauli sahihi ya ‘tuna’.
Yaani Net akijiunganisha. Akaendelea kulia.
“Sina hata nauli ya basi, nitaweza wapi ya ndege!?” “Kwanza umekubaliana na wazo langu?” “Wazo ni zuri, lakini utekelezaji wake ndio mgumu.
Nikifikiria pakuweka hivyo vitu ndio nachanganyikiwa kabisa. Sina ndugu wala
rafiki kwenye ule mji.” “Kwanza naomba unyamaze. Acha kulia. Halafu
nashauri twende wote kwanza tukaviangalie ndio tutajua pakuviweka.” “Asante Net.”
“Basi usilie. Tufanye kile
kinachowezekana sasa hivi kwanza. Hatua moja hadi nyingine. Sawa?” Hapo
Tunda akawa ameelewa kuwa na yeye atasaidia. “Sawa?” Tunda akatingisha kichwa kukubali. Net akaingia ofisini
kwake, akamwambia Tunda akae pale kwenye meza ya mapokezi amsubirie kidogo.
Walishinda siku nzima pale
kazini. Net akionekana ana kazi nyingi zakufanya. Alibaki ofisini kwake bila
kutoka. Tunda akahisi amemsahau. Akaangaza macho akijiuliza kitu chakufanya.
Maana muda ulizidi kwenda, yeye amekaa tu. Mwishoe akaamua kusafisha na kupanga
ile ofisi iliyokuwa imejaa vitu vizuri,
lakini hakuna mpangilio.
Akazunguka hapo ndani akakuta
jiko na choo. Akapata vifaa vya usafi. Akaanza kusafisha. Net bado alikuwa
ofisini kwake. Tunda hakujua kinachoendelea huko ndani. Ofisi yake ilikuwa
ndani na mlango umerudishiwa. Pako kimyaa. Tunda akaanza kusafisha na kupanga
ofisi nzima bila kusababisha kelele. Aliendelea kusafisha kwa haraka huku
akimsubiria bosi wake atoke ampe kazi.
Baada ya muda ndipo Net akatoka
nakubaki akishangaa. “Nimesafisha na
kupanga. Sijui ni sawa?” Tunda alimuwahi huku akimalizia kuweka mafaili
yaliyokuwa sakafuni, na kuyapanga kwenye kabati ambalo bado lilionekana jipya
tu, zuri sana lenye milango ya kioo mbele, lakini lilikuwa tupu kabisa. “Ona kulivyopendeza! Angalau panaeleweka
sasa hivi. Halafu unasema huwezi kufanya kitu chochote! Hapo si umefanya kitu
kizuri kabisa? Pamependeza sana. Mama akija kurudi tena atashangaa sana.”
Tunda alifurahi kuona amepongezwa.
“Nimewasiliana
na watu wa ndege, tumepata tiketi ya asubuhi sana. Utaweza kusafiri asubuhi
hiyo?” “Nitaweza. Asante.” “Twende basi tukale, uwahi kulala. Kesho nitakuja
kukuchukua mapema sana.” Net alimpeleka sehemu ambayo alidhani Tunda
hapafahamu kumbe vilikuwa ndio viwanja vyao yeye na Gabriel. Net alimwambia
waende wenyewe jikoni wakachague nyama.
“Mzee
yuko wapi?” Yule kijana alimuuliza akiwa ameonyesha
kumchangamkia kweli Tunda huku akiendelea kuchoma nyama. Tunda akaanza
kubabaika, Net alibaki kimya pembeni. “Au
leo uko peke yako?” “Sikuja naye.” Tunda akajibu kwa shida kidogo huku
akijikanyaga kanyaga.
Walirudi mezani Tunda alishindwa
kuongea kabisa. Wahudumu wote walimuulizia Gabriel, mwishowe Tunda akaamua
kuondoka pale. “Naomba nikakusubirie
kwenye gari, Net.” “Basi ngoja niwaambie watuletee chakula hukohuko kwenye
gari, tutaenda kula hotelini.” Tunda alijisikia vibaya sana. Akatoka pale
bila hata kusubiria zaidi.
Walirudi hotelini Tunda akiwa
kimya kabisa na Net hakutaka kuuliza. Net aliwasha tv mara tu alipoingia
chumbani kwa Tunda na kujitupa kwenye kochi. Alikula chakula chake huku
akiangalia tv. Alibadilisha tv huku na kule ili kupata taarifa ya habari wakati
akiendelea kula. Alipomaliza kula na kuangalia taarifa ya habari, akataka
kuondoka. Tunda na yeye alikuwa ameshamaliza kula.
“Nitarudi
kesho asubuhi na mapema, Tunda. Usichelewe kulala.” “Lakini Net.” Tunda
alimuwahi Net akiwa anataka kutoka, akiwa amesimama, na yeye akasimama huku
akibabaika sana. Alimuogopa sana Net, hata hakuwa akiweza kumwangalia vizuri.
Net alibaki akimwangalia vile anavyotetemeka mbele yake. “Kuna nini?” Net akamuuliza taratibu. “Au usiku mwema.” Tunda alishindwa kuongea kwa hofu, akaamua
kumuaga tu.
Net akarudi kukaa. Taratibu
machozi yalianza kumtoka tena Tunda. “Vipi
Tunda?” “Naona
tuache tu.” “Nini?” Net akauliza. “Hiyo safari ya Dar. Nitakuja kwenda wakati mwingine.”
“Kwa nini? Unajua nimeshakata tiketi?”
“Samahani,
lakini nadaiwa. Siwezi kurudi mikono mitupu, bila pesa za watu.” Net
akatulia kidogo.
“Nani
anakudai?” Net akauliza. Tunda akajifuta machozi na kujaribu kutulia. “Kodi ya miezi 3, kampuni ya ulinzi na
kijana niliyemwajiri wa kazi.” “Kwa
hiyo unataka kukimbia deni?” Net akamuuliza taratibu tu. “Sijui
chakufanya Net. Sielewi nitafanya nini. Kwa mfano yule kijana wa kazi alikuwa
akinipigia simu siku nzima ya leo akitaka nimpe pesa yake. Ndio jioni hii
nimemtumia ujumbe, wakumtaarifu kuwa bado sijapata pesa, ila anaweza kwenda
kuchukua kitu chochote kwenye vitu vyangu kama kujilipa. Hajanijibu. Haya, yule
mmiliki wa kampuni ya ulinzi alinipigia simu siku ya jana akinitishia
kunipeleka polisi kama sitampa pesa yake. Ameniambia jumatatu ndio mwisho.
Nataka na yeye nimuombe kama anaweza kuchukua baadhi ya vitu vyangu, akae navyo
mpaka nitakapo mlipa. Ila kodi ndio inanichanganya zaidi, sijui nitafanyaje!”
“Usiwe
na wasiwasi, wewe twende tu. Watumie ujumbe sasa hivi, waambie ukutane nao wote hapo nyumbani kwako, siku ya kesho
asubuhi ya saa nne. Na uwaambie wasichelewe, kwa kuwa tunarudi kesho hiyo hiyo
huku Arusha. Hatutakuwa na muda wa kumsubiri mtu.” Tunda alifuta machozi
kwa mikono yake, akafuata simu yake, akatuma ujumbe kwa wote kama alivyoambiwa
na Net.
“Nimeshawatumia.” “Naomba uniambie kila mmoja anakudai kiasi gani.
Nitawalipa kwa hundi. Unafikiri ni sawa? Maana sina pesa hapa mfukoni.”
“Hawatakuwa na shida. Wanachotaka ni kulipwa.” Tunda akajibu na kumtajia
kwa woga sana kiwango anachodaiwa na kila mmoja wao. “Lakini Net, naweza kuwaomba niwalipe
kidogo kidogo. Sio lazima kuwalipa zote kwa pamoja.” Net akasimama. “Usiwe na wasiwasi. Wewe lala. Nitakufuata
kesho.” “Asante sana Net. Nakushukuru.” “Karibu.
Usiku mwema.” “Na wewe.” Net akatoka.
Alipofunga mlango tu, Tunda akaanza kulia kwa uchungu sana. Net alibaki nje ya mlango akimsikiliza jinsi anavyolia kwa kuugua. Alitamani arudi ndani, lakini aliona aache tu. Tunda aliendelea kulia kwa muda mrefu sana huku akigugumia kama mtu asimsikie. Alifika mwisho kabisa. Kama ni kuzama kisimani, basi alishazama na kunywa maji mengi sana, akabaki akielea kama mzoga.
Aibu ilikuwa imemuandama, hofu
ndiyo ilizidi kumtesa. Net ndiye mtu wa mwisho kabisa kwenye Maisha yake
angetamani kuwa naye karibu, kwa vile anavyomfahamu kwa uchafu wake. Alijua Net
anamjua jinsi alivyo mchafu, yeye mwenyewe alijionea kinyaa. Net je? Alijiuliza
huku akitamani asiwe Net anayemsaidia. Lakini hakuwa na namna nyingine.
Alibanwa vyakutosha. Net aliposikia kimya, akajua amepitiwa na usingizi, ndipo
alipoondoka.
Net arudi Dar akiwa na Tunda, Kumlipia madeni.
|
Net alifika hotelini hapo asubuhi
hiyo na mapema akamkuta Tunda alishajiandaa, anamsubiria akiwa mnyonge na macho
mekundu. Alionekana aliamka na kuanza kulia tena. Net aliogopa kuuliza asije
akaanzisha kilio kingine na kushindwa kuwahi ndege. Waliondoka mpaka uwanja wa
ndege, akaacha gari lake uwanjani hapo, wakaenda kupanda ndege kuelekea Dar.
Tunda alipofika tu kwenye ndege, alilala mpaka Net alipomuamsha kuwa wamefika.
Alikuwa amechoka, zaidi akili.
Ndege ilitua jijini Dar, Net
akamkuta Wanja, mtu anayemtumia kwa maswala ya usafiri hapo Dar. Alikuwa
akimiliki magari makubwa na madogo anayofanyia biashara. Ndiye aliyemuomba
afike hapo awasaidie usafiri wa kuwapeleka kwa Tunda akijua hata huko atakuwa msaada
wakupata usafiri mwingine. “Nakushukuru
sana Mkuu, na samahani kwa kukusumbua najua leo jumapili ni siku ya familia.”
“Hamna shida kabisa. Nilipomwambia tu wife kuwa ni wewe, akaniambia nikimbie
haraka sana.” Wote wakacheka. Tunda
alikuwa ameingia chooni mara tu walipotoka kwenye ndege. Kwa hiyo Net alikuwa
na mwenyeji wake tu wamesimama wakiongea wakati wakimsubiria Tunda.
Alitoka chooni, na kuwasogelea
pale walipokuwa wamesimama. Jicho kwa jicho na mteja wake huyo Wanja. “Judy!” Tunda aliinama. Net akabaki
akiwatizama, kama aliyeshtuka. Hakutegemea hata Wanja! Alionekana mtu wa
familia na mwadilifu. Wanja akajaribu kupotezea, lakini asijue Net anaelewa
kila kitu. “Nafahamiana na huyu dada
alinisaidia lifti kipindi gari langu lilipoharibika. Hata jina lake simfahamu
vizuri.” Akajichanganya. Gafla akasahau kuwa alitoka kumwita Tunda, jina la
Judy na wala Tunda hakuwahi kumiliki gari. Akajitetea kwa kubabaika sana
huku akiongopa. “Ooh! Kumbe hamna haja ya
utambulisho? Basi twendeni.” Net akajibu na kuwaacha wakitizamana nyuma
yake. Kisha wakamfuata.
Tunda alipanda garini akabaki
ameinama bila hata kuongea. Tunakutegemea wewe Tunda ili utuambie ni wapi
unaishi na utuongoze njia. Nataka tuone vitu vyenyewe kwanza ndipo nijue ni
aina gani ya gari itahitajika
kuvibeba.” Tunda akanyanyua uso. Hakuwahi kutaja jina la mtaa anaoishi hata
mara moja. Ni kama alilifuta hilo jina kichwani mwake kwa makusudi ili asije
wahi hata kuropoka kwa mtu. Akabakia kujua njia tu.
“Nielekee
wapi?” Wanja ambaye ni dereva akauliza wakati anatoa gari pale uwanja wa ndege.
“La Dolce Vita.” Tunda akajibu taratibu. Mpaka Net akamgeukia. “Unamaanisha
unaishi mitaa ya karibu ya ile hoteli ya La Dolce Vita ya Oyster bay!?” Net
akauliza kwa mshangao. “Ndiyo. Twendeni mpaka kule baharini kabisa. Nyumba
haipo mbali na ilipo hoteli.” Tunda alijibu kwa upole, Net akaelewa ni kwa nini
anadaiwa kodi kubwa vile. Dereva akakanyaga mafuta, Tunda akarudisha uso wake kuangalia
chini .
Dereva alipofika mpaka baharini akataka kuelekea
Coco Beach, Tunda akamwambia akate kona kulia. Akamuelekeza mpaka kwenye nyumba
aliyokuwa akiishi.
“Hapa ndio kwako Tunda!?” Net akauliza kwa
mshangao. “Ndiyo.” Nyumba ndogo lakini nzuri sana. Ilikuwa ya kisasa. Kuanzia
getini mpaka ndani, ungependa. AC ilikuwa nyumba nzima. Pasafi. Kuja kuona
hivyo vitu vyenyewe vya Tunda, ambavyo baadhi vilishaanza kutolewa nje, Net
akamwangalia Tunda.
Vilikuwa vitu vizuri, vilivyotangaza utajiri mtupu
kwa kuviangalia tu kwa macho. Marembo ya dhahabu nzuri iliyokatwa kwa ustadi
yalizungushiwa kwenye kila kifaa cha Tunda. Kitanda, meza zake, makabati, vioo
vyakujiangalia, meza yakujitengenezea na viti vyake, kila kitu kilikuwa na
marembo mazuri sana na manyoya mazito meupe.
“Ulipata
wapi haya makochi, meza…!? Kila kitu!” Wanja aliuliza kwa kushangaa sana.
“Nilienda kununua Arabuni.” Tunda alijibu kiunyonge bila ujasiri.
“Daah!
Ni vizuri sana. Sijawahi on ahata kwenye picha! Na vinaonekana ni vya thamani
sana. Kwa ile lori yangu, Mkuu, itabidi kubeba hata mara tatu. Hivi vyombo ni
vingi sana na vyote vinaonekana ni vya thamani sana. Tukivibebanisha,
tutaharibu.” Net alibaki kimya akiwaza huku akiangalia vile vitu vyote,
akifikiria pakuviweka. “Unapakuviweka lakini?”
Wanja akamuuliza Net. “Maadamu tupo hapa, lazima tutatafutia ufumbuzi. Hatutashindwa.
” Net akajibu na kuendelea. “Ili kuokoa muda, naomba ukatutafutie usafiri
unaweza kubeba hivi vitu.” Wanja akaondoka na kuwaacha Tunda na Net.
Baada
ya muda kidogo, akaingia mwenye nyumba na mwenye kampuni ya ulinzi. Ni kama
waliongozana. Tunda akasalimia. “Ulituambia tuje leo.” Mwenye nyumba akavunja
ukimya. Net akawasogelea. “Nashukuru kwa kuwa hapa. Niombe kama mtaridhia,
mpokee hundi.” “Bila shida. Ilimradi tumalizane kwa amani.” Mwenye kampuni ya
ulinzi akajibu.
Net
alikuwa ameshawaandikia hundi zao kutokea Arusha. Alichofanya ni kumkabidhi
Tunda anayewafahamu, ili awakabidhi bila kuchanganya. Tunda akazipokea huku
akitetemeka. Hata mikono yake ilikuwa ikionyesha jinsi anavyo tetemeka. Akasoma
kiasi kwenye kila hundi, akawakabidhi kila mmoja wao.
Net
hakuwa ameandika majina yao, ila pembeni ya sahihi aliandika sababu. Ya kwanza,
‘Kodi ya Tunda.’ Hundi ya pili, ‘Ulinzi wa Tunda.’ Hundi ya tatu, ‘Mfanyakazi.’ Tunda mwenyewe akashangaa vile
alivyoandika. Alimtajia tu walipokuwa hotelini, aliondoka pale Tunda akiwa hana
uhakika kama atakumbuka. Lakini alikumbuka na akaandika kiasi kwa usahihi.
Aliwakabidhi
hao wawili. Wakashukuru. Wakamsikia
mwenye nyumba akimwambia mwenye kampuni ya ulinzi angependa waendelee kulinda
hapo mpaka mpangaji mpya atakapohamia hapo week inayokuja. Wakakubaliana,
wakaondoka. “Nashukuru Net.” Net akamgeukia
Tunda, akamuona anafuta machozi. “Karibu.” Net akajibu.
Baada
ya muda wakati Tunda akikusanya vitu vyake vizuri, Net akifungua vitu kama
kitanda, nakumsaidia Tunda kuweka vitu vyake pamoja na kirahisi ili viweze
kuhamishika, kijana wake Tunda, wa usafi na yeye akafika hapo akiwa na usafiri
wa baiskeli akiwa na maboksi mengii. Tunda akamtambulisha kwa Net. “Wewe naomba
tumalizane ukishatusaidia kuhamisha hivi vitu hapa. Nitakulipa. Ni sawa, au
kuna mahali unataka kuwahi?” Net akamuuliza. “Hamna shida Mkuu.” Akakubali kwa
haraka bila shida.
Walifanya
kazi kubwa. Mpaka lori linafika hapo, walikuwa wameshakusanya karibu kila kitu.
Net alimwambia Tunda yeye asibebe vitu vizito. Wao watasaidiana kubeba. Kazi
yakupandisha ikaanza, huku Tunda akipandisha nguo zake na viatu. Alikuwa
ameweka kwenye masanduku na maboksi aliyoletewa na yule kijana wake wa usafi.
Alimuagizia usiku uliopita. Alimwambia afike hapo kuchukua pesa zake, aje na
maboksi makubwa na magumu. Na kweli yule kijana alifanya hivyo. Yakamsaidia
sana Tunda.
Net
na yule rafiki yake, Wanja pamoja na kijana wa Tunda na dereva wa lile lori
walisaidiana kupandisha vitu vyote kwa tahadhari. Net akihakikisha hakiharibiki
kitu hata kimoja. Akasimamia upangwaji wake, vitu vingine vikawekwa kwenye hiyo
gari kubwa iliyokuwa imekuja kuwapokea uwanja wa ndege. Hasa viatu na nguo za
Tunda. Walipohakikisha kila kitu kipo ndani ya magari, ndipo Net akamwambia
rafiki yake apande kwenye lori, yeye ataendesha gari lake na Tunda. Wawafuate
nyuma. Tunda akamuona akizungumza nao yeye akiwa anasubiri ndani ya hiyo gari
ya Wanja, akamuona Net anarudi. “Tuondoke sasa.” Akawasha gari na kuondoka, Tunda
hata hakuwa akijua wanaelekea wapi. Akaamua kunyamaza tu.
Akaona
Net akiongoza njia mpaka Salasala. Tunda alikuwa ametulia kimya akimtizama na
kumtafakari bila jibu. Kijana mtulivu. Alionekana kila kitu anakipigia mahesabu
na kukifanya kwa makini sana kama asiyetaka kufanya kosa. Yupo makini, na kila
walipopita na Tunda, alikuwa ameshaandaa mazingira. Kuanzia wanatoka Arusha,
mpaka hapo walipo wanahamisha vitu vyake. Watu waliokutana nao pia aliwaandaa
siku moja kabla. Anakwenda kwa muda na mpangilio. “Huyu kweli mzungu.” Alijisemea Tunda.
Waliendesha
kimya kimya. Hakuna aliyemuongelesha mwenzake. Kutoka hapo Oysterbay mpaka
Salasala. Tunda alikuwa amejiegemeza kimya, haamini kama Net anamtua mzigo
mkubwa vile! Akaona wamefika. Net alipiga honi mara moja tu, geti
likafunguliwa. “Hapa ni wapi?” Ikabidi Tunda aulize sasa. “Ni kwangu, lakini
siishi hapa kwa sasa. Naishi na mama na mdogo wangu akiwa likizo. Kwa hiyo
vinaweza kukaa tu hapa.” Tunda akajiweka sawa pale kitini ili kuangalia.
Na
yenyewe ilikuwa nyumba nzuri sana. Ilijengwa peke yake ndani ndani kidogo
kwenye huo mtaa wa Salasala. Juu ya mlima. Ukisimama kwa nyuma, unaona bahari
kwa kwa mbali na nyumba nyingine. Madhari yake na ramani, Tunda akabaki
akishangaa. Ni kama kulipitishwa gari kubwa la greda ili kuchonga sehemu fulani
fulani za bustanini. Kulizungushwa rembo za namna yake. Mbele ya hiyo nyumba
kulikuwa na sanamu ya kipekee, inayotoa maji mdomoni, yaliyotengeneza bwawa la
rangi ya bluu, humzunguka huyo sanamu. Na lile bwawa lilijengewa kisanifu.
Tunda akabaki anakodoa macho.
Net
akavuta gari mpaka pembeni ili kupisha lori iliyokuwa imebeba vitu vya Tunda.
Akawaonyeshea ishara wapite kama wazunguke nyuma kidogo. “Twende tukawaelekeze,
halafu ndipo tutakuja kuchukua vitu vya humu ndani ya hili gari.” Net akashuka,
Tunda naye akafuata. Net akamuelekeza dereva wa lori mpaka kwenye kinyumba cha
nyuma. Tunda na yeye anafuata nyuma. Kumbe ilikuwa stoo. Walipoingia, palikuwa
pakubwa. Humo ndani ni pasafi na kumepangiliwa pia.
Akaingia
kijana aliyemsalimia kwa heshima sana Net. Tunda akajua ni mfanyakazi wake.
“Vipi Max?” Akamsikia akimuulizia yule kijana. “Nimetoka kumuogesha sasa hivi
na kumpulizia dawa. Yupo sawa.” “Chakula chake bado kipo?” Net aliendelea
kuuliza. “Bado kipo kingi tu. Week hii ndio ya chanjo. Nakumbuka. Nitampeleka.”
Akajibu yule kijana. “Sawa sawa.” Net akajibu na kumgeukia Tunda.
“Huyu
anaitwa Emma. Ndiye anayeishi hapa.” Akamtambulisha kwa Tunda. “Emma, huyu ni
Tunda, ndiye mwenye hivi vitu vyote.” Wakasalimiana, Tunda akawa anajiuliza
sasa Max ni nani!? Ila kama kawaida yake, akajua hayamuhusu. “Karibu dada.”
Akampa mkono Tunda. “Asante.” Tunda akashukuru na kumgeukia Net. Macho
yakagongana. “Asante Net.” “Karibu. Njaa inauma sana?” “Hapana. Sijisikii kula
kabisa.” Tunda akaanza kutokwa na machozi. Dereva na rafiki wa Net wakaingia na
wao.
Net
akamshika mkono Tunda na kumsogeza pembeni mpaka sehemu iliyokuwepo makochi.
“Naomba utulie. Tumeshapata hii sehemu. Tunaweza kuhifadhi hivi vitu kwa muda
wote mpaka utakapokuwa tayari kuvichukua. Kaa hapa kwenye makochi, ni pasafi
tu. Nisubiri tusaidiane kushusha vitu, tuondoke. Unataka soda?” “Hapana.” Tunda akakataa. “Basi nitamtuma Emma
akuletee maji ya kunywa.” “Asante.” Ndilo
neno ambalo Tunda lilikuwa likimtoka kila mara. “Naomba utulie. Naamini kila
kitu kitakuwa sawa. Sawa?” Tunda akajifuta machozi, na kuvuta pumzi. “Nakushukuru Net.” “Karibu. Basi ngoja tuanze
kazi.” Akamuacha amekaa hapo, akawasogelea wengine.
Akamuona
anawaonyesha sehemu ya kuviweka vile vitu vya Tunda. Ukweli palikuwa pakubwa na
pazuri. Ilikuwa ni bohari ndio, lakini sakafu yake ilionekana nzuri sana.
Upande yaliopo hayo makochi, kulikuwa na kinanda cha kawaida tu. Tv kubwa
imening’inizwa na meza yakuchezea tenesi. Kuliwekwa kapeti chini. Zuri sana.
Upande
kulikuwa na vifaa vilivyofunikwa na mashuka makubwa. Tunda hakujua ni nini
kilichofunikwa humo ndani ya hayo mashuka. Ila nakwenyewe kulikuwa kusafi. Kona
ingine kulikuwa na chumba alichohisi ni choo. Ndio upande mwingine ulikuwa wazi
kabisa. Ndipo alipoona akielekeza watu waweke vitu vya vyake.
Alimuona Net akivipangilia vizuri.
Walisaidiana wote wanne. Net, Emma, rafiki wa Net, Wanja, ambaye alishakuwa
mteja wa Tunda na dereva wa lile lori. Walifanya kwa haraka mpaka wakamaliza.
Net akamlipa yule kijana wa lori, akatoa lori yake pale.
Net
alilisogeza ile gari ndogo karibu kabisa na mlango. Tunda alipomuona anashusha,
akamsogelea. “Usibebe vitu vizito. Emma atatusaidia.” Net na Emma wakashusha
mpaka wakamaliza. Vitu vyote vya Tunda viliweza kutoshea kwenye huo upande tena
bila kubebanisha. Tunda alibaki na maswali lakini aliogopa kuuliza zaidi kwani
alijua Net ndiye ana maswali mengi zaidi yake. “Asante sana Net. Nakushukuru.”
“Karibu.” Akabaki amesimama kama anataka kuuliza swali, Net akaelewa. Akaomba
Emma na rafiki yake wasubiri nje.
Wakabaki
wao wawili. Akamgeukia Tunda. “Sijui nibebe nini kwa kuwa sijui nitakuwa kule
kwa muda gani!” Tunda akaonge kinyenyekevu. “Inategemea na wewe. Unataka kuwepo
Arusha?” “Sina uchaguzi Net. Kama unafikiri naweza
kufundishika, nikaelewa, nitashukuru.” “Naamini utaweza tu. Ondoa hofu.”
Tunda akajifuta machozi tena. “Basi naomba muda
mfupi wa kuchukua baadhi ya nguo na vitu nitakavyovihitaji.” “Sawa.” Net
akatoka nje kama kumpa nafasi.
Tunda
alichukua begi kubwa. Akaanza kufungasha. Kila kitu alitamani kubeba. Kila kitu
aliona kina umuhimu. Akaanza kulia kuacha vitu vyake. Alilia Tunda, asiamini
kuwa ndio ni kama anaanza tena maisha. Alipenda kwake. Alifurahia kila kitu
chake kwani alinunua si kwa bahati mbaya. Kila kitu alinunua kwa kusudi. Leo
anaviacha stoo! Mpaka lini! Hilo ndilo lilimuogopesha Tunda.
Net
akarudi. “Nikusaidie nini?” Akasimama kwa haraka kama aliyefumaniwa tena.
“Unaweza kuchukua mabegi hata mawili au matatu. Beba vile utakavyo. Tutalipia
kwenye ndege.” Net akaongeza. “Asante.”
Tunda akainama kuendelea kufungasha mpaka akamaliza na kujifuta machozi vizuri.
“Naona hivi vitatosha. Asante.” “Basi acha nikusaidie kubeba. Wewe beba huo
mkoba mdogo. Tuondoke sasa hivi, tuwahi.” Net akachukua yale mabegi wakaondoka.
Tunda Arudi Arusha Kuanza Maisha Mengine Akiwa na Net.
|
Walirudishwa uwanja wa ndege, na
Wanja tayari kwa safari ya kurudi jijini Arusha. Wakiwa kwenye ndege Tunda
akiwa amekaa dirishani, Net alimuona akivuta pumzi mara kadhaa na kuzishusha
huku akifuta machozi. Baadaye alimuona akijivuta karibu naye, akajiegemeza
pembeni yake, akalala. Net alimuhurumia sana Tunda. Alionekana amechoka, zaidi
mawazo. Akabaki akimtizama akiwa usingizini, akamfunika vizuri na mtandio wake,
akabaki akimtizama huku akimtafakari.
Walifika
Arusha, Net akachukua gari yake sehemu alipokuwa ameegesha asubuhi, akamrudisha
hotelini kwake. Wakaingia ndani, kama kawaida yake, alikaa kwenye kochi, kwa
mara ya kwanza Tunda akakaa pembeni yake, kama anayetaka kuzungumza kitu lakini
anasita. Net aliligundua hilo kwa hiyo hakutaka kuaga kwa haraka, akataka
kumsikiliza. Akaamua kuagiza chakula kiwafuate palepale chumbani.
Baada ya
muda kikaletwa. Net akiwa anaangalia luninga kama kawaida yake, huku
amejiegemeza kwenye kochi, akimsubiri aongee. Kimya. Alimuona vile
anavyotetemeka mpaka mikono iliyokuwa imeshikilia ile sahani ya chakula.
Mwishoe akamuona amekiweka mapajani, napo sahani ikawa inacheza. Kwamba
anatetemeka mpaka miguu. Net akaendelea kula na kubadili channels kama kumtoa
kwenye mawazo.
Walimaliza
kula bado Tunda alishindwa kuongea. Net naye akawa kama hana haraka. Akaendelea
kuangalia tu luninga. Akibadili hiki na kile. “Huwa unapenda kuangalia nini
kwenye tv?” Akamuuliza Tunda. Tunda akaanza kufikiria. Hakuwa hata akiangalia
tv. Ilikuwepo kwake kama haipo. “Sio mpenzi sana wa tv.” Akajibu taratibu. Net
akamwangalia. “Lakini huwa nawasha na kuangalia chochote kilichomo.” Akaendelea
Tunda kama anayejitetea.
“Na
movie?” Akamuuliza tena. “Napenda ila isiwe za vita au watu wasipigane.” Net
akacheka. Nia yake ilikuwa kumtuliza tu ili aongee. Wakatulia kidogo. “Net!”
“Vipi?” “Asante.” Net akatabasamu. Maana alishapokea hizo asante, kama
nikuziweka kwenye gunia, zingekuwa zikifurika. “Asante kwa kila kitu.
Namaanisha kila kitu. Angalau sasa hivi naweza kulala vizuri. Sidaiwi tena.
Hiyo kodi ilikuwa inanifanya sipati usingizi. Nilijiingiza kwenye gharama
ambazo sikuwa najua nitajitoaje.” “Pole.” Tunda akatulia kidogo.
Kisha
akaendelea. “Sitaki kurudia yale maisha tena Net. Hapa hotelini ni gharama sana
na kwa kuwa nitakuwa hapa Arusha kwa muda, labda nitafute chumba cha kupanga
kwa muda.” “Wazo zuri. Lakini naomba tufikirie kazi kwanza. Tuna mambo mengi
sana pale ofisini, hizi gharama za hapa hotelini unapoishi, ofisi italipa.” “Je
nikishindwa hiyo kazi Net? Huoni mtakuwa mmepoteza pesa bure? Kwa nini usione
kwanza utendaji kazi wangu, ukiridhika ndipo angalau utajua hata kama mnanilipa
kiasi gani?” “Acha wasiwasi Tunda! Kila kitu kitakuwa sawa.” Akajibu hivyo tu,
tena kirahisi tu. Akakaa tena kidogo, akamuaga kwa makubaliano yakumfuata hapo
kesho yake kwenda kazini.
Ilipofika saa mbili kamili, Net
alikuwa akigonga mlangoni. Hakuingia hata ndani. “Kama upo tayari, twende.” Tunda akachukua pochi yake kwa haraka na
kutoka. Walifika kazini siku hiyo ya jumatatu asubuhi, Net akapokea simu kutoka
kwa dada aliyekuwa amemuajiri pale ofisini na kumwambia anauguliwa na mumewe
hataweza kufika kazini mpaka atakapopona. Tunda aliingiwa na hofu sana. “Usiogope,
nitakuelekeza utaelewa tu. Hata yeye mwenyewe mimi ndiye niliyemfundisha.
Halafu mimi mwenyewe nitakuwepo, nitakusaidia.” Tunda akakubali lakini bado
alikuwa na hofu sana.
Na hivi
Net alionekana makini, hakurupuki! Ni kama hana mlango wa makosa kwenye maisha
yake, wasiwasi ulizidi kumwingia Tunda. Hata wateja aliokuwa akiwahudumia kwa
ngono, wote waliokuwa wakikutana na Net, au aliofumaniwa nao na Net, walianza
kutoa sifa za Net hata kabla hawajakutana naye. Hata Tunda alipokuwa akiwaambia
wamwambie Net wakutane club au baa, walikuwa wakisita na wengine kukataa
kabisa. Kwamba yupo makini, anakwenda na muda, muadilifu, hataki hata kugusa
pombe na kadhalika. Sasa leo umkutanishe na Tunda aliyekwisha kumfumania mara
kadhaa, na kila wanayekutana naye, ameshamuhudumia!
Hofu
iliyokuwa imemjaa Tunda, alitamani yeye ndio akakae na huyo mgonjwa, muhusika
arudi pale kazini. Lakini akajikumbusha hayupo kwenye kuchagua. Amewekwa
hotelini ili afanye kazi. Vitu vyake vipo kwenye stoo ya Net, juhudi zake ndio
zitakazomfanya avirudishe chini ya himaya yake. Hana pakwenda, hapo alipo ndipo
mwisho. Lazima atulize akili, aelewe.
Tunda
akatulia kuelewa kwa makini. Na Net naye alimuelekeza taratibu bila haraka,
kuhakikisha hapaniki na anaelewa ni nini wanafanya bila shida. Ilikuwa ni
Kampuni mpya ya usafirishaji. Walihusika na watalii pamoja na kusafirisha
bidhaa ndani na nje ya nchi. Net alimwambia ndio wanaanza tu. Kwa upande
wawatalii wao walikuwa ni wakala tu. Wanafanya kazi na mahoteli mengi makubwa
ya hapo nchini, walioingia nao ubia.
Wakipokea
wao wateja, watatumia usafiri wao kina Net. Lakini watalala kwenye hoteli zao.
Kisha hoteli kuwalipa wao asilimia fulani kwa kuwaletea watalii au wateja. Iwe
mbugani au mijini na vijijini. Kina Net wao ndio walitumika kama wasafirishaji.
Unahama kutoka sehemu moja kwenda nyingine, basi wanakuwa na malori makubwa na
madogo, inategemea na ukubwa wa nyumba au ofisi unayotaka kuhamisha. Unayo
bidhaa kubwa au ndogo, unataka usafirishe ndani ya nchi au nje, wao kina Net,
watakusafirishia.
Kampuni
yao ilikuwa ikiitwa African Cote transit. Jina
la Net alikuja kugundua kuwa ni Nathaniel Cote. Kwa hiyo akahisi labda ile
kampuni ni yake. Ila kama kawaida ya Tunda, haulizi kisichomuhusu, ila kufuata
yake. Akaweka akili na kuendelea kumsikiliza Net. Kazi yake ikawa kupokea kazi
zote kutoka kwa wateja. Kujua aina ya mzigo au watalii. Anaandika kwenye
kompyuta kutokana na aina. Kwa urahisi tu, kompyuta yenyewe inamletea aina ya
magari ambayo yapo.
Kama ni
wateja wa kuzungushwa mjini, basi itampasa kumsomea mteja aina ya magari ambayo yapo kwa wakati huo. Kama ni
mbugani hivyohivyo. Kama mtu anayehama kutoka sehemu moja kwenda nyingine,
Tunda alifundishwa aina ya maswali ya kuuliza. Ukumbwa wa vifaa vya hiyo nyumba
anayohamisha. Umbali, na kadhalika.
Kama ni
bidhaa, alimfundisha maswali yakuuliza pia. Ukubwa wa hiyo bidhaa, aina yake, umbali
wakupelekwa na kadhalika. Kwa hiyo kazi kubwa ilikuwa ni kuelewa vizuri wateja,
kuandika na kutoa lugha nzuri kwa kila mteja.
Hilo kwa
Tunda likawa halina shida. Kwanza hana tatizo kubwa la lugha. Angalau lugha
mbili muhimu alikuwa akizifahamu bila shida. Kingereza na Kiswahili. Pili,
Tunda alijaliwa ulimi laini. Mtulivu na anayo lugha ya ushawishi. Akizungumza
na wewe hata ukitaka kugairi, atakupanga mpaka ukubali.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kazi
ikaanza. Tunda na Net wakisaidiana bega kwa bega. Kwa kuwa ilikuwa siku ya
kwanza, Net alikuwepo kumsaidia. Walikuwa naye hapo mezani wakifanya pamoja.
Alimsikia Net jinsi anavozungumza na wateja. Maswali gani anayajibu. Akawa
anaandika yale maswali aliyoona wateja wengi wanauliza.
Tunda
alijua ni kweli wanatengeneza pesa. Walikuwa busy kupita kiasi mpaka ile hali
ya hofu kwa Net ikaanza kupungua kwa kuwa walikuwa wamekaa naye hapo mezani
siku nzima. Wakizungumza wao wawili, wateja na Tunda ilimlazimu kuuliza maswali
ili akija kuachiwa pale, asiharibu.
Hakuna
aliyekumbuka kula. Mpaka inafika jioni ya saa kumi na mbili, ndio pakatulia.
Simu zikaacha kupigwa. “Mambo yatabadilika Tunda. Utakuja kupata muda
wakupumzika. Mwanzo mgumu.” “Hamna shida kabisa. Nimefurahi kuweza kuwa busy
hivi. Imenisaidia sana.” Net akacheka kidogo.
“Hujuti
kukubali?” “Hata kidogo. Angalau akili yangu imetulia kwa muda nakuacha
kujifikiria. Lakini najua wewe njaa itakuwa ikikuuma.” “Na wewe?” “Mimi sio
mlaji sana. Umeona kile kichupa nilichokunywa mchana?” Net akakumbuka kumuona
akinywa kitu. “Ni meal replacement. Inachukua nafasi ya mlo mmoja. Imebeba
virutubisho vingi tu. Kwa hiyo wakati mwingine ni kinywa ile, nikapata na
matunda, inakuwa inanitosha.” Net akatabasamu. Maana kwa kumwangalia tu, utajua
huo mwili unatunzwa vizuri.
“Mbona
na mimi hukunipa sasa?” Tunda akababaika kidogo. Akataka kujitetea, Net
akimtizama. “Unisamehe tu. Sikujua kama ungependa. Nimebakiza vingine hotelini.
Nilikuja navyo kutoka Dar. Naweza kwenda kukupa.” “Nashukuru. Ila sasa hivi
njaa inaniuma sana. Nataka kula chakula chakueleweka. Twende tukale chakula
kabisa.” Wakaanza kufunga kazi kwa siku ile, na kutoka pale.
Walirudi
hotelini na kuagiza chakula. Kililetwa chumbani. Wakaanza kula. “Nikuulize
Net?” “Uliza tu.” Net akajibu huku wakila. “Nimeona ofisi ndio mpya. Lakini
mnao wateja wengi. Mnafanyaje?” Net akameza chakula kilichokuwepo mdomoni ili
aweze kuzungumza.
“Chakwanza, kujitangaza.
Nimejitahidi kutangaza na nimehakikisha watu wengi wametusikia na kufahamu
huduma yetu. Nilitangaza kwenye maredio, televisheni, na kugawa vipeperushi kwa
wingi. Mjini, mitaani na maofisini. Ukiangalia hapa nchini, wengi wanatumia
kupanga. Kama sio nyumba anayoishi, basi ofisi. Sasa ili kuwapata hao watu,
basi, nimeweka uwanja mkubwa kwa watumiaji wote. Wenye pesa na wasio na pesa
nyingi wanaweza kutumia huduma zetu. Ndio maana utakuta kuna aina tofauti
tofauti za magari. Hiyo inategemeana na uwezo wa mtu. Sijui nimejibu?” Net
akauliza.
“Hapo
nimeelewa.” “Lakini umeonaje? Si ni kazi inayowezekana?” “Nafikiri. Si bado
tutakuwa wote ili kuhakikisha siharibu?” Net akacheka. “Tunda wewe ni muoga
sana. Acha kufikiria kuharibu kwanza. Naomba ufikirie ni jinsi gani utaboresha.
Ni vipi pale patanufaika kwa Tunda tu kuwepo pale. Tunda huyohuyo unayemfahamu
wewe, mfikirie ni kwa jinsi gani pale pamebahatika kupata uwepo wako.
Ukifikiria kwa namna hiyo, utaona mambo yatakavyokuwa rahisi.” Tunda akatoa
tabasamu kama anayefikiria.
“Niamini
Tunda, kila mtu anahaiba yake na kitu kinachomfanya awe yeye. Wewe unajijua.
Sasa jifikirie hivyo ulivyo unawezaje kupanufaisha pale! Jiweke kwenye nafasi
ya kama ile kampuni ndiyo imebahatika kumpata Tunda. Jiambie kwanza hivyo.
Hivyo tu. Weka mbali maswala yakukaa darasani na elimu. Wewe tu kama ulivyo.
Jiambie kampuni ya Cote, imebahatika kumpata Tunda. Sasa utainufaisha vipi!
Utaona jinsi itakavyokusaidia kukubadilisha mtazamo wako. Kwanza hofu
itaondoka, na utashangaa utapata ujasiri wa umiliki.” Tunda akacheka kidogo.
“Kesho
tutaanza kwa kukupa nafasi upokee simu.” Tunda akastuka. “Net!” “Si umenisikia
leo jinsi nilivyokuwa nikipokea simu?” Tunda akakubali. “Basi fanya hivyohivyo
na usiogope kuuliza mteja maswali kuhakikisha unamuelewa. Ukiona anaomba huduma
ngumu kwako, au humuelewi, mwambie ili kumuhudumia vizuri, unamuunganisha na
mtu atakayeweza kumsaidia vizuri zaidi. Basi, niunganishe naye kwenye simu
yangu. Ila kwa kesho, pia tutakuwa wote. Usiogope.” Tunda akacheka kwa hofu.
“Sawa.
Nitajitahidi Net.” “Hayo ndio maneno. Na ninakuhakikishia utaweza tu. Sio ngumu
kabisa. Kwanza ile kompyuta ipo pale kukusaidia kukupa kila jibu. Si umeona?”
“Nilikuona jinsi unavyofanya.” “Sawa sawa.” Wakazungumza kidogo, Net akaondoka.
Siku ya Pili, Tunda kazini.
Tunda alitegesha alamu ili
imuamshe mapema kidogo. Akaoga na kujitayarisha. Kwa kuwa alirudi na baadhi ya
vitu vyake kutoka Dar, Tunda alijitengeneza kawaida, kiofisi kama vile
alivyokuwa akiwatengeneza kina Fina mwilini mwake anapokwenda kulaghai wanaume.
Alivaa vizuri. Kiofisi. Kama msomi mwenye majukumu mazito. Ila kiheshima kwa
kuwa alikuwa na Net.
Akaagiza
kifungua kinywa. Chake akala. Cha Net, akaomba wamfungie maalumu kwa ajili ya
kula ofisini. Alimuona akinywa kahawa, na walikuwa na microwave ofisini.
Akaomba waweke kila kitu tayari na kuwaambia atapitia hapo mgahawani.
Net
alifika hapo. Hakupanda juu kwenye chumba cha Tunda. Akampigia simu kuwa
ashuke. Kwa haraka bila kuchelewa, akapitia mgahawani akachukua kifungua kinywa
cha Net, akatoka nje. Alitoka kwenye mlango wa hoteli, Net akiwa kwenye gari
akimtizama. Hakika Tunda alikuwa amependeza. Kigauni chakuchanua chini kama
mwamvuli, juu kilimshika na kilikuwa kata mikono. Kilimfika chini kidogo tu ya
magoti. Kiatu cha kufunika, cha juu. Hereni ndefu bila cheni shingoni ila
hakuacha kuvaa ile ya mguuni na mkononi.
Pochi inayoendana na kiatu alibeba mkono wa kushoto, mkono wa kulia chakula cha
Net.
“Waw!” Akajisemea
Net mwenyewe wakati akimwangalia akimsogelea. Mwishoe akaamua kwenda kumpokea. “Hii
ni kwa ajili yako.” Tunda aliwahi wakati Net amemsogelea na yeye akawa
ameshafika karibu ya gari. “Asante. Sasa mbona ya kwako sioni?” “Uliniambia leo
ni zamu yangu kupokea simu. Sasa wakati mimi nazungumza na wateja, wewe
unakula.” Net akacheka. “Naona mudi wa kazi ameanza kukuingia.” Wakacheka. Net
alikuwa ameshapokea kile chakula. Akamfungulia mlango, Tunda akapanda. Na yeye
akaingia garini nakuanza kunywa kahawa yake. Kimya mpaka kazini.
Walipoingia tu, simu zikaanza. Net akakimbilia na
kupokea. Tunda akaanza kuwasha kompyuta akijua wazi Net atahitaji. “Naomba nikupe mtu ambaye atakusaidia.” Tunda
akashtuka na kumgeukia Net. Net akamkabidhi simu. Tunda akavuta pumzi. “Halow!” Tunda akaipokea. Net akavuta kiti nakuanza
kula pale pale kwenye meza bila hata kumtizama Tunda.
Mteja alikuwa akisafirisha mzigo kutoka Arusha
mpaka Moshi. “Ni mzigo wa aina gani na unaukubwa gani?”
Alimsikia Tunda akiuliza taratibu tu. Akamuona anaandika huku akisikiliza kwa
makini tu. “Kwa aina hiyo ya mzigo, tunaweza kusafirisha.
Lakini naomba nishauri.” Mpaka Net mwenyewe ikabidi atulie asikilize huo
ushauri. “Asante.” Akamsikia Tunda akishukuru na
cheko kidogo. Akahisi amesifiwa huko kwenye simu. Sauti ya Tunda ni kweli
ilikuwa nzuri.
“Nimesikia aina ya gari unayotaka. Na
ukisisitiza unakwepa garama. Lakini naona mzigo wako unathamani kubwa.
Isingekuwa vizuri kwanza tukufikishie pale ukiwa haupo kwenye hali nzuri. Lengo
letu kama kampuni sio kukusafirishia tu. Tungependa kuhakikisha tunafikisha mzigo
wako ukiwa salama pia.” Net mwenyewe
akashangaa. Tunda akaendelea kusikiliza, akamuona anacheka.
“Hapana. Nitakupa kwa bei nzuri tu. Naomba
nipe kama dakika moja au mbili, nikutajie aina ya magari yatakayofaa kwa bidhaa
yako.” Tunda akabonyeza spika, akaweka simu chini,
akaanza kuperuzi kwenye kompyuta. Net kimya. “Lakini
hujanitajia jina lako.” Wakamsikia yule mteja. Tunda akaanza kuogopa. “Mrembo? Maana nataka kila nikipiga, niwe nasikia hiyo sauti
nzuri. Au siruhusiwi?” Tunda na Net wote walikuwa wakisikiliza.
Tunda
akanyanyua simu. “Naitwa Tunda na nimepata aina mbili
ya magari ambayo nafikiri yatafaa kwa mzigo wako.” Tunda hakutaka
kuendeleza maongezi juu yake. Akamtajia hayo magari na bei yake. Akampa nafasi
achague. Akachagua moja na kutaka namba ya simu ya Tunda. “Naomba utumie hii ya ofisi kwa kikazi.” Net akajua
anatongozwa na ameombwa namba yake binfsi ya simu. Yule mteja akaendelea
kuongea, Net akamuona Tunda anakosa raha, akamuomba yeye hiyo simu.
Tunda
akamkabidhi Net simu. “Malipo ni kama alivyokwisha
kukwambia. Tutajitahidi kufika sehemu ya kuchukua mzigo kwa wakati na wewe
tunaomba uwataarifu kuwa dereva wa kampuni ya Cote, atafika hapo akiwa na
kitambulisho chetu. Asante.” Net alizungumza hivyo tu, na kukata simu.
Tunda akasimama na kutaka kuondoka.
“Njoo
kwanza Tunda.” Tunda akarudi. “Nisikilize. Kwanza umefanya vizuri sana. Hata
mimi sikutegemea.” Tunda akatabasamu na kufuta machozi. “Kweli kabisa. Na
ninataka uelewe hivi, kazi kubwa hapa au utakayofanya ni kuhudumia wateja wa
aina tofauti tofauti. Usiogope kwangu au kwao. Fanya kazi vizuri, wakifika
kwenye mambo yao binafsi, wajibu vile unavyotaka wewe. Usiogope. Sijui kama
unanielewa?” Tunda akavuta pumzi.
“Lazima
ufikie hatua uweze kutofautisha kazi na mambo binafsi. Na ile kauli ya ‘sina
uwezo wa kuchagua’, ufike mahali ijifute. Wewe ndio ubakiwe kiongozi wa
maisha yako. Yaani wewe ndio unajukumu lakuongeza nafasi kwenye maisha yako.
Uchague chakufanya ukiwa unafikiria ili kuepuka majuto ya baadaye. Sijui kama
umenielewa?” “Nimeelewa.” “Haya. Tuendelee na kazi.” Tunda akacheka na kurudi
kukaa.
Kufika
mchana, hofu ikawa imemuisha kabisa Tunda. Anapokea simu kwa ujasiri wote. Net
alishangaa vile Tunda anavyozungumza kingereza kizuri. Akahisi Tunda
alimdanganya. Alimwambia hajasoma. Na ni mtanzania! “Kingereza amekijulia wapi?” Akajiuliza Net kwa kadiri alivyokuwa
akimsikiliza akikizungumza na wateja kwa ufasaha bila hofu na ujasiri usoni.
Hakuna
aliyekumbuka chakula cha mchana. Kukawa busy mpaka jioni tena kama jana yake,
ila siku hiyo walikaa hapo mpaka usiku wa saa moja. “Naona utajuta.” “Kwa
nini?” “Si hivi unavyotumia muda mwingi hapa ofisini!” “Kwanza ndio nafurahia.
Kwa mara ya kwanza maishani naona nafanya kitu cha kueleweka na mtu
anakifurahia. Nashukuru kwa hii nafasi Net.” Tunda aliongea kwa upole. “Karibu.
Na ninaona umeshakuwa mtaalamu.” Tunda akacheka taratibu wakati wanatoka.
“Ni
hivyo hivyo tu, tena naona na umejaliwa lugha ya ushawishi. Hiyo pia
itakusaidia zaidi.” Tunda akatabasamu. Walikuwa kwenye gari. “Hata nikiwa mbali
na pale. Ukipata mteja ambaye unataka nizungumze naye, kama nilivyokufundisha
jinsi ya kuunganisha. Kwa simu ya mezani na ya mkononi. Rahisi tu. Niunganishe
na yule unayetaka nizungumze naye.” “Sawa.” Tunda akaitika `.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Tunda na
Net wakaendelea kufanya kazi kwa bidii zote. Wakisaidiana bega kwa bega. Wateja
wao wengi walikuwa wafanyabiashara wakubwa hapo nchini na watalii.
Walisafirisha bidhaa kubwa na za thamani huku wakipokea watalii nje na ndani ya
nchi. Walikuwa wakipokea watalii kutoka nchi mbali mbali. Net alijitangaza
kwenye website iliyokuwa ikivutia watalii kutoka nchi mbali mbali.
Tunda
alimshangaa uwezo wake wakuzungumza lugha. Alikuwa akiongea lugha tano tena
kifasaha. Kama sio kingereza au Kiswahili, Tunda alimuhamishia simu Net popote
alipo azungumze na aina hiyo ya wateja. Na Net aliacha kusafiri. Akawepo Arusha
kwa muda huo aliokuwa na Tunda hapo. Kwa hiyo, hiyo miezi ya mwanzoni ikawa
rahisi kwa Tunda.
Wafanyabiashara
wengine waliomsikia Tunda kwenye simu walipatwa tamaa. Baada yakushindwa kupata
namba zake za simu, walikuwa wakiamua kufika kabisa hapo ofisini, ilimradi tu
kumuona nakujaribu kumtongoza. Tunda akashangaa sana. “Kipindi nilipokuwa na shida
nao, wote walijificha, sasa hivi ndio wanajitokeza!” Tunda
akajiuliza. Net alikuwa akimtizama kwa karibu na alijua nia ya wengi wao.
Kila
walipofika pale, Tunda alipowasukumia kwa Net, bado walitaka kuzungumza naye
Tunda zaidi. Ghafla yeye akawa wamuhimu kuliko mwenye kampuni! Tunda akajua ni
janja yakumpata tu . Akawa
akiwakwepa kiustarabu lakini akimaanisha kabisa. Alishatendwa na kuwatumikia
hao wanaume, hakuwa na hamu tena. Alikinahiwa na swala la mapenzi, Gabriel
akawa amegongelea msumari wa mwisho.
Hakuwa
akijua kama anaweza kufanya kazi kama wasomi wengine kwenye ofisi kama ile.
Tena alifanya vizuri sana, mpaka mama yake Net aliyekuwa akizungumza naye
kwenye simu alikuwa akimfurahia sana. Tunda alifanya kazi kwa bidii sana bila
kuchoka wala kulalamika na Net alimwambia atamlipa. Akajiambia hana sababu
yakuuza mwili wake tena. Kwa mara ya kwanza akawa amepata nafasi ya kuchagua
nini afanye kwenye maisha yake. Kuuza mwili au kufanya kazi ili kujipatia
kipato. Sasa kwa kuwa wanaume walishamtenda na kutumia huo mwili vibaya, kwenye
swala la biashara ya ngono, akaona aweke kikomo. Hakuna aliyemkubalia.
Hakuwa
na jumamosi wala jumapili, pale alipokuwa na mambo yake yakufanya ofisini,
hakuangalia muda hata kidogo. Aliongeza juhudi kazini. Hakujiangalia yeye tena.
Akataka kumfurahisha Net na kulipa fadhila. Tunda alijua pesa inayomtoka Net
kwa kuwekwa pale hotelini. Sasa ili kulipa fadhila, ni kuweka juhudi. Net
mwenyewe alikuwa mchapa kazi. Wakaendelea kuchapa kazi kwa pamoja
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Siku
moja ilikuwa jumamosi. Walifanya kazi hiyo week, kuanzia asubuhi mpaka usiku.
Jumatatu mpaka siku hiyo jumamosi usiku. Net akamwambia Tunda wanastahili
kwenda kula chakula kizuri sehemu kama kujipongeza. Tunda akacheka akijua wazi
amefurahia. Waliingiza pesa hiyo week. Kuanzia dola mpaka pesa ya madafu.
“Unahamu
ya kula nini?” Akamuuliza Tunda. “Mimi ikishafika usiku kama hivi,
nilishakwambia, siwezi kula kitu kigumu. Sitaweza kulala.” Tunda akajibu na
kumalizia kufunga kompyuta aliyokuwa akitumia.
“Lazima
tujipongeze.” Tunda akacheka. Siku za jumapili ilikuwa wakionana jioni. Tena
kwa muda mfupi. Net alikuwa akimpitia hapo hotelini kama kumsalimia tu. Wakati
mwingine alikaa kidogo, wakati mwingine aliondoka. Tunda hakujua anaishi wapi.
Kama ameoa au la. Anaye mwanamke hapo Arusha au la. Katika watu aliowaogopa
hapa duniani ni Net. Alimuogopa huyo kaka kupita kiasi. Mbali na mambo ya kazi,
hakuwa na ujasiri wakumuuliza chochote.
“Nishushe
mimi hotelini. Wewe nenda tu Net.” “Hapana bwana. Hii ni tunajipongeza
wafanyakazi wa Cote. Wewe vipi Tunda?” Tunda akacheka. “Twende basi ukale hata
matunda wakati mimi nakula nyama choma. Njaa inaniuma.” Wakakubaliana.
Walitafuta
hoteli nzuri. Ni kweli Net hakupenda sana kwenda baa, labda awe anakutana na
rafiki zake au mambo ya biashara, ndipo itamlazimu kwenda. Waliingia sehemu ya
chakula. Tunda akaagiza maji na fruits salad. Akiwa hana hata habari kama
atamwingiza Net matatizoni siku hiyo. Alikuwa amependeza japo alikuwa ameshinda
kazini siku nzima tena siku ya jumamosi.
Aibu ya Mwaka kwa Tunda Mbele
ya Net. Ya Nyuma Bado Kumfuata Tunda.
Net
aliagiza chakula chake na juisi ya embe. Hiyo hoteli juu ilikuwa na vyumba na
kumbi ya mkutano. Hali ya Tunda ikabadilika ghafla hata kabla chakula
hakijaletwa, Net asielewe ni kwa nini. Meza ya pembeni, mbele kidogo, akaona
wamekaa wanaume wakila na kunywa huku wakiongea na kucheka. Watatu wa hao
waliokuwa wamekaa hapo kwenye hiyo meza, Tunda alishawahudumia. Tena wakiwa
kwenye baa.
Wote
waliokuwa wamekaa pale walikuwa marafiki, walikuja mjini Arusha kwenye mkutano.
Na wote walikuwa wakifanya kazi ofisi moja. Kwenye NGO ya kigeni. Vijana wenye
pesa na wasomi tu. Sasa watatu wao pale ndio hao Tunda alishawahudumia zaidi ya
mara moja. Mmoja alimpata kwa kuiba namba ya simu kwenye simu ya mteja
mwingine.
Wawili
aliwatongoza baada ya kukutana nao baa. Akafanya ule mtindo wake wakumchomoa
mmoja baada ya mwingine. Siku ya kwanza akampata mmoja wao wakiwa wamekaa wote
mezani wakinywa. Akatoka naye nje, akamalizana naye kwenye gari. Akamuomba
namba yake Tunda. Wakaja kukutana tena kwenye nyumba za kulala wageni. Akampa
kwa mapana na urefu. Wakati akiwa anaoga aondoke pale hotelini, kabla Tunda
hajamfuata huko bafuni, akaiba ya watatu. Kwa kuwa aligundua hao wawili
walikuwa karibu akajua lazima atakuwa na namba yake ya simu. Na kweli
akafanikiwa.
Siku
inayofuata, akampigia simu huyo wa tatu, akijidai anamuulizia yule wa kwanza
kabisa ambaye alienda naye baa ndipo akakutana nao wote. Akamzungusha kwa
maneno mazuri kwenye simu, mpaka akajikuta na
yeye anaomba penzi. Tunda akajidai kumkatalia kwa kumwambia wenzake
watajua kwani alishaonekana na wote akiwa na yule rafiki yao. Akambembeleza
akimwambia yeye ni mtu mzima, sio mropokaji. Basi, akachukua chumba mahali,
Tunda akaenda kumpa kwa mapana na marefu. Na yeye huyu wa tatu akajua kuwa
anamuibia rafiki yake. Ikawa siri yao wawili, ila nafuu zaidi kwa Tunda
anayewazunguka wote. Marafiki hao watatu wasijue wanapewa uroda na mwanamke
mmoja.
Siku
ingine aligonganisha magari wakiwa baa. Alijikuta na wote watatu meza moja,
akiwa ameenda na yule yule wa kwanza, yule wa pili aliyemsaidia kumpata wa tatu
akapewa penzi kwenye gari mpaka akatafuta chumba, akamtumia ujumbe wakiwa pale
pale mezani kuwa watoke nje. Tunda alipopata ujumbe akiwa anacheza game yake
pale kwenye meza ya wale marafiki walevi, akarudisha ujumbe akamwambia anatoka,
ila asubiri baada ya dakika mbili kamili ndipo amfuate.
Basi wakafanya hivyo. Alipotoka
tu, yule watatu naye akatuma ujumbe kuwa anamuhitaji. Akiwa anamsubiria yule wa
pili, ndani ya zile dakika mbili akachat na watatu. ‘Ushawahi
kuonja vya garini?’ Akamtumia ule ujumbe. Watatu akajibu kwa haraka. ‘Hapana mama. Ila nipo tayari kujifunza.’ ‘Basi nisubiri.
Nikija kuomba funguo za gari hapo mezani. Unifuate baada ya dakika tatu tu.’
‘Asante mama.’ Usiku huo akawapa dozi marafiki wote watatu bila wao
kujijua.
Kwani
alipomalizana na wa pili, akamwambia arudi ndani haraka na asiseme kitu. Baada
ya muda, akarudi na kumwambia yule wa kwanza tumbo limejaa gesi. Anaomba funguo
za gari yake aende akatafute dawa za gesi kwenye duka la madawa. Katikati ya
pombe na vile anavyohudumiwa na Tunda, akatoa funguo za gari. Tunda akatoka,
yule rafiki wa tatu akafuata nyuma. Alichofanya Tunda nikuhamisha upande
lililokuwepo hilo gari. Akaenda kulificha mbali kidogo, hapo hapo baa. Dakika
tano zikawa nyingi. Akamalizana na rafiki watatu. Akamshukuru sana na kufurahia
ule wepesi. Akampa mahela, akamwambia arudi ndani kwa haraka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Sasa
wote watatu wakawa wanajua uwezo wa Tunda wa mapenzi, na wale wawili
walishapewa penzi la garini tena kwa muda mfupi sana na wote wakijua wanamwibia
mwenzao. Na hawakuwahi kukamatwa hata mara moja. Yule mwizi wa halali, wa
kwanza akawa amemuona Tunda pale kwenye meza. Akaamua kwenda kumsalimia Tunda
pale pale mezani alipokuwa amekaa na Net.
“Habari
Lina?” Akanyoosha mkono kwa Tunda. Net akamgeukia yule kijana na kumtizama
Tunda. Tunda akakwepa ule mkono kwa kunyanyua glasi ya maji. “Nzuri tu.”
Akajibu Tunda na kunywa maji. “Nikuombe msamaha. Majuzi ulipokuwa ukinitafuta,
nilikuwa nimebanwa kweli ndio maana nikashindwa kabisa kupokea simu yako.” Yule
kijana alijieleza kwa Tunda. “Hamna neno. Nilielewa.” Akajibu Tunda taratibu,
Net akisikiliza.
“Vipi,
umehamia Arusha nini?” Akamuuliza Tunda. “Nipo kikazi. Huyu ni bosi wangu.”
“Oooh! Nimefurahi kukufahamu Kiongozi.” Akampa mkono Net, yeye Net akaupokea
mkono na kujibu salamu. “Nipo hapa Arusha na wenzangu. Tumekuja kikazi. Nipo
gorofa hii ya pili tu. Hapa hapa hotelini. Nakukaribisha.” Akamgeukia Tunda. “Asante,
lakini hapana. Nipo busy na kazi.” Tunda alimjibu kwa msisitizo tena akimtizama
machoni.
“Kesho ni jumapili Lina. Najua hufanyi kazi.
Na mimi kuanzia asubuhi nitakuwepo tu hapa hotelini. Kwa nini usije? Sitakuweka
sana.” Tunda alitamani kama aondoke lakini ikamlazimu kujibu tu. “Nina mipango
mingine. Tafadhali naomba uondoke ili nile. Unanisimamia hapa, tunashindwa
kula. Nimeshakwambia hapana, inatosha.” Chakula kilikuwa kimeshaletwa.
“Au
umekasirika sababu sikupokea simu yako?” Akaendelea kusisitiza. Mpaka Net
akaweka kisu na uma chini. “Hapana sijakasirika ila sitaki kuonana na wewe
tena. Naomba utupishe.” “Daah! Sawa Lina. Lakini…” Tunda akavuta kiti kwa nguvu
na kusimama. Akamtizama machoni. “Samahani Lina, sikutaka kuwakwanza.” Tunda
akaondoka kuelekea chooni, yule kijana naye akaondoka. Harufu ya pombe ndiyo
ilikuwa ikitoka mdomoni kwake na kuenea pale kwenye meza ya Net na Tunda.
Wakati
anarudi, ndio anatoka choo cha kike anaingia pale mgahawani alipomuacha Net,
akakumbana na wale wengine wawili. “Samahani Lina, tunaweza kuzungumza kidogo
hapo nje?” Mmoja wao akaanza na yule mwingine akabaki ameduaa. Kumbe wote
waliaga pale mezani kwa rafiki zao kuwa wanakwenda msalani, kumbe walikuwa
wakimfuata Tunda. Mmoja akawa amewahi.
Kabla
Tunda hajajibu, mwenzie akadakia. “Mimi ndio nataka kuzungumza naye mara moja
hapo nje. Hatutachukua muda mrefu, si ndio Lina?” Watatu akadakia, akijua Lina
mwenyewe anaelewa. Huwa wanamalizana kwa muda mfupi sana, asijue na rafiki yake
naye anachomtakia huyo Lina sio mazungumzo. Ni huduma kama anayoitaka yeye.
Wakiwa
wote wamelewa, wakaanza kubishana. “Mimi sitachukua naye muda mrefu. Dakika
tano tu.” “Aliyekwambia mimi ninamchukua kwa muda mrefu ni nani? Natoka naye
mara moja tu, tunarudi.” Wakajibishana wale marafiki wawili, mmoja akiwa
amemshika mkono Tunda. Tunda alitamani kukimbia lakini akajikuta wote
wamemshika mkono. Mmoja huku mwingine kule. Ndipo ulipozuka ugomvi, wote
wakimng’angania huyo Lina, hakuna anayetaka asubiri kwanza.
“Nakwambia
mimi ni mara moja tu! Mbona unafanya mambo ya kitoto, Zimbe?” “Wewe ndio
nakuona huelewi. Nimekwambia hata mimi sitamkawisha. Anarudi sasa hivi.” Watu
wote mle ndani macho ya kawa kwao wote watatu. Tunda anatetemeka, anataka
kubebwa juu juu ili watoke naye pale ndani. Uzuri wakaanza kurushiana wao
ngumi, na kumuachia Tunda. Hakujua Net alipotokea, akamsogelea pale akiwa
ameshika funguo za gari na pochi yake. Akamshika mkono kwa nguvu, akamvuta
kumtoa pale.
Waliingia
kwenye gari, Net akaondoa gari kwa haraka Tunda akitetemeka kama aliyetoka
kwenye friza. Hata asante alishindwa kusema kwa aibu. Alipofika hotelini,
alichukua pochi yake na kushuka kwa haraka kama anayekimbia. Net akaona amuache
tu usiku huo. Hata yeye hakumfuta nyuma. Akaondoka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kuanzia
siku hiyo Tunda alijiapia kutotembelea tena sehemu za starehe au kwenye mabaa.
Na kwa kuwa Net alikuwa mstaarabu, hakuwahi kumuuliza tena juu ya ule mkasa.
Ila alimuona ile hofu ya mwanzoni kabisa imerudi vile vile. Tunda aliacha hata
kumuangalia machoni. Mara nyingi ilipomlazimu kumuongelesha alimuongelesha
akiwa anaangalia pembeni. Kama yupo ofisini basi macho kwenye kompyuta au
mafaili. Labda Net afanye juhudi za makusudi kumwita jina lake. Hapo atageuka
na kukwepesha macho kwa haraka. Alikosa ujasiri kabisa, akapooza hata tabasamu
likamwisha.
Wakajikuta
muda mwingi wanakuwa pamoja ofisini, wakitoka hapo, anamrudisha hotelini. Week
ya tatu Net alipata kijana wa usafi. Akamwambia Tunda atakuwa akifika hapo
kusafisha na kutoka mchana. Na huyo ndio mara nyingi Net alianza kumtuma kwenda
kuwanunulia chakula na kuwaletea hapo ofisini au wanapitia sehemu. Net anaingia
ndani. Ananunua chakula, wanaenda kula hotelini huku Net akiangalia taarifa ya
habari. Aliondoka muda alioona Tunda anataka kulala. Hakuna maongezi. Kimya
kimya.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Karibu
ya mwezi kuisha tangia aanze kazi, Net alimwambia inamlazimu kwenda Dar kwenye
ofisi nyingine ambapo yupo mama yake. “Kuna mambo kadhaa yakuweka sawa.
Ungependa tuongozane?” Akamuuliza Tunda. “Hapana. Wewe nenda tu. Niache mimi
hapa. Nikikwama nitakujulisha.” “Hutaki kuona ofisi ya Dar?” “Halafu hapa
tufunge!?” Tunda akauliza kwa mshangao kidogo.
“Hapana.
Si unajua hiyo kazi unaweza kufanya popote tu?” Akamuuliza na kumuelekeza kuwa
nikupokea simu ambazo wanaweza kuzihamishia hata kwenye simu ya Net au yake. Na
kompyuta wanaweza kutumia laptop tu ambayo wanaweza kwenda nayo popote. Tunda
akaelewa ila akanyamaza. “Hatutakaa muda mrefu.” “Kama sio lazima, naomba
uniache hapa Net. Tafadhali.” Tunda akaongea kwa upole.
“Sio
lazima Tunda. Ila sikutaka ubakie hapa peke yako kazi zikakulemea.” “Nitakuwa
sawa. Nikishindwa jambo, nitakutafuta unisaidie. Ila nakuahidi kila kitu
kitakuwa sawa.” Akasisitiza, Net akamwangalia. “Samahani lakini. Naomba
usifikiri nakukaidi au nakataa kazi. Ndio maana nimeuliza kama kunakitu
chakikazi natakiwa kufanya mimi huko. Uliponiambia hapana, ndio maana nimeomba
nibaki tu.” Tunda aliongea kwa utaratibu na kujihami.
“Sasa
hivi natamani maisha haya niliyonayo Net. Napenda hivi ninavyoweza kukufanyia
kazi. Au kujiona nafanya kitu chamaana. Acha akili zangu zitulie kazini kwa
muda. Nimepoteza muda mwingi sana kwenye lile jiji. Mbaya zaidi nimepoteza ‘kwangu’!
Inaniuma sana kujiona nimegeuka kuwa mgeni kwenye nchi yangu mimi mwenyewe!
Nyumbani kwangu ndio ilikuwa kimbilio langu. Nikishahangaika huko, nilikuwa
nikijifariji ninalo kimbilio. Sasa hivi sina. Hii kazi ndio imegeuka kuwa
kimbilio. Nikiamka asubuhi, najiambia ninakitu chakufanya. Inanipunguzia
mawazo. Kuja kurudi Dar kama mgeni, nikijua sio kwangu tena, itaniumiza zaidi.
Ndio maana nakuomba kama sio lazima, kwa sasa naomba nibaki tu hapa.”
“Nimeelewa.
Hamna shida. Tutawasiliana basi. Ukikwama usisite kunipigia. Na bado zile simu
unazotaka mimi nijibu, endelea kuwahamishia kwangu.” “Asante Net. Ungependa
nikusindikize uwanja wa ndege?” Tunda akauliza kwa upole akionyesha kujali. “Ningeshukuru.
Tena itakuwa vizuri nikuachie gari. Nitaondoka na ndege ya mchana. Utanipeleka
na wakati wakurudi ningeomba uje kunipokea.” “Sawa. Lakini naomba usinielewe
vibaya.” Bembeleza hiyo ya Tunda. Net mwenyewe alikuwa akilainika.
“Nimeelewa
kabisa. Usiwe na wasiwasi.” Wakatulia kidogo. “Basi nitakuona kesho. Nitakuja
kukuchukua asubuhi twende kazini, mchana ndio utanisindikiza.” “Sawa. Usiku
mwema.” “Na wewe.” Net akaondoka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Net na
Tunda walifika uwanja wa ndege, wakabaki kwenye gari upande wa kuegeshea
magari. Hawakushuka. Kila mtu kimya kwa muda. Net macho kwenye simu yake, Tunda
ametulia tu pale kwenye kiti kama hayupo garini. Hana simu mkononi. Ametulia
kimya.
Baada ya
muda akaita. “Net!” Akaita kwa upole. Net akamgeukia. “Unarudi lini?”
“Nitajitahidi nisikae sana. Kuna kitu ulitaka kuniagiza? Hata kwenye vitu
vyako. Nitakwenda kule Salasala kumuona Max.” “Max ni nani?” Ikabidi kwa mara
ya kwanza Tunda kuuliza kitu mbali na kazi.
“Kumbe
siku ile sikukuonyesha?” Tunda akatingisha kichwa kukataa. “Ni mbwa. Nilimnunua
na akapatiwa mafunzo ya kiulinzi. Mzuri sana. Ananisaidia sana pale kwa ajili
ya ulinzi. Yeye tu na Emma wanatosha.” Tunda akatabasamu. Net akacheka. “Ni
mzuri sana. Nampenda.” “Mimi muoga wa mbwa.” “Max utampenda. Tutakuja kwenda
wote siku moja, nikutambulishe. Kwa sasa ananijua mimi, Emma na daktari wake.
Ni mkali au hatari kama akijua sio mtu salama.” Tunda akacheka na kutulia.
Wakatulia
hapo kwa muda. Net alianza kuona uzito wa ile safari. Walishakuwa kwa karibu
sana na Tunda karibia mwezi sasa. Kula na kuwa pamoja kila siku, tena kwa
ukaribu! Tunda anautulivu fulani hivi, huchoki kuwa naye. Akaona uzito
kumuacha. Akamwangalia, akamuona amegeukia dirishani kama anayewaza. Na yeye
akatulia tu akimwangalia na kupotelea mawazoni.
Tunda
akageuka, akamuona amejiegemeza kwenye kiti chake akimwangalia. “Huna haja
yakunisindikiza mpaka kule.” Ikabidi amuwahi. “Sawa.” Tunda akakubali. “Kama
hutataka lakini.” Akajihami Tunda asijefikiri anamkwepa. “Hamna neno.” Akajibu
taratibu. “Au ungependa kufika mpaka kule ninapoingia kupanda ndege?”
Akababaika tena kwani aliongea bila kufikiria baada ya Tunda kugeuka na
kugundua anamwangalia. Akapaniki. “Ni sawa tu. Wakati wakuja kukupokea pia
nikusubirie hapa hapa?” Tunda akauliza taratibu bila kuonyesha tatizo lolote. “Utakavyopenda.
Ila tutawasiliana.” “Sawa. Uwe na safari njema.” “Asante na wewe ubaki salama.
Unipigie ukikwama.” “Naamini kila kitu kitaenda sawa.” Tunda akajibu.
“Inamaana hatutawasiliana mpaka nirudi?”
Akajiuliza Net. Akaona amejifunga kwa maneno yake mwenyewe. “Unarudi hotelini
au kazini?” “Sasa hivi nimapema sana. Acha nirudi ofisini tu. Nifanye fanye
kazi upaka usiku, ndio nirudi kulala.” “Basi nikifika tu nitakujulisha.”
Akachomekea Net na kujishtukia. “Na kujua umefikia wapi huko kazini.” “Sawa.”
Tunda akajibu. Net akaona asije kuongea mengi na kuharibu zaidi, akashuka
garini japo muda haukuwa umefika. Tunda akarudi kazini akitumia hiyo gari ya
Net.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Net
alitua jijini Dar, akili zikiwa Arusha. Mama Cote alikuwepo uwanja wa ndege
kumpokea mwanae. Hawakuwa wameonana karibia mwezi. Kila weekend alipokuwa
akimpigia simu nakumtaka arudi nyumbani, Net alisema yupo busy labda weekend
ijayo. Siku zikazidi kwenda akahisi lipo jambo tu huko Arusha. Net sio mtu wa
kung’angania Arusha na kushindwa kumuona mama yake zaidi ya majuma matatu tena
akiwa hapo hapo nchini! Akajua lipo jambo kwa kijana wake. Na kwa kuwa
alishazungumza na Tunda kwenye simu, akamsikia sauti yake, vile anavyoongea,
akajua huyo Tunda pengine ndiye anayembakisha huko Arusha.
“Vipi
Tunda?” Mama yake akauliza kiuchokozi tu na Net akajua. “Naona anaendelea
vizuri. Kazi nyingi ameshazijua. Wateja wengi amewamudu.” “Lazima. Ana lugha
nzuri. Namaanisha sauti.” Net akacheka. “Umeanza mama Cote.” “Jamani!” Wote wakacheka. “Sasa kwa nini hukuja naye?”
“Si yupo kazini mama jamani!” “Sawa, namaanisha weekend zile nyingine?
Mkaribishe nyumbani. Hizo kazi mnaweza kufanyia hata huku Dar kama ulivyokuwa
ukifanya.” Net akatingisha kichwa. “Sawa mama.” Wakacheka.
Net
alikaa Dar siku mbili tu, tayari akawa anataka kurudi Arusha. Ghafla chakula
cha Dar kikaanza kuwa hakiliki vizuri, masaa hayaendi. Ofisi ya Arusha ikawa
inamuhitaji sana, basi ikawa vurugu. Akamuaga mama yake. “Nilijua week hii
utamalizia huku urudi jumatatu! Maana leo ni ijumaa. Jumapili twende wote
kanisani. Hata mchungaji amekuwa akikuulizia.” “Nitarudi weekend ijayo.” Mama
yake akajichekea moyoni.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Jioni
hiyo akampigia Tunda simu. “Nimepata tiketi ya
asubuhi.” “Basi nitakuja kukupokea.” “Sawa. Ila kama utakuwa na mambo mengine
naweza kuchukua taksii.” “Hamna neno. Nitatokea ofisini. Nitakuja kukupokea,
halafu unirudishe ofisini kama umechoka unaweza kuniacha tu wewe ukapumzike.”
“Sawa. Lakini nafikiri na mimi nitarudi ofisini.” “Sawa.” Tunda akajibu
taratibu kama kawaida yake.
Kesho yake Net alitua uwanja wa
ndege wa Arusha, Tunda akiwa anamsubiria hapo nje, wala si kule kwenye gari.
Net akafurahi sana kumuona pale. “Pole na safari.” “Asante. Na asante kwa kuja
kunipokea.” Tunda akatabasamu. “Nimefurahi umerudi.” Tunda akaongea kwa upendo
kama aliyekuwa ameachwa hapo kwa muda mrefu. Net kijana wa kizungu akacheka. Na
macho yake yale ya rangi ya bahari, Tunda akakwepesha huku akinyoosha mkono
ampokee.
“Sio
mzito!” Net akajihami kama asiyetaka kupokelewa, anaweza kubeba kila kitu yeye
mwenyewe. “Lakini angalau nikupokee. Usibebe kila kitu peke yako.” Akampa mkoba
wa laptop. “Nimekuletea movie za stori kama unazopenda.” Tunda akacheka. “Asante.
Nitaangalia kesho jioni. Asubuhi nataka niende kazini kidogo.” Net akanyamaza.
Ni siku ya jumapili. Yeye alikuwa lazima kwenda kanisani. Wakarudi ofisini
mpaka jioni.
Jumamosi
huwa kijana wa usafi hafiki hapo ofisini. Walikuwa wao tu wawili. Net alifikia
kwenye meza ya Tunda. Tunda akashangaa haingii ofisini kwake. Yupo tu hapo
mezani kwake akifanya kazi zake hapo hapo. Japokuwa alikuwa akimuogopa, lakini
alifurahia uwepo wake hapo. Hawakuwa wameonana kwa ‘Siku mbili! Nzima’.
Wakashinda wote hapo wakifanya kazi pamoja. Hapakuwa na maongezi mengi. Tunda
anamuogopa Net. Zaidi ya kumjibu endapo atauliza, basi hatazungumza chochote.
Net naye kimya akifanya kazi zake kwenye laptop yake, Tunda asijue ni nini
kinachomfanya kijana huyo kuwa busy kwenye hiyo laptop kila wakati. Kazi
zikaendelea kwa utulivu siku hiyo ya jumamosi.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Wakaendelea
kufuatana. Kazini, hotelini kwa Tunda mpaka wakiagana kwenda kulala. Mwishowe
Net akaonelea kutafuta vitu ambavyo angefanya pamoja na Tunda kila wawapo
pamoja, baada ya kazi angalau wazoeane au kupata kitu chakuzungumza mbali ya
kazi. Akaanzisha siku na muda wao wakuangalia movie pamoja.
Wakitoka
kazini, badala ya kukimbilia rimoti na kuanza kuangalia taarifa ya habari peke
yake, alimtaka Tunda wakae wote hapo waangalie movie pamoja, au wacheze karata.
Basi watacheza hapo kisha anaondoka na kumuacha Tunda. Lakini hakuwahi
kumuuliza Tunda swali hata mara moja juu ya mara zote alizowahi kumkuta na
wanaume au hata kisa kile alichotaka kubembwa juu juu. Tunda alishindwa
kumuelewa kabisa Net. Walicheza na kuzungumzia kile kilichopo mbele yao tu kana
kwamba hakuwa akimfahamu.
Kitu
alichokigundua kwa Tunda kila walipokuwa wakiangalia tv hapo kwenye kochi,
chumbani kwa Tunda, Tunda alijivuta pembeni yake, alikunja miguu yake vizuri na
kuweka mikono yake juu ya kochi kama mto na kulala usingizi mzito sana. Net
alijaribu kubadili aina ya movie. Alileta za visa vya kusisimu, wakati mwingine
historia za kusisimua lakini mara zote Tunda aliishia kulala kabla hata
hazijafika hata nusu! Na ulalaji wake ulikuwa wa usingizi mzito sana, na mara
nyingi Net aliishia kumfunika pale pale kwenye kochi na Tunda aliishia kulala
hapo mpaka asubuhi, kwani alishamuomba wakati akiwa anaondoka asiwe anamuamsha ili ahamie kitandani, alitaka
aondoke kimya kimya amwache tu vile vile alivyolala.
Yeye Net
alikuwa akifurahia sana kuwa na Tunda, lakini wawe wanazungumza. Macho na sauti
ya Tunda ni kweli vilimsumbua Net. Alikuwa akipenda awe anamtizama sio vile
anavyokwepesha macho au basi angalau azungumze ili tu asikie ile sauti yake
akizungumza naye yeye. Na iwe kwa muda mrefu. Kila alivyojitahidi Net, Tunda
hakuwahi kubadilika. Wakati mwingine anaweza akanyamaza hapo chumbani kana
kwamba hayupo. Atatulia kimya, akijitahidi ni kutoa tabasamu.
Net
alijua kwa hakika anamuogopa sana. Swala la afanye nini kuondoa ile hofu ndio
ukawa mtihani mkubwa. Tunda kimya. Kila alipoanza maongezi alianza kwa kumwita
jina lake, kumfanya angalau Tunda
amtizame ayaone hayo macho.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
“Uliniambia unapenda sana kuangalia movie za stori,
Tunda. Kwa nini kila nikiweka movie unalala? Nataka tuwe tunaongea bwana!
Tunakuwa ofisini busy week nzima, angalau jumamosi jioni au jumapili tuseme
ndio tunapata muda wakupumzika na wewe unalala! Au hufurahii hizi movies
ninazochagua mimi?” “Ni nzuri sana tu. Mbona mwenzako huwa naangalia tena kwa
kuzirudia rudia? Kila nikitoka kazini, ukiondoka au nikishtuka usiku nakujikuta
nimebaki peke yangu, naziangalia.” Net hakuelewa.
“Sasa
kwa nini hutaki kuangalia na mimi?!” “Hata nikikwambia hutaelewa Net.” “Bila
kunijaribu!?” Tunda akanyamaza. “Au nakukera nikiwepo hapa?” “Nisingelala Net.”
Net akakunja uso kidogo kama ambaye hajaelewa.
Kwa Mara ya Kwanza, Tunda aamua kufunguka kwa Net
Tunda
akajiweka sawa. Net akajua anataka kuongea jambo. “Tokea siku ile nitolewe au
niseme nifukuzwe kwa bibi yangu nikiwa darasa la pili, sikuwahi kupata utulivu
wa akili. Nakumbuka kwa mara ya kwanza siku ile jioni nikisikia ndugu zake mama
wakitaka nitolewe pale kwa mtu niliyedhani ndiye mama yangu au nikidhani
nyumbani kwetu, na ndio nikajua mwanamke aliyekuwa akinichukia sana hata
alipokuwa akija pale kijijini mara zote hakutaka nimwangalie, ndiye alikuwa
mama yangu wa kunizaa.” Tunda akaanza taratibu.
“Nilimsikia
jinsi anavyobisha kunichukua akitaka niendelee kuishi pale pale kwa bibi na
babu, yaani kwa wazazi wake. Walipomlazimisha sana, wakitaka lazima niondoke
pale ili kupunguza matumizi ya pale kwa bibi, pale nilipodhani ni nyumbani
kwetu, na mimi ni mdogo wao wa mwisho, ndipo nilipoona jinsi mwanadamu
anavyoweza kubadilika na kuwa mnyama mkali kuliko hata simba.”
“Alinichukua
kwa hasira sana kwa kuwa walimlazimisha lazima anitoe pale. Njia nzima yule
mwanamke ambaye nilisikia wakisema ni mama yangu, alikuwa akinifinya na
kunipiga sana. Kama sio makonzi ya kichwani, basi ngumi nzito sana kwa
kutofanya alichoniagiza kwa mtoto wake. Ni kweli sikuwa nikimuelewa. Kwanza
alinitajia majina ya vitu ambavyo sikuwahi kusikia mimi mtoto mdogo,
niliyekuzwa kijijini, tena wakati huo hata Kiswahili chenyewe sikuwa nikielewa
sawa sawa. Wakati wote tulikuwa tukizungumza kilugha pale kijijini. Pili,
nilikuwa kwenye mshtuko wa kutolewa kwa kufukuzwa kwenye nyumba niliyokulia,
kwa watu niliojua ni wazazi wangu.” Tunda akaendelea taratibu.
“Nakumbuka
ile hali ya kuchanganyikiwa, hofu na wasiwasi nisijue huyo mwanamke
anayenichukia waziwazi, alikuwa akinipeleka wapi! Yeye ndiye alikuwa dereva,
nilikaa kiti cha nyuma na mtoto wake. Mbali na usafiri wa vibasi vya pale kijijini
kututoa kijiji kimoja kwenda kijiji kingine, sikuwahi kupanda gari aina yeyote
ile. Sikujua jinsi ya kushusha kioo cha gari au kupandisha. Na wala sikuwa
nikijua wanafunga na kufungua vipi mlango wa gari! Hilo ni kosa pia
lililonifanya nipigwe njia nzima. Kila aliporudisha mkono wake nyuma tukiwa
njiani ilikuwa ni kunifinya sana au kunipiga kofi.” Net alikuwa akisikiliza kwa
makini huku akishangaa.
“Alijawa
na hasira juu yangu, hata uso wake alionyesha. Nilishindwa kujua ni kwanini,
lakini matusi aliyokuwa akinitukana ndiyo yalinifanya baadaye nihisi labda baba
yangu alimtendea kitu kibaya sana ndio maana alinichukia kwa kiasi kile.”
“Tokea
siku ile, ndipo maisha yangu yalipobadilika kabisa, Net. Na ndio ukawa mwisho
wa kila kitu ambacho wanadamu wengine walibahatika kuwa navyo hapa duniani,
wakichezea na kudharau. Mimi ndio ukawa mwisho wangu.”
“Jina la
Tunda liliisha kabisa. Kila aliyeniona
aliniita vile anavyotaka yeye. Mama yangu mzazi aliniita majina mengi lakini
ambalo lilibaki masikioni mwangu ni ‘Paka’.
Alichukia rangi yangu, macho yangu na sauti yangu ndio ilikuwa kero kabisa,
kwani ilikuwa ikinichukua muda mrefu kidogo kutengeneza sentensi moja ya
Kiswahili, mtu akanielewa. Aliishia kuniwasha vibao vya usoni kila wakati na
kunigeuza bubu.”
“Mambo
hayakuwahi kugeuka tena, mpaka sasa wewe ndiye mtu wakwanza kupongeza kazi
ninayofanya na kunipokea jinsi nilivyo ukijua jinsi nilivyooza, lakini bado
unaniheshimu Net. Ndio maana kila ninapokuwa na wewe, najikuta sina hofu Net.
Sina sababu ya kujificha, au kujibaraguza au hata kubadili jina langu. Napata
amani ya ajabu, najua nipo na mtu anayeweza kunitazama kama binadamu mbali na
maovu yangu yote.” Machozi yakaanza kumtoka Tunda.
“Huu usingizi ninaopata nikiwa na wewe sio ninaopata nikiwa peke
yangu. Tena afadhali sasa hivi naweza kulala hata masaa machache nikijua kesho
nitaenda kazini, kitu ambacho sikuwahi kufikiria kama naweza kufanya maishani.
Wanadamu nilioishi nao wote, walihakikisha wananikandamiza na kunihubiria jinsi
nilivyo kiumbe dhaifu na siwezi kufanya chochote hapa duniani, mpaka kweli na
mimi nikaamini hivyo.” Net alikuwa akimsikiliza kwa kumuhurumia.
Akajifuta machozi.
“Ushawahi
kukaa kwenye jua kali sana mpaka ukachoka, halafu gafla ukahamishwa kwenye
kivuli tena chenye upepo mzuri? Kitu cha
kwanza utakachotamani ni maji ya kunywa ya baridi. Sio kwamba hata ukipewa soda
hutakunywa, utakunywa tu. Lakini kitakachoburudisha moyo wako ni maji pekee.
Ndivyo ilivyo kwangu. Utulivu wa akili ninaopata ukiwepo hapa na mimi,
unanifanya nilale. Ndio maana sitaki hata uniguse wakati ukiondoka, ili angalau
pakuche nikiwa katika ile hali ya utulivu akilini mwangu.” Net alianza kuelewa.
“Mama
alikupeleka wapi siku hiyo alipokutoa kwa bibi na babu kijijini?” Net akauliza
taratibu. “Ilikuwa siku ya maajabu sana kwangu siku hiyo. Alinipeleka kwa baba
yangu. Tena hata sikutambulishwa. Baada ya kushindwa kufungua mlango
aliponiambia tumefika, ilimbidi ashuke aje kunifungulia yeye. Lilikuwa nikosa
ambalo alishindwa kunisamehe. Alifungua mlango kwa hasira. Akanipiga sana,
kisha akanitupia nje ya gari huku akinifinya mdomo nisilie hata kidogo.
Alinivuta mpaka ndani ya hiyo nyumba ambayo alipofunguliwa mlango tuliingia
huku ananivuta kama mwizi, na kuniacha hapo kati kati ya sebule nikiwa
nimesimama na wenyeji wakiangalia tv. Sikuambiwa
kuwa yule ndiye baba yangu ila nilimsikia akimwambia baba, ‘nimekuletea jaluo mwenzako, sijui kabila
gani! Mtajijua wenyewe’. Kisha akaondoka na kuniacha pale.” Tunda
akajifuta machozi.
“Pale pale pakaibuka tena ugomvi kuwa sitakiwi na pale tena.
Baba alikuwa na yeye ameoa, mkewe alianzisha zogo jingine pale pale akitaka
niondolewe usiku uleule, lakini nikafanikiwa kuishi pale kwa muda wa miaka
miwili iliyokuwa migumu na iliyosaidia kuharibu akili yangu kabisa, mpaka
nilipotolewa pale nusu mfu na jirani kama nilivyotolewa nusu mfu nyumbani kwa
mpenzi wako.” Net akakunja uso.
“Mpenzi
wangu mimi?!” “Ndiyo.” “Nani mpenzi wangu!?” “Si Sera? Au mliachana?” “Sera
hakuwahi kuwa mpenzi wangu bwana.” Tunda akakunja uso kidogo. “Sisemi Samatha
yule mdogo, nasemea Sera yule mkubwa.” “Namfahamu Sera na Samatha vizuri sana.”
“Sasa mbona unakataa kama sio mpenzi wako wakati ulikuwa ukija kumuona pale
hata mara mbili kwa siku?” “Nani alikwambia nilikuwa nikimfuata Sera?” Tunda akawa
kama ameshachanganywa kidogo.
“Net
jamani!? Au umesahau?” “Nakumbuka kila kitu. Lakini sikuwa nikimfuata Sera.”
Tunda akatulia kidogo kama anayefikiria. “Kwanza wewe umejuaje kama nilikuwa
nikifika pale? Maana kila nilipokuwa nikija sikuwa nikikuona?” Net akauliza. “Mle
ndani ya ile nyumba, ulikuwa kama lulu! Zilikuwa zikianza kutajwa sifa zako,
hamtahema. Mimi mwenyewe nilikufahamu hata kabla sijakuona.” Tunda akacheka
kidogo.
“Siku ya
kwanza unakumbuka nani alikufungulia mlango?” Net akatabasamu kama anayefikiria
kidogo. “Siwezi kusahau.” “Basi ulipoingia tu na Joe, nilipokuona tu nikajua
ndio Net aliyekuwa akisifiwa mle ndani.” Net akacheka.
“Sera
alikupenda sana. Mliishia wapi?” “Kwani tulianzia wapi?” “Net!?” “Nini?”
“Safari zote zile ulizokuwa ukija pale, ukamfanya Sera achanganyikiwe! Mpaka
wazazi wake walijua mtaoana!” “Walijichanganya wenyewe tu.” “Mmmh! Siamini kama
hapakuwa na mwendelezo wa yale mahusiano. Uliwaalika mpaka nyumbani kwenu?”
“Tunda! Hebu achana na hayo. Naona wote hamkuwa mmeelewa. Kwanza nijibu kwa
nini ulikuwa unanikimbia?” “Weee! Nilipigwa marufuku mwenzio, tena kwa
kumwagiwa ndoo ya maji nikiwa nimelala.” Net akashangaa.
“Kwa
nini!?” “Wewe unacheza na wale watoto nini? Halafu walivyo washenzi, eti siku
inayofuata wewe ulinikuta naingiza godoro ndani baada ya kutoka kuanika baada
ya wao kunimwangia maji wakati nimelala, tena nakumbuka ukauliza, ‘vipi mbona kama kuna wanao hama?’. Eti
wakakwambia huwa nakojoa kitandani. Hivi uliamini?” “Mimi sio mjinga Tunda.
Nilishawasoma watu wote pale ndani, kwa muda mfupi niliwafahamu kwa asilimia
kubwa sana. Kila nilichokuwa nikiambiwa nilikuwa nikijua ni kweli ama sivyo.”
Tunda akatulia kama anayefikiria.
“Unajua
siku uliyoondoka, nilikuja pale kutaka kuongea na wewe?” Tunda alishtuka
kidogo. Akageuka nyuma na pembeni kisha akajishika kifuani. “Mimi?” “Ndiyo.”
“Unamaanisha mimi Tunda?” “Acha utundu Tunda, tupo wawili tu hapa ndani. Kwani
hawakukwambia kama nilimuomba shangazi yako kuja kesho yake, usiku ili
kuzungumza na wewe?” Tunda afikiria harakaharaka.
“Basi
wewe ndiye uliyenisababishia matatizo Net!” “Nilifanya nini?” “Kama uliwaambia
wale, ujue wewe ndio sababu kubwa yakutoka pale nusu mfu.” “Nusu mfu tena?
Wakati mimi nilipofika siku hiyo kuja kuzungumza na wewe kama nilivyowaomba,
waliniambia ulitoroka tena baada ya kuiba!” Tunda akaumia sana, Net akamuona
anaguna.
“Kwani
ilikuwaje?” “Aiii! Haina hata haja yakusimulia, haisaidii chochote.” “Mimi
nataka kujua.” “Tuache tu.” “Kwa hiyo unataka mimi nibaki na sifa yako ya
wizi?” “Nina madhambi mengi sana unayoyajua Net. Kutokuwa mwizi pekee,
hakutasafisha uozo wangu. Tuache tu.” “Siwezi kuacha kama mimi ndiye
niliyekusababishia matatizo Tunda. Nieleze kilichotokea.” Tunda akatulia
kidogo, usoni alibadilika kabisa.
“Tunda?”
Net akaita akitaka Tunda amueleze tu. Tunda akaona amuelezee tu. “Tuliamka siku
ile, shangazi akilalamika amepoteza mkufu wake wa dhahabu. Yeye na watoto wake
wote walisema mara ya mwisho waliona huo mkufu usiku uliopita wakati wanakuja kwenu.
Kwa hiyo tukabaki wezi ni mimi na Nyangeta. Haa!” Tunda akashtuka. “Nini?”
“Jamani Nyange! Hivi bado yupo?” “Sijui. Mimi mwenyewe sikurudi tena pale.”
“Kwa nini!?” Tunda akauliza kwa mshangao.
“Aaah!”
Net alitaka asitoe sababu ya msingi iliyomfanya asirudi tena nyumbani kwa kina
Sera. “Lakini hata hivyo muda wangu wa kurudi chuo ulikuwa umeshafika.
Niliondoka nchini.” “Shule iliisha sasa?” “Nashukuru Mungu iliisha. Niambie
nini kilitokea.” “Kuhusu nini tena?” “Sababu ya kukutoa pale nusu mfu.” “Husahau!?”
“Hilo ndilo tatizo langu Tunda. Sisahu na nikikusudia kufanya jambo fulani, ni
lazima nifanikishe. Hata kama lina gharama kubwa kiasi gani, lazima nilitimize.
Mpaka bibi yangu huwa ananihurumia.” “Lakini ndio maana umefanikiwa Net”
“Nimefanikiwa kwenye nini?” “Ona bishara ulizo nazo.” Net akatabasamu.
“Chakwanza nataka uelewe zile ni biashara za mama
yangu. Mimi ni mwajiriwa kama wewe tu. Nampa tu mawazo kama hivi unavyonishauri
mimi, na yeye anachagua kipi chakutendea kazi, basi.” “Lakini kwa hapo ulipo
Net, ni kama huna kitu unataka maishani.” Net akatabasamu akabaki akifikiria
kidogo.
“Nikikwambia pesa hainunui kila kitu hapa duniani,
huwezi kuniamini.” “Mimi tena? Naamini sana tu Net. Nimezihangaikia hizo pesa
jamani! Sitakaa nikasahau maishani. Nilidhani nikiwa na maisha fulani ndio
itanisaidia kurudisha ile hali ya kabla sijatolewa kwa bibi yangu kwa mara ya
kwanza, lakini wapi Net! Nimetafuta kurudisha ile hali kwa mateso sana, lakini
sijafanikiwa. Nimeishia kudhalilika tu.” Tunda aliongea kinyonge.
“Sijui nilipatwa na nini!? Nilikuwa kama mbwa, tena
mbwa wa uswahilini. Mchafu kuliko, sijui nini!” Tunda akatulia kidogo. Net naye
kimya. Hapo hakuongeza.
“Turudi kwenye swali lako Net.” “Ehe!” Tunda akajifuta machozi. “Kweli wewe
king’ang’anizi.” “Sitaondoka leo mpaka nijue.” “Haya bwana. Basi yule Mzee
akaanza kutukaba mimi na Nyange, tutoe huo mkufu wa mkewe.” Tunda akatulia
kidogo.
“Sikukuzwa au kulelewa kwenye mazingira ya
kusikilizwa Net, kwa hiyo sijui kabisa kujitetea. Vile mtu anavyosema juu
yangu, huwa mara nyingi inabaki vile vile. Kwa kuwa siwezi kukanusha, hasa pale
ninaposhutumiwa moja kwa moja. Nakuwa kama ninapatwa na ganzi mwili mzima.
Mwenzangu Nyangeta alijitetea haraka haraka akapona. Mimi nikabaki kama bubu.
Basi pale mimi ndio nikaonekana mwizi moja kwa moja.”
“Yule Mzee akaamuru iletwe mifuko yangu ya nguo.
Maana nilikuwa na mifuko miwili ya plastiki, ndio nilikuwa nikiwekea vitu
vyangu vyote. Hatukuruhusiwa kutumia makabati ya mle ndani chumbani.” “Kwa
nini!?” Tunda akacheka kidogo. “Mimi waliniambia wanaogopa naweza kusababisha
wadudu kwenye hayo makabati ya ukutani. Yalikuwa yamejengewa kwenye ukuta.
Mazuri kweli. Lakini yalikuwa yakifungwa kabisa na funguo ambazo alikuwa
akitunza shangazi. Kwa hiyo tukawa tunaweka vitu vyetu kwenye mifuko tu ya
plastiki.” Net alibaki na mshangao.
“Basi mifuko yangu ikaletwa. Walipomwaga chini vitu
vyangu ili kukagua, ule mkufu wa shangazi si ukaanguka kutoka kwenye huo mfuko
wangu! Tena mfuko wa kwanza tu, hata hawakwenda wa pili. Net! Nilipigwa mimi.
Nafikiri Mungu alinihurumia. Maana alinipiga sehemu iliyonisaidia kupoteza
fahamu, sikujua kinachoendelea mpaka nilipopata fahamu nikiwa hospitalini.”
“Nilijua nilipigwa sana kutokana na maumivu
niliyokuwa nayo, na jinsi nilivyokuwa nimepasuka. Nilipasuka hapa juu ya macho,
midomo, mbavu zilivunjika. Mkono huu ulivunjika, mpaka mifupa ilikuwa
ikionekana kwa nje kuwa imetengana. Bega lilitenguka.”
“Nilikaa hospitalini
zaidi ya mwezi sababu ya kuvuja damu kwenye mbavu, na kutobolewa kuwekwa vyuma,
kama mshikaki. Halafu sikuwa na pakwenda. Kila mahali nimefukuzwa. Ikabidi
kuomba kuendelea kukaa pale pale hospitalini mpaka nipone. Mtu aliyekuwepo hapo kuniuguza ni baba, naye alifungwa
nikiwa bado hospitalini.” Tunda alinyamaza na kufuta machozi.
“Na yeye ni mtu mwingine aliyenikubali vile
nilivyo. Mpaka nilikuwa namshangaa. Alikuwa akipewa habari zangu mbaya tupu,
lakini wakati wote alinithamini. Nililia sana baada ya kumkuta tena kwa mara ya
pili pembeni ya kitanda changu hospitalini.” “Mara ya pili?” Net akauliza.
“Mara ya kwanza ni pale mama aliponiacha
hospitalini baada ya kunitoa mimba. Nilikuwa peke yangu na barua aliyokuwa
ameniachia niisome mara baada ya kuzinduka usingizini, akinitaarifu yeye na
ndugu zake wote hawataki kuniona tena, kwa kosa la kuwa na mahusiano na mumewe.
Lakini hata baba alipoambiwa hilo kosa langu, alikuja kuniuguza mpaka
nikatoka.” Tunda alitulia akainama kwa
muda.
Kisha akaendelea. “Na mara ya pili nilizinduka
hospitalini nikamkuta baba tu, tena hata hapo nikiwa ninatuhumiwa za wizi wa
huo mkufu wa shangazi. Lakini mara zote hizo baba amekuwa akinihudumia bila
shida. Siku aliyokuwa ananiaga kuwa anaweza asirudi tena, aliniambia nisiwahi kufikiri kama mimi ni mtoto wa bahati mbaya. Alinieleza
kuanzia mwanzo wa kuzaliwa kwangu mpaka nilipoishia kijijini.”
“Ilikuwaje?” Tunda alimsimulia Net kila kitu juu ya
baba yake na mama yake, mpaka alipoenda kutelekezwa kijijini. “Daah!
Unahistoria ngumu Tunda!” “Lakini wewe pia ulichangia Net!” Net akaanza
kucheka. “Jamani mimi nilifanyaje?” “Nikifikiria juu ya kile kisa cha mkufu wa
shangazi, sasa hivi ndio naelewa kuwa ni mpango shangazi alifanya na wanae.
Walimtumia yule baba kuniadhibu bila yule baba mwenyewe kujua kinachoendelea.”
Net hakuwa ameelewa vizuri.
“Ukweli kile kitendo cha kuwa na mahusiano na mume
wa mama yangu kilinipotezea uaminifu kwa watu wengi sana. Hakuna aliyeniamini
na mumewe au hata marafiki zao wa kiume. Shangazi mwenyewe alinipiga marufuku
hata kupita pale sebuleni mumewe akiwepo. Sasa na wewe walijua kabisa ungemuoa
Sera, kwa hiyo hawakutaka mimi niwe hata nakuona. Waliniambia kila unapokuja
niwe natoka nje kabisa, nisirudi mpaka wewe utakapokuwa umeondoka.” Hapo Net
akawa ameelewa.
“Samahani sana Tunda. Sikukusudia kukusababishia
matatizo.” “Wala usijisikie vibaya Net. Nilikuwa navuna nilichopanda. Nilikuwa
nalipa uovu wangu.” “Sio kwa njia hiyo Tunda.” Tunda akacheka tena taratibu,
huku akifikiria.
Akawa kama amekumbuka. “Ulitaka kuniambia nini
Net?” Tunda alinyanyua uso, nakumuuliza. “Tuache tu. Sasa hivi haina maana
tena.” “Kwa nini unasema hivyo!?” “Tunda wa wakati ule niliyetaka kuzungumza
naye sio Tunda huyu wa sasa. Umebadilika sana Tunda. Hata nikikwambia sasa
hivi, haitaleta maana tena.” Tunda aliumia sana moyoni.
“Naelewa Net. Naelewa kabisa, wala sikatai. Mimi
mwenyewe wakati mwingine sijitambui kabisa. Nahisi ni kama mtu ninayeangalia
watu wengi tofauti tofauti ndani ya mwili mmoja wakiishi kwa kupeana zamu. Mimi
mwenyewe sijitambui. Nimepotea kabisa. Hata sasa hivi hapa sijui anayeishi kwa
kutumia huu mwili wangu ni nani! Kuna umbali mkubwa sana kati yangu mimi
binafsi na watu wote unaowafahamu kupitia huu mwili wangu. Kuna mambo nilikuwa
nikifanya mpaka mimi mwenyewe nilikuwa naogopa Net! Nilikuwa nikirudi nyumbani
kwangu nashindwa hata kulala kwa mshtuko.” Tunda akaendelea kuongea huku
akivuta kumbukumbu taratibu.
“Ni kweli mwanadamu ana uwezo mkubwa sana. Siku
chache zilizopita kama mtu angeniambia wale kina Anna, Judy, Irini, sijui
Pamela, Nancy, Mwajuma, Latifa, Fina,
Lina wanaweza kuja kuwa mimi nikakaa ofisini nikafanya kitu kinachoweza
kuonekana, nisingekubali. Nilishapotea kabisa katika ulimwengu mingi tofauti,
tofauti.” Tunda aliongea taratibu huku ameinama akichezea vidole vyake.
“Sikuwahi kujua kama kuna siku naweza kula chakula
kwa pesa ninayoweza kutengeneza kupitia kuajiriwa kihalali na si kwa kutumia
kulala na watu, tena wengine walevi, wavuta bangi, wengine wachafu huwezi hata
kuvumilia harufu zao, nisingeamini. Nashindwa kujielewa kama huyu tena sasa
hivi kwenye huu mwili wangu kama ni mtu mwingine kati ya wale watu wengi ambao
wanaishi kwenye huu mwili wangu au la!”
“Nikiwa peke yangu naogopa nasema itakuwaje wale
watu wengine kina Nancy wakaamua kurudi tena, wakaishi? Nina hofu ya kurudia
yale maisha Net. Pesa mnayonilipa wewe na mama yako kwa kuwafanyia kazi mwezi
mzima, nilikuwa na uwezo wakuitengeneza hata ndani ya siku mbili, au moja.
Inategemea na mtu niliye naye. Lakini siyo maisha ninayotamani kuja kurudia
Net. Yanatisha.” “Unao uwezo wakutorudia tena Tunda.” “Sidhani kama ni uamuzi
wangu Net. Sijui.” “Kwa nini unasema hivyo?” Tunda alifikiria kidogo kisha
akacheka na kuguna.
“Unajua watu wote wananilaumu kwa nini nililala na
mume wa mama yangu. Najua hata wewe utakuwa huelewi. Lakini hakuna mtu hata
mmoja aliyewahi kuniuliza ilikuwaje! Hata baba mwenyewe hakuniuliza. Kila mtu
ananilaumu na kunishangaa.” “Ilikuwaje Tunda?” “Kwa
nini unaniuliza leo Net, wakati ulinifahamu muda mrefu tu?” Tunda
akauliza kwa upole huku akijifuta machozi.
“Kumbuka hatufahamiani Tunda. Nimekufahamu kwa
kutambulishwa na watu. Na kote nimekuwa nikitambulishwa majina tofauti tofauti,
nimeamua kubaki na la Tunda, kwa kuwa ndilo nililotambulishwa na ndugu zako. Na
kila nilipokutana na wewe nilikuta upo kwenye matatizo makubwa sana, au tuseme
mazingira ambayo hayakuniruhusu hata kukusalimia kwa kukushika mkono. Nina
habari zako nyingi na nasikitika zote ni mbaya na ni za kuogopesha.” Net
akaendelea.
“Sijui
nauliza nini naacha nini? Nashindwa naanzia salamu kwa kukushika mkono kwanza
ndipo nikuulize jina lako, au nijipe muda labda ipo siku nitajua wewe ni nani!
Nina hofu sijui mwisho wa yote hayo naishia kumfahamu Tunda, au Judy! Yeyote
yule sasa hivi aliyepo ndani yako sikuwa na ujasiri wa kukimbilia
kukuuliza ilikuwaje ukawa na mahusiano
na baba yako wa kambo, wakati nina maswali makubwa sana na ya msingi nilitaka
kujibiwa kabla ya swali kama hili ambalo nilijua nikipata majibu ya maswali ya
msingi, mengine yangejijibu yenyewe.” Net akaendelea.
“Huwa sipendi na ninahofia sana kufikia mwisho wa
maamuzi ya jambo lolote lile maishani mwangu, kwa kuwa ninatatizo la kutosahau
na huwa ni mgumu sana kurudi nyuma. Siwezi na sijawahi. Nikifika mwisho wa
jambo, nikakubali kuwa hapo ni mwisho ujue hakuna mwanadamu mwingine anayeweza
isipokuwa Mungu ameingilia kati. Kwa kuwa huwa natumia kila kitu Mungu
alichonipa katika kukabiliana na mambo yangu, na huwa ni mvumilivu sana.”
“Mpaka mimi nikikwambia nimefika mwisho, ujue
hakuna mwanadamu angeweza kuvumilia. Ndio maana naogopa sana kufika kwenye
kumuhukumu mtu. Kama ni mwanadamu, nataka kumjua si kwa maneno yake tu bali
nataka nimfahamu vile alivyo kwa kuishi naye. Nione na kujua jinsi alipopita
mpaka akafika hapo, na kujaribu kuangalia anatumia vipi nafasi ya pili ambayo
Mungu amempa? Hapo ndipo nachora mstari, si vinginevyo.” Tunda alikuwa ametulia
akimsikiliza Net.
“Leo nimepata ujasiri wa kukuliza kwa kuwa kwanza
nimeona umekuwa tayari wewe mwenyewe kuongea. Nimehisi umeniamini, kitu
kilichonifurahisha. Sikutaka mimi nigeuke kuwa hakimu wako, kukuhoji. Nilijua ipo
siku kama utataka, basi utazungumza na mimi. Lakini sikutaka mimi ndio niwe
naanza kukukera na maswali, nilijua utakosa raha. Ndio maana nilikuwa
nikinyamaza kabisa.” “Asante Net. Asante sana.” Tunda
akajifuta machozi, nakujiona mdogo zaidi. Aliona vile Net alivyokuwa
akimfikiria bila majibu. Akatamani kujua mawazo yake juu yake, lakini Net
alionekana ni mtu makini sana. Hakuwa mropokaji hata kidogo na alikuwa makini
sana kwa kila anachoongea.
“Tunda!” “Abee!” “Nakusikiliza.” Ilikuwa ni mtu wa
kwanza maishani mwake kutaka kumsikiliza Tunda, bila hukumu. Tena mtu wa maana,
msomi, pesa ipo na tena mwenye heshima kwenye jamii! Japokuwa alijua uozo wake
tena kwa kushuhudia, lakini bado alimuonyesha kutaka kumsikiliza. Tunda
aliinama kwa muda akaficha uso wake nakuanza kulia kwa uchungu sana.
Alilia sana hapo mbele ya Net nakushindwa
kujisaidia. Kimya kimya ila kwa kwikwi. Aliruhusu maumivu yote aliyokuwa
ameyaficha moyoni mwake akivumilia akijua kesho itakuwa nafuu, aliyatoa siku
hiyo. Alilia bila kunyamaza. Picha ya mapito yake yote tokea utoto mpaka
siku Net anamtoa kwenye mvua na radi
ilimjia, na kuendelea kulia. Alipoona anashindwa kunyamaza akaamua kuingia
bafuni kuoga.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Alitoka
akiwa amevaa nguo zake za kulalia nzuri na huku amejifunika shuka. “Nasikia
baridi sana. Naomba nilale tutaongea wakati mwingine.” Tunda akapanda kitandani
na kujifunika blangeti. Ulikuwa msimu wa baridi kali sana jijini Arusha. “Naweza
kukusubiri mpaka utakapo lala.” Net akasogea pale kitandani akakaa pembeni
yake. Akabaki akimwangalia Tunda kwa utulivu na macho yake yaliyokuwa
yakimpeleka kasi Sera, binamu wa Tunda. Tunda alikuwa ndani ya mablangeti
akitetemeka baridi.
Net akavuta
blangeti vizuri na kumfunika zaidi. Tunda aliendelea kujikunja ndani ya lile
blangeti huku akificha kila kiongo chake ndani, akabakiza uso tu. “Asante.” Net
alitoa tabasamu. “Ninayo machine ndogo ya joto, {Space Heater} pale nyumbani,
kesho nitakuletea.” “Na wewe utatumia nini?” “Mimi sio muoga wa baridi kama
wewe. Jione unavyo tetemeka.” Tunda akatabasamu.
“Unawasiliana
na mama?” Net akauliza. “Nilikwambia jinsi alivyoniambia Net. Mama alisema
nisikanyage tena nyumbani kwake. Hata hivyo hatukuwahi kuwa na mahusiano yeyote
na mama hata tulivyokuwa tukiishi pamoja. Nilimsaidia sana kumlelea yule mtoto
wake wa pili, kwa hiyo hapo ilimbidi awe akizungumza na mimi, kunipa maelekezo
ya mtoto wake na si vinginevyo. Na hiyo ndiyo sababu kubwa iliyonifanya niwe
karibu na mumewe.” Tunda akatulia kidogo.
“Yeye
alikuwa akifanya nini?” “Ni nesi. Nilimuacha akifanya kazi katika hospitali ya
Muhimbili lakini pia alikuwa na miradi iliyokuwa ikimfanya hatulii nyumbani.
Alikuwa akiingia kazini mida tofauti tofauti. Na kama hatakuwepo kazini, basi
yupo kwenye biashara au miradi yake. Halafu walikuwa pia na msichana wa kazi
naye alikuwa akiishi humo humo ndani. Ila alikuwa muhuni sana. Hatulii
ndani. Mama alipokuwa akiondoka na yeye
alikuwa akiondoka, anaaga labda anaenda kusuka au dukani. Na akitoka hapo
kurudi ni majaliwa.”
“Sasa
huyo baba hakuwa akimuuliza?” Net akaendelea kudodosa japo alishaambiwa
wataendelea wakati mwingine. Ila alikusudia kujibiwa usiku huo. Akaendeleza
taratibu. “Hapana. Ndio muda na yeye alikuwa akiusubiri kwa hamu sana. Kwani
ndio tulikuwa tukibaki naye. Mimi na yeye tu.” Tunda akatulia kidogo.
“Hatukuanzia
kwenye kufanya mapenzi moja kwa moja! Alihakikisha anajenga mazoea ambayo
hakuna mtu alimtilia mashaka. Alimuonyesha mama kuwa ananipenda kama mtoto
wake. Kutoka katika mateso makali ya mama wa kambo, nikaangukia kwenye mikono
ya baba wa kambo aliyekuwa akinipakata na kunitekenya wakati wote.”
“Nilikwambia
nilitolewa kwa baba nikiwa nusu mfu kwa kupigwa. Baba alikuwa na mtoto mwingine
aliyekuwa akiitwa Chale. Yule mtoto alikuwa mwizi Net, hawezi kujisaidia.
Alikuwa akiiba kila pesa anayoona mbele yake. Sasa mara ya mwisho aliiba pesa
kwenye pochi ya mama yake, akanisingizia mimi. Na yule mama alikuwa akijua
kupiga, na ana mkono mwepesi sana. Basi. Alinipiga siku hiyo zaidi ya siku
zote, wakaenda kunitupa nje, majirani wakanipeleka hospitalini. Bibi akaja
kunichukua, nakunirudisha kijijini.” Tunda akatulia kidogo.
“Kosa
alilolifanya bibi, akiwa na nia nzuri, akampigia simu huyo mume wa mama ambaye
hata hakuwa akijua kama mama ana mtoto mwingine.” “Kwani hamkuwahi kuonana?”
Net akauliza.
“Alishawahi
kufika kijijini wakati anamlipia mahari mama, akanitambulisha kama mimi ni
mdogo wake.” Net akashangaa sana. “Basi. Bibi akanitambulisha kwa yule baba
mbele ya mama, akitaka wawe wanatuma pesa za matumizi angalau kila mwezi. Chakushangaza kila mtu mpaka mama, yule baba akanipokea
kwa upendo. Akataka nirudi nao mjini ili wanisomeshe.” Tunda akajifuta
machozi.
“Huwezi
amini hayo mapokezi yake! Alikuwa akinipenda sana. Akiona mama ananigombesha,
basi yeye ananibembeleza na kunitetea hata kwa mama, akimuelewesha kuwa mimi
bado ni mdogo. Natakiwa nifundishwe. Yale mateso ya kwa mama wa kambo, huku
ikawa faraja ya baba wa kambo. Nilikuwa nikivalishwa vizuri. Vyakula vya kila
namna ananinunulia. Akiona kama kuna chakula ambacho yeye hajakipenda mle
ndani, basi alikuwa akitutoa na Tom, mtoto wao mkubwa, kwenda kula nje. Chips
yai na kuku.”
“Wakati
mwingine alikuwa akitupeleka sehemu tofauti tofauti zakucheza. Mara nyingi mida
ya jioni alikuwa akitupeleka kwenye sehemu zinazo uzwa Icecream. Hata kama ni
siku za shule. Anatoka kutuchukua shuleni, anatupitishia mahali kula au kupata
icecream. Na ilikuwa hivi, kama dereva hakuwa akitufuata kuturudisha nyumbani,
basi ni yeye mwenyewe anatufuata. Tulikuwa tukisoma shule yakulipia, kwa hiyo
kama mzazi alitaka watoto wakae zaidi, unaongeza pesa, mnakaa mpaka saa 12
jioni. Hapo mtasaidiwa kusoma na kunakuwa na michezo tofauti tofauti.” Tunda
akaendelea.
“Sasa
kwa kuwa Tom yeye alikuwa mtundu sana, na alikuwa akicheza mpira wakati mwingi,
basi kila alipokuwa akiingia kwenye gari, alikuwa akiishia kulala njia nzima
wakati tunarudishwa nyumbani. Na hapo yule baba ndipo alipokuwa akipata nafasi
nyingine nzuri ya kunichezea ipasavyo. Kumbuka nilikuwa darasa la nne, sio
mkubwa sana, lakini nilikuwa nikielewa kiasi. Mwanzoni nilikuwa nikifikiri ni
mchezo aliokuwa akicheza akitutekenya mimi na Tom hata mbele ya mama, lakini
niliona mimi inaanza kuwa tofauti.”
“Akijua
jioni hiyo mama haingii kazini, atalala nyumbani, basi lazima atakuja kutufuata
yeye shuleni. Akijiridhisha Tom amelala kabisa kwenye gari, alikuwa
akisimamisha gari pembeni ya barabara na kuniambia nifungue mkanda niruke kiti
cha mbele, kisha anaanza kunichezea. Alianza kwa kunisifia nimeanza kuwa mkubwa
nimuonyeshe matiti yangu huku akinitekenya na kujifanya anashika juu ya gauni
na kucheka cheka.”
“Siku
ambazo tupo nyumbani mama hayupo, akawa anataka niwe nakwenda kuangalia tv
chumbani kwake. Na kwa kuwa nilikuwa nikifeli sana shuleni, basi alitaka niwe
nafanya kazi za shule pembeni yake. Kumbuka nilitoka kijijini sijui kuzungumza
hata Kiswahili. Nikapelekwa kwa baba, nikaishi huko miaka miwili ya mateso.
Darasani wanafundisha Kiswahili kitupu na kingereza. Nimetolewa hapo darasa la
nne, sijajifunza chochote kwa hiyo miaka miwili. Nikahamishiwa kwa mama,
nikapelekwa shule ya kingereza kitupu. Hakuna hata wakumuomba maji ya kunywa
kwa kilugha au kiswahili. Nikajua kuongea kingereza kwa mawasiliano tu, lakini
hakuna ninachoeleweka darasani. Kumbuka hapo nipo darasa la 4 ambalo ilibidi
nirudie, sababu kwanza sikufanya mitihani ya kitaifa ya darasa la nne kuingia la tano kule kwa baba. Mkewe
alinipiga na kunivunja mkono huu wa kulia.” “Tunda!” Net akazidi kushangaa.
“Kweli
Net. Mama Chale au mke wa baba, alikuwa mama wa nyumbani, halafu baba yeye anakwenda
kazini asubuhi mpaka usiku, hapo bado safari za kikazi za baba. Kwa hiyo
nikaishia kulelewa na mama wa kambo, huyo mama Chale. Alikuwa akinitesa yule
mama, siwezi kusoma wala kufikiria. Kwenda shule ni siku ambazo anaamua yeye.
Mateso, akili ikawa haitulii kabisa. Nilikuwa kama mwehu kwa hofu. Akinikuta
nimekaa sehemu, kosa. Atanipiga wee na kunipa kazi. Nikifanya asivyopenda yeye,
pia kosa. Atanipiga tena. Wenzangu walifanya mitihani ya darasa la nne, mimi
mkono umefugwa POP kwa kipigo.” “Pole sana Tunda.”
“Asante.
Haya, sasa huku kwa mama nako sina nilichokuwa nikielewa. Nafeli kwenye hiyo
shule ya kingereza kitupu. Ndio yule baba naona akapata mwanya huo. Akamwambia
mama yeye atakuwa akinisimamia masomo. Yaani ni kama alikuwa akijitengenezea
njia yakutoshtukiwa. Basi ikawa inajulikana kwamba kila nikitoka shule, lazima
baba anisimamie kufanya homework zangu.”
“Hapo
sasa ikawa inategemea na ratiba ya mama au alipo yule msichana wa kazi. Inaweza
kuwa sebuleni kama tupo mimi na yeye tu au chumbani kwake. Kama nilivyokwambia.
Tom alipenda sana mpira. Kila alipokuwa akitoka shule, alikuwa akiingia mtaani
kucheza. Yeye hakuhimizwa kufanya homework. Alikuwa anataka awe anatoka hapo
ili atupishe. Na yule msichana ni kama nilivyokwambia kuwepo kwake nyumbani ni
mpaka ajue mama yupo au anakaribia kurudi nyumbani.”
“Na ikitokea msichana wa kazi
yupo hapo nyumbani, basi hiyo homework tunaenda kufanya chumbani kwao. Eti
nikiwa na elimu ya darasa la pili ya kijijini, unipe homework niliyofundishwa
kwa lugha ya kingereza darasani! Mimi niliyekuwa nikizungumza kipogolo tu! Hata
Kiswahili sikuwa naongea vizuri. Kwanza niseme sikuwa nikikijua. Nilikwenda
kukijua kule nilipopelekwa kwa baba. Nilijifunza Kiswahili kwa kupigwa.
Alidhani ni kiburi, kumbe sikuwa na muelewa. Ndio msichana wa kazi akamwambia
simuelewi. Ndio kipigo kikageuka kuwa mimi ni mjinga, mzito kuelewa.” “Jamani!”
Net akashangaa.
“Sasa
eti kwa hali hiyo nikaanza hiyo shule ya kingereza, bila msaada wa mtu. Mama ni
mkali, baba anamalengo yake. Usifikiri hata hiyo homework basi alikuwa anania
nifanye?” “Hakuwa akikusaidia?” “Hata kidogo Net. Ukitukuta chumbani, ujue
mikono yake kama haipo kwenye maziwa yangu, basi ataniambia nilale kama
naandika. Yaani nilale kifudifudi. Niweke daftari mbele. Yeye atakaa huko nyuma
yangu. Atanifunua gauni mpaka kiunoni, ataanza kunichezea. Anakwambia usihangaike
tulia tu. Atakuchezea hapo, wakati mwingine anaweza akanitoa hata chupi kabisa
ananichezea tu.”
“Mwanzoni
hakuwa akiniingilia. Ananichezea tu. Ila alikuwa anapenda sana sauti yangu na
nimwangalie. Kwa hiyo alipokuwa akifika juu sana, ananiambia nimwite dad, dad,
mpaka amalize. Hapo sasa anakuwa amenitoa kitandani, amenipakata. Mikono kwenye
sehemu za chupi nyuma. Ananiminya minya.” Tunda aliogopa kusema makalio. Lakini
Net akaelewa.
“Halafu
huku ananinyonya tumaziwa twangu. Basi hapo utamwita dad taratibu huku
anakuchezea mpaka anamaliza. Na usifikiri anamaliza ndio inakuwa basi. Anaweza
kwenda kuoga. Anakwambia endelea na kazi za shule wakati akioga. Niambie Net,
hapo utasoma tena?” “Huwezi. Pole Tunda.” “Nilikuwa nashindwa. Hasira. Na akitoka kuoga anapumzika kidogo, na mikono
yake anapopumzika inakuwa mwilini mwako. Akikuvua nguo ya ndani, ujue hutaivaa
tena mpaka akuruhusu utoke hapo chumbani kwake. Na ujue hapo sio kitu cha muda
mfupi. Ni mpaka aridhike kweli kweli.” Tunda akajifuta machozi.
“Akaanza
kuzoea ile tabia. Baadaye akaanza kuniita usiku chumbani kwake wakati watu wote
wamelala, mama yupo kazini, kisha anavua nguo na kunifundisha vitu vya
kumfanyia. Nilipomwambia naogopa, aliniambia vile mama yangu asivyonipenda,
hataki niwepo pale, yeye ndiye aliyenitoa kijijini na anauwezo wakunirudisha
kwa baba yangu kama sitamfurahisha.”
“Akawa
ananiambi kukaa kwangu pale, kunategemea na kumfurahisha kwangu. Mama alikuwa
akijua kunitukana Net! Bila aibu wala huruma, hata mbele za watu alikuwa
akinitukana. Ndio ikawa silaha ya yule baba Tom. Akawa ananikumbusha vile
ambavyo mama yangu hanipendi. Na vile nilivyoteswa kule kwa baba yangu. Akawa
ananiambia yeye ananipenda. Hata hayo macho mama anayoyaita ni ya paka na
kuyachukia pamoja na weusi wangu, yeye anavipenda ndio maana anapenda
nimwangalie na nimwite dad.”
“Aliniahidi
kunipa vitu vingi, kama nikimfanyia kile anachotaka na kweli alikuwa akininunulia
vitu. Basi. Nikaanza kujifunza jinsi ya kumfanyia anachotaka. Sina mtu wa
kuniuliza hata ninaendeleaje! Hakuna anayenitizama usoni kama nina furaha au
la. Maisha yangu yakawa ni huyo baba tu. Ndiye anayejua kula yangu, soma, na
vaa. Furaha yangu ikawa inategemeana na kumridhisha. Na kweli, akilala ukiwa
umemridhisha, utafurahia jinsi anavyokuwa mstaarabu.”
“Kazi
yangu ikawa ni yeye tu. Nimejawa hofu na wasiwasi wakati wote. Alianza
kunizoeza kumzoea kumtizama akiwa uchi. Akanifundisha mwili wake na viungo
vyake ili kuweza kuvichezea, na kumfurahisha. Na mbaya zaidi hakuwa akitosheka.
Ukidhani umemaliza, anakwambia unamwamsha zaidi. Labda macho au sauti yangu
ndivyo vinamsababisha asitosheke. Hapo inabidi kuanza upya.”
“Maisha
yangu kielimu yakawekwa pembeni kabisa. Nikageuka faraja yake. Nikiingia
chumbani kufanya homework, anafunga mlango, ananitoa nguo, na yeye anatoa nguo,
tv inawashwa kwa sauti ya juu, kazi inaanza mpaka dada aje agonge kuwa chakula
kipo tayari. Hapo ndio anatumwa kwenda kumfuata Tom huko anakocheza mtaani, ili
aje aoge, ale, alale.”
“Na
usifikiri atakuacha usiku ulale kama mama hayupo?” “Anataka mlale naye!?” Net
akauliza kwa mshangao. “Alikuwa anaanza hivi. Nakwenda kulala kama kawaida.
Tulikuwa tunatumia chumba kimoja na Tom. Tom akisha lala, anakuja kuniamsha.
Tena wakati mwingine ananibeba nikiwa nimelala. Akishanifikisha kitandani
kwake, naweza kushtuka kiwa ananivua nguo au anakunyonya sehemu ambayo lazima
uamke tu.”
“Ukishaamka
tu, anataka uanze kumchezea yeye mpaka aridhike. Na usifikiri ni mchezo wa
masaa mawili au ataridhika kwa safari moja! Hapana. Kwa hiyo alikuwa akinimbia
niendelee mpaka nikimuona amelala, nimsafishe, ndipo na mimi nirudi chumbani
kwangu. Haya, akiwa amekwenda muda mfupi usiku, ujue lazima asubuhi atakuja kuniamsha
tena, nimfanyie kabla hajakwenda kazini na mimi hajanipeleka shule.”
“Ikawa
ndio mtindo huo. Mama akiwepo nyumbani week mbili tatu mfululizo, alikuwa
akitutoa mimi na Tom kwenda kutembea na njiani nilimfanyia hivyo. Au siku za
jumamosi ambazo mama yupo nyumbani, alianzisha tuition ambayo hata sikuwa
nikienda. Alimwambia mama amenianzishia ili niwe nafundishwa inisaidie kuelewa
zaidi. Basi, jumamosi yeye hakuwa akienda kazini. Alikuwa ananichukua, kama
hatutaenda ofisini kwake, anaweza hata kunitafutia nyumba za kulala wageni
niende nikamchezee huko mpaka jioni, ndio ananirudisha nyumbani.” Tunda akaanza
kulia.
“Nilikuwa nachoka
Net, sina jinsi nikakwambia ukaelewa.” “Pole Tunda.” “Unachoka mwili mzima. Hulali vizuri. Sehemu pekee
yakupumzika ni shuleni. Na ukifika hapo darasani kwa kuwa sielewi hata
wanachozungumza, basi nikulala tu. Ukumbuke hapo labda niliamshwa kwenye
alfajiri sana ili kumchezea kabla hatujatoka nyumbani. Haya, unaingia darasani
umechoka, na hapo unajua jioni akija kukuchukua kazi inaanza upya. Kwa hiyo
darasani ikawa ndio kama kitanda. Sikuwa nikielewa chochote kwa usingizi na
hofu.” Tunda alitulia kidogo.
“Nilipofika
darasa la saba wakati mama amejifungua, alikwenda kwa bibi kama likizo ya
uzazi. Mbaya zaidi kwangu, alikwenda na yule msichana wa kazi. Kwa hiyo
tukabakia mimi, Tom, yeye na kijana wa kazi ambaye alikuwa akilala kwenye vyumba
vya nje. Hapo ndipo niligeuka kuwa mke wa yule baba kihalali. Kila Tom
alipopitiwa na usingizi, alikuja kunitoa chumbani na kunihamishia chumbani
kwake, na ndipo kipindi hicho alipofanya majaribio ya kuniingilia mpaka
alipofanikiwa.”
“Haikuwa kazi ya siku moja Net. Ilinichukua miezi kuja kuweza,
na kumudu bila maumivu. Kwa kuwa alikuwa baba mkubwa kimaumbile, usitake kujua
maumivu yake.” “Mama yako hakuwahi hata kuhisi!?” Net aliuliza akiwa
anamaumivu, mpaka uso ulikuwa mwekundu.
“Nilikwambia
mama yangu hakuwa na muda na mimi, Net. Hata hivyo alikuwa busy sana na kazi na
biashara zake nyingine. Na yule mzee alikuwa akiniuguza kwa makini sana. Yeye
ndiye alikuwa akitupeleka shule kwa hiyo kabla hajanishusha alihakikisha
ananipa dawa kali sana zakuzuia maumivu. Kwa hiyo sikuwa nikiishi kwa maumivu,
ni pale tu wakati ananifanyia, na labda nikiwa najisaidia. Napo mwanzoni
alikuwa akinipaka mafuta. Na akawa ananiambia kila nikioga, nikakikishe napaka
mafuta huko chini ili pasikauke, au nisiumie wakati najisaidia. Basi. Mchezo
huo ukaendelea.”
“Nilipozoea
na yeye akanogewa, akazua ugonjwa ambao ukawa unajulikana pale shuleni. Basi
anaweza kuja hata katikati ya muda wa shule, ananiombea ruhusa kuwa ananipeleka
kwa daktari wangu. Na ndio akaeleza huo ugonjwa ndio unaosababisha niwe nalala
sana darasani na kuwa nikifeli vile. Basi walimu wote wakanichukulia kama nina
matatizo.” “Haiwezekani Tunda!” Net akashangaa sana.
“Kweli
Net. Basi, akawa anakuja kunichukua. Nakwenda naye alipopaandaa yeye.
Atanitumia mpaka achoke au muda wa kwenda kumchukua na Tom. Ndio tunamchukua
Tom, na kurudi nyumbani. Alinifundisha kumfanyia hapo hapo kwenye gari. Kwa
hiyo anaweza kuja mida ya mchana. Wakati wa chakula. Anakuita nje, unaenda
kumfanyia kwenye gari. Alikuwa na gari kubwa. Vioo vya nyuma alivifanya vikawa
kama silver kwa nje. Inawakaa. Huwezi kuona ndani. Basi. Mnahamia kiti cha
nyuma. Unamuhudumia, akiridhika, narudi darasani na yeye anarudi zake kazini
mpaka tena jioni. Hayo yakawa maisha yangu. Sasa hebu fikiria utoke kufanya
uchafu kama huo, unarudi darasani, hapo utaelewa nini?” “Huwezi. Pole sana
Tunda.”
“Mchezo
wake ukaendelea hivyohivyo mpaka nikaja kuvunja ungo. Na yule baba alikuwa
hawezi kusubiri Net. Hajui siku za hatari zakushika mimba au siku salama. Yeye
anataka kila wakati na ndipo nikapata na hiyo mimba. Kila nilipokuwa
nikimwambia naogopa, au nikimsihi tuache huo mchezo tutakuja kukamatwa, alikuwa
akiniambia hataweza kuacha tena, na nisiwe na wasiwasi hata mama akitukamata,
atanitafutia pakuishi nitakuwa na maisha mazuri.”
“Siku za
jumamosi ndio tution ikawa kisingizio chakututoa pale nyumbani, tunahamia
nyumba za kulala wageni. Ujue hiyo siku nzima ni kufanya naye mapenzi tu.
Atakuchezea siku nzima mpaka aridhike, ndio anakwambia rudi nyumbani. Ananipa
pesa, nachukua taksii. Ukifika nyumbani kama baada ya masaa mawili au matatu,
na yeye ndipo anaingia. Na akiingia hapo anakuwa mkali kweli kweli. Ataniita
mbele ya mama kuniuliza habari za tuition siku hiyo. Kama nimeelewa au nahitaji
msaada zaidi. Yaani yeye ndio akawa wakunifuatilia zaidi. Na alikuwa mkorofi
kweli. Mama mwenyewe alikuwa akimuogopa. Akianza kufoka hapo, nyumba nzima
inatetemeka.”
Tunda
akatoka ndani ya blangeti akakaa. Akavua ile nguo nzito ya juu ya kulalia huku
amempa mgongo Net. Net akashtuka sana. “Ona huko mgongoni.” Tunda alikuwa na
alama nyingi sana mgongoni mwake. “Hata yeye alikuwa akinipiga sana. Siku zile
nilizokuwa nikimwambia nimechoka sitaweza kutoka kwenda kufanya naye mapenzi,
hapo nilikuwa nikivizia mama yupo. Basi alikuwa akitafuta sababu yeyote ile
ilimradi anichape sana, tena mbele ya mama huku akitutishia mimi na mama
atanifukuza mle ndani. Mama naye alikuwa akiniongezea kwa kosa hilo atakalokuwa
amechagua baba Tom siku hiyo.”
“Kama ni
kuvunja kioo cha dirisha au glasi, basi ilimradi tu. Lakini sikuwa na jinsi
Net. Kunakipindi mwili ulikuwa ukichoka. Nilikuwa mtoto na yeye alitaka niwe
nikimuhudumia kila siku. Kumbuka mimi sikuwa nikipata ladha yeyote, kwa hiyo
nilikuwa siishiwi vidonda. Kwa kuwa nilijua hatanifukuza, nilikuwa nikiwageuzia
mgongo wanipige mpaka wachoke ilimradi angalau nijiuguze, vile vidonda vipone,
ili tukianza tena nisiwe naumia.”
“Na
nilipovunja ungo kila nilipokuwa nikijaribu kumdanganya nipo kwenye siku zangu
haamini mpaka ahakikishe. Kwa hiyo pia nikawa najikata hata kidole napaka
kwenye pedi kumdanganya nipo kwenye siku zangu, ilimradi nipumzike kuingiliwa.
Labda nimchezee tu aridhike au aniache kabisa.”
“Nilipofika
kidato cha kwanza nikaamua kuachana na huo mchezo na nimwambie mama, nilikosea
sana nilipomwambia nia yangu. Akaniwahi kunisemea kwa mama kuwa usiku uliopita
wakati mama yupo kazini, nilitoraka nyumbani sikurudi mpaka asubuhi hiyo.”
“Jamani
sitakaa nikasahu kipigo alichonipa yule mwanamke nakunifungasha mpaka kwa
shangazi yake. Sio bibi. Shangazi yake ambaye hata sikuwa namfahamu. Kijijini
huko, hamna hata umeme. Nilikaa huko karibia mwezi. Hamna chakula, hali mbaya
hata maji ni shida. Nikajua mama alinipeleka kule makusudi. Halafu huyo
shangazi yake mwenyewe alikuwa mzee, hajiwezi. Lakini ikabidi kukaa
hivyohivyo.”
“Nikaishia kuja kuchukuliwa tena na yule yule baba na hapo ndipo
hapo aliponihakikishia sina haki juu ya huu mwili wangu, isipokuwa yeye. Net!
Yule baba alinifanya vile atakavyo. Yeye alipanga ni muda gani na wakati gani
atumie huu mwili wangu. Huku akinihakikishia kuwa yeye ndio aliyebaki kuwa
mkombozi wangu. Na ndipo nikashika na hiyo mimba.” Net
alivuta pumzi kwa nguvu na kufikicha macho yake. Alinyoosha mkono na kushika
yale makovu ya majeraha ya Tunda mgongoni kwake, taratibu sana kama
anayefikiria kitu. Tunda alisikia faraja ya ajabu. Machozi yalikuwa yakimtoka
kama mvua.
Japokuwa
kulikuwa na baridi sana, lakini alitamani Net asitoe mkono wake mgongoni mwake.
Net aliendelea kupitisha vidole vyake taratibu mgongoni kwa Tunda, akishika
kila kovu taratibu. “Pole sana Tunda.” Alijibiwa maswali yaliyokuwa yakimsumbua
kwa asilimia 90. Alimrudishia lile shati
bila Tunda kugeuka, kisha Tunda akavaa vizuri ndipo alipogeuka na
kujilaza tena. Net akamfunika tena kila mahali, kisha akajinyoosha pembeni yake
akalala pembeni yake, huku akimwangalia.
“Tunda!”
Akamwita taratibu. Tunda akanyanyua uso
kidogo kutoka kwenye blangeti na kumtizama Net, kwa macho yake
yaliyokuwa yakimchanganya sana Net tokea siku ya kwanza alipomuona. “Ulishaenda
kumuona baba gerezani?” “Sijamuona tena tokea siku
ya mwisho aliponiacha pale hospitalini. Hata sijui yupo gereza gani!” “Kwa
nini hukutafuta kujua?” “Wazo lilinijia Net. Nilitamani sana kumtafuta, japo
kumwambia nilitoka hospitalini, na kumuonyesha ninaendelea vizuri. Lakini
niliogopa.”
“Kwa
nini uliogopa tena?” Net hakuwa anaelewa.
“Kwa kuwa aliniachia pesa ndogo sana Net. Nilijua angeniona tu na hali
ile angekuwa na maswali mengi ambayo nisingekuwa tayari kuyajibu. Mojawapo
najua angetaka kujua nafanya kazi gani, na mimi sikutaka kumdanganya mwanadamu
mmoja tu aliyenipokea maishani mwake vile nilivyo. Tena wakati wote tumekutanishwa
kwenye mazingira ambayo yote nimekamatwa na uhalifu, na pia sikutaka kumwambia
ukweli wa maisha machafu niliyokuwa nikiishi kuhofia kumuongezea machungu akiwa
gerezani. Niliona ni heri niache tu.” Net akatulia kidogo kama aliyeridhika na
ile sababu.
Kisha
akauliza tena. “Ulikwenda wapi baada ya kutoka hospitalini?” “Naomba
nisikwambie Net. Tafadhali.” “Kwa nini?” “Inatosha.” Net akabaki akimwangalia
Tunda, Tunda akajifunika vizuri na kuficha uso wake, akabakiza sehemu ndogo
sana ya macho ambayo hakutaka kumtizama tena Net, akaangalia chini.
“Nikwambie
siri yangu?” Tunda alishtuka sana. “Uniambie mimi siri yako?!” “Ndiyo wewe
Tunda.” Tunda akiwa na wasiwasi asijue ajibu nini, akaamua anyamaze. “Ushajiuliza
ni kwa nini tunapokuwa ofisini mara kwa mara napenda usiwe unanipa ujumbe kwa
simu, bali uje ofisini kwangu wakati kuna simu ya mezani unaweza kunipigia tu
tukaongea?” Swali lilikuwa gumu sana kwa Tunda ambaye hakuwahi kufanya kazi
kwenye ofisi yeyote. Yeye mwenyewe Net ndiye aliyemfundisha kazi kwa mara ya
kwanza.
“Sijui
Net! Mimi nilijua ndivyo inavyokuwa. Sijawahi kufanya kazi ofisini.” “Basi huwa
wanatumia simu kuwasiliana watu wakiwa ofisini, labda iwe kuna kukabidhiana
kitu ndipo watu hutembeleana kwenye maofisi yao.” Tunda akajivuta kidogo nje ya
blangeti kwa mshangao.
“Wewe unafikiri kama bosi ni
mmoja na anawatu kumi au ishirini chini yake, halafu wote wakitaka kuuliza
swali, au kumpa taarifa wanamwendea ofisini kwake, si hiyo ofisi ya bosi
ingekuwa imejaa watu kila wakati na angeshindwa kufanya kazi? Ndio maana pia
kuna email,{barua pepe}. Kwa hiyo kila mwenye swali lisilo na haraka au ripoti
zote hutumwa huko ili bosi ajibu anapopata nafasi.” Tunda akatabasamu kama
aliyepata wazo.
“Basi na
sisi tuanze hivyo!” Net akacheka. “Mimi sikukufundisha hivyo Tunda. Nilikwambia
kila ukiwa na swali uwe unanifuata ofisini kwangu.” “Kwa nini sasa!?” “Ndio
swali na mimi nimekuuliza muda mfupi uliopita. Kwa nini unafikiri ninataka uwe
unakuja ofisini kwangu na sio kunipigia simu au kuniandikia ujumbe?” Tunda
akafikiria kidogo huku akitabasamu kama anayetaka kucheka. Net aliweza kuona
meno yake mazuri, yaliyokuwa yanang’arishwa zaidi na rangi yake nyeusi.
Akamgeukia
Net. “Sijui.” “Unataka kujua?” Tunda akatingisha kichwa kukubali huku akicheka.
Tunda alikuwa na uzuri wa aina yake, hasa anapotulia, akiwa na furaha
hakuchosha kumtizama.
“Kwa
kuwa huwa napenda nikiongea na wewe uwe unanitizama, Tunda. Napenda
kukuangalia.” Tunda alishtuka sana, akajificha tena uso kwa mikono yake
nakuanza kurudi ndani ya blangeti. Katika watu ambao hakuwafikiria hata
kuwatega ni Net. Alimuogopa sana tokea mwanzo kitu kilichomshangaza hata asijue
ni kwa nini amuogope Net, wakati hakuwa akimfahamu hata kidogo.
“Napenda
sana macho yako Tunda. Napenda kukuona mara kwa mara, lakini usifiche macho
yako. Napenda kuona macho yako yakinitizama mimi. Sipendi ninapozungumza na
wewe uangalie pembeni. Nataka unitizame mimi. Kwa hiyo nimekupa siri. Ukitaka
kuniadhibu ufanye kama hivyo ulivyofanya sasa. Nataka uwe ukinitizama kila
tunapoongea ndio nafurahia maongezi yetu.” Tunda aliogopa sana. Hakujua baada
ya kutoka pale alipojificha, atamtizamaje tena Net. Wakatulia kidogo.
Net
akaendelea. “Nimekuuliza swali Tunda. Ulipotoka hospitalini ulikwenda wapi?”
“Net jamani!? Bado tu unataka kujua? Nilimekuomba nisikwambie. Naomba
nisizungumzie hilo. Tafadhali.” Tunda alikuwa ameinama. “Kwa nini?” Tunda
alibaki kimya. “Tunda!?” “Abee.” Tunda akamtizama.
“Ujue
unaongea na mimi, sio mtu mwingine? Huna cha kuficha kwangu.” “Itasaidia nini,
Net?” Tunda akauliza kwa upole huku akimtizama. “Bila ya kuniambia, siwezi
kujua jinsi yakusaidia. Nataka kufahamu kila kitu. Tafadhali usinifiche au
usibakize kitu. Nataka kusikia kutoka kwako wewe mwenyewe.” Tunda alivuta pumzi
huku akionekana kujishauri. Mwishowe akaamua kumaliza tu, kwani ni kama
alishaongea kila kitu. Na kweli hakuwa na chakuficha kwa Net, aliyefanikiwa
kumfahamu kwa majina yote, wakati wengine walimfahau kwa jina moja moja tena ya
uongo. Hata hivyo Net ndio ameshika mpini wa maisha yake kwa wakati huo. Aliona
amalize tu, aone mwisho wake.
“Sikujua pakwenda Net. Baba aliniachia pesa chache
sana. Ilinitosha nauli na kula siku chache. Nilipotoka pale hospitalini nilikwenda
kula kwenye kibanda kimoja cha chips pale pale kituo cha Mwenge, ndipo
nilipokutana na mmiliki wa pale au mkewe ndiye aliyekuwa mmiliki. Nilipojua
anapesa na anasehemu nyingi za biashara, nikajua atanifaa.” Tunda akanyamaza.
“Nakusikiliza Tunda.” “Nimemaliza.” “Sijaelewa
chochote. Nimeishia upo kwenye kibanda cha chips.” “Kumbuka historia yangu Net.
Maisha yangu yote sikuwa na elimu bali ujuzi niliokuwa nimepata kutoka kwa baba
Tom. Mapenzi. Ndipo nikaamua kutumia huo uzoefu wangu kuishi mjini.” Tunda
akaanza kulia.
“Nilikuwa silali Net. Kazi yangu
ilikuwa kutongoza wanaume mchana na usiku! Nilikuwa nikilala na wanume hata
watatu kwa siku, na wengine ilikuwa sio lazima kufanya nao mapenzi, nilikuwa
nikitumia utundu wangu tu kuwaridhisha ilimradi kupata pesa ambazo sijui hata
zilikuwa zikiishia wapi! Nilikuwa nikinunua mavazi ya gharama ili kupata wateja
wa maana.”
“Nilitaka kulipa machungu kwa kuishi
nyumba nzuri na kununua vitu vya kisasa ili kulipiza kisasi kwa manyanyaso yote
niliyopitia, lakini haikusaidia hata kidogo. Ukweli nilikuwa nikipata pesa
ndiyo, lakini nilikuwa nikiteseka sana. SANA.”
Tunda akatulia kidogo. Akafuta machozi.
“Nimefanya mambo ya ajabu hapa duniani! Wakati
mwingine silali kwa hofu na ndoto mbaya. Huyo mwanaume wa kwanza niliyemtongoza
baada ya kutoka hospitalini, nikakwambia nimfanyabiashara mkubwa lakini Net,
kuna maajabu huku duniani, hujawahi ona. Watu wanahangaika kupata pesa, mpaka
unaweza usiamini.” “Vipi?” Net akauliza.
“Yule baba alinitoa pale akanipa maisha. Lakini
nililipia Net. Na sijui nilikuaje. Ni kama akili yangu ilibadilika! Nakwambia
sasa hivi silali sababu ya hofu, utafikiri siye mimi nilifanya.” “Ulifanya
nini?” “Ushirikina.” “Ushirikina!?” Hilo mzungu Net akawa hajalielewa
“Uchawi ule wa hali ya juu! Usiku badala yakulala,
tulikuwa tunakwenda makaburini kufanya ibada za kichawi.” Mpaka mwili wa Net
ukasisimka. “Na usifikiri mnaenda tu? Hapana. Mnafanya
mambo ya ajabu Net. Mnaita majini mpaka majoka yanatokea. Mnafanya hiyo ibada
mpaka yaondoke. Haya, wakati mwingine mnakwenda kwa huyo mganga mwenyewe. Usiku
Net. Giza. Mtakaa huko mpaka pakaribie kupambazuka. Tena mpo ndani ya mto huko,
chini ya miamba. Giza, mnafanya ushirikina. Mpaka alipokufa.” “Kufa
tena!?” Net akashtuka. Tunda akamuelezea mkasa mzima wa Sadiki na kumuacha Net
hoi.
“Ilikuwa ni shida Net! Nimeishi kwa
kuhangaika sana, mpaka wewe uliponitoa mvuani nikijificha kwa hofu ya radi.” “Daah! Pole sana Tunda.” Net alitulia kama
anawaza.
Akamfuta machozi. Akamgeukia vizuri. “Hivi Tunda,
unajua unaweza kubadilisha hayo maisha ukaamua kuishi wewe kama wewe na ukaweza
kuwa mtawala mzuri wa maisha yako?” “Sidhani Net.
Mimi mwenyewe sijijui mimi ni nani!” “Ukitaka kujitambua unaweza Tunda.
Na ukawa kiongozi mzuri sana wa maisha yako. Unaweza ukajiamuru kuwa na maisha
mazuri na matulivu. Najua au tuseme nimeelewa mazingira uliyopitia tokea
unazaliwa, yamekupelekea kuishi maisha uliyoishi. Lakini Mungu amekupa nafasi
ya pili. Nafasi ambayo hukustahili, lakini Mungu amekupa. Kubali kubadilika ili
uitumie vizuri.”
“Mbona nimeshaanza kubadilika?” “Kweli Tunda?”
“Sijalala na mwanaume tokea…” Tunda akafikiria. “Hujalala na mwanaume kwa kuwa
yeye alikukataa Tunda, sio wewe ndiye uliyekataa. Hebu fikiria kama siku ile
Gabriel angekukubali akakupokea, sasa hivi ungekuwa wapi?” Tunda akajifunika na
kuanza kulia.
“Usinifikirie vibaya wala sina nia ya kukuumiza ila
nataka kukuelimisha kwa kukufungua macho. Upo hapa ulipo kwa kuwa mimi
nilikutoa pale. Je, kama na mimi ningetaka kulala na wewe sio kukusaidia, au
tuseme kama ningekutoa pale nikakuweka hapa hotelini nikaanza kukutumia kama
wanaume wengine, ungekataa?” Ulikuwa ukweli mtupu ambao Tunda aliogopa hata
kumtizama Net.
“Inamaana mpaka sasa, ningekuwa na wewe nikiutumia
mwili wako kwa furaha zangu, na wewe ukiteseka moyoni na mwilini, ilimradi tu
utengeneze pesa! Kwa hali niliyokukuta nayo siku ile, maisha hayakukupa uhuru
wa kuchagua kitu gani ufanye ni wewe kupokea kitakacho kujia. Au niambie ukweli
Tunda, ikitokea nakufukuza kazi sasa hivi, utaenda wapi? Huna cheti hata cha
kidato cha nne. Unafikiri akitokea mtu kama Gabriel akakupokea tena mtaani
baada ya mimi kukufukuza kazi hapa, je utamkataa?” Tunda hakujibu, akaendelea
kulia.
Net anampa nafasi nyingine Tunda.
Net
akaendelea. “Ndio maana nakuambia hii ni nafasi ya pili Mungu amekupa Tunda,
anataka uanze upya. Usikubali kuiachia.” “Mungu
mwenyewe hata simjui, Net!” “Ukikubali, mimi nitakufundisha. Lakini
lazima ukubali wewe mwenyewe kwanza. Na usikubali kwa kuwa mimi ndiye
ninayekwambia, hapana. Pata muda wakufikiria kwanza. Na hata ukisema hapana,
siwezi kukuchukia na sitaacha kukuombea. Lakini nakuhakikishia ni maamuzi
ambayo hutakaa ujute.” Kidogo akamchanganya. “Ulikuwa
ukiniombea Net?” Tunda akauliza kwa upole sana huku akimtizama Net na
uso uliojaa machozi, nakumfanya atabasamu.
“Wewe ni mzuri sana Tunda, hutakiwi kuchezewa na
watu. Thamani yako haipo kwenye nyumba unayoishi au kiasi cha pesa unachomiliki
au elimu uliyonayo. Usikubali mtu akakwambia vinginevyo.” Tunda hakuwa
akiamini. “Hata wakikutupa jangwani bila kitu chochote, thamani yako inabaki
palepale.” “Unaongea na mimi, Net! Au umesahau?”
“Nimekwambia huwa sisahau kitu. Na hilo ndilo tatizo langu.”
“Sasa hiyo thamani naitoa wapi? Sina
thamani yeyote ile Net. Sipo huru kwenda popote tena. Sina mtu anayeweza
kunisaidia hivi au hata kunisikiliza zaidi yako. Tena hata wewe sikuelewi, Net!
Jinsi ninavyo kudhalilisha, aibu ninayokutia! Kweli sikuelewi! Mimi mwenyewe
nimechoka, nimeamua kujifungia humu ndani. Maana kila ninapoenda naishia
kudhalilika tu. Kama sitakutana na watu niliokwisha lala nao, basi
nilishawahudumia kimapenzi kwa namna moja au nyingine.”
“Kwa kuwa najua kuwa, kila mtu ananafasi ya pili,
hapa duniani. Unayo nafasi ya kuanza upya Tunda. Upya kabisa wewe mwenyewe.
Haijalishi nini umefanya kwenye maisha yako, unaweza kuanza upya na Mungu
asikumbuke kabisa ulichofanya. Hata kama wanadamu tutakumbuka, lakini si kwa
Mungu ambaye ndiye wa muhimu sana. Atakusamehe, atakutakasa, atakupa furaha ya
ajabu moyoni kwako. Atafanya upya nafsi yako na roho yako pia.” “Kwani na mimi
nina nafsi kweli!?” Net akacheka.
“Sitanii. Nahisi hivyo vyote vitakuwa vilishakufa
au mwenye navyo, huyo Mungu alishavichukua.” “Unanafasi ya pili Tunda.
Yakupatanishwa na Mungu. Fanya maamuzi sahihi. Atakurejeshea vyote ambavyo
shetani alivichukua.” “Umesema utanisaidia?” “Kwa asilimia mia moja. Sitakuacha
hata kwa hatua moja.” Tunda alifurahi sana.
“Asante sana Net. Sasa ndio natakiwa nifanyaje?”
“Swali zuri sana. Kwanza nataka kujua kama upo tayari.” “Umeniambia nijaribu.
Nataka nijaribu na mimi nione.” “Najua sasa hivi umechoka. Naomba nikuache
upate muda wa kupumzika, kisha kesho nikupeleke kwa mtu atakayekuambia nini
chakufanya.” “Kesho huendi nyumbani?” “Tutaenda wote Dar, na huko ndiko
nitakupeleka kwa mtu atakayekwambia chakufanya.” “Net!” Net alikuwa akivaa
viatu ili atoke. Tunda akakaa.
“Asante
kwa kila kitu. Asante sana.” Net akatabasamu. “Asante kushukuru, na mimi asante
kwa kuniamini na kuniambia kila kitu tena kwa uwazi.” Tunda akafikiria kidogo. “Nikuulize
kitu Net?” “Uliza tu.” “Baada ya kujua uchafu wangu wote niliofanya,
unanifikiriaje?” “Ninafikiria hiki unachotaka kufanya sasa hivi Tunda, sio
maisha uliyoishi zamani. Wewe hukupata nafasi ya kulelewa kama wengi wetu.
Hukubahatika. Ila sasa hivi umekubali kupokea nafasi mpya kwenye maisha yako,
tena ukiwa na mimi niliyekuahidi kuwa na wewe katika kila hatua ya maisha yako,
hilo tu ndilo linanipa nafasi ya kuweza kuongea kitu juu ya maisha yako, si
vinginevyo.” Tunda hakuamini, akabaki ametulia tu akimwangalia kama
asiyemsadiki.
“Nina kusifu Tunda. Ikifika kesho kama sasa hivi,
utakuwa kiumbe kipya kabisa. Pata muda wakupumzika kesho tutaongea vizuri
tukiwa njiani.” Net akaondoka akamwacha Tunda akiwa amelala, kwani alikumbuka
Tunda alivyomwambia kuwa, huwa anapata usingizi pale anapokuwa naye. Alirudi
kukaa pembeni yake, akawasha tv akiwa bado amevaa viatu. Tunda alibaki
akishangazwa na Net alijua. “Pumzika, ulale. Nataka nikuache ukiwa umelala.”
Tunda alitoa tabasamu zuri, lililofanya azidi kuvutia. “Asante Net.”
Alijirudisha ndani ya yale mablangeti na
shuka, huku Net akimsaidia kumfunika vizuri. “Usiku mwema.” “Na wewe Net.”
Tunda akalala na ndipo Net naye alipoondoka.
Tunda akiwa safarini kuanza maisha mapya.
Wakiwa
kwenye ndege kuelekea Dar, Net alimueleza Tunda umuhimu wakuanza upya na faida
nyingi atakazopata katika hayo maisha aliyoyachagua. “Naona kama ndege
inachelewa, natamani kufika haraka!” Net akacheka. “Lakini kwanza tunapitia
nyumbani.” “Kwa mama yako!?” “Tena atakuwa akitusubiri uwanja wa ndege.
Amefurahi uamuzi uliofikia, akaomba tupate muda wa pamoja mfahamiane kwanza
kabla ya kwenda kwa Mchungaji. Ni sawa?” “Hamna shida, ndio vizuri na mimi
nimfahamu bosi wangu. Tumekuwa tukizungumza kwenye simu tu. Na mimi nitafurahi
kumuona. Yeye ni mzungu?” Swali la Tunda lilimfanya Net acheke sana.
“Nini
sasa?” “Hapana bwana. Mama yangu ni Mtanzania. Baba ndiye alikuwa mtu wakutokea
Canada.” “Sera alikuwa akiringa kuwa anaolewa na Mzungu.” “Mzungu gani?” “Si
wewe?” Net akazidi kucheka. Alikuwa kijana mstaarabu sana na muungwana.
Alijaliwa utulivu ambao mtu yeyote angetamani kuzungumza naye.
“Hakuwa
amenielewa vizuri. Nilijitahidi sana kuwa muwazi kwake na sikuwahi kumuonyesha
hisia zozote za kimapenzi. Sijui kwa nini alifikiria ndoa!” “Atakuwa alikupenda
sana.” Net akamtizama Tunda. “Nini sasa? Kweli! Sera alikupenda.” Net akatabasamu
kisha akapotelea mawazoni.
“Net!
Nikuulize swali?” “Mmh!” “Kwani unamchumba?” “Sijui!” Tunda alikunja uso, kama
ambaye hakuwa amemuelewa Net. “Vipi? Umenipatia mchumba nini?” “Hapana, lakini
nashangaa kwa nini hukumpenda Sera wakati naona alikuwa msichana ambaye mlikuwa
mkiendana sana!” “Unamaanisha nini?” “Wote mmelelewa kwenye mazingira mazuri, mmesoma,
wazazi wenu wanauwezo mzuri, yaani mnapesa. Ni msichana mzuri, na yeye ni
mweupe, halafu Sera hakuwa muhuni kabisa. Hakuwa na mambo ya wanaume.
Alijiheshimu sana.” “Daah! Kama ungekuwa mshauri wangu wa ndoa, ningekufukuza
kazi sasa hivi.” “Kwa nini tena!?” Tunda akaanza kucheka.
“Vigezo
vyako viko dhaifu sana, havimsaidiii mtu kupata mke hata kidogo!” “Jamani Net!”
Tunda akazidi kucheka. “Hebu niambie, weupe, usomi, pesa na nini tena?” Net
akauliza huku Tunda akicheka. “Kulelewa na wazazi wenye uwezo, yaani wote
mmetoka kwenye malezi yanayoeleweka.” “Ehe! Sasa hivyo ndio vinasaidia kuwa na
mke bora?” “Ndiyo. Na mwanamke aliyetulia. Sasa ukioa mwanamke ambaye hajatulia
ndio inakuaje sasa?” Net alicheka kwa kuguna kisha akageuka pembeni. Tunda naye
akaanza kuwaza maisha yake mapya aliyoamua kuanza.
Kwa Mara ya Kwanza Tunda na Mama Cote.
Ndege ilitua viwanja vya ndege
vya Mwalimu Nyerere, Dar. Kweli walimkuta Mama yake Net na msichana mwengine
aliyeonekana mzungu kwa asilimia kubwa sana kuliko hata Net. Alikuwa mzuri sana
na nywele za rangi ya thahabu, tofauti na Net,
zilianguka mpaka chini ya mabega. Macho ya rangi ya blue kama Net. Tunda
alimsalimia mama yake Net baada ya Net kumsalimia mama yake kwa kumkumbatia na
kumbusu.
“Kuna nini tena?” Net akauliza baada yakumuona yule
dada hajawasalimia. “Am leaving with you.” Alijibu yule dada kwa lugha ya
kingereza huku akionyesha uso wakutaka kulia. “I just got here, Maya! What’s
going on?” Net akamuuliza kwa upendo huku akimwangalia mama yake. “Siwezi tena Net. I got enough of her. I want to go.”
Yule dada aliendelea kumlalamikia Net, huku machozi yakimtoka. “Can at list
have a hug first?” Net akamuuliza kwa upendo kama kumbembeleza.
Yule dada akamsogelea Net na kumkumbatia kisha
akaanza kulia. “She doesn’t take me out of her
sight! She took everything away from me.
She is ruining my life, Net.” Aliendelea kumlalamikia Net. “Can
we talk about it later?” Yule dada akanyamaza kwa muda.
“Mwambie anirudishie funguo zangu za gari kwanza.
She listen to you Net. Tell her, NOW.” “You know we have to talk first, Maya.
Naomba utulie kwanza kisha tutaongea tukifika nyumbani.” “I don’t want to talk,
I want my life back.” “I understand, but let’s go back home first.” Walikuwa
wamewapa mgongo Tunda na yule mama, wakati wao wawili wakizungumza.
“Naomba umsalimie Tunda.” “Tunda? Is that a name or
fruit!?” Yule dada akauliza kama kwa kejeli akitaka kujua kama Tunda kweli
linaweza kuwa ni jina la mtu! “I know you are upset Maya, but can you try to be
nice?” Net akamwambia anaelewa kuwa
amekasirika, ila ajaribu kuwa mwema kwa mgeni. “Am sorry.” Maya akaomba msamaha
na kumgeukia Tunda.
“Hey! Am Maya.” “Kiswahili Maya!” Mama yake Net
akaingilia akitaka azungumze kiswahili na Tunda si lugha ya kingereza. “See! Everything am doing to her it’s a problem.”
“She speaks Swahili, Maya. Just use Swahili, please.” Net aliweka msisitizo
akiungana na mama yake kuwa Maya atumie kiswahili. “Fine!”
Akakubali Maya nakufuta machozi.
“Habari yako. Naitwa Maya Cote.” Tunda akajua
lazima ni mdogo wake Net kwani ndiyo jina alilokuwa akitumia hata Net,
Nethaniel Cote. Tunda akanyosha mkono. “Naitwa Tunda, kama vile fruit.” Maya
akacheka kwa aibu kidogo. “Samahani. Mama ananiudhi sana.” “Usijali. Hata shule
walikuwa wakinitania hivyo hivyo.” Tunda alijibu huku akitabasamu, wakacheka.
“You have a pretty face. I love your sleeping eyes.
The way you talk and smil..” “Swahili, Maya.” Mama yake alimkata Maya akitaka
azungumze kiswahili. “See Net! I told you she…” “Maya!” Net akamwita kama
kuweka msisitizo. “Fine!” Maya akamjibu kaka yake. “Wewe ni mzuri sana. Napenda
macho yako na, anyways everything. You pretty.” Tunda akacheka akiona aibu. “Asante
Maya.” Akamgeukia kaka yake na kumwambia, “I like her.” Akisema amempenda
Tunda. Wote wakacheka.
“Ukiondoka unichukue na mimi, sitaki kubaki hapa na
Mama Cote.” Alimnong’oneza Tunda masikioni, lakini kwa sauti iliyoweza kusikika
na kila mtu pale. Tunda akacheka. “Mama akiruhusu, tutaenda wote.” Tunda akajibu
huku akicheka. “Trust me, she wont. Labda Net ndio amwambie. Anafanya chochote
anachoambiwa na Net, lakini siyo mimi.” “That’s enough Maya.” Mama yake akamkatisha.
“See! That’s why I want to go away.” Maya akalalamika na kurudi nyuma akiwa
amenuna. Walionekana wawili hao hawapatani.
“Karibu sana Tunda. Samahani umetukuta katika
wakati mbaya, lakini nimefurahi kukufahamu. Mimi ndiye Mama Cote. Mama yake
Maya.” Maya akamwangalia na kujisogeza kwa kaka yake. Alikuwa mama wakawaida
tu. Hakuwa mweupe wala mweusi. Mswahili kabisa mwenye rangi ya kawaida. Maji ya
kunde. Lakini alizaa watoto wote weupe sana, yaani wazungu. Maya alikuwa ndio
anamwili wa kizungu, nimpaka aongee hicho Kiswahili chake na akuonyeshe mama
yake ndipo utajua amechanganya. Wote walikuwa na nywele nyeusi lakini Maya
alizibadili rangi nywele zake.
“Net aliniambia mnataka kwenda kumuona Mchungaji.”
“Ndiyo.” “Umefanya vizuri. Lakini twende kwanza nyumbani mkale ndio twendeni
kwa Mchungaji.” Walikwenda mpaka nyumbani kwa huyo mama. Alijenga sio mbali
sana na alipokuwa amejenga Net. Maeneo hayo hayo lakini lazima utumie usafiri
kufika kutoka kwa Net kwenda kwa mama yake. Palikuwa na umbali kidogo.
Tunda akabaki ametoa macho. Lilikuwa ni jumba la
kisasa. Kumbwa picha za familia zilijaza hiyo nyumba kwa wingi. Kuanzia
unaingia mlangoni mpaka sebuleni. Kubwa na nzuri. Na hapo ndipo alipoiona picha
ya baba yake Net. Kweli alikuwa mzungu kabisa. Na alifanana sana na Net. Tunda
alipita akiangalia.
Heshima ikaongezeka kwa hiyo familia. Kwa vile alivyoona
pale, na biashara huyo mama anafanya, Tunda akakubali kuwa huyo mama kichwa
yake inafanya kazi. Alimshukuru Tunda kwa kazi nzuri aliyokuwa akifanya kwenye
ofisi yao huko Arusha. Akamsifia kuwa anampunguzia majukumu makubwa yeye na Net
kwa utendaji wake mzuri.
“Net anakusifia sana. Hata wateja wetu wanakusifia.
Asante sana na ninakuomba uvumilie tu, baada ya muda nitaongeza mtu mwingine
wakukusaidia.” “Hamna shida mama. Kwa sasa naona nimeweza kumudu kazi zote,
hata hivyo Net ananisaidia sana.” “Utalemewa pindi Net atakaposafiri.” Tunda
alishtuka sana akamgeukia Net.
“Sisafiri sasa hivi Tunda. Acha kuogopa.” Tunda
akacheka taratibu lakini wazi alionekana ameingiwa hofu. Walikaa pale
wakizungumza mambo mbali mbali. Zaidi Net na mama yake ndio waliokuwa wakiongea
zaidi. Walikuwa wakizungumzia mambo yao ya biashara. Tenda alizoshinda huyo
mama. Tunda alibaki kusikiliza huyo mama, nakumtamania. Alionekana ni mama
aliyefanikiwa sana.
Walikaa hapo mpaka mida ya jioni ndipo walipoamua
kwenda kanisani. Tunda alikuwa amepewa chumba pale pale, akaacha baadhi ya vitu
vyake kwenye hicho chumba, kwani Net alimwambia wangelala hapo siku hiyo mpaka
kesho yake.
Tunda na Mkasa wa Kanisani.
Walipofika
kanisani wakakuta ndio wanamalizia kikao cha wazee wakanisa, ofisini kwa
Mchungaji. Ilibidi wasubiri kwenye viti vya nje. Alikuwa Tunda, Net na Mama
Cote. Waliendelea kuongea mambo mawili matatu wakiwa pale nje, mpaka walipoona
wazee wengine wakitoka kwenye ofisi ya Mchungaji. Mama Cote akasimama
akatangulia humo ndani, baada ya muda, Tunda na Net walianza kusikia vicheko
mle ndani ofisini wakahisi wamesha sahauliwa. “Ngoja nikawashtue.” Net
akasimama na kuingia ndani.
“Shikamooni.”
Tunda akamsikia Net akisalimia huko ndani. Mchungaji akaongea na Net maneno
mawili matatu huku akimtania na kumuuliza habari za Arusha kisha Net akaamua
amkumbushe baada ya kukuta bado kuna wazee wengine watatu mle ndani. “Bado
utakuwa na nafasi yakuongea na Tunda?” Net akauliza. “Kabisa. Umekuja naye?”
“Yupo hapo nje.” “Mkaribishe awasalimie na hawa wazee wa kanisa.” Mchungaji
akajibu. “Ni kweli. Yaani Tunda ni binti mzuri sana.” Mama Cote naye akaanza
kumwaga sifa za Tunda, akimsifia utendaji kazi wake. Net akatoka kwenda kumwita
Tunda.
Net
alimtanguliza Tunda aingie kwanza, yeye akafuata nyuma. Tunda aliingia na
kusalimia “Shikamooni.” Huku akinyoosha mkono akitaka kuwapa mkono wale wazee
na wachungaji kwa heshima zaidi. Wakati anasogea mbele kidogo ili aanze
kuwashika mikono huku akiwaangalia vizuri, Net akamuona Tunda ameshtuka sana,
akainama na kurudi nyuma huku akishusha mkono wake. Mama yake na Mchungaji
hawakuelewa, lakini Net alishaelewa kwani alishakaa na Tunda kwa muda mfupi
lakini alishamuelewa vizuri sana. Net alikasirika sana.
Wakiwa wengine
hawajaelewa kilichompata Tunda, akamgeukia Net na kumsogelea kwa karibu. “Naomba
kuondoka Net.” Tunda akataka ampishe sehemu ya mlangoni. “Vipi tena!?”
Mchungaji akauliza kwa mshangao, huku akisimama. “Eti Tunda?” Tunda alishaanza
kulia. “Naomba niondoke tu.” Hakuna
aliyeelewa, Net aliwageukia wale wazee, akashangaa kuona wawili wameinama. “No
way!” Net alisikika akilalamika huku ameshika kichwa. “Seriously!?” Net
akawauliza kwa mshangao huku akiwatizama wale wazee wawili. Tunda akamsogeza
kidogo Net kwa mkono wake, akatoka nje.
“Tunda!
Tunda! Naomba nisubiri.” “Umenidanganya Net.
Umeniambia nakuja kuanza upya, halafu unakuja kunikutanisha na waliokuwa wateja
wangu, tena mbele ya mama yako! Nilikuamini Net, umenigeuka!” Tunda
alikuwa akilia. “Tunda please. Naomba usiondoke.” Tunda alikuwa ameshatoka nje
ya geti la kanisa, alikuwa akitembea kwa mwendo wa kasi, Net akimkimbilia kwa
nyuma.
“Naomba
usimame Tunda, Please.” Tunda akasimama huku akilia. “Naomba unisikilize.
Unafikiri mimi ningejuaje kama wale walikuwa wateja wako? Sikuwa nafahamu hilo!
Wale wazee wanaheshimika sana hapa kanisani, sikuwahi hata kuwaza kama wanaweza
ku..” Net akasita. “Sasa unataka nifanye nini na
wale watu tena? Ni maisha gani mapya unataka nianze na watu kama wale? Si
yatakuwa ni yale yale tu?” Tunda alikuwa akiongea ukweli kabisa. Net akapooza,
alishindwa chakujitetea kabisa.
Mahali
ambapo alimwahidi Tunda angepata msaada na kubadili maisha yake, anakutana na
wazee aliokuwa akiwaamini sana na wao walikuwa wakiishi yale maisha machafu.
Alibadilika sura akawa mwekundu, nakushindwa kushusha mikono yake. Alibaki
ameweka mikono kichwani akizunguka zunguka pale mbele ya Tunda.
“Naomba niondoke Net.” “Kumbuka tumekuja na mama!
Naomba nikamchukue mama ili tuondoke pamoja. Sawa?” Tunda akatingisha kichwa
kukubali. “Asante sana Tunda.” Net alikuwa amesha changanyikiwa. “Twende basi
ukasubiri kwenye gari.” Akarudi naye mpaka kwenye gari, akawasha gari,
akamuacha Tunda amekaa humo ndani ya gari.
Alikuta
Mchungaji akimsubiri, bado haelewi kilichotokea. “Kuna nini, Net?” “Naomba
tuwaulize hawa wazee, kwa nini Tunda amekimbia mara baada ya kuwaona.” Mmoja
wao akasema sijui. “Wewe hujui lakini Mzee Meto namwenzie wao wanafahamu.” Net
alikuwa amekasirika sana.
“Hivi unajua ni kwa muda gani nimekuwa
nikitaka huyu binti afikie haya maamuzi? Hivi mnajua ni jinsi gani
nilivyomuhubiria? Nimemwambia huku kanisani lipo tumaini. Ameteswa na shetani
kwa muda mrefu sana, nimemuahidi atapata pumziko. Halafu anakuja kukutana na
nyinyi watu wa kanisani mliokuwa wateja wake!” “Wateja?” Mama Cote alishtuka
sana. “Ndiyo. Tunda alikuwa akifanya biashara ya kikahaba.” Net alikuwa
amekasirika sana, hata hakuwa akifikiria alichokuwa akiongea. Aliendelea
kuropoka. Wote walikuwa kimya wakimsikiliza.
“Hivi
mnajua mlichofanya nyinyi? Mmechukua tumaini la pekee lililokuwa limebaki kwa
yule binti! Mtamfanya asiamini tena.” “Tulia Net. Kwa kuharibu kwa hawa wawili,
hakuchukui nafasi ya Mungu hata kidogo. Kama wao wameshindwa, bado tunayo mifano
mizuri ya watu wengi wanaoweza kuishi maisha maadilifu. Naomba ukamwite Tunda.”
Mchungaji akapiga simu kwa baadhi ya wazee aliojua wanaweza kufika pale kwa
haraka, wakaanzisha kikao.
Tunda akarudi
ndani, wakamuomba aelezee mahusiano aliyokuwa nayo na wale wazee. Tunda akakiri
kila kitu huku akilia na kusema ni kweli amechoka anatafuta njia ya kupumzika
nakuondoa ile hukumu moyoni mwake lakini si pale. “Hamuwezi
nyinyi kunisaidia. Hamtaweza hata kidogo.” Tunda akatoka. Net
alimkabidhi funguo mama yake na kumfuata Tunda.
Ilikuwa
ni aibu ya miaka kwa kanisa. Hakuna aliyeamini uchafu Tunda aliosema alikuwa
akiwafanyia wale wazee. Net ndiye aliyeishiwa maneno kabisa. Alishindwa aongee
nini na Tunda. Tunda alikataa kabisa kurudi kwa mama yake Net, akaishia kulala
hotelini. Aliomba Net akamchukulie mizigo yake nyumbani kwao, usiku uleule.
Tunda Arudi Arusha bila Msaada wa kiroho.
Kesho
yake asubuhi na mapema, bila hata kumuaga Net, Tunda aliondoka jijini Dar
kurudi Arusha kwa kutumia usafiri wa basi. Usiku ule ulikuwa mrefu sana kwa
wale viongozi wa kanisa lile. Wale wazee walikiri uchafu waliokuwa wakifanyiwa
na Tunda, na kesho siku ya jumapili kwenye ibada, walisimamishwa mbele ya
kanisa na Mchungaji akawatenga.
Ilikuwa
ni hali ya kusikitisha, kushtua na aibu kubwa. Kwani ni wazee walioheshimika
sana pale kanisani na wao ndio walikuwa wakitoa michango mikubwa ya kifedha
pale kanisani, wakisaidiana na Mama Cote. Mmoja alikuwa ana mke wake pale pale
kanisani. Watoto wao walishakuwa wakubwa tu. Na Meto yeye alifiwa na mkewe,
japo naye alikuwa Mzee wakuweza kumzaa hata Net. Alitambulishwa Tunda na huyo
Mzee mwenzake. Tunda akamridhisha kwenye gari kitu alichopenda. Hakuhitaji
kwenda naye popote. Kwa hiyo walimpenda Tunda, wakijua hawataweza kukamatwa.
Waliegesha magari yao sehemu tulivu mida ya usiku giza limeshaingia. Tunda
anafika hapo kwenye magari yao, anawahudumia, wanamlipa, maisha yanaendelea.
Mchungaji Amfuata Tunda.
Baada ya
ibada yule Mchungaji alipanda ndege kuelekea Arusha na Net, kumfuata Tunda.
Walimkuta amelala chumbani kwake. Mchungaji alimuomba waongee. Tunda alishtuka
sana. Hakutegemea kuja kufuatwa tena baada ya kugundulika uchafu wake. Yule
Mchungaji aliongea kwa muda mrefu na Tunda. Akimpa mifano hata ya watu
waliokuwepo kwenye bibilia walioaminiwa na Mungu, lakini walikuja kumkosea
Mungu, lakini baadaye walipotubu tena Mungu aliwasamehe. Alimpa mfano wa Petro
aliyemsaliti Yesu mara tatu, lakini baada ya kutubu alisamehewa, na akamueleza
jinsi Petro alivyokuja kuwa msaada mkubwa kwa kanisa mpaka sasa.
“Kama sio Petro kukubali kosa, kazi kubwa ya kanisa
iliyoifanya baada ya kutubu isingekuwepo leo. Kikubwa ni kukubali kuwa umekosa
na kuhitaji msaada wa Mungu. Halafu Tunda, wale wazee hawatakuwa mfano wako
wakuiga pindi utakapoamua kumpa Yesu maisha yako. Wote tunamwangalia mmoja tu,
ambaye aliishi hapa duniani bila kutenda dhambi, Yesu.”
“Wote tunamtizama yeye peke yake. Hata mimi huwa
najikwaa kwa namna nyingine, na ndio maana tupo kanisani. Kanisani ni kama
hospitalini, Tunda mwanangu. Wote tuliogundua tunahitaji msaada wa Mungu, ndio
tumekimbilia pale kama wagonjwa wanavyokimbilia hospitalini. Kanisani ndio
mahali pekee utakapopata msaada. Sisemi kama utakuwepo kanisani na uendelee
kutenda dhambi, hapana. Lakini ujue kuna madhaifu mengine yanachukua muda
kuondoka, lakini utakapotulia kwa Mungu, ukanyenyekea, ipo nguvu na uwezo wa
kushinda dhambi endapo utakusudia.” Yule mchungaji aliendelea.
“Mungu halazimishi mwanadamu kuacha kufanya dhambi.
Mimi na wewe ndio tunachagua. Kwa hiyo unaweza ukawepo kanisani, na ukachagua
kuendelea kutenda dhambi kama mtu wa nje kabisa, lakini haiondoi uweza na nguvu
za Mungu. Utende dhambi, usitende, bado Mungu atabaki kuwa Mungu ila wewe ndiye
utakayeteseka.” Net aliendelea kusikiliza na yeye kwa makini tu akiomba Mungu huo
ukweli umuingie Tunda.
“Hakuna pumziko kwa mwenye dhambi, si sasa au
baadaye. Bali ipo faraja, amani na utulivu kwa wale walioamua kweli kuishi
maisha yakumpendeza Mungu. Mpe Yesu nafasi kwenye maisha yako uone. Mruhusu Net
awe mwalimu wako, utajifunza mengi sana kupitia yeye. Nikijana aliyetulia sana
na anamjua Mungu. Anaishi maisha ya kikristo kweli kweli, najua wewe ni
shahidi.” Tunda akatingisha kichwa kukubali. Kidogo Mchungaji akapumua.
“Basi, na wewe unaweza kuwa kama yeye, kama
utakubali, ukatii na kutubu. Je upo tayari?” Tunda alishatulia kabisa.
Alimuelewa vizuri sana yule Mchungaji. Akakubali kuombewa. Aliongozwa sala ya
toba na Mchungaji akamuombea. Tunda alikuwa na mapepo mengi sana.
Alikuwa amefungwa na nguvu za giza, nyingine tokea
alipokuwa mtoto mdogo kwa baba Tom. Mashetani na majini mengine aliyapata akiwa
na Sadiki. Tunda akiwa amepagawa hayo mapepo, aliongea mengi sana. Basi ikawa
vurugu tupu hapo chumbani. Mchungaji na Net walimuombea, wakikemea yale mapepo
yamtoke. Kuna yaliyokuwa mabishi. Yakidai hiki na kile. Lakini yule mchungaji
alikazana akisaidiana na Net. Haikuwa kazi rahisi wala ya masaa machache.
Lilitoka pepo hili, na kuibuka jingine ndani yake.
Wakidhani wamemaliza, linaibuka jingine. Mara liseme ni jini lililomuoa Tunda.
Jingine lilisema ndilo linalomfanya awe na bahati na kuvutia wanaume kwake.
Ikawa fujo. Tunda alijawa nguvu za giza. Lakini Net hakushangaa. Tunda
alishamsimulia ibada za kipepo alizokuwa akifanya makaburini na huko Handeni
alipokuwa na Sadiki.
Maombi hayo yaliendelea, mpaka yote yakamtoka
Tunda. Akawekwa huru. Kuja kuangalia saa ni saa saba usiku. Ikabidi Mchungaji
achukuliwe chumba hapo hapo hotelini. Kesho yake asubuhi akaondoka kurudi Dar,
akiwa amefanikiwa kumpatia Mungu roho ya Tunda.
Maisha ya Tunda baada yakumpokea Yesu.
Net ndiye alikuwa na furaha
kuliko hata Tunda mwenyewe mpaka Tunda akashangaa. Alikabidhiwa rasmi kazi ya
kumtunza Tunda kiroho. Kitu cha kwanza alichomnunulia Tunda ni bibilia. Akaanza
kumfundisha Tunda jinsi ya kusoma bibilia. Kitu alichogundua Tunda kwa Net, ni
muombaji. Net alikuwa ni muombaji sana, kitu kilichokuwa kikimshangaza Tunda.
Kwa jinsi alivyo Net, na maisha anayoishi, ingekuwa ngumu kumdhania kama ni
mcha Mungu wa kiasi kile. Lakini Tunda alijua ndiyo siri yake kubwa ya hekima
na utulivu alio nao.
Kwa
harakaharaka wasichana wengi walikuwa wakichanganywa na Net, pindi wamuonapo.
Lakini baada ya kukaa naye kwa muda mfupi, wengi walimkimbia. Mara nyingi Net
alikuwa akimshukuru Mungu kwa kumuwahi. “Unamaanisha nini?” “Najijua hivi
nilivyo Tunda. Si watoto au watu wazima wanao nijaribu kunitongoza. Isingekuwa
Yesu kunificha, pengine sasa hivi ningeshakuwa nimekufa. Nashukuru Mungu kwa
kunipa baba na babu wenye msingi imara wa dini, zaidi babu. Walinikuza kwenye
maadili mazuri.”
“Yuko
wapi sasa hivi baba?” “Alishafariki.” “Pole sana.” “Asante, lakini ilimuathiri
zaidi Maya. Unajua yeye ndiye alilelewa sana na baba wakati mama yupo shuleni.
Kwa hiyo baba alipofariki, ndipo mama alipoamua kurudi huku Tanzania.” “Kwani
hamkuzaliwa hapa?” “Hapana. Tulizaliwa Canada. Mama alienda huko kimasomo,
ndipo akakutana huko na baba. Hata msingi wa shule niliyokuwa nayo ilikuwa ni
hukohuko, ndio maana ilinilazimu kurudi hukohuko kumaliza shahada yangu ya pili.”
“Alitangulia kurudi huku mama peke yake. Akatuacha kule mimi na Maya tukilelewa na bibi na babu. Mama alipoweka mambo sawa, nikaanza kuja huku mimi ndipo tukamchukua Maya. Maya hana muda mrefu sana hapa nchini. Na hapapendi kabisa. Anataka sana kurudi kwa bibi na babu. Lakini mama hataki, anaona kule hana uangalizi mzuri. Pale alipo hataki kufanya kitu chochote hapa nchini, anataka kurudi kwa bibi na babu.” “Labda mngemruhusu ili akasome.” Tunda akajaribu kushauri.
“Mama
hawezi. Ni mtundu sana Maya. Na amedekezwa sana na kina bibi. Hana maadili
mazuri hata kidogo. Hata huko pia shule yenyewe hataki kwenda. Amemaliza high
school tu, anatapanya pesa ya bibi na babu. Ndio maana mama ameamua kumchukua.”
“Natamani kama mimi ndio ningepewa hiyo nafasi Net.” “Mungu amekupa nafasi
nyingine Tunda. Unaweza kuwa chochote utakacho.” Tunda akainama kama
anayefikiria kidogo.
“Lakini
sikurudi tena shule. Naanzia wapi?” “Sio lazima ukasomea elimu ya msingi au
sekondari. Kwa sasa unaweza kutafuta ujuzi wa kitu fulani unachopenda, kisha
ukaanza kukifanyia kazi.” “Ni kweli. Labda nianze kufikiria na mimi nikitu gani
napenda. Maisha hayakuwahi kunipa nafasi kama hii. Sasa hivi ninafuraha na
amani. Siamini kama na mimi Tunda, nipo kwenye nafasi yakuchagua.” Net akacheka.
“Nikwambie
ukweli Net, zile ndoto mbaya zimeisha. Halafu nilikuwa nina hofu fulani hivi.
Kama wasiwasi moyoni. Umeshawahi kulala usiku au hata kuwa umekaa tu hivi,
ukasikia moyo unashtuka?” Net akawa anafikiria. “Unaweza usijue, lakini
nilikuwa na hiyo hali. Hofu kila wakati kama moyo unashtuka kila wakati.” “Kwa
hiyo sasa hivi imeisha?” “Imeisha. Namshukuru Mungu. Najisikia huru.”
“Afadhali.”
Cheni ya Mguuni ya Tunda!
Ilikuwa jioni wametoka kazini. “Nikuulize
kitu Tunda?” “Niulize tu.” “Hiyo cheni ya mguuni ulipata wapi?” Tunda akakunja
mguu akaitizama na kuizungusha kidogo. “Alinivalisha Sadiki. Nimeshindwa kuitoa
Net.” “Kwa nini?” Tunda akafikiria. “Kuna jinsi Sadiki alikuwa akinifanyia,
sijui niseme kunidekeza au nini! Lakini kuna jinsi alikuwa na mimi, alikuwa
akinifanya kama yai! Alikuwa hapendi niwe na shida. Kabla sijalia shida,
ananipa pesa. Manguo haya yote, ni ya pesa nyingi sana Net.” “Nakuona.” Net
akaongeza.
“Basi ni
Sadiki. Nilikuwa nikiwa naye, japo nilimdanganya jina, lakini sikuwa
nikijitahidi kujifanya kuwa sivyo. Alinipenda yule kaka, karibu
kuchanganyikiwa. Wakati mwingine nilikuwa nikimgombesha sana, lakini
anavyojishusha, mpaka utamuhurumia. Sikuwa na shida na pesa nilipokuwa naye.
Sikuwa nikihangaika kwa yeyote na chochote. Alinilipia kila garama, tena bila
kuchoka au kulalamika.”
“Alikuwa
akiniona nimetulia tu hivi nawaza kitu, basi hata kama alikuwa anafanya kitu,
ataacha, anakuja japo aniguse. Nitakuwa mawazoni, naweza kushtuka kwa sababu
ananisugua mahali kwa upendo. Kiganja, bega, ilimradi tu kunionyesha yupo na
mimi.”
“Japokuwa
alikuwa anasema ananufaika na mimi, lakini Net, Sadiki alihakikisha nina furaha
wakati wote. Alinipenda sana. Nilipata miaka miwili ya aina yake na yule kaka.
Hii cheni nimeshindwa kuitoa kabisa. Wakati mwingine najiona ni kama nipo na
ule upendo wake. Sijui kama unanielewa?” Tunda akauliza na kuendelea bila
kusubiri jibu.
“Sijapata
mwanaume anayenipenda vile Net. Labda nikija kubahatika upendo kama ule tena.
Huyo mwanaume ndiye atakayekuja kuitoa hapa mguuni kwangu. Lakini mimi
nimeshindwa.” Tunda aliongea taratibu huku akiiangalia ile cheni na kuizungusha
pale mguuni mwake. Net akavuta pumzi kwa nguvu maana alikuwa akimsikiliza kwa
makini sana.
“Lakini
sasa hivi hauhitaji upendo wa Sadiki, Tunda. Unaye Mungu aliye hai. Upendo wake
unatosha. Usijifunge na upendo ambao haukuwa halisi. Nilivyokusikia juu yako na
Sadiki, mlifanya mengi na ya kutisha huku akikutumia wewe kama chambo yakuvuta
utajiri. Hudhani kama hiyo kitu inaweza ikawa imebeba mambo mengine?” Tunda akashtuka
kidogo.
“Nikuombe
kitu?” Tunda akamwangalia. “Naomba mimi niitoe, halafu nije niweke hapo
nyingine.” Tunda akajifuta machozi. “Hamna sababu
yakufanya hivyo Net. Acha tu. Lakini naomba nipe muda wakuja kuitoa. Isiwe sasa
hivi. Najiona sipo tayari Net. Mmeniombea, naamini hii cheni haiwezi kuwa na
madhara yeyote. Alininunulia cheni tatu. Shingoni, mkononi na mguuni.
Akaniletea na kuniambia ni ishara ya upendo wake kwangu. Najiona sipo tayari
kuviachia.” Net alibaki akimtizama.
“Ni sawa?” Tunda akauliza kwa upole. “Sio sawa Tunda.”
Tunda akaumia sana. “Tena kwa maelezo hayo, ndio sio sawa kabisa. Kwa nini
unataka kukumbatia upendo wa mtu aliyepita vibaya kwenye maisha yako?” Tunda
akanyamaza.
“Unakuwa
unang’ang’ania agano la mapenzi yaliyowekwa kwenye msingi mbaya na hatari sana
kwako! Tumekuombea, na tunaendelea kuomba. Lakini unakuwa uko kwa Mungu huku
umekumbatia maagano ya mtu mwingine kwenye ufamle mwingine! Hujui nia ya
kukuvalisha hiyo ki ukweli.” “Aliniambia ni ishara
ya mapenzi yake kwangu.” Tunda akatetea.
“Ndivyo
yeye alivyokwambia. Unajuaje kama ni kweli? Halafu Sadiki alikuwa mume wa mtu.
Unajifunga kwenye maagano ya ndoa ya mtu! Si sawa Tunda. Unatakiwa ubadilike
hata kifikira. Kuwa upande wa Mungu huku ukitetea mapenzi ya wizi, unajifungulia
milango mingine mibaya. Naomba ufikirie zaidi.” “Nimeelewa Net. Nitatoa.” Tunda
akaongea taratibu.
“Lini?”
Net akauliza bila kutaka kumpa nafasi Tunda. Tunda akanyamaza. “Tunda?” Net
akamwita. “Unataka kuishi kama Tunda au Ani wa Sadiki?” Tunda akashtuka kidogo
akamwangalia. “Ani alikufa na Sadiki, Net.” Tunda akajibu. “Haionyeshi hivyo.
Bado yupo na maagano yake yapo hai!” Akamuona anaizungusha ili aitoe.
Net
akasogea pale mguuni. Akapiga magoti. “Naomba mimi niitoe.” Tunda akamwangalia
kama ambaye hamuelewi vizuri. “Ni sawa?” Tunda akatingisha kichwa kukubali. Net
akaitoa. Nakubaki ameishika. “Utaifanyia nini?” Tunda akauliza. “Sijui.
Tumuombe Mungu. Kwanza akutoe kwenye haya maagano na akupe amani. Mengine Roho
wa Mungu atatusaidia.” “Basi acha nikupe vyote. Na cheni ya mkononi na
shingoni.” Tunda akaenda juu ya meza hapo hapo hotelini alipokuwa amening’iniza
mikufu yake.
Akarudi
na hizo cheni zote, akamuwekea Net mkononi. Ni kweli zilikuwa nzito. Net
akamwangalia. “Nipo sawa Net. Nimeridhia kutoa.” “Hilo ndilo la muhimu. Wewe
mwenyewe ukubali kutengana navyo kwanza. Ndio hata tukiomba na kuvunja hayo
maagano, itawezekana.” “Basi tuombe wote.” Tunda akapiga magoti pale alipokuwa
amepiga magoti Net akimvua. Net akacheka kwa furaha.
“Mungu
atakupa mtu anayekupenda kwa dhati.” Tunda akacheka kidogo huku akifikiria. “Mmmh!
Sidhani Net. Acha tu tuombe, niachane na Sadiki nitulie kwanza. Nishahangaika
na wanaume mpaka nimekinahiwa nafsi. Umenipa mapumziko ambayo, hujui tu! Mungu
atakuja kukulipa Net. Hujui kile umekifanya kwangu. Mungu akuonekanie na wewe
siku utakapomuhitaji. Kwa lolote lile. Akumbuke kile ulichonifanyia mimi.”
“Amina.” Wakatulia.
Net
akaweka vile vitu pale kwenye kochi akaanza kuomba. Ameanza tu, akashangaa
Tunda anaanguka tena na mapepo. Akajua ndio maana alikosa amani na ile cheni
pale mguuni. Yale mapepo yakasema yalikuwa hapo kutunza agano. Na lile agano
ilikuwa ni kama ndoa kati ya Tunda na Sadiki. Net alijua tu.
Kijana
huyo wa kizungu, alitumia mamlaka yote aliyopewa na Mungu. Akiwa peke yake pale
chumbani na Tunda akigaragara chini. Akaanza kutambaa kama nyoka na kutema mate
kama nyoka. Safari hii Net hakutumia muda mrefu, akayaamuru yale mapepo yamtoke
na yasirudi tena kwa kuwa Tunda ameshavunja yale maagano na amekiri kifo cha
Ani.
Akajinyonga
pale chini, yakatoka. Ndipo Tunda akazinduka sasa pale sakafuni. Net akamsaidia
kusimama. Alijawa mate. Akawa amejichafua sana. “Nini kimenipata Net!?”
“Ulikuwa na mapepo Tunda.” “Tena!?” Tunda hakuamini. Siku anaokoka alitolewa
mapepo kwa majini.
“Yalikuwa
yakilinda maagano yako na Sadiki. Mlikuwa mpo kwenye maagano yaliyoshikiliwa
kwa nguvu za giza Tunda. Hizi cheni zilikuwa ni ishara za hilo agano.” “Mungu
wangu!” “Usiogope. Umewekwa huru.” “Basi yeye Sadiki alijua anachokifanya. Mimi
nikijua ni zawadi tu, kumbe ni mambo yake. Tena aliniletea akiwa ametoka
safari. Ukute alizinunua ndio akaenda nazo kwa babu, wakazifanyia dawa. Sadiki
alitamani sana anioe nijulikane mimi ni mke wake kihalali. Nilipokataa
akaniomba angalau nimzalie hata mtoto mmoja! Napo nilikataa.” “Basi mshukuru
Mungu upo huru. Anza upya ukitumia uhuru wako vizuri. Nenda kaoge. Nakusubiri.”
“Acha nifute hapo chini sakafuni kwanza.” “Nenda ukaoge. Mimi nitaita mtu wa
hoteli apige deki.” Tunda akaingia bafuni akamuacha Net akiita muhudumu kwa
ajili ya kusafisha.
Tunda
alitoka bafuni na kumuomba Net waombe tena. “Acha woga Tunda.” “Tuombe tena ili
kuwa na uhakika yametoka yote.” Net akacheka. “Usinicheke bwana! Tena tupige
magoti. Ujue mwenzio nilijua nimewekwa huru kabisa na hayo mapepo!” “Yapo
maagano mtu unaingia. Kama si ya kimungu ni mpaka ukubali kuyavunja. Shetani
anakuwa na haki nayo, Mungu hawezi kuingilia. Ukikubali kuyavunja, hapo Mungu
anakuwa na uwezo wakukudai kwa shetani. Anakuwa na haki zote.” “Sasa hivi
sitaki tena Net.” “Na Mungu ameliheshimu hilo, sasa hivi wewe ni wake.”
“Kwani
wewe ulionyeshwa na Mungu juu ya hii sheni?” “Sio moja kwa moja. Ni kweli
inakupendeza sana. Huwa siachi kuitazama hapo mguuni. Lakini kila nilipokuwa
nikitazama sipati amani kama jinsi ilivyokukaa. Unajua kuna kitu kinavutia.
Ukikitazama kwa karibu, kinatakiwa kifurahishe sio kukukosesha amani! Ndivyo
sasa ilivyokuwa hiyo cheni kila nikiitazama kwa karibu, nilikuwa sipati amani.”
Tunda akatulia.
“Tutakuja
kurudisha nyingine hapo mguuni.” Tunda akacheka. “Sio lazima Net. Nakushukuru
kwa kusimama na mimi. Hujanikatia tamaa.” Net akacheka akijiambia ‘hujui hata nusu yake!’ Wakapiga
magoti, wakaomba, ndipo Net akaondoka pale na kumuacha Tunda amelala.
Maajabu ya zile Cheni!
Asubuhi Net alifika na kumpigia
simu ashuke chini waende kazini. Tunda akamwambia aende chumbani kwake. Net
akajua kuna jambo. Akatafuta sehemu ya kuegesha, akapandisha juu kwa haraka. “Vipi?”
“Nimeamka asubuhi, zile cheni hazipo. Au ulizitupa?” “Hapana. Niliweka hapo juu
ya meza. Zote tatu. Na niliziacha hapa wakati umelala.” “Basi zimetoweka.” “Mwache
shetani achukue mali zake.” “Nimeshtuka Net! Yaani nilikuwa nimevaa na
kujifunga mapepo!” “Lakini unachotakiwa kuwa nacho ni kuwa, umebakiwa na
uhuru.” Wakaomba tena na kwenda kazini.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Net
alitafuta kanisa pale pale jijini Arusha, wakawa wakienda na Tunda. Alipata naye muda mwingi wakumfundisha kila
baada ya kazi. Tunda alibadilika sana kimaisha hasa kimtazamo. Ile hukumu aliyokuwa
nayo zamani iliisha kabisa. Tunda alisahau shida zote akawa akiishi kwa furaha.
Net alijitahidi sana kumuelekeza kwenye neno la Mungu. Alimjengea msingi wa
kusoma bibilia. Kila alipomuuliza swali Net, Net alijitahidi kumuelekeza
kwakupitia bibilia.
Maya jijini Arusha, amtaka Tunda aishi nao.
Babu yao
aliugua huko nchini Canada, ikamlazimu mama yao aende kumtizama, ndipo ikabidi
Maya aende akaishi na Net jijini Arusha. Kwa kuwa Net ni kama alihamia Arusha,
na kushindwa kurudi tena Dar kwa kila sababu. Kazi anazofanya Net haikumlazimu
awepo Arusha na kushindwa kusafiri kwenda popote, lakini hakuacha kutoa sababu
zilizoonyesha ugumu wakuliacha hilo jiji.
Ofisi ya
Dar ambayo ilimuhitaji zaidi, kazi zake nzito ndio akawa akizifanya sasa kwa
simu na kompyuta, tena kwa juhudi ili kumnyima mama yake sababu. Tunda hakujua
anayopitia Net, ili kuwepo naye hapo Arusha. Alikuwepo hapo kwenye ofisi za
usafirishaji, lakini alifanya na kazi za mama yake pia huko Dar.
Tunda
alishangaa siku hiyo asubuhi Net anampigia simu kumtaka ashuke waelekee kazini,
akiwa na Maya. Alifika garini akamkuta Maya anamsubiria kwa hamu. Walikwenda
naye ofisini akiwa na Tunda wakati wote. Maya alionyesha kuvutiwa na Tunda kitu
kilichomshangaza hata Net.
Alikuwa
muongeaji sana tofauti na Net. Lakini binti mdogo tu na nadhifu. Baada ya kazi,
waliamua kwenda kula wote watatu kwenye mgahawa wa pale pale hotelini anapoishi
Tunda. Wakati wanakula wao watatu, akumuomba Tunda akaribie kuishi nao nyumbani
kwao. Tunda akashangaa kujua kuwa Net ananyumba kule Arusha. “Nilifikiri
unaishi hotelini Net!” “Hapana. Tulinunua nyumba.” Hata Maya akashangaa.
“Hujawahi
kufika!?” Akamuuliza Tunda kwa mshangao. Tunda akacheka. Maya akamgeukia kaka
yake. “You must be kidding me!” Akamwambia kaka yake. “Acha fujo Maya.” “Tatizo
la Net, yupo sooooo..” Akawa anafikiria Maya jinsi ya kumsimulia Tunda jinsi
alivyo Net. “Aaah! Sijui hata nikwambie nini! Lakini umenishangaza kushindwa
hata kumkaribisha sehemu unayo ishi!” “Ningemkaribisha bwana. Sema tumekuwa na
mambo mengi.” Tunda alishamjua Net ni mwadilifu sana na hana haraka.
Maya aliaga kuwa anakwenda kutumia choo. Net
akamgeukia Tunda. “Upo huru kuja kuishi naye kama unataka. Labda itamsaidia.
Hana rafiki hapa nchini na kila kitu mama anachomwambia anaona anaonewa. Labda
wewe unaweza kuwa karibu naye, ukamsaidia.” Tunda akashangaa Net anazungumza nini!
“Net!
Namwambia nini mimi Maya!? Mwenzangu amezaliwa uzunguni, mimi mtoto wa mtaani.”
Wakacheka. “Inawezekana historia yako, ikawa msaada mkubwa sana kwake.
Usidharau.” “Mmmh!” Tunda akaguna na Maya akawa amerudi akawakuta wanacheka. “Sasa
Tunda umeamua nini? Nakuja kuishi hapa na wewe au wewe unakuja tuishi kule?”
“Upo kama kaka yako!” Wote wakacheka.
“Kweli.
Wote hamsahau jambo, na mking’ang’ania kitu, kinakuwa hichohicho na mpaka
mpate.” “Hiyo ipo kwenye damu. Sasa hujakutana na Nana. Nana ndio mbaya zaidi.
Hajui jibu la ‘hapana’ anapotaka jambo lake. Na hapendi mtu aombe kitu
ambacho hajakifikiria, au hana umuhimu nacho. Na anashangaa ukiwa unataka kitu
halafu ukakikosa, ukatulia. Anasema inamaana unataka kitu ambacho kwanza
kinakuwa hakina umuhimu. Na inamaana hujafikiria ndio maana ukikikosa inakuwa
rahisi kuridhika.” Tunda akapata hapo somo.
“Nana ni
nani?” Tunda akamgeukia Net. “Bibi ndio tunamwita Nana.” Net akajibu. “Oooh!
Anaonekana ni smart.” Tunda akasifia. “Hujawahi kuona mwanamke kama huyo hapa
duniani.” Tunda na Net wakacheka. “Lakini ni kweli. Nana yupo very smart.
Wakati wote huwa anajua anachokitaka. Na kama alivyosema Maya, huwa hajui jibu
la hapana, linapofika swala la kukamilisha jambo lake. Anaweza kuhamisha
milima, ili kukamilisha swala dogo ambalo kwako linaweza hata lisilete maana.”
Net akaweka msisitizo.
“Kwa
hiyo tunakwenda au tunabaki?” Maya akarudia swali. Wakacheka. “Eti Net?
Haitakuwa usumbufu?” “Hata kidogo. Ni sehemu kubwa. Utapata chumba chako na
utanisaidia kusikiliza kelele za Maya, ili niweze kufanya kazi.” “Heeee!” Maya
akalalamika nakukunja mikono kifuani kwake kama mtoto, akimtazama kaka yake.
Wakacheka. “Basi nitahamia kesho. Acha nifungashe usiku wa leo.” Tunda akubali
kwenda kuishi nao nyumba moja.
Tunda afanyika Msaada kwa Maya.
Nikweli
alibadili maisha ya Maya. Kwa kuwa na yeye alikuwa akiongea kingereza kizuri,
ilimrahisishia sana Maya kwenye mawasiliano, kwani mama yake ndiye aliyekuwa
akimlazimisha kujifunza kiswahili. Tunda alimweleza maisha ya shida aliyopitia,
bila kwenda kiundani zaidi, na kumwambia kama angepata nafasi kama yake,
angeitumia vizuri sana.
Ilikuwa
ni muujiza hata kwa Net. Maya alikuwa akimsikiliza sana Tunda kuliko mwanadamu
yeyote yule aliyekwisha kuwa naye karibu. Kwa asili Maya alikuwa mbishi sana.
Haambiliki na alilelewa maisha ya kudekezwa sana na bibi na babu yao. Hakuwa
akijua shida hata kidogo. Tunda aliongea na Maya mpaka akakubali kurudi shule.
Net alifurahi sana, akamshukuru Tunda. Alimpigia simu mama yake akiwa kule kule
nchini Canada, Maya akarudishwa Canada kwa ajili ya kuanza chuo.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Hali ya
babu yao ilizidi kuwa mbaya huko nchini Canada, ikamlazimu Net aende. Hawakuwa
ni babu tu na bibi. Waliwalea Net na Maya tokea wadogo sana tokea baba yao alipoanza kuugua mpaka akafariki. Na
hata mama yao alipoondoka nyumbani kwa wakwe na kurudi nchini Tanzania, wao
walibakia kwa bibi na babu yao. Walitunzwa wakachukua nafasi ya watoto kwa hao
wazee waliokuwa wamepata mtoto mmoja tu ambaye ndiye baba yake Net na Maya.
Net
alichukuwa jina la babu yake. Natheniel Cote. Ilibidi kuwa wakiandika sehemu
muhimu wawe wanaandika Jr au Seniour ili kujua ni yupi. Shule zote za mahela
yote hayo alizosoma Net, alikuwa akilipiwa na babu yao. Alipendwa sana, na
alimkuza Net kwenye maadili ya msingi. Ndio maana Net alikomaa mapema japo
alitoka kwenye familia ya kitajiri sana. Kila mtu alijua Net ndiye mrithi wa
mali nyingi za huyo mzee Cote.
Kwa kuwa
Maya alishaondoka nchini, wawili hawa walibaki wakiishi pamoja, kazini pamoja,
kwenye gari pamoja. Japo haikuwa kwa muda mrefu, lakini palishajengeka ukaribu
kati yao.
Net Arudi nchini Canada, Nakumlazimu kutengana na Tunda.
Tunda ndiye aliyemsindikiza Net
uwanja wa ndege. Alikuwa amepooza. “Utakuwa sawa Tunda. Na nitakuwa nikikupigia
simu kila siku. Kama ukiwa na maswali yeyote kazini, nikipiga simu nitakuwa
nakusaidia.” “Lakini haitakuwa sawa kama tulivyokuwa wote! Najiona kama bado
nakuhitaji sio tu ofisini, hata kwenye maisha ya kawaida. Naomba uniahidi kuwa
utarudi Net.” Net alimuhurumia Tunda akajua aliingiwa na hofu na ndio maana
hakumuaga mapema.
Tunda
hakujua huyo Net alikuwa akisubiriwa kwa muda mrefu sana, lakini akawa
akiahirisha safari kwa ajili yake. Kila alipojiambia ataondoka, alikuwa anaona
bado hili na lile. Akawa akimwambia bibi yake nitakuja hivi karibuni. Lakini hakwenda
mpaka alipoambiwa hali mbaya, anaweza asimkute babu yake, ndipo ikamlazimu kuondoka.
Akamgeukia
vizuri. “Niangalie Tunda.” Tunda akamwangalia vizuri. “Nikikwambia hata mimi
natamani nisiondoke, utaamini?” Tunda akatingisha kichwa kukubali. “Basi ujue
nitarudi haraka. Niombee mambo yaende vizuri.” Walitafuta sehemu wakakaa,
wakati wakisubiria muda wa Net wakuondoka. Tunda alikuwa amejisogeza karibu
yake, ameinama. Hakuondoka mpaka Net alipoingia kwenye ndege.
Maisha bila Net.
Tunda
alitulia, akashika usukani. Ni kweli aliiendesha ile ofisi bila shida, huku
akitumia gari ya Net na kuishi kwenye nyumba yao. Tunda hakuacha kuwasiliana na
Net kumpa taarifa kwa kila kinachoendelea na kumtaka ushauri. Na kwakuwa na
yeye alifanywa kuwa muweka saini benki, hata malipo mengine alifanya yeye
mwenyewe, tena kwa uaminifu sana. Kila mwishoni mwa juma, alimtumia Net benki
statement na ripoti ya matumizi yote. Walishauriana kwenye simu, na Net aliweza
kuendesha mambo ya pale ofisini, akiwa mbali, kirahisi sana kwa msaada wa
Tunda.
Tunda apambana na Mama Cote.
Tokea
aachane na Mama Cote pale kanisani hakuwa amemsikia tena huyo mama. Hata
kupokea simu yake ya salamu hakupokea tena. Haikumsumbua Tunda kabisa, alijua
ni hali ya ubusy kwani yule mama alikuwa muhangaikaji sana kisha akawa
amekwenda nchini Canada kumuona huyo mgonjwa ambaye ni mkwewe.
Ilikuwa
siku ya jumamosi ambapo Tunda alishazoea kufanya nusu siku alipokuwa na Net,
lakini sababu ya kuwa peke yake aliitumia hiyo siku kukaa ofisini mpaka usiku.
Alifanya mambo mengi, na akatayarisha ofisi ile kwa siku ya jumatatu. Kijana wa
usafi hakuwa akija siku za jumamosi, kwa hiyo kila alipotumia ofisi siku za
jumamosi, alijitahidi kuacha safi ili asimsumbue kijana wa usafi anapokuja siku
ya jumtatu.
Alishaongea
na Net wakati Canada ilipokuwa usiku wakapeana maelekezo na miahadi yakupigiana
tena simu siku inayofuata, pale Tunda atakapo amka. Tunda akarudi nyumbani
akiwa amechoka sana. Mlinzi akamfungulia geti, akamsalimia kwa kumpungia mkono
akaingia ndani.
Alipoingia ndani, akakuta Mama
Cote amekaa na msichana mwingine pale sebuleni. “Net hakuniambia kama mnaishi
naye hapa!” “Sikuwa nikiishi na Net peke yake, mama. Maya ndiye alinikaribisha
hapa.” “Maya!?” “Ndiyo mama. Shikamoo.” “Mwanzoni ulikuwa ukiishi wapi?”
“Hotelini, mama.” “Kweli Net alikubali kukutoa kwenye nyumba za kulala wageni
akakuweka hapa na mtoto mdogo kama Maya!?” Tunda akanyamaza. Hakuwa ameelewa
kabisa, kwani Mama Cote aliyemfahamu yeye alijawa na hekima na mwingi wa
shukurani. Na alimkarimu sana nyumbani kwake, akampa hata chumba chakuweka
mizigo yake na kukitumia kama angelala.
“Kuna
nini mama!?” “Nimeshtuka sana kukukuta nyumbani kwangu!” “Samahani mama,
itakuwa Net amesahau kukwambia. Hata hivyo naweza kuondoka tu hata sasa hivi.”
“Kabla hujaondoka nataka kukutambulisha kwa bosi wako mpya, huyu hapa. Anaitwa
Safia. Safia amesoma na anauzoefu wa kazi, kwa hiyo atakusaidia sana.” “Karibu
sana Safia. Basi jumatatu nitakuonyesha pale ofisini.” “Sio kumuonyesha tu!
Nataka umkabidhi kila kitu, yeye ndiye atakuwa akikwambia kitu gani
chakufanya.” Tunda alishtuka kidogo, lakini hakujali. “Sawa mama.” Tunda
akaitika.
“Na
atakuwa akitumia hicho chumba ulichoweka mizigo yako.” “Hakuna shida mama
yangu. Nitaondoka na kila kitu.” Tunda akaingia ndani, akakusanya vitu vyake
vyote, akaweka kwenye begi lake akaanza kulivuta kulitoa nje pamoja na mizigo
yake mingine iliyokuwa na nguo, viatu pamoja pochi zake nyingi tu ambazo
alipenda kubadili kama viatu. Akakumbuka amesahau funguo za gari ndani.
Akarudi
wakati ameacha mizigo yake yote nje. Alipoingi tu, “Halafu binti!” Tunda
hakujua kama anaitwa yeye, aliendelea kuelekea kule alipokuwa ameacha pochi
yake aliyotumia siku hiyo. “Wewe Tunda, umeanza lini kiburi?” “Kwa nini mama?”
“Nakuita kwa nini unanyamaza!?” “Sikujua kama unaniita mimi. Samahani.” Tunda
aliendelea kujibu kwa heshima sana.
“Naomba
na funguo za gari. Atakuwa akitumia yeye hilo gari, kabla hatujamnunulia la
kwake.” Tunda alifikiria kidogo. “Sasa hivi ni usiku mama. Naomba niondoke na
gari, kisha nitarudisha gari asubuhi ili nisipate shida ya usafiri na mizigo
yangu.” “Naweza kukuitia taksii.” Tunda akatulia kidogo, kisha akamsogelea Mama
Cote.
“Kwani
kuna tatizo lolote mama yangu? Mbona kama..” “Hakuna tatizo lolote. Mimi ndiye
mmiliki wa kila kitu, au Net hakukwambia hilo?” “Nafahamu.” “Sasa unauliza nini
endapo mwenye mali anadai mali zake!?” Tunda akabaki ameduaa.
“Na
ninaomba funguo za ofisini kabisa, pamoja nafunguo za safe. Kwa kifupi naomba
funguo zote za ofisi na simu ya ofisi pia naomba.” “Unamaanisha simu yangu ya
mkononi!?” “Si ulinunuliwa kwa matumizi ya ofisini? Sasa unapunguziwa majukumu,
huhitaji tena simu ya mkononi.” Tunda alibaki ametoa macho kwa muda.
“Vipi?
Au uliahidiwa nini na Net? Isijekuwa navunja makubaliano fulani.” Tunda alivuta
pumzi kwa nguvu, kisha akanyanyua pochi yake, akatoa simu na funguo zote za
ofisi na gari kisha akamkabidhi. “Asante mama, usiku mwema.” Tunda akaondoka.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Ulikuwa
ni mshtuko mkubwa sana kwa Tunda. Alijiuliza maswali mengi bila kupata jibu.
Alifikiri hili na lile bila kuhisi kosa lake. Alikuwa na wakati mgumu sana
akisubiria hiyo siku ya jumatatu, hata kanisani alishindwa kwenda.
Hakuwa
na simu ya kuwasiliana na Net, kwa kuwa simu alinyang’anywa. Simu yake ilipotea
kwenye mazingira ya kutatanisha. Hakujua kama aliiacha sehemu au aliibiwa
kwenye pochi. Alijikuta hana simu ndipo Net akampa iliyokuwepo tu pale ofisini
na kumtaka aitumie akisema ni muhimu kwa kazi kwa kuwa yeye alimwambia hana
shida tena na simu. Hana mtu wakuwasiliana naye. Lakini yule mama alimpokonya.
Ilikuwa simu nzuri sana.
Jumatatu
ya machungu na mapinduzi!
Siku
hiyo ya jumatatu aliamka mapema, na kuwahi ofisini. Alifika ofisini na kumkuta
Mama Cote yupo ofisini kwa Net, na Safia yupo kwenye meza yake. Tunda aliweka
pochi yake pembeni ya meza, akaingia kumsalimia Mama Cote. “Shikamoo mama.”
“Naona hapa mambo yamekuwa yakiendeshwa kienyeji enyeji kweli! Sioni faili lako
la kuajiriwa. Sioni vyeti vyako wala barua zako zakuomba kazi.” Tunda akabaki
kimya, lakini mwili mzima ukitetemeka.
“Naomba
ukaniletee vyeti vyako vyote vya shule,
ili tujue kama ni kazi ninakuajiri upande upi.” Tunda alibaki kama
amepigwa na butwa. Kimya. “Umenisikia?” “Sina vyeti mama.” “Kwa nini huna
vyeti?” “Sina vyeti kabisa.” “Kwani hukusoma!?” Yule mama akamuuliza kwa namna
yakumdhalilisha mbele ya Safia na yule kijana wa usafi, waliokuwa wakisikiliza
pale nje. Tunda akanyamaza.
“Hata
cheti cha kidato cha nne huna!?” “Sina mama.” Tunda alishaanza kupaniki. Hofu
yakufukuzwa kazi ikamjaa. “Wewe ulilemea upande mmoja tu, kutembea na wanaume
za watu! Ukapata ujuzi wa kuvutia wanaume, ukakosa ujuzi wa ofisini! Sasa hapa
Net wa kumrembulia macho ili aendelee kukuweka hapa ofisini, hayupo. Hii ni
ofisi yangu. Nimehangaika sana kufika hapa nilipo. Sikutafuta pesa kwa kuvulia
nguo waume za watu, nimehangaika mimi mwenyewe. Uzembe mdogomdogo sitaki.
Hamkawii kunirudisha chini kimaendeleo!” Yule mama alianza kupiga mahesabu,
kisha akanyanyuka.
Akafungua
safe akatoa pesa. “Huu ndio mshahara wako wa mpaka siku ya leo. Rudi shule
binti, acha kuruka ruka na wanaume. Ukishapata vyeti ndipo urudi tuzungumze.”
Bila kuongeza neno, Tunda akapokea pesa yake, na kuondoka pale.
Historia Yajirudia! Maisha mengine tena kwa Tunda mara baada ya
kufukuzwa ‘Tena’ kwa kina Cote.
Tunda alirudi hotelini, akakaa
chini asiamini kinachomtokea. Aliumia sana kusikia anatukanwa na Mama Cote, kwa
kupitia maneno aliyosema kanisani, tena akiwa ameambiwa ni sehemu pekee ambapo
atakuwa salama! Tunda akalia sana, lakini alikumbuka jinsi alivyofundishwa na
Net kuomba.
Akapiga
magoti akamuomba Mungu kwa kulia sana. Tunda akamlilia Mungu kwa uchungu
akirudia rudia kumweleza maumivu aliyonayo. Hakuwa mjuaji sana wakuomba, lakini
alijua kumueleza Mungu kile alichokuwa akijisikia. “Naogopa
sana Mungu wangu. Nimeumia, nina maumivu makali sana. Sijasoma, sina kimbilio,
sijui naanzia wapi tena maisha. Katika yote naomba nisaidie nilinde mwili wangu
usiteswe tena. Sitaki kurudia yale maisha tena. Nisaidie kwa njia yeyote ile
ili niweze kuishi kwa uwezo au karama yeyote uliyoniumba nayo, ukaweka ndani
yangu kama alivyoniambia Net, kuwa kuna kipaji lazima umekiweka ndani yangu
ambacho kitanisaidia. Usiniache tena. Milango yote naiona imefungwa, lakini
najua Mungu wewe unaona kwa tofauti. Nisaidie.” Tunda akamaliza kuomba,
akapata faraja ya ajabu.
Wazo
la kurudi Dar likamjia. Hakutaka kupoteza muda tena pale hotelini, akabeba
mizigo yake yote, asubuhi hiyo hiyo akaenda kituo cha mabasi pale jijini
Arusha, akakata tiketi yake akapanda basi kurudi Dar. Alionelea ni heri kurudi
Dar, mji alioufahamu vizuri kuliko kuendelea kuishi Arusha. Hata hivyo vitu
vyake vyote aliviacha huko.
Tunda arudi jijini Dar na kupambana Njiani na Jaribu akumrudisha
kule Yesu alikomtoa kupitia Net.
Tunda alipata
siti ya upande wa watu wawili. Pembeni yake alikaa baba mmoja mtu mzima kidogo.
Walisha salimiana, lakini yule Mzee hakutosheka kumtizama Tunda. Na Tunda
alijua. Akaamua kutoa bibilia yake asome ili kumfanya yule baba amuogope. “Soma
kwa sauti basi na mimi nisikie neno.” Yule mzee alimtupia neno Tunda.
“Naweza
nikakupa tu, usome mwenyewe.” Tunda akataka kumkabidhi. “Unakwenda kanisa
gani?” Tunda hakuwa hata na kanisa analolifahamu huko Dar. “Ndio nahamia Dar,
bado sijajua nitapata wapi kanisa.” “Ooh! Karibu sana jijini. Kwa hiyo hata
sehemu yakuishi bado hujapata?” “Ndio naelekea huko. Naamini nikifika huko
nitapata.” “Basi mimi niwe mwenyeji wako. Nina nyumba yangu napangisha vyumba
huko Temeke. Naweza kukupangisha. Tena kuna mpangaji mmoja ametoka juma lililopita
tu, nilikuwa nakikarabati hicho chumba. Ni chumba kimoja na sebule yake. Kwa
kuwa ndio unahamia hata huna haja yakunilipa kodi kwa sasa, tutakatana juu kwa
juu.” Tunda alitabasamu kisha akageukia dirishani.
“Vipi?”
Akaendelea kutaka Tunda amsikilize. “Na kanisani nitakupeleka usiwe na
wasiwasi.” Tunda akamgeukia yule Mzee akamtizama kwa muda, asiamini kama historia inajirudia kwa haraka kiasi hicho! “Au hutaki
kuishi Temeke? Tunaweza tukashukia hotelini wakati tunatafuta nyumba nzuri ya
wewe kuishi.” Tunda alifunga bibilia yake akairudisha kwenye pochi yake....
0 comments: